CHADEMA si kimbilio la wasomi!

Tumewachoka chadema wanaoshabikia hawakijui undani wake ila ukiwa mchunguzi utagundua kile ni chama cha ukoo wa kaskazini mwa Tanzania.

Mfano Mbeya kwa Sugu, Mbozi kwa Silinde, Kigoma kaskazini kwa Zitto Kabwe, Mwanza, iringa, Msoma, Na sasa dalili za S'wanga, nk.
 
Waacheni wafu wawazike wafu wenzao hivi humu JF tu mnapata picha gani nyie CCM mbona hamsomi alama za nyakati kama tulio JF ni wa kijiweni subiri muone.

Subiri tuone! Mnatutisha, mnadhamiria kushika bunduki. Nawaogopa kama ukoma, maana ile kauli ya mpaka kieleweke sijaielewa mnadhamiria nini?

Jamani ioneeni huruma TZ.
 
Nisingetaka kujibizana na wanaJF kuhusu allegations kwamba CDM ni chama cha kikanda au kwamba mikakati yetu inaleta fujo au uvunjifu wa amani.

Ukweli unajionyesha katika matokeo ya chaguzi ambazo zimetupa Wabunge tangu Tanzania iingie katika mfumo wa vyama vingi vya siasa: Kigoma Mjini, Kigoma Kaskazini, Tarime, Mwanza, Ukerewe, Mbeya, Iringa, Singida na Dar es Salaam. Hizi ni sehemu ambazo tumeweza kuwa na majimbo yaliyowachagua wana-CDM tangia 1995. Sitaji Kilimanjaro na Arusha ambako ni chimbuko langu, na ilitegemewa ituelewe kwa urahisi zaidi.

Kuhusu fujo na tishio la uvunjifu wa amani, naweza kusema sio dhamira ya CDM kuleta fujo. Sera zetu zinaelezwa kwa mantiki na ufasaha. Viongozi wetu ni jasiri na wana uzalendo wa hali ya juu. Tuna huruma kwa wanyonge wanaotaabika kutokana na tunawapa ujumbe wa matumaini.

Inaonekana kwamba Serikali na CCM wameishiwa mbinu na mikakati ya kuleta maendeleo. Wamechoka.

Baya zaidi ni kwamba, jinsi inavyodhihirika wengi wao wamebakia kukwapua tu mali ya umma, wanalazimisha taasisi kama Polisi kutumia risasi za moto kutishia uhai wa wananchi wanaotuunga mkono. Chini ya Katiba ya sasa vyama vya siasa vina uhuru wa kuandamana kwa amani. Polisi jukumu lao ni kusindikiza maandamano hayo kuhakikisha amani na katika mikutano kuona kwamba watu wenye nia mbaya hawaleti fujo.

Ukweli kwamba wengi wa Wabunge wa CDM hawatoki vijijini, unatokana na historia na uchanga wetu. Nchi yetu ni kubwa na chama kichanga hakina uwezo wa kuwafikia wananchi wote wa vijijini. Katika kipindi hiki cha miaka 3 kufikia Uchaguzi Mkuu wa 2015 ni lazima mbinu zibuniwe kuwafikia Watanzania huko vijijini. Na helikopta nyingi zitahitajika.
 
Nisingetaka kujibizana na wanaJF kuhusu allegations kwamba CDM ni chama cha kikanda au kwamba mikakati yetu inaleta fujo au uvunjifu wa amani.

Ukweli unajionyesha katika matokeo ya chaguzi ambazo zimetupa Wabunge tangu Tanzania iingie katika mfumo wa vyama vingi vya siasa: Kigoma Mjini, Kigoma Kaskazini, Tarime, Mwanza, Ukerewe, Mbeya, Iringa, Singida na Dar es Salaam. Hizi ni sehemu ambazo tumeweza kuwa na majimbo yaliyowachagua wana-CDM tangia 1995. Sitaji Kilimanjaro na Arusha ambako ni chimbuko langu, na ilitegemewa tuelewe kwa urahisi zaidi.
Kutokana na jinsi tunavyowakilishwa Bungeni, sio kweli kwamba CHADEMA ni chama cha ukanda.

Kuhusu fujo na tishio la uvunjifu wa amani, naweza kusema sio dhamira ya CDM kuleta fujo. Sera zetu zinaelezwa kwa mantiki na ufasaha. Viongozi wetu ni jasiri na wana uzalendo wa hali ya juu. Tuna huruma kwa wanyonge wanaotaabika kutokana na tunawapa ujumbe wa matumaini.

Inaonekana kwamba Serikali na CCM wameishiwa mbinu na mikakati ya kuleta maendeleo. Wamechoka.

Baya zaidi ni kwamba, jinsi inavyodhihirika wengi wao wamebakia kukwapua tu mali ya umma, wanalazimisha taasisi kama Polisi kutumia risasi za moto kutishia uhai wa wananchi wanaotuunga mkono. Chini ya Katiba ya sasa vyama vya siasa vina uhuru wa kuandamana kwa amani. Polisi jukumu lao ni kusindikiza maandamano hayo kuhakikisha amani na katika mikutano kuona kwamba watu wenye nia mbaya hawaleti fujo.

Ukweli kwamba wengi wa Wabunge wa CDM hawatoki vijijini, unatokana na historia na uchanga wetu. Nchi yetu ni kubwa na chama kichanga hakina uwezo wa kuwafikia wananchi wote wa vijijini. Katika kipindi hiki cha miaka 3 kufikia Uchaguzi Mkuu wa 2015 ni lazima mbinu zibuniwe kuwafikia Watanzania wengi iwezekanavyo huko vijijini. Labda helikopta nyingi zitahitajika.
 
Hakuna anaye dhamiria kushika bunduki! Ccm ndio wanaaendelea kutumia bunduki kuzima harakati za ukombozi wa taifa hili.
Mpaka kieleweke tuna maana mpaka tuakikishe ukombozi wa taifa hili una patikana,

mpaka kielewe tuna maanisha kuhakikisha walala hoi na hao unao waita wa vijiweni wanapata na fuu ya maisha kama wengine.

Mpaka kieleweke tuna maanisha kupambana kuhaakikisha kuwaondoa madarakani mafisadi kwa njia ya box la kupigia kura.

Bora umekuwa muwazi ili ueleweshwe, nimependa uwazi wako zawadi.
Subiri tuone! Mnatutisha, mnadhamiria kushika bunduki. Nawaogopa kama ukoma, maana ile kauli ya mpaka kieleweke sijaielewa mnadhamiria nini?

Jamani ioneeni huruma TZ.
 

Sikutaka niwachoshe kwa taarifa nzima ya utafiti, mkashindwa kusoma. Kumbuka niliiandaa hii taarifa nikijua kuwa watu wengi watakaosoma ni wakijiweni, hivyo hawana haja ya manamba mengi.

Taarifa ikiwa ndefu na minamba mingi hupoteza mvuto kwa watu wa kijiweni kuisoma.

Point zako ni nzuri na pengine wewe ni msomi pekee wa CDM, lakini kwa bahati mbaya nilipenda watu wengi wa kijiweni wausome muhtasari huu.

Lengo kuu la kuandika taarifa hii ni kuwataharadhisha Uongozi wa CHADEMA moto wanaouandaa kwa nchi yetu. Hii inamaanisha kuwa bado hawajachelewa wanaweza kujinasua sasa hivi.

Sababu nyingine ni kuwataharadhisha waTZ wapiga kura, kuelewa kitachowapata pindi CHADEMA ikichukua nchi.

Haya yote nimeyaandika kwa sababu ya kuipeneda nchi Yangu.
 
Mimi sioni hata implentation ya wasomi wanaotajwa. Badala ya kufanya tafiti wanagombea ubunge. Mimi naamini msomi ni mtu anayetafuta solution ya mambo. Kumbe hata Rage ni msomi ndio maana yuko CCM? Hongereni kwa wana ccm kuwa na wasomi wengi kama makatibu kata wa chama na w/viti wa Wilaya na Mikoa
 
Kwa maneno hayo niliyoyawekea alama ya fungua na funga semi Hata form six hujafika!.
 
Tumewachoka chadema wanaoshabikia hawakijui undani wake ila ukiwa mchunguzi utagundua kile ni chama cha ukoo wa kaskazini mwa Tanzania.
Kweli kabisa CHADEMA ndiyo iliyoteua Mawaziri wakuu 6 kutoka kaskazini na wanaobaki wanne toka Dodoma, Mpanda, Songea na Zanzibar. Na tena ni chama kilichowabangua Wazanzibar kwa kuwapa Waziri mkuu mmoja tangu uhuru! Tena kikatoa Mawaziri wakuu waislamu wawili tangu uhuru!.
 

Our ancestors fought for this land even before colonialism, during colonialism and after, and we will continue to do so, and our children children will continue after us, haijalishi cdm wameshinda au hawajashinda.....what we need is opportunity for us and our children!! Kama wewe unazani kuongoza nchi kunakofanywa na ccm is a big deal, think twice!! if your a scientist, you ask the wrong question and you got the wrong answer......na kama unadhani wewe msomi basi ulichokisoma is out of date, ..go back ukajitafakari vizuri!!
 
Eti unaitwa Zawadi!kama hii ndo zawadi aliyoamua kutuletea watanzania heli angeichomoa tu hiyo mimba,,na hiyo mbegu iliyosabisha ukazaliwa bora baba yako angezipigia punyeto(kujichua)kuliko kukuzaa wewe,kwa taarifa yako me ni mmoja wa wasomi wa chuo kikuu,zaidi hapa chuoni Gwanda za kikamanda ni kama sale za chuo,kila darasa tumejaa makamanda,wanachadema na wengi wanakadi za CDM mpaka za kupigia kula,wewe kma ni msomi bt bado hayupo CDM,ujue ukoo wao magamba,nenda pale UDOM kisha umalizie SAUT utanenepa kwa hasira,japo usalama dhaifu wa ccm wapo na wanatupiga mikwala daily,hebu cheki kalenda,mwisho wa mwezi huu,isije CDM wakakusababishia round kuwa ndeeeeefuuuuuu. Nani aliikagua hiyo reseach?
 

Mkuu Zawadi Ngoda, naomba kutofautiana na wewe kiasi fulani katika haya;

1. Kama msomi uliyefanya utafiti na kutumia pesa, nguvu, akili na muda wako/wenu..ni ajabu kusema UTATUCHOSHA na taarifa ya utafiti ulioufanya, then if ni hivyo why bringing up the topic at all?

-Uliposema "ulitegemea vijana wa vijiweni wasome"..ulimaanisha nini mkuu? kuwa wengine haiwafai? then itakuwa ulisahau kuandika title "kwa vijana wa vijiweni wa CHADEMA"..then kama ni vijana wa "vijiweni" wanapatikana huku jamvini mkuu?



2. Katika aya ya pili umesema utafiti ni mrefu na ungekosa mvuto?..Mkuu, naomba nikuulize swali ulishawahi kusoma hotuba ya Mh. Rais ya mwisho wa mwezi? vipi kuhusu taarifa za wizara za Bunge n.k ...nakuhakikishia ni NDEFU unaweza kutengeneza jarida!!

Ukaongelea suala "MVUTO" , ni mvuto upi unaousema? mvuto kwa nani? ni kipi bora kati ya mvuto au umakini wa taarifa?


3. Mkuu katika aya ya tatu umesema mimi ni "msomi pekee wa CDM" ..ningependa kukukumbusha kuwa siko CDM, lakini hadi sasa sijaona ubaya wa mimi kufikiria kuwa huko!


Kwa ushauri tu mkuu, ni ngumu..narudia tena ni ngumu sana, kushawishi watu kwa "ubaya" wa watu wengine kuliko kushawishi watu kwa mema uliyofanya/mliyofanya.
 

Ongea pumba zako kisha ukalale wakati Nyerere anaongoza wimbi la kupigania uhuru kulikuwa na mkuuwa wilaya yeyote mwananchama wa TANU? mbona nyie wabeza chadema mnaongea kama sio wasomi? reasoning zenu ni hafifu maana elimu zenu ni za kiwango cha chini. Kwa taarifa yako wasomi wengi wako nyuma ya chadema hawawezi kujitokeza hadharani wanapokonywa nyadhifa zao na kufanyiwa unyama kwa sababu ya serikali ya CCM ni ya kidhalimu, kimabavu, kifisadi, kinyanyasaji na yenye kutawaza wana wa masultani kutawala.

Hata wakati wa Mwalimu wafuasi wa TANU waliokuwa serikalini kama Joseph Kasela Bantu na wengine hawakuwa hadharani kujitokeza sana kama wale waliokuwa hawana ajira serikalini mfano Kawawa, Mzee Tambaza, akina Skyes, Paul Bomani na wengine na wenye professional za malipo hafifu kama Kambona nao walijitokeza wazi maana alikuwa mwalimu walimwaga manyanga mapema na kuwa mstari wa mbele kwa sababu hawakuona hasara sawasawa na leo wenye kazi nzuri sana serikalini wanaimba CCM kutetea unga subiri 2015 uone watakavyogeuka kwa haraka na CCM hutaisikia tena kama UPC nchini Uganda, KANU huko Kenya, UPRONA nchini Burundi, UNIP nchini Zambia, chama cha Gadhaffi huko Libya na National Party cha Mubarak huko Misri ila unaruhusiwa kuweka bendera za jembe na nyundo kama ukumbusho nyumbani kwako.
 
Ujumbe wako upo clear mkuu. Bahati njema wananchi wanazijua mbinu chafu za CCM. M4C inasonga mbele.
 
Nadhani kama ungekuwa umemsikiliza sitta vizuri na ukamsikiliza Dr slaa wala ungejua jinsi sitta anavyo jichanganya.

Kifupi sitta hata wana ccm wana mjua ni mnafiki labda wewe peke yako!

Naona umeamua kumsezesha ngudu yako maneno( kikanda)
je umeona haya majimbo?
-mbeya mjini
-singida
-kigoma
-mwanza
-ubungo
-moshi
-Arumeru
-Arusha mjini
sijui hizo propaganda zenu wewe una ziweka wapi sidhani kama una maanisha unacho kiongea?

Swala la cdm heti haifiki vijijini ilikuwa propaganda yenu ya zamani lakini wewe bado unayo na kushangaa sijui kama kweli wewe ni mfatiliaji wa mambo vizuri.
Tumeamua kufika vijijini mmechanganyikiwa na mmeanza kutumia risasi kuuwa watu, kama mnajua hatufiki vijijini na huko ndiko kuna wapiga kura wengi,je kwanini mnatumia nguvu nyingi kuzuia chama ambacho hakiwezi kuwa fikia wananchi walio wengi?

 
unajua sion sababu ya kubishana juu ya chama kuwa na wasomi wengi ama la kwani usomi wa wanachama kama hautusaidii kwenye kupambanua mambo ili kuleta suluhisho la kudumu la matatizo ya watanzania bado hauna maana.

ishu hapa je ni mtu gani ambaye anaweza kutuongoza ili kuifikia Tanzania yenye neema awe anapatikana ndani ama nje ya chama basi tumruhusu atuongoze. na kama katiba hairuhusu mgombea binafsi basi tumsihi ajiunge na chama fulan ili tu tuwe nae.
 
Chadema ni kimbilio la watu wengi walionyimwa fursa mbalimbali na chama dhalimu CCM, wakiwemo hao vijana wa mtaani! kama utakuwa mkweli katika tafiti zako, vyuo vikuu wengi wanaisupport chadema. Refer matokeo ya uchaguzi wa 2010 vituo vyote vya UDSM chadema kiliongoza kwa kura nyingi sana za uraisi na ubunge. Sasa utasemaje kwamba si kimbilio la wasomi?
 
Je magamba ndio kimbilio la wasomi? nakama magamba na chama chao wameenda shule wanawezaje kuliingiza taifa katika mikataba kandamizi,au huo usomi wao wamesomea kuwanyonya watanzania maskini?kumbuka kuwa ukombozi wa taifa unahitaji dhamira safi,moyo safi,ujasiri na wala siyo kuwa na phd wala masters,wakina simba wa vita nyerere na wengine hakuwa na elimu ya kutisha ila waliweza kumuondoa mkoloni,leo CDM hatuhitaji watu wenye Phd bali tunahitaji watu wenye dhamira njema na taifa letu ambao tutashirikiana nao katika kulikomboa taifa zidi ya mkoloni mweusi.kumbuka kuwa ma revolutionist wengi waliopita duniani hawakuwa na elimu ya kutisha bali walikuwa na dhamira njema juu yao.CDM hatuhitaji watu wenye dr za kupewa au za kuhongwa tunaitaji watu wenye elimu inayo weza tatua matatizo na changamoto zinazo likabili taifa.hatuitaji wasomi kama wakina dr balali,wakina chenge,kalamagi nawengine sample hiyo wanaopatikana ndani ya CCM bali tunahitaji watu safi na wenye nia njema na taifa lao bila kujali kiwango cha elimu walicho nacho.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…