CHADEMA, punguzeni mikutano ingieni mitaani!

CHADEMA, punguzeni mikutano ingieni mitaani!

mikutano iendelee

Sababu unayoona kuendelea na mikutano kutaongeza wanachama zaidi wa chadema wa papo kwa papo kuliko waliko wengi mitaani ambao wametulia na wengi wao hawana nafasi au kupendelea mambo ya kufuata kila ngoma ya mdundiko inakoelekea?
 
Mimi kwa maoni yangu ni kwamba mambo yote yaendelee, ila mikutano iwe ya viongozi wa ngazi za mahali husika(kanda, mkoa, wilaya kata na matawi). viongozi wa kitaifa wahutubie mikutano maalumu tu na si kila wakati/sehemu iwe wao tu!
 
Mpaka hapo walipofika CDM pamoja na upingamizi mkubwa wanaoupata toka kwa mpinzani wamejitahidi sana. Tuwape heshima na shukrani pale wanapostahili. Kuweza kuwakusanya watu wengi hivi sio mchezo. Ni lazima kuna kitu unachowapa ambacho hawawezi kukipata mahali pengine. Hilo tusilipuuzie. Mimi binafsi ninawashauri viongozi wa CDM wazidishe nguvu. Watanzania wameshagundua kwa kiasi kikubwa jinsi serikali inavyotunyanyasa kwa kutumia kodi tulizozitokea jasho sisi wenyewe. Nitatoa mfano. Shule haina mwalimu, chaki, ubao, madirisha, library, laboratory, bweni, wala chochote kinachomwezesha mwanafunzi afaulu masomo yake. Hapo hapo serikali haina haja ya kuyaangalia matumizi haya muhimu kwa shule kuweza kufaulisha. Watoto wamefeli kwa asilimia 65. Serikali ile ile inakumbuka kuwa watanzania wanalipa kodi na kodi hiyo itumike kuunda tume ya kuchunguza ni kwa nini wamefeli. Swali ni kuwa hiyo tume inayoundwa kuchunguza shule ambayo haina mwalimu wala kifaa cha kufundishia inachunguza nini? Hao watoto wangefaulu kwa mwuugiza? CCM imeshindwa kuiongoza Tanzania na watanzania tunajua ndiyo maana tunahudhuria kwa wingi kusikia Dr. Slaa atakapochukua kiti ataipeleka wapi nchi yetu hii. Tuelimishane sisi kwa sisi kwani ni kipofu tu nduye atakayeikumbatia tena CCM hiyo 2015.
 
Mikutano kama hii imekuwa ikifanyika kabla ya uzinduzi wa kanda zetu,kwa sasa tumeshafungua kanda zetu kwa hiyo viongozi wa kanda wataendesha mikutano na si viongozi wa kitaifa kama awali,your advice has been noted.
 
Nimeipenda sana comment yako, maana kinachoongelewa kikidharaurika matokeo ndio ya kulalamikia kuibiwa kura kumbe wenzako wanaofukua mitaani kama mnyama FUKO wamefanikiwa kuwakokotoa wapiga kura. Siasa za leo zinaendeshwa kisayansi.

Nadhani ungefahamu maudhui ya habari zaidi. Kundi kubwa hilo si wapiga. Nani aliye kazini ataacha kazi na kwenda mkutanoni kuanzia na wewe mwenyewe mdau utaacha kazi uende mkutanoni wakati unawajibika?

Chief mimi nakushauri tu wakati mwingine jitahidi kufanyia analysis za kisomi na kuwa na uhakika wa kile unachotamka na si kuongea ongea tu ili mradi nawe uonekani unachangia. Mara nyingi sana CDM wanapofanya mikutano huwa wanazingatia sana ushiriki wa watu katika makundi tofauti tofauti. Ndio maana mikutano mingi hufanyika siku ya jumamosi unadhani sababu huwa nini? ni kuwatarget hasa wafanyakazi kwa kuwa ni siku ya mapumziko kwa walio wengi. Alafu ni lazima uwe na heshima kidogo kwa watu hata kama hukufundishwa kwenu, watu wote wanaokuja kwenye mikutano si wahuni kama unavyodai wewe na pia elewa kwamba hata hao wahuni wana haki ya kupiga kura na ndio maana ni wengi wameweza kujiandikisha na ndio wamesaidia sana kuongeza kura za CDM na kupunguza za CCM kwa kuwa wanaona ndio tumaini lao kwa sasa. Pia inawezekana kabisa kazi za chama huzijui hata kidogo ndio sehemu unaangalia kipengele kidogo tu cha mikutano na kudhani ndio approach pekee ya chama kuwafikia wananchi. Nakushauri jaribu kutafuta taarifa zaidi hata kwenye mitandao tu ya chama kabla hujaweka porojo zako hapa jamvini.
 
Chief mimi nakushauri tu wakati mwingine jitahidi kufanyia analysis za kisomi na kuwa na uhakika wa kile unachotamka na si kuongea ongea tu ili mradi nawe uonekani unachangia. Mara nyingi sana CDM wanapofanya mikutano huwa wanazingatia sana ushiriki wa watu katika makundi tofauti tofauti. Ndio maana mikutano mingi hufanyika siku ya jumamosi unadhani sababu huwa nini? ni kuwatarget hasa wafanyakazi kwa kuwa ni siku ya mapumziko kwa walio wengi. Alafu ni lazima uwe na heshima kidogo kwa watu hata kama hukufundishwa kwenu, watu wote wanaokuja kwenye mikutano si wahuni kama unavyodai wewe na pia elewa kwamba hata hao wahuni wana haki ya kupiga kura na ndio maana ni wengi wameweza kujiandikisha na ndio wamesaidia sana kuongeza kura za CDM na kupunguza za CCM kwa kuwa wanaona ndio tumaini lao kwa sasa. Pia inawezekana kabisa kazi za chama huzijui hata kidogo ndio sehemu unaangalia kipengele kidogo tu cha mikutano na kudhani ndio approach pekee ya chama kuwafikia wananchi. Nakushauri jaribu kutafuta taarifa zaidi hata kwenye mitandao tu ya chama kabla hujaweka porojo zako hapa jamvini.

Sijasema wote wote ni wahuni, ungenielewa niliposema kati ya umati huenda watakaotumbukiza kura sandukuni huenda ni robo ingawa umati ni mkubwa. Hiyo ni hoja yangu ya kutosha kujenga utetezi kwamba walio wengi katika mikutano si wapiga kura kama unavyoona imezoeleka mtu akipiga mluzi tu utaona wote wanageukia huko na kabisa ikionekana kuna watu wanaongea au kufanya kitu wasichokifahamu utaona vijana wanaenda mbio kuelekea huko na kuongeza genge. Hiyo ndiyo hali halisi. Lakini mitaani na vitongojini ndiko wanakopatikana waliotulia na wenye malengo ya kweli ukiwapa msasa wa kutosha. Hatutaki halaiki isiyotumbukiza kura masandukuni, ila wawafuate wale ambao hata uhakiki kabla ya uchaguzi mkuu ni rahisi kukadiri kuliko dhana ya sasa kutumia kigezo cha watu kuitikia mkutano kwani hata miziki na matamasha watu hujaa hivyo hivyo na wengine ni kwenda kushangaashangaa tu.

Mikutano michache inatosha kwa ajili ya kuhamasisha lakini si kwamba mikutano inawahakikishia kupata wanachama wa kupiga kura au wafuasi wa kupiga kura.

Imezoeleka mikutano ni kisiasa zaidi kama mchezo wa kuigiza kwa kuendesha zoezi la kurudisha na kupata kura mpya. Kesho watapokea za CCM hadharani kisha keshokutwa watazitupa kwa Chadema na kupokea mpya, basi ni mzunguko huo kutwa kucha.
 
Kabla ya kuchangia chochote ninaomba majibu ya maswali hapo chini(Kama unafikiri mikutano ya CHADEMA haina Political Positive impacts kwa sasa)

1/Kwanini CCM tuko tayari kubeba watu hata na maroli, kuleta wasanii, Kutoa Posho na Ubwabwa ili kujaza mikutano?

2/Kwanini hao 'wazururaji' wajae kwenye mikutano ya CHADEMA zaidi na sio mikutano ya vyama vingine kama CCM nk?

3/Kwanini Serikali na vyombo vya dola wako tayari kuizuia mikutano ya CHADEMA kwa gharama yoyote isifanyike au isifanikiwe?

4/Kwanini Mwenyekiti wa CCM rais Kikwete anaigopa sana mikutano ya CHADEMA mpaka kufikia hatua ya kuamrisha makada wa CCM nao wajibu mapigo kwa kufanya mikutano kama CHADEMA?

5/Kwanini CHADEMA wako tayari kuhakikisha mkutano walioupanga lazima waufanye hata kama wamewekewa vikwazo na vitisho vya serikali na vyombo vya dola?

6/Kwanini CCM tuko tayari kuihujumu mikutano ya CHADEMA kwa gharama yoyote pale inapotakiwa kufanyika?

*Nitatoa maoni yangu na mapendekezo yangu positively, punde baada ya kupata majibu au ufafanuzi wa maswali yangu hapo juu.
Keep on watching!!!
 
Kabla ya kuchangia chochote ninaomba majibu ya maswali hapo chini(Kama unafikiri mikutano ya CHADEMA haina Political Positive impacts kwa sasa)

1/Kwanini CCM tuko tayari kubeba watu hata na maroli, kuleta wasanii, Kutoa Posho na Ubwabwa ili kujaza mikutano?

2/Kwanini hao 'wazururaji' wajae kwenye mikutano ya CHADEMA zaidi na sio mikutano ya vyama vingine kama CCM nk?

3/Kwanini Serikali na vyombo vya dola wako tayari kuizuia mikutano ya CHADEMA kwa gharama yoyote isifanyike au isifanikiwe?

4/Kwanini Mwenyekiti wa CCM rais Kikwete anaigopa sana mikutano ya CHADEMA mpaka kufikia hatua ya kuamrisha makada wa CCM nao wajibu mapigo kwa kufanya mikutano kama CHADEMA?

5/Kwanini CHADEMA wako tayari kuhakikisha mkutano walioupanga lazima waufanye hata kama wamewekewa vikwazo na vitisho vya serikali na vyombo vya dola?

6/Kwanini CCM tuko tayari kuihujumu mikutano ya CHADEMA kwa gharama yoyote pale inapotakiwa kufanyika?

*Nitatoa maoni yangu na mapendekezo yangu positively, punde baada ya kupata majibu au ufafanuzi wa maswali yangu hapo juu.
Keep on watching!!!

Ieleweke kwamba Siasa inaendeshwa kisayansi siku hizi. Ubunifu ni muhimu katika uendeshaji chama. Kuendelea kung'ang'ania mbinu na njia ile ile ni kuishiwa ubunifu.

Sijaona haja ya kuendelea kulumbana juu ya vibali vya maandamani na mikutano wakati mikutano ya ndani iko huru na haizuiliwi na inaweza kuleta manufaa zaidi na baadaye CCM kushtukia yamebaki mabua matupu kama alivyonena mdau mmoja.
 
Ieleweke kwamba Siasa inaendeshwa kisayansi siku hizi. Ubunifu ni muhimu katika uendeshaji chama. Kuendelea kung'ang'ania mbinu na njia ile ile ni kuishiwa ubunifu.

Sijaona haja ya kuendelea kulumbana juu ya vibali vya maandamani na mikutano wakati mikutano ya ndani iko huru na haizuiliwi na inaweza kuleta manufaa zaidi na baadaye CCM kushtukia yamebaki mabua matupu kama alivyonena mdau mmoja.
Nakuunga mkono mkuu
 
Back
Top Bottom