CHADEMA, punguzeni mikutano ingieni mitaani!

CHADEMA, punguzeni mikutano ingieni mitaani!

Nadhani unakasirika tu bure mkuu, watanzania hivi sasa ndivyo wanachukulia CHADEMA kuwa ni wahuni hasa ukizingatia kuwa hakuna hata siku moja wamefanya mkutano bila kuwepo na vurugu, maandamano tena ya kulazimisha na vitu kama hivyo, unafikiri watu watawaelewaje? Ni vibaka na wahuni.

Sasa wewe ndio unataka kutuaminisha uongo kuwa ukweli. Wanaokwenda mikutano si wahuni kama unavyotaka tuamini, ni watu waliojikomboa kifikra, ni kundi kubwa la watu ambao wamekuwa sensitized ndio maana wanatembea kwa miguu kuifuata mikutano hiyo bila kubebwa kwenye malori na bila kupewa posho ya sh. 5,000. Mbona umati huo hatuuoni kwenye mikutano mingine ya vyama vingine?

Pamoja na kuongeza strategy nyingine, mikutano inatoa nafasi watu kufahamu sera za chama na kupata elimu ya uraia. Mikutano kama hiyo hawatoki watupu, amini nakuambia wengi hubadilika na kama walikuwa hawapigi kura sasa wanaamua kupiga kura, kama walikuwa hawajajiandikisha sasa watajiandikisha n. k. Kujenga chama is a long process.
 
Kila siku hakuna wanachozungumza zaidi ya ufisadi kwanini watu wasiwachoke.Wabadilishe maneno kwenye mikutano yao basi

Hiyo ndio siasa wewe mchizi. Ajenda iliyopo ndio inayozungumziwa. Mwanasiasa mzuri kama mabomu yamelipuka na kuua watu hataacha kuzungumzia madhara ya mabomu aende kubembea nje ya nchi....come to your senses!
 
Sasa wewe ndio unataka kutuaminisha uongo kuwa ukweli. Wanaokwenda mikutano si wahuni kama unavyotaka tuamini, ni watu waliojikomboa kifikra, ni kundi kubwa la watu ambao wamekuwa sensitized ndio maana wanatembea kwa miguu kuifuata mikutano hiyo bila kubebwa kwenye malori na bila kupewa posho ya sh. 5,000. Mbona umati huo hatuuoni kwenye mikutano mingine ya vyama vingine?

Pamoja na kuongeza strategy nyingine, mikutano inatoa nafasi watu kufahamu sera za chama na kupata elimu ya uraia. Mikutano kama hiyo hawatoki watupu, amini nakuambia wengi hubadilika na kama walikuwa hawapigi kura sasa wanaamua kupiga kura, kama walikuwa hawajajiandikisha sasa watajiandikisha n. k. Kujenga chama is a long process.

sasa tuelewe kipi? Mleta mada anasema wanaoenda mikutanoni ni wahuni, wewe unakanusha na kusema ni watu waliokomboka kifikra. Jipangeni magwanda.
 
Unajijachanganya sana mkuu unaposema watu wanaokuja mikutanoni ni watu wasio na kazi na wasio na makazi. Kama unahisi kuwa idadi kubwa ya wapiga kura ni watu wenye kazi na makazi basi utakuwa unajidanganya sana. Kwa taarifa yako ni asilimia mbili ya hao watumishi wako unaowathamini na kuwalenga ndiyo huwa wanaojitokezaga kupiga kura siku ya uchaguzi.
Sababu za Chadema kutoshinda chaguzi kama inavyotarajiwa inaenda zaidi ya kutopata idadi ya kura za kutosha. Pamoja na kutosimamisha wagombea wanaokubalika, kuna tatizo la nchi kiujumla la watu kutojitokeza siku ya uchaguzi. Hili sidhani kama lipo ndani ya uwezo wa Chadema kusuluhisha, kwasababu linahitaji elimu zaidi itolewe kwa watu kuelewa umuhimu wa kupiga kura kwenye maisha yao.
Chadema wanaweza kugonga hodi kila nyumba, lakini kama watu hawajaona uhusiano kati ya kupiga kura na mabadiliko yao hakuna kitakachotokea.

Radhia baby wasikuzingue hao na hoja zao zisizo na mashiko. Kama uchaguzi ungekuwa unafanyika freely and fairly wasingezungumza hayo wanayoyazungumza. Kwani 2010 ilikuwaje? nguvu kubwa ilitumika kuiba kura na kushirikiana na TISS kubadilisha matokeo nani asiyejua hilo? kwanini hawaachi watz wenyewe wakaamua wanayemtaka? ipo siku demokrasia ya kweli itasimama.
 
sasa tuelewe kipi? Mleta mada anasema wanaoenda mikutanoni ni wahuni, wewe unakanusha na kusema ni watu waliokomboka kifikra. Jipangeni magwanda.

Cool down baby, hujanielewa. Mimi sikubaliani na mtoa hoja kuwa wanaoenda kwenye mikutano ni wahuni. Si kweli, kwani wanaoenda mikutanoni hawatoki majumbani? wanaosombwa kwenye malori na CCM wanatoka mbinguni? kama wanaojaza mikutano ya CDM ni wahuni, kwanini wanaojaza mikutano ya CCM nao wasiwe wahuni? nawaita ni watu waliojikomboa kifikra kwasababu wameamshwa usingizini na wameanza kujitambua.
 
Nafikiri hujamuelewa mtoa mada.......suala ambalo analizungumzia ni kuhusu strategy ambayo CDM wanaweza kuitumia....i.e. tumeshuhudia umati mikubwa kwenye mikutano mbali mbali ya CDM....lakini hiyo haikutosha ku-turn out into votes za ukweli in favor of CDM!!.....bado unataka kuamini wahudhuriaji wa mikutano ile ni for REAL!!......you must be joking......mwishowe ndio maana CDM wanaishia kulalama wameibiwa kura......

wenzenu Magamba mkiwaona wanapeleka "viduku" kwa wananchi mjue kuwa ile ni marashi tu....nguo za kuvaa (kura) zilishajulikana...............
Mkuu, we kweli hukumaliza fomu 4 mwaka Jana Kama hao wanaokurukupuka kuchangia bila kujua mtuma thread amelenga nini. Ndio maana nasema Siku zote Hawa watu hawawezi kuongoza nchi hii kwani hawana tofauti na magamba. Hawapendi kukosolewa hata kukiwa kwa nia njema ya kuboresha gwanda Lao.
 
huna adabu kamshauli unaweza hata kumshauli mamayako aachane na babayako
 
Mikutano iendelee, na sasa zaidi maeneo ya vijijini. Umati kwenye mikutano haishawishi tu wahudhuriaji au wasikilizaji, bali kwa kiasi kikubwa unawaaminisha watu kwamba chama kiko hai. Hata mtu ambaye hajahudhuria, akiona umatu ule basi anashawishika kuwa chama kile kipo hai...
Wakati mikutano ikipamba moto, mikutano ya ndani nayo iimarishwe ili kusuka network imara kwa ajili ya kulinda kura wakati wa uchaguzi.
Jambo moja ni kwamba CDM imeanza kupata mwitikio mkubwa baada ya uchaguzi wa 2010. Na tangu wakati huo hakujawa na fursa ya watu kujiandikisha. Wengi wa wanaosapoti cdm ni watu wasioiunga mkono CCM na hawa, hawakujiandikisha kwa kuwa walidhani kwamba hakujawa na upinzani wa kutosha. Lakini sasa watu wengi wanaona nguvu ya upinzani na watajiandikisha na kupiga kura katika uchaguzi ujao

Well said Tuko
 
Umenena kweli, maana tunachopigania ni mabadiliko yenye kuleta maendeleo kwa nchi yetu tofauti na mitazamo ya baadhi yetu kuawa na mapenzi kwa chama fulani. Tunachohitaji vikuu viwili nchini kuwa na nguvu na hivyo pale inapotokea kubadilishana uongozi wa nchi kwa kutumia sanduku la kura kuchochee maendeleo na mafanikio kwa watanzania kiushindani maana ukiteleza dola inachukukuliwa.

Tataizo ninaloliona ni kama ulivyoainisha kwamba mfumo wa Chadema kujitembeza wanaona kama ndio kuvutia wapiga kura kumbe wengi wa wahudhuriaji na wale wanaoshangaashangaa kila kitokeacho mitaani kama mmoja akipiga mluzi au filimbi utaona wote wanageukia upande ule na kufuata kuna kuna nini. Nadhani watu wa aina hiyo ni wengi na ndio Chadema inadanganywa kwamba inawavutia sera zao na ndio wapiga kura wao.

Pamoja na ushari wa wao kujitembeza kwa njia zo zote, tatizo wao wanaona njia bora na mbadala ni mikutano kitu ambacho kimeashachosha wengi, wanahitaji kuwa wabunifu, licha ya kupewa ushauri nasaha wanaonekana kutoshaurika na kuona wanachokiona kutoka ofisini kwao ndio bora. Wawasikilize wananchi ndicho kinachotakiwa si wananchi kuwasikiliza wao.
Sina cha kuongeza kwa sababu umegonga utosini mwangu. Labda tu niseme, Kuna baadhi ya viongozi ndani ya CHADEMA ambao ukiwangalia usoni utagundua wako tayari kusikiliza mawazo ya wananchi na kuyafanyia kazi, pia kuna wengine ambao dhana ya uongozi wanaitumia vibaya kwa kudhani wao wako pale kuwaongoza tu wananchi. Alfa na Omega. Kama ilivyotokea kwa CCM, ikiachiwa hali kuwa hivi, hiki ni kichocheo cha migawanyiko na chama kukosa dira. Yetu ni macho na masikio.
 
sasa tuelewe kipi? Mleta mada anasema wanaoenda mikutanoni ni wahuni, wewe unakanusha na kusema ni watu waliokomboka kifikra. Jipangeni magwanda.

Kifalsafa kuwa watu wa tabaka tatu:
  1. Ambao hupenda kuongelea mambo ya watu katika maisha yao ya kila siku.
  2. Ambao wanapenda matukio wapi na wapi, kule na pale nini kimetokea katika maisha yao ya kila siku.
  3. Ambao huhangaikia namna ya kuinua hali ya maisha yao wayaendeshi vipi ili wawe na maisha bora katika maisha yao ya kila siku.
Radhia Sweety kati ya makundi haya watatu, ni kundi lipi kundi lipi linaongoza kujaza zaidi mikutano, lipi linafuatia na lipi la mwisho kwa idadi ya wahudhuriaji mikutano na maandamano hayo?

 
siasa za kuwatembelea watu majumbani ni ngumu kwa sababu lazima uwe na hoja ya kuwaambia watu na vilevile ujiandae kuwa na majibu ya maswali watakayouliza. Chadema hawawezi kujibu hoja face to face ndio maana wanapendelea kupanda jukwaani kusema maneno wanayotaka halafu wanatawanyika.

hivi wewe ni binti na kama ubinti umeshaolewa na kama bado nikijitokeza ni vibaya na kama sio vibaya natangaza ndoa.
 
Acha dharau. waingie mitaani kwani wamekua wamisri?
chadema+10.jpg



Mikutano
ya hadhara imezoeleka kuvuta watu wengi. Mvuto huo wa watu wengi
sijausahau tangu uchaguzi mkuu uliopita, lakini wahudhuriaji hawa walio
wengi si wapiga kura, bali ni wazururaji, wasio na makazi maalum na
wasio na kazi zinazowashinikiza kutohudhuria mikutano hiyo.
Pengine wapiga kura katika umati kama huo hapo
juu ni robo ya huo umati.

Chadema waige tabia ya mnyama mdogo sana
anayeitwa
FUKO ambaye
anafurukuta na kufukua chini ya ardhi na kumaliza mihogo na viazi,
mwenye shamba akija ni kuchomoa makuti ambayo matupu wakati viazi na
mihogo imeliwa. Ndiyo tabia wanayotakiwa kuifanya sasa hivi
Chadema.


Chadema baada ya kuelekeza nguvu za kanda, ni mbinu nzuri ambayo itaweka
mwenya wa kupenya hadi ndani viijini, na mijini kupenya mitaani. Kuunda
makada wa kuzunguka nyumba kwa nyumba kusaka na kuwashawishi wapiga
kura.

Wapiga kura wazuri ni watu wenye makazi yao mitaani, na kuwapata wakazi
ni huko mitaani wanakoishi, na kampeni za uchaguzi zinapofanyika ni huko
mitaani unakuwa na hakina nani anapiga kura na anamwelekeo wa kukipigia
chama au la. Kutegemea huu umati wa mikusanyiko mikubwa ni kwa nafasi
chache sana na mara chache kwani tumejifunza walio wengi katika umati
ule ni vibaka, wazururaji, wasio na makazi maalum nk.

Mpiga kura anakuwa na makazi maalum ndio maana
kitambulisho chake kabla ya kupata lazima serikali za mitaa zitambue na
kuridhia uwepo na ukazi wake.


Wapiga kura wazuri
ni wale wenye makazi na wanapatikana mitaani kwenye makazi yao, sio
wazururaji na wababaishaji mitaani.
Kuwa makini na makundi makubwa ambayo hayapigi kura lakini wahudhuriaji
wazuri wa mikutano.

:nono::nono::nono::nono::nono::nono::nono:​
 
hivi wewe ni binti na kama ubinti umeshaolewa na kama bado nikijitokeza ni vibaya na kama sio vibaya natangaza ndoa.

Kwani wamisri ni uzuzu uliowapeleka mitaani au mazingira ya utawala yaliwatikisa hadi kuamua kuzamia mitaa ya Farao?
 
Siasa za kuwatembelea watu majumbani ni ngumu kwa sababu lazima uwe na hoja ya kuwaambia watu na vilevile ujiandae kuwa na majibu ya maswali watakayouliza. Chadema hawawezi kujibu hoja face to face ndio maana wanapendelea kupanda jukwaani kusema maneno wanayotaka halafu wanatawanyika.
Ar U sereous about whar U'r collectin here or ur koromarin from dat day call 'usngiz wa mang'amng'am???'Yaani kweli kweli kweli ni kweli kwa akili yako na kuchanganya na ya kuambiwa na kuona ukiwa na akili timamu bila ya kilevi cha madafu ya kibongo au chimpum,bila soni KATI YA CCM NA CHADEMA (ITA HATA CHANDIMU) NI CHAMA KIPI KINATOKA NDUKI KINAPOONA KUNA HOJA ZA USO KWA USO KWA KUOGOPA ZA USO KINATOA CHOGO??????????KweeeeeeeeeeeeeeeeeeeliWajameni nisaidine,ar we s'rous na maisha yetu hasa ya next gen??????Oooooooh pls DON'T PULL DA NATION DOWN SUCKER.
 
Ar U sereous about whar U'r collectin here or ur koromarin from dat day call 'usngiz wa mang'amng'am???'Yaani kweli kweli kweli ni kweli kwa akili yako na kuchanganya na ya kuambiwa na kuona ukiwa na akili timamu bila ya kilevi cha madafu ya kibongo au chimpum,bila soni KATI YA CCM NA CHADEMA (ITA HATA CHANDIMU) NI CHAMA KIPI KINATOKA NDUKI KINAPOONA KUNA HOJA ZA USO KWA USO KWA KUOGOPA ZA USO KINATOA CHOGO??????????KweeeeeeeeeeeeeeeeeeeliWajameni nisaidine,ar we s'rous na maisha yetu hasa ya next gen??????Oooooooh pls DON'T PULL DA NATION DOWN SUCKER.

Tofautu ya kuhonga wananchi kwa kanga, T-shirt, Caps na usafiri wa dezo wa kujaza kwenye malori kwenda kuwamwaga kwenye mikutano kisha kuwagawia pesa ndipo wapate wahudhuriaji, tofauti na yule ambaye wanamfuata kwa ridhaa.
 
Nakuunga mkono japo sijafurahia maneno yako ya kejeli uliyotumia kwa wanaohudhuria mikutano ya cdm kuwa ni wazururaji.
 
Tofautu ya kuhonga wananchi kwa kanga, T-shirt, Caps na usafiri wa dezo wa kujaza kwenye malori kwenda kuwamwaga kwenye mikutano kisha kuwagawia pesa ndipo wapate wahudhuriaji, tofauti na yule ambaye wanamfuata kwa ridhaa.
Akhsante ndugu,kwani kuna watu wanachangia humu utadhani hawaoni au hatuishi pamoja au hawana vizazi na kama wanavyo hawajali wala kufikiri wataviacha vipi.
 
Back
Top Bottom