CHADEMA, punguzeni mikutano ingieni mitaani!

CHADEMA, punguzeni mikutano ingieni mitaani!

Mikutano iendelee, na sasa zaidi maeneo ya vijijini. Umati kwenye mikutano haishawishi tu wahudhuriaji au wasikilizaji, bali kwa kiasi kikubwa unawaaminisha watu kwamba chama kiko hai. Hata mtu ambaye hajahudhuria, akiona umatu ule basi anashawishika kuwa chama kile kipo hai...
Wakati mikutano ikipamba moto, mikutano ya ndani nayo iimarishwe ili kusuka network imara kwa ajili ya kulinda kura wakati wa uchaguzi.
Jambo moja ni kwamba CDM imeanza kupata mwitikio mkubwa baada ya uchaguzi wa 2010. Na tangu wakati huo hakujawa na fursa ya watu kujiandikisha. Wengi wa wanaosapoti cdm ni watu wasioiunga mkono CCM na hawa, hawakujiandikisha kwa kuwa walidhani kwamba hakujawa na upinzani wa kutosha. Lakini sasa watu wengi wanaona nguvu ya upinzani na watajiandikisha na kupiga kura katika uchaguzi ujao

Pamoja na maoni yako mazuri, kuna jambo ambalo naliangalisha sana katima mienendo ya siasa, mambo ya kufikirika zaidi yakwepwe inavyowezekana. Kwamba kuona umati ndio dalili njema za kuvutia watu ni jambo ambalo pengine linaweza kusababisha majuto wakati wa kupiga kura.

Pendekezo lako la mikutano ya ndani ndilo naliona lina uzito mkubwa sana na ndi siri ya mafanikio ya CCM. Kwenye mikutano ya hadhara kila mtu atanyosha mikono kuashiria kuunga mkoni lakisi sio watanyosha mikono kutumbukiza kura sandukuni.

Sina maana ya kupinga mikutano, lakini iwe ya mara chachaze zaidi ya mikutano ya ndani. Huko vitongojini wanakojifungia CCM ingieni nanyi mjifungie na wanavitongoji siri ya kura ndio huko. Jukwaani ni kutangaza seria kisha nendeni kuwafuata mlio wanadisha kura mitaani.
 
Candid Scope bandiko lako ni zuri kwa wenye fikra pevu ambao wana embrace positive and negative political challenges but I'm afraid, jiandae kupokea madongo kutoka CHADEMA chauvinist kwa kuwachoma kwa maneno yenye hekima.
 
Last edited by a moderator:
Analysis ya kipuuzi sijawahi kuona tangu nizaliwe. Eti unawaita wanaohudhuria mikutano ya Chadema kuwa ni vibaka, wazururaji na watu wasio na makazi maalum?! Ulifanya utafiti gani kulibaini hilo? Hata kama ushauri wako ni mzuri kiasi gani, umeshauharibu kwa kauli zako za kashfa. Ulipaswa utambue umuhimu wa hayo makundi yanayojaza mikutano ya Chadema kisha utoe huo ushauri wako.

At least today you are positive kudos!!
 
Candid Scope bandiko lako ni zuri kwa wenye fikra pevu ambao wana embrace positive and negative political challenges but I'm afraid, jiandae kupokea madongo kutoka CHADEMA chauvinist kwa kuwachoma kwa maneno yenye hekima.

KATUNI(741).jpg
Vinginevyo watatuchoshwa kwa malalamiko kuibiwa kura, mara kanuni kukiukwa na longolgongo nyingi. Vyama vya upinzani vinaingia kwenye kinyang'anyiro cha kushiriki uchaguzi mkuu huku hawana hakina nani ataenda kuwapigia kura, wakati wenza CCM wameshajihakikishia wapiga kura wao huko mitaaani kutokana na mikutano ya ndani. Pengine ndivyo Odinga wa Kenya alivyoangukia pua, hata kwenda mahakamani nafasi ya kubadili matokeo ni finyu mno.
 
Kama wameweza kuuza sera kwa wananchi na mafanikio yameanza wananchi kuamka usingizini na kudai haki zao, unafikiri itashindikana hilo? Au mbinu zinazotumiwa na CCM kuwapata wapiga kura unaona zitakuwa zimetifuliwa?

Hii dhana ya kusema wananchi walikuwa wamelala unaitoa wapi?. Hoja kama hizi zinabeba ujumbe wa dharau kwa jamii. Unataka kutuaminisha kuwa nchi iliingia kwenye mfumo wa vyama vingi kwa sababu wananchi waliamuka?. Una maana pia wananchi kuwa na political choices na kuamua kutokuchagua opposition party or candidate nako ni dalili ya wananchi kulala.

Hivi kwa mtazamo wako, mwananchi aliyeamuka ni yupi na tabia zake zikoje?. Mbona unawalazimisha wananchi kufanya jambo la kisiasa unalolitaka na kwa kutokufanya hivyo, unawabandika mihuri na kusema bado wamelala?.
 
Ulilolijadili ndiloninaloliongelea. CCM ushindi wao ni kutokana na kuhakiki na kuhakikisha wapiga kura wao kuanzia shina, matawi na vitongoji, wakati Chadema wanategemea mkusanyiko wa mikuano ambao hauhakikishi nani kati ya wahudhuriani ni mpiga kura. Hilo ndilo linalotakiwa kufanyiwa kazi, na upatikanaji wa wapiga kura hali kadhalika kuhakiki wanachama hai ambao watakipigia chama kura ni huko kwenye vitongoji wanakoishi. Hii ndiyo siri ya ushindi wa CCM ambao chadema wanatakiwa kuipiku CCM kwani dawa ya moto ni moto ati.

Unaweza kuwahakiki wapiga kura wako na bado wasikuchague siku ya uchaguzi. After all, wengi wanaojitokezaga kupiga kura huwa siyo ''affiliated members'' wa chama fulani. Hao CCM wenyewe ukiwauliza wana idadi gani ya wanachama staunch watakuambia hawatimii hata asilimia 5 ya watu wenye haki ya kupiga kura. Tanzania bado hatuna idadi ya watu ambao wako loyal kwa vyama vyao kama ambavyo ilivyo Marekani na Democrats na Repubics zao. Ili kushinda uchaguzi Tanzania unahitaji kutumia mbinu za zima moto kama kumuweka mgombeaji mwenye mvuto au umaarufu fulani na kuahidi ahadi ambazo ziko relevant kwa wakati huo. Ushauri wako kuwa Chadema waende kwa wananchi nyumba hadi nyumba ili kupata kura zaidi HAUTEKELEZEKI na HAUENDANI na mazingira ya Tanzania.
 
Hii dhana ya kusema wananchi walikuwa wamelala unaitoa wapi?. Hoja kama hizi zinabeba ujumbe wa dharau kwa jamii. Unataka kutuaminisha kuwa nchi iliingia kwenye mfumo wa vyama vingi kwa sababu wananchi waliamuka?. Una maana pia wananchi kuwa na political choices na kuamua kutokuchagua opposition party or candidate nako ni dalili ya wananchi kulala.

Hivi kwa mtazamo wako, mwananchi aliyeamuka ni yupi na tabia zake zikoje?. Mbona unawalazimisha wananchi kufanya jambo la kisiasa unalolitaka na kwa kutokufanya hivyo, unawabandika mihuri na kusema bado wamelala?.

Nimejaribu kusoma comment hii haijibu quote yange, hivonimeshindwa kuijibu maana kuna ukinzano.
 
Unaweza kuwahakiki wapiga kura wako na bado wasikuchague siku ya uchaguzi. After all, wengi wanaojitokezaga kupiga kura huwa siyo ''affiliated members'' wa chama fulani. Hao CCM wenyewe ukiwauliza wana idadi gani ya wanachama staunch watakuambia hawatimii hata asilimia 5 ya watu wenye haki ya kupiga kura. Tanzania bado hatuna idadi ya watu ambao wako loyal kwa vyama vyao kama ambavyo ilivyo Marekani na Democrats na Repubics zao. Ili kushinda uchaguzi Tanzania unahitaji kutumia mbinu za zima moto kama kumuweka mgombeaji mwenye mvuto au umaarufu fulani na kuahidi ahadi ambazo ziko relevant kwa wakati huo. Ushauri wako kuwa Chadema waende kwa wananchi nyumba hadi nyumba ili kupata kura zaidi HAUTEKELEZEKI na HAUENDANI na mazingira ya Tanzania.

Ukweli unabaki, ujazaji wa mikutano ya Chadema na sera nzuri si suluhisho la kupata kura nyingi kwa maana ya kuangalia jambo kwa jumla jumla tu lakini si kwa undani. Wanaofika kwenye mikutano hiyo ya Chadema ni watu gani?
 
acha usisimizi wewe. Unajifanya unanijua sana siyo? Behewa la treni nini wewe.

akili ya mpumavu ni matusi!wala ukiniita sisimizi sitageuka sisimizi au siwezi kuwa treni mimi ni binadamu tuu,.offcourse sihitaji kukujua ila naifahamu sana michango yako hapa jukwaani ambayo mingi ni negative and illusions,.so nilishangaa kuona upo positive na thread hasa inayohusu chadema ndio maana nikakupa kudos,..wewe unajibu kwa matusi na kebehi ndio maana nikasema akili ya mjinga ni matusi!
 
Candid Scope , CHADEMA na mikutano ya hadhara huwezi kuwatenganisha, na pale wananchi wanapopungua/ mahudhurio kutokutarajiwa kwenye hiyo mikutano viongozi waandamizi wameanza kuwalalamikia wananchi. Imefikia kiwango cha watu kuwa mazuzu na umati wa watu kama ndiyo kipimo pekee cha kukubalika. Huwezi kuleta habari ya mkutano bila kuombwa picha ili waone linganisho.

Mikutano ya hadhara lazima iendelee kufanyika lakini pia msisitizo iwekwe kwenye door to door canvass. Hili ni zoezi gumu kwa sasa kwa vile chama hakijawa na safu ya viongozi wazuri na mahili wa kutosha nchini.

Kwa mtu mwenye fikra pevu anatambua kuwa, CCM hawahitaji kujipima kujua kama wanapendwa kwa kuangalia umati unaokuja kwenye mikutano yao kuwasikiliza kwa sababu hakuna kitu ambacho Serikali ya CCM inakifanya (ilani ya uchaguzi na sera) ambacho majority ya wananchi hawakifahamu/hakiwagusi na hii inatokana na CCM kuwa chama tawala toka uhuru. Ilani ya Uchaguzi na sera za CCM zinaonekana kwa kile serikali inakifanya na pia hazionekani kwa yale ambayo serikali haijafanya.

CCM inachofanya kwa sasa ni kujiuza na CHADEMA inabidi wajitembeze sana kwa wananchi kwa njia zote mwanana.
 
Mikutano na maandamano ndani ya CHADEMA ni zaidi ya siasa mkuu kama haujui, kuna siri nzito imejificha huko, suala la kupata kura na watu wachache kujitafutia umaarufu ni vitu viwili tofauti. Mikutano ile inayoambatana na maandamano ni mahsusi kwa ajili watu wachache kujipatia umaarufu ha haizalishi watachaguliwa au la ilimradi umaarufu huo unawawezesha wao kula. Usitemegee waache.

Msaghane unachoongea haukielewi nyie ni wivu unawasumbua umaarufu gani wanatafuta wakati tayari washakuwa maarufu wewe hana kitu hauwezi kusema kwamba hiyo mikutano ndiyo inawafanya wale kwa utajiri hauwawezi ni tofauti na wewe mpaka uandike majungu ndio upewe posho sasa nani zaidi
 
Go to the grassroots! Chama chochote kinachidhamiria kupata ushindi katika uchaguzi mkuu ni lazima kijenge ngome katika kiwango cha kijiji. Mjini ni sawa, lakini Chadema kimekuwa mjini sana kuliko kijijini. Sasa nguvu ielekezwe kule kwenye msingi au shina.
 
Pamoja na maoni yako mazuri, kuna jambo ambalo naliangalisha sana katima mienendo ya siasa, mambo ya kufikirika zaidi yakwepwe inavyowezekana. Kwamba kuona umati ndio dalili njema za kuvutia watu ni jambo ambalo pengine linaweza kusababisha majuto wakati wa kupiga kura.

Pendekezo lako la mikutano ya ndani ndilo naliona lina uzito mkubwa sana na ndi siri ya mafanikio ya CCM. Kwenye mikutano ya hadhara kila mtu atanyosha mikono kuashiria kuunga mkoni lakisi sio watanyosha mikono kutumbukiza kura sandukuni.

Sina maana ya kupinga mikutano, lakini iwe ya mara chachaze zaidi ya mikutano ya ndani. Huko vitongojini wanakojifungia CCM ingieni nanyi mjifungie na wanavitongoji siri ya kura ndio huko. Jukwaani ni kutangaza seria kisha nendeni kuwafuata mlio wanadisha kura mitaani.

Unless kuwe na jambo fulani linalotakiwa kuvumishwa hadharani, lakini binafsi nadhani maeneo kama Arusha, Kilimanjaro, Daressalaam, Mbeya, Mwanza, Shinyanga, Mara, Simiyu, Iringa na maeneo mengine ambapo CDM ina mizizi kwa sasa haihitaji sana mikutano ya hadhara ya mara kwa mara.
Maeneo kama haya CDM inaweza kupata viongozi hata katika ngazi za nyumba 10. Then kinachotakiwa sasa ni kuhakikisha nafasi zote zinazohitaji kiongozi kwa mujibu wa katiba ya chama, katika mikoa hii zinajazwa, na viongozi hawa wanakutana mara kwa mara wenyewe lakini pia na viongozi wa juu kupanga miakakati ya kushawishi wapiga kura na kudhibiti wizi wa kura.
Kwa ile mikoa ambayo bado chama hakijajisimika sawasawa, then mikutano ya hadhara iambatane na kujengwa na kuzibwa kwa nafasi zote za uongozi za chama kuanzia nyumba kumi.

Mathalani, Tanzania ina kaya takribani milioni 9 (kwa kutumia sensa ya mwaka jana na ku-assume kwa wastani kila kaya ina watu 5). Ukigawanya milioni 9 kwa 10, utapata laki 9. Kwa maana hiyo CDM inatakiwa iwe na wawakilishi laki 9 wa nyumba kumi. Halafu kila kwenye nyumba kumi kuwe wajumbe wengine wawili watakaowakilisha chama katika kamati ya siasa ya kitongoji. Kwa maana hiyo, jumla ya wajume wa kamati ya siasa ya kitongoji ni 1,800,000 nchi nzima. Then kutoka hawa, kuna viongozi wa vijiji, kata, tarafa, wilaya, mkoa, kanda na taifa. Kwa makadirio ya chini CDM itakuwa na viongozi milioni 2 nchi nzima. Hapa nimeongelea tu uongozi wa General, sijagusia BAWACHA wala BAVICHA...
Kila wilaya itakuwa na viongozi na viongozi wasiopungua elfu 5. Kwa hiyo siku Slaa akisema anasema kufanya mkutano wa ndani na viongozi wa wilaya fulani, members ni watu 5000, na kama wakihudhuria 10%, ni watu 500. Kwa hali kama hii hatutarajii kituo chochote cha kupiga kura kikose wakala mmoja na 'walinzi' 10 katika uchaguzi wa 2015.

Haya niliyoyastipulate hapa ni magumu kuyatekeleza, but hata yakitekelezwa kwa ufanisi wa 50%, yet uchaguzi ujao CCM hatoki...
 
Ukweli unabaki, ujazaji wa mikutano ya Chadema na sera nzuri si suluhisho la kupata kura nyingi kwa maana ya kuangalia jambo kwa jumla jumla tu lakini si kwa undani. Wanaofika kwenye mikutano hiyo ya Chadema ni watu gani?

Ujazaji wa watu kwenye mikutano kutokuwa suluhisho la ukosekanaji wa kura za kutosha haihalalishi case yako kuwa kwenda nyumba hadi nyumba ndiyo suluhisho. Kuna sababu zaidi ya moja zinazofanya CCM ipate kura nyingi kuliko Chadema ikiwamo kuweka wagombea wenye mvuto. Narudia, unaweza kutembea nyumba hadi nyumba lakini wapiga kura wasikichague chama chako mwisho wa siku kwasababu tu hujaweka mgombea anayekubalika.
 
Siasa za kuwatembelea watu majumbani ni ngumu kwa sababu lazima uwe na hoja ya kuwaambia watu na vilevile ujiandae kuwa na majibu ya maswali
watakayouliza. Chadema hawawezi kujibu hoja face to face ndio maana wanapendelea kupanda jukwaani kusema maneno wanayotaka halafu wanatawanyika.



Tofauti ya hoja kati ya chadema na ccm tunaiona bungeni na wewe shaidi acha unafiki,
 
Candid Scope wakati hoja ni mujarabu bado nadhani dhana yako ya kwamba wenye makazi na kazi zao ndio wenye kuipa ushindi CDM.
Kwa mtazamo wangu nadhani hao wenye kazi zao (wewe na mimi inclusive) ndio hasa tunaikwamisha hii nchi kwenda mbele kwa sababu tuna tunachopigania kisipotee.

tanzania inazalisha nguvu kazi 700,000 (NBS) kila mwaka na inakadiriwa wastani wa ajira 100,000 huzalishwa. Sasa kama CDM wakiweza kuwabadili hawa unaoita wazururaji na waso na makazi kuwa wapiga kura it makes more sense maana ni wahitaji wakuu kuliko mimi na wewe. Ninajua watu katika jamii yangu wenye kadi za kupiga kura lakini hawajapata kupiga kura...wenye kazi zao hao.

Notoe mfano: Miaka ya 80 na 90 ilikuwa ukihudhuria mkuano wa mahubiri ya mzee Kulola, kabla ya mkutano kuisha new converts walikuwa wanaitwa kando ili watambuliwe wanakotokea na kuelekezwa kwa viongozi watakao wa-monitor. Na ndivyo ilivyo kwa dini ya kiislam pia new converts wanafuatiliwa maendeleo yao. Maana kuamini ni jambo moja lakini kuendelea kuwa muumini ni jambo jingine kabisa.

Kwa msingi huo mimi si muumin wa headlines za CDM yavuna wanachama wapya 5,000.....swali langu huwa wana/wataenda wapi wakishavunwa??.

Hao wasiokuwa na kazi na wazururaji ni wazuri kuliko mimi na wewe ambao we have something to protect na kwa namna moja ni washirika wa mfumo uliopo sasa. CDM waanze na hawa kwanza after all sisi wenye kazi na makazi huwa hatushindi majumbani watatupata lini kiongozi????
Kuwashika wapiga kura hawa lazima CDM wawe na uongozi mashinani.....

Wenye kazi na makazi tumeshafikiwa kwa njia zote magazeti, redio, tv na hata kwa njia ya keyboard lakini mioyo yetu bado migumu.
 
Last edited by a moderator:
KATUNI(741).jpg
Vinginevyo watatuchoshwa kwa malalamiko kuibiwa kura, mara kanuni kukiukwa na longolgongo nyingi. Vyama vya upinzani vinaingia kwenye kinyang'anyiro cha kushiriki uchaguzi mkuu huku hawana hakina nani ataenda kuwapigia kura, wakati wenza CCM wameshajihakikishia wapiga kura wao huko mitaaani kutokana na mikutano ya ndani. Pengine ndivyo Odinga wa Kenya alivyoangukia pua, hata kwenda mahakamani nafasi ya kubadili matokeo ni finyu mno.

Acha kuongelaea uchaguzi wa Kenya unaijua katiba yao wewe? Mbona Watanzania tumekuwa wasemaji sana wa mambo ya watu wakati yetu yanatushinda? Siasa za kwenye vijiwe na kahawa usilete humu,haya umekuwa hakimu kwamba haitawezekana kupata haki yake mahakamani angejua hawezi kupata asingeenda,nikwambie acheni kuongea ya watu wakati kwako kubovu na nu umbea tu unawasumbua,wewe huyo msemaji wewe huyo hakimu unahukumu Siasa za kenya si zza kinafiki kama za huku na pia katiba yao huijui acheni kutoa povu kwa msichokielewa
 
Candid Scope , CHADEMA na mikutano ya hadhara huwezi kuwatenganisha, na pale wananchi wanapopungua/ mahudhurio kutokutarajiwa kwenye hiyo mikutano viongozi waandamizi wameanza kuwalalamikia wananchi. Imefikia kiwango cha watu kuwa mazuzu na umati wa watu kama ndiyo kipimo pekee cha kukubalika. Huwezi kuleta habari ya mkutano bila kuombwa picha ili waone linganisho.

Mikutano ya hadhara lazima iendelee kufanyika lakini pia msisitizo iwekwe kwenye door to door canvass. Hili ni zoezi gumu kwa sasa kwa vile chama hakijawa na safu ya viongozi wazuri na mahili wa kutosha nchini.

Kwa mtu mwenye fikra pevu anatambua kuwa, CCM hawahitaji kujipima kujua kama wanapendwa kwa kuangalia umati unaokuja kwenye mikutano yao kuwasikiliza kwa sababu hakuna kitu ambacho Serikali ya CCM inakifanya (ilani ya uchaguzi na sera) ambacho majority ya wananchi hawakifahamu/hakiwagusi na hii inatokana na CCM kuwa chama tawala toka uhuru. Ilani ya Uchaguzi na sera za CCM zinaonekana kwa kile serikali inakifanya na pia hazionekani kwa yale ambayo serikali haijafanya.

CCM inachofanya kwa sasa ni kujiuza na CHADEMA inabidi wajitembeze sana kwa wananchi kwa njia zote mwanana.

Umenena kweli, maana tunachopigania ni mabadiliko yenye kuleta maendeleo kwa nchi yetu tofauti na mitazamo ya baadhi yetu kuawa na mapenzi kwa chama fulani. Tunachohitaji vikuu viwili nchini kuwa na nguvu na hivyo pale inapotokea kubadilishana uongozi wa nchi kwa kutumia sanduku la kura kuchochee maendeleo na mafanikio kwa watanzania kiushindani maana ukiteleza dola inachukukuliwa.

Tataizo ninaloliona ni kama ulivyoainisha kwamba mfumo wa Chadema kujitembeza wanaona kama ndio kuvutia wapiga kura kumbe wengi wa wahudhuriaji na wale wanaoshangaashangaa kila kitokeacho mitaani kama mmoja akipiga mluzi au filimbi utaona wote wanageukia upande ule na kufuata kuna kuna nini. Nadhani watu wa aina hiyo ni wengi na ndio Chadema inadanganywa kwamba inawavutia sera zao na ndio wapiga kura wao.

Pamoja na ushari wa wao kujitembeza kwa njia zo zote, tatizo wao wanaona njia bora na mbadala ni mikutano kitu ambacho kimeashachosha wengi, wanahitaji kuwa wabunifu, licha ya kupewa ushauri nasaha wanaonekana kutoshaurika na kuona wanachokiona kutoka ofisini kwao ndio bora. Wawasikilize wananchi ndicho kinachotakiwa si wananchi kuwasikiliza wao.
 
Unless kuwe na jambo fulani linalotakiwa kuvumishwa hadharani, lakini binafsi nadhani maeneo kama Arusha, Kilimanjaro, Daressalaam, Mbeya, Mwanza, Shinyanga, Mara, Simiyu, Iringa na maeneo mengine ambapo CDM ina mizizi kwa sasa haihitaji sana mikutano ya hadhara ya mara kwa mara.
Maeneo kama haya CDM inaweza kupata viongozi hata katika ngazi za nyumba 10. Then kinachotakiwa sasa ni kuhakikisha nafasi zote zinazohitaji kiongozi kwa mujibu wa katiba ya chama, katika mikoa hii zinajazwa, na viongozi hawa wanakutana mara kwa mara wenyewe lakini pia na viongozi wa juu kupanga miakakati ya kushawishi wapiga kura na kudhibiti wizi wa kura.
Kwa ile mikoa ambayo bado chama hakijajisimika sawasawa, then mikutano ya hadhara iambatane na kujengwa na kuzibwa kwa nafasi zote za uongozi za chama kuanzia nyumba kumi.

Mathalani, Tanzania ina kaya takribani milioni 9 (kwa kutumia sensa ya mwaka jana na ku-assume kwa wastani kila kaya ina watu 5). Ukigawanya milioni 9 kwa 10, utapata laki 9. Kwa maana hiyo CDM inatakiwa iwe na wawakilishi laki 9 wa nyumba kumi. Halafu kila kwenye nyumba kumi kuwe wajumbe wengine wawili watakaowakilisha chama katika kamati ya siasa ya kitongoji. Kwa maana hiyo, jumla ya wajume wa kamati ya siasa ya kitongoji ni 1,800,000 nchi nzima. Then kutoka hawa, kuna viongozi wa vijiji, kata, tarafa, wilaya, mkoa, kanda na taifa. Kwa makadirio ya chini CDM itakuwa na viongozi milioni 2 nchi nzima. Hapa nimeongelea tu uongozi wa General, sijagusia BAWACHA wala BAVICHA...
Kila wilaya itakuwa na viongozi na viongozi wasiopungua elfu 5. Kwa hiyo siku Slaa akisema anasema kufanya mkutano wa ndani na viongozi wa wilaya fulani, members ni watu 5000, na kama wakihudhuria 10%, ni watu 500. Kwa hali kama hii hatutarajii kituo chochote cha kupiga kura kikose wakala mmoja na 'walinzi' 10 katika uchaguzi wa 2015.

Haya niliyoyastipulate hapa ni magumu kuyatekeleza, but hata yakitekelezwa kwa ufanisi wa 50%, yet uchaguzi ujao CCM hatoki...

Kiongozi umepiga mule mule...bahati mbaya kitufe cha like sikioni.

Yaani kwa mchakatuo uliojadili ni kwamba unakuwa na kura karibu 1.5 milioni hata kabla ya uchaguzi.
 
Back
Top Bottom