Candid Scope
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 11,897
- 6,933
Chadema waige tabia ya mnyama mdogo sana anayeitwa FUKO ambaye anafurukuta na kufukua chini ya ardhi na kumaliza mihogo na viazi, mwenye shamba akija ni kuchomoa makuti ambayo matupu wakati viazi na mihogo imeliwa. Ndiyo tabia wanayotakiwa kuifanya sasa hivi Chadema.
Chadema baada ya kuelekeza nguvu za kanda, ni mbinu nzuri ambayo itaweka mwenya wa kupenya hadi ndani viijini, na mijini kupenya mitaani. Kuunda makada wa kuzunguka nyumba kwa nyumba kusaka na kuwashawishi wapiga kura.
Wapiga kura wazuri ni watu wenye makazi yao mitaani, na kuwapata wakazi ni huko mitaani wanakoishi, na kampeni za uchaguzi zinapofanyika ni huko mitaani unakuwa na hakina nani anapiga kura na anamwelekeo wa kukipigia chama au la. Kutegemea huu umati wa mikusanyiko mikubwa ni kwa nafasi chache sana na mara chache kwani tumejifunza walio wengi katika umati ule ni vibaka, wazururaji, wasio na makazi maalum nk.
Mpiga kura anakuwa na makazi maalum ndio maana kitambulisho chake kabla ya kupata lazima serikali za mitaa zitambue na kuridhia uwepo na ukazi wake.
Wapiga kura wazuri ni wale wenye makazi na wanapatikana mitaani kwenye makazi yao, sio wazururaji na wababaishaji mitaani.
Kuwa makini na makundi makubwa ambayo hayapigi kura lakini wahudhuriaji wazuri wa mikutano.
:nono::nono::nono::nono::nono::nono::nono:
Kuwa makini na makundi makubwa ambayo hayapigi kura lakini wahudhuriaji wazuri wa mikutano.
:nono::nono::nono::nono::nono::nono::nono: