Anyway mimi sio mshabiki sana wa siasa za majitaka lakini wakati mwingine huwa napata mashaka sana na Zitto. Ukijaribu kuangalia yeye kwa asili ni mwanasiasa wa upinzani lakini tabia na rafiki zake wote wanapambana na upinzani na CCM wanageuka kuwa ndio support yao. Kwa mfano wale wote wanaoonekana kuipinga cdm tena kwa propaganda za kiccm kama Mtela, Juliana, Mchange, Mwigulu nk ndio marafiki zake wa karibu sana na wanajitahidi kuharibu haiba ya cdm kwa mambo ambayo mengine ni ya kweli na mengi ni propaganda.
Ukijaribu kuangalia hao wanaojinasibu kuwa karibu na yeye kama Juliana na Mtela walitimkia ccm, lakini toka wameenda ccm hatujaona wakiwa na wazo la maana au kupeleka changamoto mpya bali wao wako kila siku na Mwigulu kama vile Mwigulu ndio ccm na wao ndio walimfuata. Tulitegema kwamba wameonewa cdm basi wakifika huko ccm tuone wanakemea hizi siasa za majitaka tunazoziona humu jukwaani kama, Lowasa anaumwa hauwezi urais, Dialo alimpua Lowassa, Membe haupati urais hata akimtumia mama Salma. Lakini hawana wazo lolote la maana ndani ya ccm bali wamebaki na siasa za kipuuzi kusema Mbowe hana elimu japo anawazidi sana kimaisha, sijui cdm ni chama mfu badala ya kujenga ccm waliyohamia. Kuna huyu Mchange yeye akapewa mpaka kipindi cha kuichafua cdm na Star TV ya Dialo, lakini wapi matokeo yake tuona siasa zilezile za majitaka kati ya Dialo na Lowasa. Na kama Mungu ameamua kuuweka ukweli hadharani toka kuondoka kwa hawa vijana cdm hatuoni zile id kama za akina Tuntemeke zikitukana tena mitandaoni, na zaidi ya yote uchaguzi umefanyika katika hali ya ushwari na kiwango kikubwa japo Mbowe amerudia kiti chake na ingependeza zaidi kama kungekuwa na sura nyingine.
Sasa unajiuliza kweli cdm kama taasisi ina madhaifu yake, lakini mbona hawa waliokuwa wanajiona bora huko waliko hawana lolote la maana zaidi ya kuingia kwenye siasa za majitaka? Huyu Zitto aliyekuwa analalamika kila siku kwamba anaonewa na cdm mbona hata hao rafiki zake ameshindwa kuwapa mbinu na siasa za maana wawe kioo chake huko waliko. Ni kweli Zitto ni mwanasiasa mzuri hilo halina ubishi lakini mbona toka yeye amesimamishwa cdm mambo mengi yanakwenda bila mikwaruzano? Na chama kiko vizuri tu ukiachia mapungufu ya kibinadamu na kitaasisi ambayo yanarekebishika? Mimi nadhani ni muda muafaka wa Zitto kujiangalia upya maana huenda bila kujua, watu wamepima alipokuwa kwenye chama, na sasa akiwa nje pamoja na marafiki zake ile nguvu aliyoamini au kuaminishwa anayo ni kweli ama alikuwa anafanya bila kujitambua na kujua mapungufu yake ama kutumika dhidi ya chama? Je ni sahihi unapotofautiana na wenzako basi kwako iwe tiketi ya kuharibu haiba ya chama kama alivyokuwa anafanya. Ama inakuwa yeye ni msomi kama anavyonasibu na wapambe wake kumsifia lakini hajaelimika?