Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 4,393
- 14,500
Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA Tawi la Msimbazi (maarufu Msimbazi Mama) kimemtaka mqanachama wa Chama hicho, Patrick John Asenga kuwasilisha barua ya kujieleza kufuatia taarifa mbalimbali ambazo Mwanachama huyo amezitoa kwenye mitandao ya kijamii akionesha kwenda kinyume na msimamo na agenda ya chama hicho ya NO REFORMS NO ELECTION.
Soma: Waraka wa wagombea 2020 na watia nia wa ubunge 55 wa CHADEMA. Wapinga chama kususia uchaguzi mkuu
Waraka wa CHADEMA tawi la Msimbazi uliotolewa leo Aprili 5, 2025 kwenda kwa Mwanachama huyo mwenye kadi No. CDME11126 ya tarehe 22/06/2021 ambayo ni kadi mpya ya kidijitali umemtaka kujieleza kwa maandishi ndani ya siku 14 kwanini asichukuliwe hatua za kinidhamu kutokana na kwenda kinyume na msimamo wa vikao vya chama ambavyo ni pamoja na Kamati Kuu, Baraza Kuu na Mkutano Mkuu.
Soma: Waraka wa wagombea 2020 na watia nia wa ubunge 55 wa CHADEMA. Wapinga chama kususia uchaguzi mkuu
Waraka wa CHADEMA tawi la Msimbazi uliotolewa leo Aprili 5, 2025 kwenda kwa Mwanachama huyo mwenye kadi No. CDME11126 ya tarehe 22/06/2021 ambayo ni kadi mpya ya kidijitali umemtaka kujieleza kwa maandishi ndani ya siku 14 kwanini asichukuliwe hatua za kinidhamu kutokana na kwenda kinyume na msimamo wa vikao vya chama ambavyo ni pamoja na Kamati Kuu, Baraza Kuu na Mkutano Mkuu.