Kasanzu The Great
JF-Expert Member
- Dec 21, 2013
- 309
- 222
Kwa hali Kisiasa ilivyo, Chama Cha Demokrasia na Maendeleo kinatakiwa kifanye Mambo yafuatayo ili kiweze KUSIMAMA na kurejesha ushawishi wake Kama ilivyokuwa kabla 2015.
1. Achaneni na Magufuli
Ukifuatilia hotuba zako nyingi nikama Magufuli Yuko Madarakani. Agenda za mikutano yao imebeba "dhihaka" na kejeli dhidi ya Magufuli. Wanatakiwa wajue kwamba ni vigumh sana kupambana na mtu aliyekufa halafu ukashinda.
Inaonekana nikama walishajua kwamba kumtukana Magufuli kutaifurqhisha dola na kuwaacha wafanye mikutano yao bila "bughudha" lakini wanafanya harakati zao ziwe ziwe ngumu kueleweka.
2. Wamkabili Samia
Ukweli nikwamba CHADEMA hawataki kumuudhi Samia kwasasa ndio maana wanazunguka na kumung'unya Maneno. Ukifuatilia hotuba zao pamoja na mitandao ya kijamii Kila mtu atakubaliana namimi kwamba wanamuogopa Samia kumsema waziwazi. Yawezekana pengine wanahisi mikutano yao itazuiwa, wanavizia kuitwa Ikulu, au wanaona watazua upinzani wa kidola au ni mbinu ya kumfanya abweteke ili baadaye wake kumuattack akiwa na makosa mengi. Kitendo Cha kuendelea kuwa kuwa washangiliaji wa Samia watajikuta wanashindwa kuwarejesha wafuasi wao.
3. Waweke Mikakati yao Kanda ya Ziwa
Sio Siri kwamba baada ya Kanda ya Kaskazini, Kanda ya Ziwa iliwapa sapoti kubwa. Kwasasa wawekeze nguvu huko bila shaka wataitikisa nchi. Kanda ya Ziwa kwasasa wanahisi Kama vile wameporwa mtu wao, Wanamsiba, wanamashaka Kama watatimiziwa matarajio yao. Ukipita kwenye mitaa ya Bukoba, Mwanza, Bariadi, Nzega, Tabora, Bunda, Musoma au Shinyanga utakubaliana namimi kwamba wananchi wanawasiwasi mkubwa. CHADEMA waondoe zile dhana za ukabila wawaone watu wa Kanda ya Ziwa Kama ndugu zao. Kwasasa Kuna dhana Kichwani mwa watu wa CHADEMA Kama vile watu wa Kanda ya Ziwa ni adui zao ndio maana Kila Jambo linalohusu maendeleo ya Kanda hii wanapinga nk.
4. Watambue kuwa Samia hana watu
Samia hana eneo analokubalika zaidi ya turufu ya CCM hata huko Zanzibar mizania ya kisiasa ikiwekwa sawa anaweza kupata Kura chache. Hii kwao ni fursa wakiamua kutimia akili. CCM haiko kitu kimoja Kama ilivyokuwa miaka mitatu iliyopita. Uwezekano wa Kura za wanaccm kugawanyika ni mkubwa sana.
5. Wawasamehe wale wabunge 19
Ile time ya wabunge 19 inao uzoefu mkubwa kwenye harakati hizi ngumu. Ikiachiwa ikarudi kwenye chama itaongeza nguvu, itatumia mtaji wake kuandaa majimbo ambako 2025 majimbo mengi yatakuwa tayari yako CHADEMA. MFANO
Nusrat Hanje anaweza kuandaliwa kwenda Kigamboni
Ester Matiko - Tarime
Ester Bulaya - Bunda
Halima Mdee - Kawe nk.
Itasaidia kukusanya nguvu kutokea Bungeni na kuchagiza Harakati hizi.
Mwisho, ni Bora kusahau yaliyotokea na kuukabili ukweli wa Sasa. Kuna upepo mzuri wa kupita nao lakini tunaukataa na kutaka kupambana na Jana. Tuchukue hatua.
Kamanda Maganga
1. Achaneni na Magufuli
Ukifuatilia hotuba zako nyingi nikama Magufuli Yuko Madarakani. Agenda za mikutano yao imebeba "dhihaka" na kejeli dhidi ya Magufuli. Wanatakiwa wajue kwamba ni vigumh sana kupambana na mtu aliyekufa halafu ukashinda.
Inaonekana nikama walishajua kwamba kumtukana Magufuli kutaifurqhisha dola na kuwaacha wafanye mikutano yao bila "bughudha" lakini wanafanya harakati zao ziwe ziwe ngumu kueleweka.
2. Wamkabili Samia
Ukweli nikwamba CHADEMA hawataki kumuudhi Samia kwasasa ndio maana wanazunguka na kumung'unya Maneno. Ukifuatilia hotuba zao pamoja na mitandao ya kijamii Kila mtu atakubaliana namimi kwamba wanamuogopa Samia kumsema waziwazi. Yawezekana pengine wanahisi mikutano yao itazuiwa, wanavizia kuitwa Ikulu, au wanaona watazua upinzani wa kidola au ni mbinu ya kumfanya abweteke ili baadaye wake kumuattack akiwa na makosa mengi. Kitendo Cha kuendelea kuwa kuwa washangiliaji wa Samia watajikuta wanashindwa kuwarejesha wafuasi wao.
3. Waweke Mikakati yao Kanda ya Ziwa
Sio Siri kwamba baada ya Kanda ya Kaskazini, Kanda ya Ziwa iliwapa sapoti kubwa. Kwasasa wawekeze nguvu huko bila shaka wataitikisa nchi. Kanda ya Ziwa kwasasa wanahisi Kama vile wameporwa mtu wao, Wanamsiba, wanamashaka Kama watatimiziwa matarajio yao. Ukipita kwenye mitaa ya Bukoba, Mwanza, Bariadi, Nzega, Tabora, Bunda, Musoma au Shinyanga utakubaliana namimi kwamba wananchi wanawasiwasi mkubwa. CHADEMA waondoe zile dhana za ukabila wawaone watu wa Kanda ya Ziwa Kama ndugu zao. Kwasasa Kuna dhana Kichwani mwa watu wa CHADEMA Kama vile watu wa Kanda ya Ziwa ni adui zao ndio maana Kila Jambo linalohusu maendeleo ya Kanda hii wanapinga nk.
4. Watambue kuwa Samia hana watu
Samia hana eneo analokubalika zaidi ya turufu ya CCM hata huko Zanzibar mizania ya kisiasa ikiwekwa sawa anaweza kupata Kura chache. Hii kwao ni fursa wakiamua kutimia akili. CCM haiko kitu kimoja Kama ilivyokuwa miaka mitatu iliyopita. Uwezekano wa Kura za wanaccm kugawanyika ni mkubwa sana.
5. Wawasamehe wale wabunge 19
Ile time ya wabunge 19 inao uzoefu mkubwa kwenye harakati hizi ngumu. Ikiachiwa ikarudi kwenye chama itaongeza nguvu, itatumia mtaji wake kuandaa majimbo ambako 2025 majimbo mengi yatakuwa tayari yako CHADEMA. MFANO
Nusrat Hanje anaweza kuandaliwa kwenda Kigamboni
Ester Matiko - Tarime
Ester Bulaya - Bunda
Halima Mdee - Kawe nk.
Itasaidia kukusanya nguvu kutokea Bungeni na kuchagiza Harakati hizi.
Mwisho, ni Bora kusahau yaliyotokea na kuukabili ukweli wa Sasa. Kuna upepo mzuri wa kupita nao lakini tunaukataa na kutaka kupambana na Jana. Tuchukue hatua.
Kamanda Maganga