Mambo ya Kenya nimeshayaelezea hapo juu, huo unaoitwa Upinzani ulifanikiwa Kenya kwa sababu watu wale wale waliokuwa KANU walijimega na kuingia Upinzani, na ndio maana Kenya wanasiasa ni wale wale tu hao akina Bw.Uhuru Kenyata walikuwa KANU, hao akina Bw.Ruto wote chini ya Bw.Moi, na ndio maana hakuna jipya la maana Kenya kwa maana hakuna wakumnyooshea kidole mwenzake, hakuna wa kumshitaki Bw.Moi kwa maana woote walikuwa Serikali moja!
Hivyo la Kenya linaweza tu kutokea hapa kwetu kama CCM ikimeguka na kundi kubwa kukimbilia Upinzani, na sasa hilo likitokea tutakuwa hatujafanya kitu kwani hao hao tunaowashutumu kwa Ufisadi ndio watakaosaidia CHADEMA kushinda, watu kama akina Bw. Chenge aua Bw. Lowasa wakihamia CHADEMA hapo unaweza kutabiri kuanguka kwa CCM kwani wataondoka na timu yao, lkn pia hilo likitokea usitegemee cha watu kuhukumiwa kwa kesi ya EPA au Richmond au kesi ya RADAR!