CHADEMA MMefungua NJIA!

CHADEMA MMefungua NJIA!

Frelimo na Kanu ziko wapi? Tafakari

Nafikiri unaandika bila kuwa na Data kamili aliyekwambia Frelimo imekufa nani? Ni Chama gani kinaongoza Msumbiji sasa hivi?

Unaongelea KANU unawezaje kuafananisha KANU na CCM? Kenya na Tanzania tuna mifumo 2 tofauti na mazingira ya kisiasa tofauti kabisa, na kilichofanya KANU ishindwe siyo Upinzani 100% bali ni yale yale aliyoyasema
Mlm Bw. Nyerere kwamba upinzani wa kuiondoa CCM utatoka ndani ya CCM, hakuwa mjinga aliposema hivyo, alisema hivyo akijua jinsi Serikali inavyofanya kazi kwa maana yeye alishiriki kuiunda na ndicho kilichotokea KANU yaani wale wale waliokuwepo KANU ndio wakatoka na kuingia Upinzani, na ndio maana hakuna mabadiliko ya kweli Kenya kwa maana watu wanaojiita wapinzani leo hii ndio wale wale waliokuwa KANU hapo mwanzo hivyo hakuna wa kumshtaki mwenzie, na ndio maana unaona hakuna mtu amemshtaki Bw.Moi ingawaje ana tuhuma nyingi na za ajabu!

Hivyo kwa hali jinsi ilivyo TZ kuiondoa CCM Madarakani 2015 bila msaada au ushirikishwaji wa wana CCM wenyewe ni ngumu sana na naweza kusema ni kama haiwezekani.

Hivyo hapo labda CCM imeguke na Viongozi wengi wa CCM wakimbiliea Upinzani hapo sawa, na hilo likitokea ujue hakuna jipya kwani wale wale watuhumiwa wa Ufisadi watakuwa wamerudi madarakani ila kwa njia nyingine, na kutakuwa hakuna cha kushitakiwa mtu yoyote, na ndicho kilichotokea kwa KANU Kenya!

 
Hatakama unoauhakika wa CCM kushinda, mbona hutoi hizo sababu za msingi zilizowazi za kusapoti huo utabiri wako? vinginevyo itakuwa ni hisia zako na maono yako tuu!

Kwani wapi niliposema kwamba hizi ni hisia au maono ya mtu mwingine?

Nimeandika kulingana na jinsi nionavyo na jinsi ninavyouelewa mfumo wetu wa Uongozi, ambao Raisi wetu ana nguvu za kupitiliza, anaweza kufanya chochote kile na muda wowote ule bila kuulizwa, anateua kila mtu hapa Tanzania, anauwezo kumfukuza Kiongozi yoyote yule nchini, hata hiyo KATIBA mpya anaweza akaikataa na hakuna kitu tunachoweza kufanya, sasa kuingia kwenye ushindani (uchaguzi) na mfumo kama huo kushinda inahitaji miujiza!
 
JF Senior Expert Member
verified.png
Array


Join Date : 11th December 2010
Location : Lushoto - Kwemakame.
Posts : 1,900
Rep Power : 24446
Likes Received2768
Likes Given330


[h=2]
icon1.png
Live Updates: Mkutano wa CHADEMA uwanja wa ujenzi- Dodoma[/h]
Mkutano wa hadhara wa Chadema upo uwanja wa wajenzi karibu na sheli (Kituo cha Mafuta) mita chache karibu na kituo cha mabasi.

Kama kawaida, nyomi ipo ya kutosha.

• Maandamano makubwa sana ya magari yametusua katikati ya mji wa Dodoma, maeneo ya bunge, Makao Makuu ya CCM kueleke uwanjani. Hamasa ni kubwa sana!​

Last edited by Mohamedi Mtoi; Today at 16:19.​


 
Mleta mada ni gamba na mnachojidanganya hatuwezi kuwazuia ila hamtaamini 2015 tutakapokuwa maggoni na wezi wa mali za umma watakapokuwa wananyea ndoo!
Jiepushe na visasi kaka tatizo la Tanzania ni zaidi ya wizi wa mali za umma!! Lazima kuwa na checks and balances ambazo chanzo chake ni Katiba, nadhani umeona Kenya kwenye ruling ya rufaa ya RO/CORD the supreme court iliamua mchakato wa ununuzi wa vifaa vyote vya kupigia kura zile mashine za kisasa zote nk uchunguzwe, kama uesikia DPP kamwagiza Mwenyekiti wa Ethical and Anti corruption commission afanye uchunguzi, kuona kama kulikuwa na rushwa maana hakukuwa na transparency na kuna Mama mmoja Alisha jiuzuru kwa ajili ya interference toka kwenye Executive kwenye mchakato mzima wa manunuzi! Bila hayo kwa Katiba tarajiwa ambayo tayari ninaiangalia kwa "MIWANI YANGU YA MBAO" tayari CHAMA DOLA wamesha influence destiny ya Katiba hiyo sioni jinsi gani tutaweza kwenda mbele!!
 
Ingawa ni ukweli ulio wazi kwamba Chama cha CHADEMA hakiwezi kushinda Uchaguzi wa Uraisi na Ubunge 2015, lakini ni jambo lililo wazi pia CHADEMA wamefungua njia ya mabadilko nchini mwetu!

Serikali ijayo ya CCM, haiwezi kuwa ya kisanii ukiilinganisha na ya sasa hivi, na nathubutu kusema pia Serikali zilizopita, na sio kwa sababu haiwezekani, bali ni kwa sababu CCM hawana jinsi bali kubadilika kwani kila siku zinavyozidi kwenda ndivyo watu wanvyozidi kuhoji Uhalali wao wa kuongoza, hivyo basi naweza kusema 2015 ndiyo karata ya mwisho kwa CCM, na kama wasipobadilika basi 2020 au 2025 CHADEMA kama wataendelea na kasi hii hii walionayo sasa hivi ni lazima watashinda Uchaguzi wa Uraisi na Ubunge!

Nina hakika wewe unaijuwa vizuri CHADEMA, ila kwa vile wewe ni gamba hutaki kukiri hilo. Yaani pamoja na kujitahidi kuandika unaishia na mawazo ya kwamba CHADEMA itashinda 2020. Naamini huna tofauti na Nape.

Sasa wewe subiria 2015 uone jinsi nchi inavyo pata ukombozi wake kutoka kwa mkoloni mweusi. Mpelekee salaam nape kule Turiani anapo fukuzana na jamaa wa Mtibwa Sugar. Mwambie jamaa wamekataa 2020, kwa sababu wao wamejikita kisawasawa 2015 lazima kieleweke. Ama MAGAMBA watake wasi take lazima kitaeleweka.
 
Jiepushe na visasi kaka tatizo la Tanzania ni zaidi ya wizi wa mali za umma!! Lazima kuwa na checks and balances ambazo chanzo chake ni Katiba, nadhani umeona Kenya kwenye ruling ya rufaa ya RO/CORD the supreme court iliamua mchakato wa ununuzi wa vifaa vyote vya kupigia kura zile mashine za kisasa zote nk uchunguzwe, kama uesikia DPP kamwagiza Mwenyekiti wa Ethical and Anti corruption commission afanye uchunguzi, kuona kama kulikuwa na rushwa maana hakukuwa na transparency na kuna Mama mmoja Alisha jiuzuru kwa ajili ya interference toka kwenye Executive kwenye mchakato mzima wa manunuzi! Bila hayo kwa Katiba tarajiwa ambayo tayari ninaiangalia kwa "MIWANI YANGU YA MBAO" tayari CHAMA DOLA wamesha influence destiny ya Katiba hiyo sioni jinsi gani tutaweza kwenda mbele!!

Unajua watu wengi wanasukumwa na ushabiki na Jazba na wanasahau hali halisi ya mambo, ukweli ni kwamba kuingia kwenye Uchaguzi na kuishinda CCM kwa mfumo huu jinsi ulivyo ni ndoto, anayepuuzia nguvu ambazo Raisi wa TZ anazo ktk kila nyanja anajidanganya, hata hiyo Katiba mpya pia tunategemea huruma yake, yeye ndio akubali akikataa hakuna cha Katiba wala nini!
 
JF Senior Expert Member
verified.png
Array


Join Date : 11th December 2010
Location : Lushoto - Kwemakame.
Posts : 1,900
Rep Power : 24446
Likes Received2768
Likes Given330


icon1.png
Live Updates: Mkutano wa CHADEMA uwanja wa ujenzi- Dodoma


Mkutano wa hadhara wa Chadema upo uwanja wa wajenzi karibu na sheli (Kituo cha Mafuta) mita chache karibu na kituo cha mabasi.

Kama kawaida, nyomi ipo ya kutosha.

• Maandamano makubwa sana ya magari yametusua katikati ya mji wa Dodoma, maeneo ya bunge, Makao Makuu ya CCM kueleke uwanjani. Hamasa ni kubwa sana!​
Last edited by Mohamedi Mtoi; Today at 16:19.​



Iwe Mosie Mtoi! Tikunda tibanike mosie iwe. Maana iyo furaha ne nkuu sana mosie! Ukweli wengine tunakaribia kufa kwa furaha tukisikia habari njema kiasi hicho. Ni basi tu Mkuu, tupo mbali na Dodoma.

Pigeni jaramba hadi CHAMA CHA MATUSI wajue kwamba CHADEMA ni mpango wa Mungu. Sio sawa na CHAMA CHA MASHETANI.
 
Unajua watu wengi wanasukumwa na ushabiki na Jazba na wanasahau hali halisi ya mambo, ukweli ni kwamba kuingia kwenye Uchaguzi na kuishinda CCM kwa mfumo huu jinsi ulivyo ni ndoto, anayepuuzia nguvu ambazo Raisi wa TZ anazo ktk kila nyanja anajidanganya, hata hiyo Katiba mpya pia tunategemea huruma yake, yeye ndio akubali akikataa hakuna cha Katiba wala nini!

Mkuu!

Hivi unategemea huruma yoyote kutoka kwenye sura za MAGAMBA? Pamoja na yote "HATUWEZI KUWAACHIA NGURUWE SHAMBA LA MIHOGO". Watalimaliza tu kwa vile wanaona ni halali yao. Pamoja na mapungufu ya Katiba tuliyo nayo, ni lazima kukomaa. Kila siku iendayo kwa mungu yapo mabadiliko licha ya kuto kupenda kwao. 2015 lazima nguvu ya UMMA itakuwa mahali pake. Licha ya ubovu wa katiba isiyo endana na hali halisi ya mabadiliko ya Kidemokrasia, wataachia tu.

Unataraji kwamba CCM walitarajia kuwaona waTanzania wakiandamana kudai haki zao za msingi zaidi ya Maandamano ya Mshikamano? Ambayo kwa sasa hivi hawathubutu hata kuita watu ili waandamane. Labda kwa ahadi za khanga, kofia, mafuta ya bodaboda, n.k.
 
Ingawa ni ukweli ulio wazi kwamba Chama cha CHADEMA hakiwezi kushinda Uchaguzi wa Uraisi na Ubunge 2015, lakini ni jambo lililo wazi pia CHADEMA wamefungua njia ya mabadilko nchini mwetu!

Serikali ijayo ya CCM, haiwezi kuwa ya kisanii ukiilinganisha na ya sasa hivi, na nathubutu kusema pia Serikali zilizopita, na sio kwa sababu haiwezekani, bali ni kwa sababu CCM hawana jinsi bali kubadilika kwani kila siku zinavyozidi kwenda ndivyo watu wanvyozidi kuhoji Uhalali wao wa kuongoza, hivyo basi naweza kusema 2015 ndiyo karata ya mwisho kwa CCM, na kama wasipobadilika basi 2020 au 2025 CHADEMA kama wataendelea na kasi hii hii walionayo sasa hivi ni lazima watashinda Uchaguzi wa Uraisi na Ubunge!

iweje isiweje kwa wenyeji wa Majita kule mkoa wa Mara wanajua kuwa CCM huyu ndiye rais wa mwisho. Mtabili mashuhuri ambaye kila kizazi kimerithishwa utabili wake alisema" siku za usoni kutakuja watu wana nywere kama za watoto wadogo,lakini watu hawa watakuwa na nguvu sana na watawatawala. Watu hawa wataondolewa kwa maneno tu na mtu atakayetoka rugulu hapa mashariki (rugulu manake Zanaki kwa kijata ,kiruri na kikwaya) na akatoka Mwl JK Nyerere na kuwaondoa wakoloni. Kiongozi wa pili atatoka katikati ya maji, aliongezea kusema huyo mzee, na akatokea Ally Hassan MWINYI .Pia lisema kuwa mtawala wa tatu atatoke magharibi ya maji aliyotoka wa Pili, na hapo Mzee Mkapa akapatikana akiwa anatoka magharibi ya bahari ya Hindi. Wa mwisho (kwa kadri ya utabiri wa huyo mzee ambao haujasema uongo hata kidogo) atakuwa elembesha (yaani msawazishaji au mtulizaji au mweka mambo sawa kwa lugha za Kijita,kiruri na kikwaya) .Na kwa dalili ninazoziona kweli huyu ni elembesha ,kwani ametulia sana ni msikivu ,mwenye huruma na kwa ushahidi zaidi amekubali itungwe katiba mpya na amini usiamini katiba hiyo itakuja kukubaliwa na kila upande. Wala wapinzani wasiwe na hofu kabisa kuhusu katiba, ataiacha katiba nzuri kabisa itakayopendwa na wote. Baada ya hapo hakutakuwa tena na utawala wa chama kimoja. amini usiamini Mungu tu atujalie maisha UTABILI HUU UTATIMIA , KWANI TANGU MWANZO HAUJAKOSEA. wAAFIDHINA MNAWEZA KUNITUKANA MNAVYOTAKA LAKINI UKWELI NDO HUO
 
Saa ya kumwagika damu tanzania ni sasa, kama CCM watataka kuchukua madaraka kwa mabavu ujue umekaribisha umwagaji wa damu ambao haujawahi kutokea Afrika. CCM wasome alama za nyakati watu wana hasira sana na usanii unaoendelea. Mwanya ukitokea tu ni hatari sana, Mungu apishie mbali hali hii. Uzuri JK ameshajitayarisha kuachia madaraka kwa CDM.
 
Sio kweli, ungesema kwamba wananchi wanaanza kuchoka ningekubaliana na wewe, na ndio maana ni lazima CCM wabadilike, lkn kusema kwamba wameshaichoka ni kujidanganya, tunaona chaguzi nyingi ndogo zinafanyika kila siku,
kama unavyosema ni kweli basi tungeona huko kuchokwa kwa CCM kwenye hizi CHAGUZI.

K
wangu mimi maadamu CCM bado inashinda hizi Chaguzi ndogo tena wakati mwingine kwa kura nyingi tu hakuna ushahidi zaidi ya huo, kwamba CCM bado ina wapenzi tena wengi tu, lkn wanakwenda wakipungua, na 2015 ni karibu mno kwa Upinzani kuweza kuziba hilo pengo, na ndio maana nasema kama wakiendelea na kasi hii basi kuanzia 2020 au 2025 ndio wanaweza kushinda!

Fuatilia chaguzi zote Latest....CCM wamemwaga hadi Lushoto kwenye ngome yao...ni months ago kwenye vijiji vya huko Kagera...au wewe unazungumzia chaguzi gani...?
 
Kwani wapi niliposema kwamba hizi ni hisia au maono ya mtu mwingine?

Nimeandika kulingana na jinsi nionavyo na jinsi ninavyouelewa mfumo wetu wa Uongozi, ambao Raisi wetu ana nguvu za kupitiliza, anaweza kufanya chochote kile na muda wowote ule bila kuulizwa, anateua kila mtu hapa Tanzania, anauwezo kumfukuza Kiongozi yoyote yule nchini, hata hiyo KATIBA mpya anaweza akaikataa na hakuna kitu tunachoweza kufanya, sasa kuingia kwenye ushindani (uchaguzi) na mfumo kama huo kushinda inahitaji miujiza!

WALE MARAISI wote madictator duniani wenye historia ya utajiri mkubwa, Jeshi kubwa , Sila kubwa, Maisha ya kifahari, Walinzi wa kila aina , wenye sifa pia ya ukiukaji wa haki za binadamu, Uvunjaji wa sheria/katiba za nchi zao. WAKO WAPI????????
 
Uko sawa kabisa, na ndio maana nasema 2015 ni mapema mno kufanya yote hayo kama mpaka sasa hivi hatujaanza bado, ila hayo yote yanaweza kufanyika kujiandaa kwa 2020 au 2025


Hayo mafunzo ya Ndani morogoro unaelewa dhamira yake.....? kwa bahati hivyo vijiji tajwa baadhi nimefika...kuna pro-upinzani na wanaojua kujenga hoja than hata baadhi ya watu humu kama SUMU na BUNGENI!
 
Tutakaa na kuzogoa hapa mpaka giza linaingia. Kama wote tunataka kuona kweli tunaikomboa Tanzania mwaka 2015 basi ningetaka kuona tunakaa na kuungana vyama vyote vinavyoitwa vya upizani na kuhakisha kuwa iwavyo na iwe lengo litimie la kuing'oa chama tawala madarakani. ubinafsi na uroho wa kuingia ikulu utatufanya ndoto tunayoota isitimie ya kuiona Tanzania huru na yenye haki.
Bila kuungana hata2030 bado ni ndoto ya kufikirika.

Ishu ni kuungana watanzania...Ghana na Zambia ni mfano mzuri kwetu...
Tusifuatishe siasa za Kenya....Kenya wanaungana kuzicheza karata za ukabila nothing else....
Kuna vyama sio wapinzani....bali ni mapandikizi ya chama tawala....hata baadhi ya makada hujisahau na kuvitaja tukiwa nao bar....kujiunga nao ni sawa na kuwaita wagonjwa mahututi kuingia nao vitani...!
 
hata yesu pamoja na kuwa ni mwana wa mungu lakini alikufa ili aukomboe ulimwengu. hadi kufikia oct 2015 watakaokuwa hawana meno kwa sababu ya kupigania haki ni zaidi ya 1 million

yesu hakuwa mwanasiasa
 
Back
Top Bottom