Chadema (Mbowe): We recognise the president

Chadema (Mbowe): We recognise the president

"……..Kwa kuwa tulikwisha kukataa kutambua matokeo ya uchaguzi, na vile vile baada ya kukataa kutambua matokeo tulikataa vile vile kumtambua rais aliyepatikana kutokana na mchakato huo ambao hatuutambui……….." Dr.Slaa

Kisha Mbowe anatuuliza hii 'myth' kuwa chadema haimtambui rais imetoka wapi!
 
"……..Kwa kuwa tulikwisha kukataa kutambua matokeo ya uchaguzi, na vile vile baada ya kukataa kutambua matokeo tulikataa vile vile kumtambua rais aliyepatikana kutokana na mchakato huo ambao hatuutambui……….." Dr.Slaa

Kisha Mbowe anatuuliza hii 'myth' kuwa chadema haimtambui rais imetoka wapi!

Wananikumbusha John Kerry alivyo "vote for it before voting against it".

Walimtambua rais, halafu wakawa hawamtambui, labda sasa wanamtambua. Inabidi tuwe tunaangalia status kama hali ya hewa, leo kipimanyuzi za kumtambua rais kiko nyuzi ngapi ?
 
soon mtasikia zito karudi kundini CCM! subirini 2015
 
Kilichobaki ni Chadema wapige magoti na kuomba msamaha kwa Taifa kwa sababu hawakujua wanatoka nje kwa ajili gani na hata sasa hawajui msimamo wao ni upi na kwanini. Mbowe aongoze mwenyewe kwenda kuomba msamaha kwa Rais Kikwete.
 
Wananikumbusha John Kerry alivyo "vote for it before voting against it".

Walimtambua rais, halafu wakawa hawamtambui, labda sasa wanamtambua. Inabidi tuwe tunaangalia status kama hali ya hewa, leo kipimanyuzi za kumtambua rais kiko nyuzi ngapi ?

Na ile "chadema ni chama consistent" ya Dr.Slaa itakuwa wapi hapo?

Au ndo consistent per msemaji wa leo? :s
 
Kilichobaki ni Chadema wapige magoti na kuomba msamaha kwa Taifa kwa sababu hawakujua wanatoka nje kwa ajili gani na hata sasa hawajui msimamo wao ni upi na kwanini. Mbowe aongoze mwenyewe kwenda kuomba msamaha kwa Rais Kikwete.

:whoo:
 
Nilijua mwisho watachemsha, Mbowe na associates wanapenda ukubwa thats all! Hawana tofauti na mafisadi wengine.

Sasa wameshamtambua rais wakae na wapinzani wenzao waunde upinzani wa pamoja!
 
Nadhani inabidi nianzishe semina ya bure juu ya Mantiki na Hoja maana tuna tatizo kubwa. Kuna Tatizo la hoja za Zitto na sasa kuna tatizo la Hoja za Mbowe. Na wote wawili wanaamini wako sawasawa!!! Halafu kuna hoja ya Dr. Slaa which is more consistent with logic. Simply put - kama hutambui matokeo huwezi kutambua mshindi wa matokeo hayo. Ukishakubali hapo the next one ni: msimamo wako wa kutotambua matokeo na mshindi haubadilishi the legal situation iliyopo namely, Kikwete is still the president. This is not a contradiction; ni de facto situation. Kwa sababu, katangazwa na chombo kilichopewa madaraka hayo na hivyo wewe kutomtambua hakubadilishi ukweli uliopo. Position ya Chadema kutotambua ushindi wa Rais was/is simply a political position ndiyo maana sisi wengine tumeshangaa watu wametaharuki sana as if Chadema declared Kikwete siyo Rais kana kwamba wana mamlaka ya kutangaza hivyo!

Labda niioneshe hivi: Mtu akifunga ndoa katika taratibu zote za kisheria NDOA ILE NI HALALI (legally). Ikatokea kuwa kuna mtu anadai mmoja wao alikuwa yuko kwenye ndoa nyingine wakati ndoa ile ilipofungwa na hivyo akadai kuwa haitambui ile ndoa nyingine ni msimamo wa kweli kwa dhamira yake. Lakini haibadilishi ukweli kuwa ndoa ile nyingine ilifungwa kihalali na itavunjwa na chombo halali haivunjiki kwa sababu huyu mwingine haitambui.

This is not that hard. Msimamo wa Chadema wa kutoka Bungeni was legally and morally defensible. Lakini walipogeuka tu na kusema kuwa wanamtambua Rais wanajikuta kwenye rational impasse.

Nitafundisha mantiki.. hii ni hatari huko tunakokwenda.
 
chadema oyeeeee.......! ndiyo maana nakipenda hiki chama, maana usiku na mchana ni tofauti kwao
 
Kilichobaki ni Chadema wapige magoti na kuomba msamaha kwa Taifa kwa sababu hawakujua wanatoka nje kwa ajili gani na hata sasa hawajui msimamo wao ni upi na kwanini. Mbowe aongoze mwenyewe kwenda kuomba msamaha kwa Rais Kikwete.
..NAOMBA KUTOFAUTIANA NAWE.....MZEE WANGU UNABAKI KATI YA VIOO VYANGU......UNABAKI KATI YA WACHANGIAJI AMBAO HUPENDA KUITA BELESHI KWA JINA LAKE(japo mara moja moja unabaki ulivyo) KATIKA HILI LA CHADEMA........UMESEMA LILILOPO NA SI KONA KONA!
TUFANYE HIVYO KATIKA HOJA ZOTE NA SI USHABIKI TUTAFIKISHA TAIFA LETU MBALI
 
Mchungaji recites the litrugy that states "see no evil, hear no evil, smell no evil, speak no evil" and let the people say Amen!
 
Walk-out ya siku moja ni unafiki, CUF walikuwa na haki zaidi zanzibar waligoma kwa miaka mingi, posho hawakuwa wanachukua, wala mashangingi wala kuingia mjengoni si tu wakati karume akiingia ila muda wote mpaka muafaka ukapatikana.
Chadema hasa mbowe ni mnafiki na mpenda vyeo ndiyo maana kakimbia kuchukua gari la kiongozi wa upinzani, ofisi na marupurupu mengine, haya wabunge wamelamba posho na sasa wanasubiri magari- mashangingi, NDIYO maana Kasikia kunakuondolea kamtambua JK haraka na kutaka suluhu na serikali. Chakufurahisha wakereketwa wa chadema wanampigia makofi tu na kumpa big up bila hata kufikiri hata chembe

Hizo ni strategies za CUF na hawa ni CDM. Tatizo hapa ni kuwa watu mlitaka CDM wafanye mnavyotaka ninyi. CUF wenyewe waligoma, wakamkataa rais lakini mwisho walimtambua rais huyohuyo waliyesema haramu na wakamwomba awape vyeo. CDM wanajua kuwa kwa maksudi katiba zetu zinawahalalisha na kuwalinda marais halali na haramu ili mradi tu ametangazwa na NEC. CUF walidhani wakigoma continuaz Karume atajiuzuru ili uchaguzi urudiwe. CDM waliliona hilo na ndo maana Dr. Slaa aliomba utangazaji matokeo usimame kwa akishatangazwa hamna namna mpaka baada 5yrz. Hivyo basi kwa kutambua hayo wakachukua uamuzi waliouchukua ambao haujawapendeza ninyi lakini effectively umefikisha ujumbe. Mara ngapi wabunge wa upinzani waliokuwa wanatoka wakipinga kupitisha mambo ya kipuuzi!
 
Mimi nadhani hapa ukumbini tunapaswa kuwa tunaleta mada na kuzijadili kwa misingi ya facts na sio ushabiki.

Sijaona tatizo la ujumbe wa Mbowe maana tangu mwanzo walisema "raisi ni raisi maana ameshawekwa madarakani na hawana njia ya kupinga hilo" ila "wanakataa matokeo yaliyomuingiza madarakani" hili ndilo hata Dr Slaa alilisema wazi....njia pekee ya kumkataa "mteule wa CCM na NEC ni kwa stail ya PEPOPLE POWER.

Hivyo basi, sijaona mbowe anapoomba samahani na sitatarajia waombe samahani. Messege is already sent and delivered ndani na nje ya nchi na kwa watu woteeee....

Their walk out was very strategic, i salute them.

LONG LIVE PEOPLEs POWER

Walatini na waroma wansema "Vox pupul vox dei =sauti ya watu sauti ya Mungu!

Kumbe mlitaka zifike nje kwa mabwana wakubwa? ili??????????? utoto huu ndani ya chadema utaisha lini na hata wanachama nao tunakuwa na mawazo ya kitoto. "mawazo ya kitoto si ya vijana msinikoti vibaya"
 
Nadhani ifikie wakati cdm kiwe na msemaji mmoja ktk mambo yote makuu ya nchi, na ni kweli hawa jamaa walishakiri kuwa hawayatambui matokeo yalomuweka jk pale alipo lakini wakaenda mbali zaidi kwa kusema tatizo si jk na urais wake bali ni katiba, na ndio maana wakasisitiza 2010----- ni fight against katiba, sasa kusema kwake tena kuwa hawana ugomvi wala roho mbaya na rais lakini wame walk out of bunge mbele yake rais kutafsiriweje? Tafsiri ni look here man, we don't have any problem with you even though we are quite sure/ aware with what went wrong under nec's carpet. Our problem here is what constituted these ujangiri.e.t.c, we're out of this mjengo to make you realise the need of having fair election and that won't happen unless we tz have a new constitution which will grant all of us equal opportunity to contest in fair election.
 
Nadhani inabidi nianzishe semina ya bure juu ya Mantiki na Hoja maana tuna tatizo kubwa. Kuna Tatizo la hoja za Zitto na sasa kuna tatizo la Hoja za Mbowe. Na wote wawili wanaamini wako sawasawa!!! Halafu kuna hoja ya Dr. Slaa which is more consistent with logic. Simply put - kama hutambui matokeo huwezi kutambua mshindi wa matokeo hayo. Ukishakubali hapo the next one ni: msimamo wako wa kutotambua matokeo na mshindi haubadilishi the legal situation iliyopo namely, Kikwete is still the president. This is not a contradiction; ni de facto situation. Kwa sababu, katangazwa na chombo kilichopewa madaraka hayo na hivyo wewe kutomtambua hakubadilishi ukweli uliopo. Position ya Chadema kutotambua ushindi wa Rais was/is simply a political position ndiyo maana sisi wengine tumeshangaa watu wametaharuki sana as if Chadema declared Kikwete siyo Rais kana kwamba wana mamlaka ya kutangaza hivyo!

Labda niioneshe hivi: Mtu akifunga ndoa katika taratibu zote za kisheria NDOA ILE NI HALALI (legally). Ikatokea kuwa kuna mtu anadai mmoja wao alikuwa yuko kwenye ndoa nyingine wakati ndoa ile ilipofungwa na hivyo akadai kuwa haitambui ile ndoa nyingine ni msimamo wa kweli kwa dhamira yake. Lakini haibadilishi ukweli kuwa ndoa ile nyingine ilifungwa kihalali na itavunjwa na chombo halali haivunjiki kwa sababu huyu mwingine haitambui.

This is not that hard. Msimamo wa Chadema wa kutoka Bungeni was legally and morally defensible. Lakini walipogeuka tu na kusema kuwa wanamtambua Rais wanajikuta kwenye rational impasse.

Nitafundisha mantiki.. hii ni hatari huko tunakokwenda.

Binafsi naona hii melee haina sababu yeyote ya msingi na imetawaliwa na a lot of hot air, bila nyama au substance.

Logically kama ulivyosema, CDM whether wamekataa au hawajakataa matokeo, JK ndio mshika mpini, kwa msingi kwamba ametangazwa na NEC, whether kihalali au la, lakini kifungu 41 cha Katiba hapo kimepigia msumari. Sasa kinachowapa watu wengi tabu, pengine kutokana na ufahamu wao butu, kwa kusudi ili tuendelee kumark-time au kutaka kuwapangia CDM nini cha kufanya, walitegemea waseme kutotambua matokeo kunaambatana na kususia kila kitu kinachohusiana na JK na serikali kwa ujumla. Nadhani huu ni mtazamo butu. Kususia kila kitu ni hatua ambayo ingewafanya kukosa mtu wa ku-negotiate nae, lolote lile, maana huyo mtu au chombo itakuwa sehemu ya kinachotakiwa kususiwa!... sasa at the end of the day unakuta the whole thing inakosa maana.


Well, kuja kwene suala la kugongana kwa taarifa / maneno kuhusu kadhia hii, nadhani it is obvious inabidi CDM waimarishe kitengo cha utoaji taarifa kwa umma. Maana kila mtu akianza kuongelea habari ileile mwisho wake ni kupishana kwa lugha na sarufi, na matokeo yake wanatengeza mwanya wa maadui zao kuutumilia huu mwanya na ku-blow hii ishu nje ya malengo ya mwanzo.
 
Kilichobaki ni Chadema wapige magoti na kuomba msamaha kwa Taifa kwa sababu hawakujua wanatoka nje kwa ajili gani na hata sasa hawajui msimamo wao ni upi na kwanini. Mbowe aongoze mwenyewe kwenda kuomba msamaha kwa Rais Kikwete.

Naomba kutofautiana nawe. Waombe msamaha kwa lipi? Kutoka nje au kusema wanamtambua rais? Wabunge wote waliapa kuilinda katiba na hivyo Chadema wanalazimishwa na katiba kumtambua rais. Mimi nadhani wengi wetu ndo hatutaki kujua kwanini CDM walitoka nje na msimamo wao ni upi? Wengi tunataka CDM wasimtambue JK kwa kuwa hakuingia kwa njia halali. Dr. Slaa hakuapa anaweza fanya hivyo ila si wabunge. Katiba inamsafisha na kufanya rais halali kama ambavyo pesa Chafu zinavyosafishwa.
 
Selemani,

Facts please. Slaa was not in Dodoma. Are u sure Slaa na Mbowe pushed for it? Wabunge wana maamuzi katika mambo yanayohusu utendaji ndani ya Bunge kwa kufuata msimamo wa Chama. Nadhani kuna contradiction mahali,kama walipiga kura, walio wengi wakashinda, kuna swala la fulani ku "push".

Ni vema tukajadili kukiwa na facts lakini kwa kuzingatia misingi ya demokrasia yenyewe.

Dr. Slaa--Kwanza hongera kwa changamoto uliyotoa wakati wa kampeni. We believe this coming government will perform even better because of your work. Umeawaamsha waTanzania wengi kujihusisha na masuala ya siasa.

But, Mwenyekiti wako Mbowe is QUOTED saying decision to walk out was reached by consensus of all the people. Lakini huo sio ukweli, maana naibu katibu mkuu wako was on TBC1 saying he was against it. So as Halima Mdee. Sasa hapa tuwaelewe vipi? It is clear that the leadership pushed for something against the will of minority of your wabunge. Yes, you voted and those against it lost. Then Chairman Mbowe misled the public with his statement above. Haikuwa consensus, the decision was narrowly approved. Hapo tungewaelewa.

Pia, tunajua ulikataa matokeo, and refused to attend Mkwere's inaugural ceremony and you were quoted multiple times ukisema haumtambui Jakaya kama Raisi. Now, with this Mbowe statement--can we conclude that, Dr. Slaa anamtambua Kikwete au? I guess, I'm asking if Mbowe was speaking for the party, for you, or for himself?

Kitu cha mwisho, mpaka leo hamjaleta ushahidi wa kutosha kama Mkwere na NEC wameiba kura. Mlisema mnajipanga na mtakuja na vielelezo lakini hadi leo hakuna kitu. If you want public/international support, inabidi mje na vithabiti kwamba Usalama wa taifa did XYZ that led to misplacement of X amount of kuras, and this is the evidence. Otherwise, this will not go anywhere.
 
Naomba kutofautiana nawe. Waombe msamaha kwa lipi? Kutoka nje au kusema wanamtambua rais? Wabunge wote waliapa kuilinda katiba na hivyo Chadema wanalazimishwa na katiba kumtambua rais. Mimi nadhani wengi wetu ndo hatutaki kujua kwanini CDM walitoka nje na msimamo wao ni upi? Wengi tunataka CDM wasimtambue JK kwa kuwa hakuingia kwa njia halali. Dr. Slaa hakuapa anaweza fanya hivyo ila si wabunge. Katiba inamsafisha na kufanya rais halali kama ambavyo pesa Chafu zinavyosafishwa.

Kwa hiyo ule ulikuwa msimamo binafsi wa Dr.Slaa na hauhusiani na chama? Na kama ni hivyo kwa nini kwenye maongezi yake akawa anarejelea Chadema na sio kujitaja mwenyewe tu?
 
Kwa hiyo ule ulikuwa msimamo binafsi wa Dr.Slaa na hauhusiani na chama? Na kama ni hivyo kwa nini kwenye maongezi yake akawa anarejelea Chadema na sio kujitaja mwenyewe tu?

Kichwa cha habari kipo wazi ndugu yangu na ndicho nilichochangia kufuatia maelezo ya Mwankjj
 
Back
Top Bottom