In fact ni ishara ya wazi kua baadhi yao wanatamani wote kua na changamoto au matatizo uniform na utatuzi wa changamoto zao ambazo kila moja alizipata kwa mtindo wake, eti nazo zitatuliwe as uniform, kitu ambacho sio sahihi na haiwezekani.
hii mindset ya eti kitu fulani tukose wote au tupate wote ni dhana mbovu na mbaya sana kwa wapambanaji wenye lengo moja, mtaishia kuraruana daily na kudhoofisha nguvu ya mapambano.
wanadamu kupeana pole kwenye misiba hasa waTanzania, ni jambo la kawaida sana regardless ya utofauti wa mirengo ya kisiasa. Lakini miongoni mwa baadhi ya wanachadema hali ni tofauti kidogo, kuhani msiba ni usaliti, na kitu ambacho kinachocheo kuvuana nguo hadharani. Hili ni kosa baya sana.
Na huenda kuna mambo mengine mengi zaidi hao majamaa wanayo mioyoni mwao baina yao, inatafutwa sababu tu ya kutoa nyongo. Nadhani hali inaweza kua mbaya zaidi.
Siasa za uadui wa kiwango hiki hazina afya wala ladha aise.
Inasikitisha sana na kwakweli inafedhehesha sana 🐒