Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,470
- 911,174
Sakata la umeya Mwanza limechukua sura mpya baada ya uongozi wa Chadema kumshtaki Mkurugenzi wa Jiji la Mwanza kwa yale yanayodhaniwa ni kuvuruga uchaguzi wa Umeya na kukipendelea CCM.........................
Barua hiyo ameandikiwa Waziri wa Serikali za Mitaa.........Bw. John Nguchika...............
Wasiwasi wangu ni kuwa hivi Nguchika ni wa chama kipi? Je, anaweza kutenda haki hapo............na sheria zikoje................................nini nafasi ya NEC kwenye chaguzi hizo na mahakama zetu..................................
CHADEMA wamshtaki mkurugenzi wa Mwanza
na Sitta Tumma, Mwanza
CHAMA Demokrasia na Maendeleo mkoani Mwanza kimemshtaki mkurugenzi wa jiji la hilo, Willison Kabwe, kwa madai ya kuingilia na kuharibu utaratibu wa uchaguzi wa nafasi ya Meya na Naibu wake.
Kabwe ameshtakiwa kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), George Mkuchika, kupitia barua yenye kumbukumbu CDM/M/MZ/04/77/10 iliyoandikwa na CHADEMA ya Desemba 24 mwaka huu.
CHADEMA inamlalamikia mkurugenzi huyo kuingilia na kuvuruga uchaguzi huo uliofanyika Desemba 17 mwaka huu katika ukumbi wa jiji hilo la Mwanza.
Katika barua hiyo, iliyotolewa jana kwa vyombo vya habari na kusainiwa na Katibu wa CHADEMA mkoa wa Mwanza, Wilson Mushumbushi, imelaani Mkurugenzi huyo wa jiji la Mwanza, kwa kile kilichoelezwa kutoa taarifa za uongo katika ofisi ya Waziri wa TAMISEMI, kwamba madiwani wote wa jiji hilo wameshindwa kumchagua Meya na Naibu wake.
Kwa mujibu wa barua hiyo iliyotumwa kwa Waziri wa TAMISEMI, na kutolewa nakala kwa Katibu Mkuu wa CHADEMA, Msajili wa Vyama vya Siasa nchini pamoja na nyingine kwa Mkurugenzi huyo wa jiji la Mwanza, CHADEMA kinasema madiwani wa jiji hilo hawajawahi kushindwa kumchagua Meya na Naibu wake, bali Mkurugenzi ndiye aliyeshindwa kutimiza majukumu yake.
"Ni vema tukumbushane kuwa, Mkurugenzi kama Katibu wa mkutano wa madiwani kushindwa kufuata kanuni za kudumu kamwe hakuwezi kutoa baraka kwa hatua ambazo anawaza, ofisi yako (TAMISEMI), ichukue hatua, " inasema sehemu ya barua hiyo ya CHADEMA.
"Mkurugenzi wa jiji ni Katibu wa mkutano kwa mujibu wa tafsiri ya kanuni namba 2 ya halmashauri ya jiji la Mwanza ya mwaka 2003. Pia kifungu cha 24 (7), cha sheria ya Serikali za Mitaa na mamlaka ya miji na sheria namba 8 ya mwaka 1983 nayo inasema vivyo hivyo."
Aidha, katika barua hiyo, inamweleza Waziri Mkuchika kwamba CHADEMA kimesikitishwa na mkurugenzi wa jiji la Mwanza (Kabwe), baada ya kuitisha mkutano aliendelea kuwa mwenyekiti, Katibu na Msimamizi wa uchaguzi huo wa Meya na Naibu Meya.
Kutokana na hali hiyo, CHADEMA kimeiomba ofisi ya wa TAMISEMI kulichukulia hatua jambo hilo kwa umakini mkubwa, kwa kuzingatia sheria na kanuni za kudumu za halmashauri.
CHADEMA, imehoji juu ya Mkurugenzi huyo wa jiji la Mwanza kujihusisha na kile kilichoitwa udanganyifu na ubabaishaji kama huo, na kwamba taarifa hiyo iligusia pia matukio mbali mbali yanayosadikiwa kufanywa na Kabwe, likiwemo la kumtangaza aliyekuwa mgombea ubunge jimbo la Nyamagana na mbunge wa sasa, Ezekiel Dibogo Wenje (CHADEMA), kuwa siyo raia wa Tanzania.
Mkurugenzi wa Jiji hilo la Mwanza, Kabwe, alipoulizwa na Tanzania Daima Jumapili, kuhusiana na tuhuma hizo zilizoelekezwa kwake dhidi ya CHADEMA, alisema kwa kifupi: "Hizo tuhuma mimi sizifahamu, hata nakala ya barua yao sijaipata kwa hiyo siwezi kuzungumzia lolote kwa sababu nipo kikaoni muda huu."
Barua hiyo ameandikiwa Waziri wa Serikali za Mitaa.........Bw. John Nguchika...............
Wasiwasi wangu ni kuwa hivi Nguchika ni wa chama kipi? Je, anaweza kutenda haki hapo............na sheria zikoje................................nini nafasi ya NEC kwenye chaguzi hizo na mahakama zetu..................................
CHADEMA wamshtaki mkurugenzi wa Mwanza
na Sitta Tumma, Mwanza
Kabwe ameshtakiwa kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), George Mkuchika, kupitia barua yenye kumbukumbu CDM/M/MZ/04/77/10 iliyoandikwa na CHADEMA ya Desemba 24 mwaka huu.
CHADEMA inamlalamikia mkurugenzi huyo kuingilia na kuvuruga uchaguzi huo uliofanyika Desemba 17 mwaka huu katika ukumbi wa jiji hilo la Mwanza.
Katika barua hiyo, iliyotolewa jana kwa vyombo vya habari na kusainiwa na Katibu wa CHADEMA mkoa wa Mwanza, Wilson Mushumbushi, imelaani Mkurugenzi huyo wa jiji la Mwanza, kwa kile kilichoelezwa kutoa taarifa za uongo katika ofisi ya Waziri wa TAMISEMI, kwamba madiwani wote wa jiji hilo wameshindwa kumchagua Meya na Naibu wake.
Kwa mujibu wa barua hiyo iliyotumwa kwa Waziri wa TAMISEMI, na kutolewa nakala kwa Katibu Mkuu wa CHADEMA, Msajili wa Vyama vya Siasa nchini pamoja na nyingine kwa Mkurugenzi huyo wa jiji la Mwanza, CHADEMA kinasema madiwani wa jiji hilo hawajawahi kushindwa kumchagua Meya na Naibu wake, bali Mkurugenzi ndiye aliyeshindwa kutimiza majukumu yake.
"Ni vema tukumbushane kuwa, Mkurugenzi kama Katibu wa mkutano wa madiwani kushindwa kufuata kanuni za kudumu kamwe hakuwezi kutoa baraka kwa hatua ambazo anawaza, ofisi yako (TAMISEMI), ichukue hatua, " inasema sehemu ya barua hiyo ya CHADEMA.
"Mkurugenzi wa jiji ni Katibu wa mkutano kwa mujibu wa tafsiri ya kanuni namba 2 ya halmashauri ya jiji la Mwanza ya mwaka 2003. Pia kifungu cha 24 (7), cha sheria ya Serikali za Mitaa na mamlaka ya miji na sheria namba 8 ya mwaka 1983 nayo inasema vivyo hivyo."
Aidha, katika barua hiyo, inamweleza Waziri Mkuchika kwamba CHADEMA kimesikitishwa na mkurugenzi wa jiji la Mwanza (Kabwe), baada ya kuitisha mkutano aliendelea kuwa mwenyekiti, Katibu na Msimamizi wa uchaguzi huo wa Meya na Naibu Meya.
Kutokana na hali hiyo, CHADEMA kimeiomba ofisi ya wa TAMISEMI kulichukulia hatua jambo hilo kwa umakini mkubwa, kwa kuzingatia sheria na kanuni za kudumu za halmashauri.
CHADEMA, imehoji juu ya Mkurugenzi huyo wa jiji la Mwanza kujihusisha na kile kilichoitwa udanganyifu na ubabaishaji kama huo, na kwamba taarifa hiyo iligusia pia matukio mbali mbali yanayosadikiwa kufanywa na Kabwe, likiwemo la kumtangaza aliyekuwa mgombea ubunge jimbo la Nyamagana na mbunge wa sasa, Ezekiel Dibogo Wenje (CHADEMA), kuwa siyo raia wa Tanzania.
Mkurugenzi wa Jiji hilo la Mwanza, Kabwe, alipoulizwa na Tanzania Daima Jumapili, kuhusiana na tuhuma hizo zilizoelekezwa kwake dhidi ya CHADEMA, alisema kwa kifupi: "Hizo tuhuma mimi sizifahamu, hata nakala ya barua yao sijaipata kwa hiyo siwezi kuzungumzia lolote kwa sababu nipo kikaoni muda huu."