Chadema kulikoni? Utitiri wa Vyeo (Mpango madhubuti wa kulindana huku mkibomoa chama)

Status
Not open for further replies.

Mkuu Ben umenena vyema na kama kawaida mimi huwa nazikubali post zako. Kwa sasa Tanzania ina tatizo kubwa la ufisadi; lakini mkuu Ben umewahi kupitia Kamusi ya Kiswahili Sanifu na kudurusu maana ya ufisadi. Bahati mbaya sina citation hapa lakini kama una nafasi na una Kamusi ipitie uone maana ya ufisadi. Hii itasaidia kuwa na mijadala hai na kulitumia neno fisadi katika muktadha muafaka.

Ben Tanzania pia inasumbuliwa na ukosefu wa uadilifu. Kuna Dr. (PhD) wangu aliniambia kuwa kuna utafiti ulifanywa na kuonyesha kwamba 75% ya makampuni (taasisi) yamefanikiwa kwa sababu ya kuwa na wafanyakazi waadilifu. Unaweza ukawa na wafanyakazi wote ambao vyuoni walipata distinctions lakini kama si waadilifu kampuni haiwezi kufanikiwa. Uadilifu ni neno pana kweli (kunatofauti kubwa kati ya Honesty na Integrity). Kutokuwa mwaminifu katika mahusiano pia ni ukosefu wa uadilifu. Kama si mwaminifu kwenye mahusiano huwezi kuwa mwaminifu kwenye maeneo mengine (ni mawazo yangu tu). Pia kiongozi yeyote ni public figure na yuko subject to public scrutiny in his/her public life.

Ni vyema tukasisitiza tuwe na viongozi waadilifu. Walichokisema vijana hapa ni Rushwa ya Ngono; sijui kama kuna lugha nyingine zaidi ya hiyo.

Sitaki mtu aje hapa na mfano wa Billy Jaferson.
 
 

Mkuu wangu,

Kama utasoma post yangu tena utaona mahali nilikosizitiza kuhusu maadili.Nimesizitiza tupigania kubadili fikra na mfumo mzima unaoruhusu Kuwa na taifa lisilo adilifu.Pia mimi ni muumini mkubwa wa falsafa ya kama huwezi kuwa mwaminifu katika mambo madogo huwezi kuwa mwaminifu kwenye mambo makubwa.Ofcourse,infidelity consitutes the breach of trust and trust actually is a central character component of a good leader. Rejea mandishi ya cal thomas / infidelity and Leadership aliyoandika juu ya mgombea Urais Garry Hart na concubine mwanamama Donna Rice

Hata hivyo,post ya nuclear1 ilikuwa imekaa kuchafua watu tu.Siwezi kuwasemea wengine.Lakini mimi nazingatia uadilifu,na sijawahi kupenda kuwa promiscous naamini katika maadili.Ila pia nimetoa angalizo,tujadili ideas zitakazoondoa fursa kwa watu wasio na uaminifu katika social life kushika public office . Rejea tena maandishi ya Cal Thomas mkuu halafu rejea pia post yangu ya awali nilipomjibu nuclear1.Pia kuhusu tafsiri ya ufisadi,asante kwa ushauri na nitalizingatia hilo zaidi kwenye mjadala.
 
Mkuu hapo umeweka ***** mwingi sana, kwa bahati mbaya sina muda, ila ukiteuliwa kuwa Mkurugenzi kwa nafasi hiyo unakuwa mjumbe wa Sekretarieti hivyo sio sawa kutenganisha Ukurugenzi na ujumbe wa Sekretarieti, Mnyika pia ni mjumbe wa Kamati Kuu asiye na kura kutokana na nafasi yake ya kuwa Mkurugenzi ni ex official member, mengine mengi ni ***** tu sina muda, CDM ni chama makini soma katiba yake na kanuni utaelewa kwamba hatupeani vyeo kama sadaka.
 
Hivi kuwa mjumbe nako ni cheo? Ni vizuri CHADEMA ikawa na timu ndogo yenye tija. Ila huu ni uzushi mkubwa sana na huyu jamaa ni mharibifu. Kuwa na changamoto ni jambo jema, lakini CHADEMA iwe makini na habari zake kutoka kwa TUNTEMEKE
 

Hapa si suala la nyota ya mtu fulani kinachozungumzwa hapa ni suala la mtu mmoja kulimbikiziwa vyeo lukuki wakati wapo vijana wengi wenye uwezo kufanya kazi hizo mtake msitake huo si mgawanyo mzuri wa madaraka katika hali ya kawaida sisi wananchi mmetushtua mnathibitisha kuwa hiki chama cha watu fulani kwa manufaa yao kwa hali hii ni bora nichague CCM wanaonekana wanamgawanyo mzuri wa madaraka kuliko na wameimarika kidemokrasia kuliko CHADEMA ,NCCR au CUF hivi vinaonekana ni vyama vya watu fulani kwa masilahi yao binafsi na wala si kwa manufaa ya umma wa watanzania!
 
TUMTEMEKE ndugu yangu mpendwa, Kihoro chako kitakutoa mavi,

Hivi kweli Katibu wa wabunge dar unataka upewe wewe? hujui kuwa katibu wa wabunge dar wanachaguana wabunge wenyewe au ulitaka atoke ccm?

Hv mzigo anaopiga Mnyika ukipewa utaufikisha kweli? Kumbuka kuwa mtu anarundikiwa majukumu lukiki kutokana na jinsi wenzake wanayomwamini katika utebaji wake, na sio kupeaqna vyeo kwa kufurahishana.

Pia fahamu kuwa nyeo vingine vinaendana na nafasi aliyonayo kama Mbunge. Huwezi kupewa wewe? Hata yeye Mnyika angependa kupumzika lakini afanye je? Ndo kasha aminiwa hivyo!

BAdala la vivu tumwombee Myika kwa Mungu ili alisaidie Taifa hili kwa nafasi ya Urais kwa siku zijazo.

Mungu ibariki Tanzania, MUNGU mbariki MNYIKA JOHN
 
Ndg. Makandara nakupa BIG UP saana. Maelezo yako nayakubali 99% THANX
 
Yawezekana hili nalo lipo,ni comment iliyonitia nguvu kuwa kunawengi wanaojua maovu ndani ya chadema.Ngoja tupeleleze then tuje na data kamali juu ya huuu ufisadi.

Hayo maneno mkuu. Maumivu ya kichwa huanza polepole! Nilikuwa najiuliza siku zote. Hawa mashujaa ambao hukabiriana na risasi za moto wakiwa front line wako wapi? Nahisi hapa kuna tatizo kubwa kuliko hata CCM.
 

Topical pambaf!!!

Mbona hao wa Chama Cha Magamba wana vyeo lukuki kwa kila mmoja na hamuwasemi???Yaani kwa viongozi wa CDM kuwa na vyeo zaidi ya kimoja imekuwa nongwa???Hii ni kuonyesha kuwa mtu anapewa kushika madaraka au nafasi kutokana na uwezo wake kiutendaji. Hizi kelele zenu ni za wivu tu!

Hebu acheni hizo enyi wanafiki na wambeya!
 

Tusiwalaumu CHADEMA, ni halali kwao vyeo kupeana wachache hiyo yote kwa kuwa wana watu wachache wenye uwezo na sifa za madaraka. Walio wengi ni wafuasi wa kuandamana tu!!
!:shock::shock: Mtu kama Albedo alichozoea ni kushika bango wakati wa maandamano!!
 
By TUNTEMEKE

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) na umakini wa viongozi wake katika kuhakikisha kwamba vijana ni nguvu mabadiliko na wanauwezo wakuongoza na kulinda rasilimali za chama na mgawanyo wa madaraka.Sasa the top wa chama hicho wameamua kimyakimya kugawa madaraka/vyeo kwa watu wanaoona watatumika kulinda siri na mambo mbalimbali ya viongozi wa juu(zidumu fikra za Mwenyekiti)

Naweza kusema CHADEMA sasa imekomaa na kukua kuliko vile jamaa walivyokuwa wanategemea,kiasi kwamba imewawea vigumu kuukumbatia mbuyu huu wenye matawi yake karibia tanzania nzima.Hii imewapa wakati mgumu wamiliki wa chama namna gani wanaweza kulinda rasilimali zao na vyeo vyao....

Hao watu makini (tunaowaita sisi watanzania)wamekuja na mpango kabambe wa kuwagawia madaraka wale watu wanaoona watahakisha wanadumisha fikra za mwenyekiti

Naomba kutumia baadhi ya watu kama mifano tu...ilikuleta maana ya kile ninachokisema.

A.JOHN MNYIKA(Mbunge wa Ubungo)
Huyu ni mbunge wa jimbo la ubungo,amepewa majukumu ya fuatayo kuhakikisha nguvu ya vijana inaonekana.
1.Huyu ni mwenyekiti wa taasisi ya kiraia iitwayo ubungo foundation development.
2.Mwenyekiti wa CHADEMA mkoa wa kinondoni
3.Mkurugenzi wa vijana makao makuu ya CHADEMA
4.Katibu wa wabunge wa CHADEMA
5.Waziri kivuli wa nishati na madini
6.Mjumbe wa kamati kuu ya CHADEMA
7.Mjumbe wa sekretarait wa CHADEMA makao makuu
8.Kaimu katibu mkuu wa CHADEMA TAIFA
9.Mkurugenzi wa habari na uenezi wa CHADEMA TAIFA
10.Katibu wa wabunge mkoa wa Dar es salaam
Hivi huyu mtu anajigawaje katika majukumu yote haya,bila shaka ni kpenzi cha the top kwa sababu anadumisha fikra za mwenyekiti.

B.HEZEKIEL WENJE
1.Mbunge wa Nyamagana Mwanza
2.Mjumbe wa kamati kuu ya Chadema
3.Mjumbe wa sekretarait wa Chadema
4.Na sasa Katibu mkuu wa chadema amemteua kuwa mkurugenzi wa mambo ya nje wa chadema ambapo automatic anahudhuria vikao vya utendaji wa chama makao makuu...ambavyo karibia kila baada ya siku 2 mbili vinafanyika nainatakiwa ahudhurie,,,Jimbo lipo wazi pale mwanza kwa sababu muda wake mwingi yupo pale makao makuu kwenye vikao vya chama.

C.MWIGAMBA
1.Ni mwandishi wa gazeti la Tanzania Daima(freeman mbowe)
2.Ni mwenyekiti wa mkoa wa arusha
3.NI muhasibu wa chadema makao makuu
Huyu ameacha mkoa ukiwa hauna mwenyekiti(Dr.slaa analiona hilo) nakuitwa kuja kusimamia fedha za chama(uhasibu wa chadema makao makuu)Hadi dakika hii Arusha hapana mwenyekiti wa mkoa wa chama.

D.BENSON MLAMBA
1.Katibu wa CHADEMA mkoa wa tanga
2.Afisa wa habari wa chadema makao makuu
Huyu ameondolewa tanga kuja pale makao makuu kwa sababu za kusaidia kukumbatia mbuyu usiguswe na watu wengine.Ameacha mkoa wa tanga bila kuwa na katibu...huku Dr. akijua kwamba mkoa wa tanga hatuna diwani wala mbunge na chama kina suasua,Kwa mantiki hiyo huyu mtu alikuwa nakazi ya kujenga chama pale tanga.

MY TAKE:
Kumbuka hakuna chama chenye vijana wasomi na wenye utashi/uthubutu mkubwa wa kufanya mambo katika tanzania hii kama CHADEMA.....Lakini hili si rahisi kuliona Dr.slaa kwa sababu vijana waliowengi wameshatumika kwenye mbio za uchaguzi mkuu na sasa hawana thamani tena ndani ya chama hiki.
Kuna vijana wengi sana wamejitolea kujenga chama na wengine wameshapoteza degree zao kwa sababu wanakipenda chama.Wengine wamethubutu kuingia katika vinyang'anyiro mbalimbali vya udiwani,ubunge na wengine wamekuwa wakijitolea kuratibu kampeni mbalimbali za CHADEMA lakini kwa sasa nikama makarai mabovu ya kujengea nyumba.

Je?Kama chadema bado hawachukua dola wamesahau vijana wao,itakuwaje wakishika dola?
Au huu ndio ule mkakati madhubuti wa kulinda na kula keki ya chama watu wa chache huku mkiweka MORANI(tajwa) pembezoni msiguswe?.

Najua kunawatakao tukana na kukejeli kwa sabubu wamepofoka na mapenzi yao juu ya chama,huku wakijisahau kuwa chadema kinamapungufu yake hasa katika matumizi ya rasilimali watu(vijana) na kuwa dampu kama taka.

a. Mnyika ana uroho wa madaraka na hii ni hatari huwezi kusema no please..unajua vyao hadi 10 lol..

b. Mnyika ameziba nafasi 7 muhimu za vijana wengine kuonyesha uwezo wao...na ajira pia..

c. Mnyika either ana uwezo sana au ni kwamba ni yes man..vyeo zaidi ya 10?

conclusion: Nimesahau kumbe tunaongelea chagga development manifesto..lol

Mzazi Shetani aliyendani yako anakusumbua sana hii ya mwisho inahuska vipi unataka kueneza chuki tu Myika ni mchagga?
 

Mkuu achana na huyo jamaa mimi nafikiri kunakitu alitegemea kukipata pale chadema amekikosa labda kwa sababu ya majungu yake , uwezo mdogo au hana mvuto sasa ameamua kupandikiza chuki na majungu mimi natamani sna wamtaje huyu mtu kwani hafai na anatakiwa kutegwa kama anaukoma.
Ni kweki chama kinatakiwa kukosolelewa lakini siyo kwa staili hii ya kuattack mambo ya pesornal kwanini asiwambie privite anakuja kuanika hapa.
 

Vyeo gani hivyo Mkuu?
 

lipu kafu
 
Ben,
Kuna mahala nimekusoma ukisema hivi:- Nachotaka mimi kuelewa ni perspective gani nyie vijana mnazo ambazo hazifungamani na old ones?. Nachokiona ni unafiki mkubwa wa vijana, vijana wetu wanatumiwa zaidi kutumikia kambi za kina EL, JK, Seif, Lipumba, Mbowe, Dr.Slaa na kadhalika while hawa wote hawana jipya la kumkomboa Mtanzania tofauti na msimamo wa vyama vyao. Nyote kwa ujumla wenu mnatumikia vyama na itikadi zake.

Ikiwa vijana mnashindwa kuja na new ideas ila mnataka kutumia ujana wenu ku discredit wazee kwa kutumia kabila au dini.. Hii kweli ndio sifa mnayotaka sisi wazee tuwakubali kwamba mnaweza kuongoza nchi ilihali nyie wenyewe mna makabila na dini zenu!. Nani anapingana na mfumo wa elimu na Afya iliyopo..Nani anapingana dhidi ya jinsi wakulima, miners, na wafanyakazi wanavyo nyanyaswa na kusukumwa chini zaidi kuwa ngazi za matajiri?..

Jamani hata Ukapteni wa team ya mpira hupewa mwenye sifa na uzoefu ambao kauonyesha na experience matters. hadi sasa hivi mnashindwa kutuonyesha zaidi ya Zitto wakati ule kuonyesha msimamo wake juu ya posho na sii vijana wote wanaafiki.

Mimi nauliza nyie vijana what do you bring on the table?..Ni fikra zipi mpya mlonazo, maana nawaona mkibishana sana juu ya Ufisadi wengine mkisema Ufisadi sio tatizo bali tatizo ni uzalishaji. Ni mawazo sawa kabisa na wazee sioni tofauti yoyote baina ya vijana na wazee ikiwa upeo wenu wote unaishia palepale.. Utazalisha vipi ikiwa kila unachopanda kinakuwa sabotage.. Na hakuna kijana hata mmoja anayepiga vita Ufisadi kwanza ili tukija panda mimea ikue na tuvune kilicho bora. Wote mmejipanga nyuma ya JK, RL na wengineo kwa nini sisi wananchi tusiwaamini hao hao mnaowasujudia?
 
Kaka umekurupuka kuleta hii hoja yako hapa.Bila kuwa na sirikali kwenye Uongozi wowote ule daima kutakuwa na misuguano.Naomba tu nikushauri ufuatilie japo kwa kuadithiwa tu ni kwa jinsi gani Umoja wa Sovieti ulisambaratika na kwa nini Siasa za Urusi kwa sasa zimetawaliwa na Putin tu......T 2015 CDM.......
 
Unanambia mimi?
 

Mkuu Mkandara,

Asante sana kwa mchango wako.Wachanijisemee na nisiwasemee wengine.

1.Kwenye chama cha siasa ninapenda kuunga mkono itikadi.Kwa hali iliyopo Tanzania vyama vyetu vina mapungufu kwenye itikadi hasa kuhusu mfumo wa uchumi ambao ni kigezo kinachotoa muongozo wa aina ya Siasa nchi inafanya na uongozi kwa ujumla.Nikiwa mwanachama wa Chadema naona itikadi ya chama changu ni nzuri kulinganisha na itikadi za vyama vingine hata tuki-fanya modification hatutapata shida sana ukilinganisha na vyama vingine

2.Ukiniona naunga mkono mtu au kambi (kambi ni jambo la kawaida wakati wa uchaguzi kwenye vyama vya siasa) basi ujue naunga mkono kile anachosimamia kulingana na itikadi ninayoamini kwamba inaweza kutuondoa kutoka level moja kwenda nyingine.

3. Ninaamini tufikie hatua vijana sasa tuwashinikize wenzetu na kuwatia moyo tuachane na siasa za matukio.Suala la posho ni tukio,kiongozi wangu na rafiki yangu Zitto Kabwe alilipigania kutokana na kuona kwamba mfumo wa uongozi na itikadi inayozalisha viongozi au wawakilishi walafi kwa gharama ya walipa kodi utachukua muda kuurekebisha.Roho ilimuuama kuona watanzania wanaendelea kugharamia anasa za wawakilishi wetu huku wao wa kiteseka katika kupata huduma stahiki za kijamii.Hata hivyo,tatizo la posho kama nilivyosema ni tukio/tunda la mfumo mbovu.

Nilifurahi kuona vijana wenzangu kama akina January na Nape ingwa ni kutoka chama tofauti na changu wakiunga mkono hoja aliyoisimamia Zitto.

4. Mabadiliko tunayopigania yamekuwa yakitafsiriwa vibaya kwamba ni kuiondoa CCM.Kumbe kuiondoa CCM ni kama kuondoa tu kikwazo kilichoko mbele ya safari yetu kuelekea kwenye mabadiliko.Kuiondoa CCM ni kuruhusu uwanja mpana wa kuleta mageuzi makubwa ya kifikra ambayo in turn yatatusaidia katika kujenga taifa adilifu,linalowajibika.Ni kweli vijana wengi sasa hivi hasa wasomi na wanasiasa vijana hawajadili tatizo katika wizara ya Elimu au Afya kwa kujenga hoja na kuzishindanisha dhidi ya Itikadi fulani baina ya chama kimoja na chama kingine au baina ya kiongozi mmoja dhidi ya Mwingine

5. Wakati sisi tunafikiria miaka 2 au mitatu ijayo na kujenga mawazo/fikra tegemezi kama viongozi hatujui kwamba tunajenga taifa lenye fikra tegemezi.Ni kama kwenye corporate world,director anatoa dira ya kampuni na subbordinates wake.The smartness of directors determines the growth and success of the company.

Hatujui kwamba wenzetu mataifa ya Ulaya na Asia wote wanaweka mikakati na fursa za miaka 100 ijayo kwa ajili ya wajukuu kujinufaisha na raslimali za Afrika ikiwemo Tanzania.Waliopo sasa ulaya wanatunyanyasa kiuchumi kutokana na furasa walizowekewa na babu zao mwaka 1900's. Sisi tunajadili matukio.

Mkuu Mkandara,Tunafanya maandalizi ya kutoa darasa la itikadi kupitia taasisi ya wanafunzi wanachama wa chadema wa sekondari na vyuo vikuu (CHASO). Vijana wengi ni wanafiki kutokana na njaa,hawaamini kama wanaweza kuwa succesfully bila kujipendekeza na kupata visenti vichache.Haya yote ni matokeo ya mfumo mbovu ambao tunatakiwa kupambanan nao.Mfumo wa kuunga watu mkono bila principles ndiyo huu unaotujengea fikra tegemezi,ufisadi,kukosa maadili majungu nk.

Unategemea kijana anayegeuzwa kibaraka wa kiongozi fulani kwa ajili ya vijisenti,siku akikutana na majaribu ya Marekani au taifa lolote la magharibi (ofcourse hawajawahi kuwa na nia njema na Afrika,ingawa diplomacy inanikataza kutamka haya ila siyo Rhetorics) kumfanya awe shushu/kibaraka kwa malipo ya madola na magari ya kifahari aache?Je,kwa mazingira haya uzalendo na uhuru wa taifa hauko mashakani?

Tunachofanya sasa ni maandalizi ya kupambana kubadilisha mfumo,we need a very radical reform based on Ideologies.We need radical reform socially,politically and Economically. We nee catalyse change, to change the attitude hasa unapokuwa ndani ya chama cha siasa.Tuandae mazingira ya kuunda responsible government,responsible policy and responsible Nation

No responsible government can afford to produce and abandon graduates to roam the streets, for we know that such attitude will force them into crime as a way of earning a living. We need device methods of taking statistics on the number of graduates turns out every year. This will enable us to provide employment opportunities and meaningfully engage them in other positive areas of livelihood. Our commitment to gainful employment will have the vulnerable groups particularly the youth and women as the main targets.

We were suppose to therefore bring to reality the small and medium scale industries that will engage our youths and women so as to enable them achieve economic empowerment and self reliance. Every single person willing to work should be able to get job training that leads to a job and earn a decent living

Tanzania's problems goes beyond probing past leaders. I think we need a generational shift that will bring about a re-orientation of our national psyche which should place value on service rather than looting. The political office is so attractive now because its an avenue to share the Natural resources money and even loot the treasury without any opposition. Imagine servicing a single Mp as a stting allowance 300,000 + more than 7m per month salary. This is crazy. Yet the country is laden with poverty stricken masses. We need the change.

We will appeal to our youth to see this as a call to change. Its high time we sideline the money bags and old corrupt politicians and take our destiny in our own hands. Lets put hands together and support a worthy cause....Hayo na mengine mengi....!
 
Tuko pamoja. Ila pia mkuu sikugusia suala la Nuclear1 kwa makusudi kabisa; nilijikita zaidi kwa Ryntemeke, PAA na TII ambao wametoa sindano za moto.
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…