Bornvilla
JF-Expert Member
- Feb 17, 2011
- 924
- 271
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) wamepanga kuandamana tarehe 24 Februari, 2011.
Maandamano hayo yanayotarajiwa kua ufuasi mkubwa sikuhiyo kutokana na chama hicho kuwa na wafuasi na wapenzi wengi jijini hapa. Viongozi wa juu wa CHADEMA wanatarajiwa kuongoza maandamano hayo yaliyopangwa kuanzia stendi ya Buzuruga na kuishia kwenye uwanja wa wazi wa Furahisha uliopo Kirumba jijini hapa. Lengo kuu la maandamano hayo ni pamoja na kushinikiza Rais Kikwete ajiuzulu, kupinga mambo mbalimbali kama kupanda kwa gharama za umeme, kupinga ufisadi, kupinga DOWANS kulipwa na kuongezeka kwa gharama za maisha.
Kutokana na ughali wa maisha nchini maandamano hayo huenda yakasimamisha shughuli nyingi mjini na watu kwenda kuunga mkono maandamano hayo yanayotarajiwa kuanza mishale ya saa nne asubuhi. Wimbi hili la maandamano huenda likaenea mikoa yote ambayo ina wafuasi wengi hasa wa upinzani.
Maandamano hayo yanayotarajiwa kua ufuasi mkubwa sikuhiyo kutokana na chama hicho kuwa na wafuasi na wapenzi wengi jijini hapa. Viongozi wa juu wa CHADEMA wanatarajiwa kuongoza maandamano hayo yaliyopangwa kuanzia stendi ya Buzuruga na kuishia kwenye uwanja wa wazi wa Furahisha uliopo Kirumba jijini hapa. Lengo kuu la maandamano hayo ni pamoja na kushinikiza Rais Kikwete ajiuzulu, kupinga mambo mbalimbali kama kupanda kwa gharama za umeme, kupinga ufisadi, kupinga DOWANS kulipwa na kuongezeka kwa gharama za maisha.
Kutokana na ughali wa maisha nchini maandamano hayo huenda yakasimamisha shughuli nyingi mjini na watu kwenda kuunga mkono maandamano hayo yanayotarajiwa kuanza mishale ya saa nne asubuhi. Wimbi hili la maandamano huenda likaenea mikoa yote ambayo ina wafuasi wengi hasa wa upinzani.