CHADEMA kilichofanyika Monduli ni unafiki mkuu

Danstan Nicholaus Diwani wa Kamachumu na yeye kaenda CDM mkuu, Lembeli naye kafanya hivyo ndugu..Diwani wa Nata Nzega na yeye kaamua hivyo..Kangi Lugola na Dada wa bunda soon wanatika huko.So punguza povu dada angu maana Singida, Manyara na kwingineko wapo njiani...
Kigumu chama cha Mapinduzi.

Siyo jambo la ajabu waliomshabikia kwa uwazi Mtume wa 'Safari ya Matumaini' kusoma alama za nyakati na kujiondoa mapema CCM kwa hofu tu kwamba nafasi zao za uongozi walizokuwa nazo kwa sasa ziko mashakani. Hivyo tutawasikia na kuwaona wengi wakihama.
 
Sisi tunaanza na MUNGU na tunamaliza na MUNGU, mtu akiwa CCM lazima awe mchafu na lazima tumseme sana ili atoke jalalani, akishatoka jalalani na kujisafisha tunamkalibisha sebuleni kama mwana mpotevu aliyerudi kundini,

Madiwani wa monduli wamegundua CCM hakuna haki ccm hakuna demokrasia na sio hao tu, hata Nape akigundua ukweli na anataka kuwa mwadilifu milango ipo wazi

Wewe! mnaanza na mungu au Mungu? Mna uadilifu gani wa kuwafundisha mafisadi waliokatwa kwa demokrasia huru. Nyie muwasombe tu pamoja ila mda si mrefu mtarudi hapa kusema 'Nyoka ni nyoka tu hawezi badilika' hata hivyo wapo watakaorudi na potential information za kuwavuruga kisiasa.
 
CCM itaangukia pua maeneo yenye nguvu ya Lowassa
- itashindwa vibaya Arusha na Manyara sababu ya influence ya lowassa
- itaangukia pua mkoa wa shinyanga sababu ya nguvu ya Hamis mgeja- muumini wa Lowassa
- itaangukia pua Simiyu kutokana na nguvu ya Nzoka ya Malyenge -Andrew chenge
-hali in mbaya Kagera sababu ya Karamagi na Tibaijuka
-hali tete Ruvuma nguvu ya nchimbi
Hali tete Geita kijana Msukuma amenuna

Endeleza orodha

aa wapi? ccm ni wanasiasa na wamekomaa kweli ndo maana walimkata EL, wanaokimbia HUKU NA KULE hawatawanyima kuingia ikulu. HATA MAJIMBONI NAONA MTASALITIANA TU.
 
Mtume Mohammad (SAW) katika moja ya hadithi zake aliainisha tabia kuu tatu za mtu mnafiki.

Kwanza, mtu mnafiki akizungumza husema uongo.

Pili, mtu mnafiki akiahidi hatekelezi

Tatu, mtu mnafiki akiaminiwa hufanya hiyana.

Chama cha Demokrasia na maendeleo (CHADEMA) kimetuonesha sifa hizi za mnafiki dhahiri kwenye sakata hili la kuwapokea kwa mbwembwe madiwani waliotoka CCM Monduli.

Madiwani hawa wametoka CCM kufuatia kukatwa jina kwa Waziri mkuu 'mstaafu' Edward Ngoyai Lowassa kwenye kinyang'anyiro cha kuwania kuteuliwa kugombea nafasi ya urais kwa kupitia CCM.

Kitendo cha kuwapokea madiwani hawa kwa mbwembwe tena huku pakitumika maneno kama "safari ya matumaini bado inaendelea" ni kitendo cha fedheha sana kwa chama.

Wakati Zitto Kabwe akiondoka/ akiondolewa CHADEMA tuliona wale walioamua kuondoka nae walivyoitwa kila jina baya mitandaoni na hata baadhi ya viongozi walijitokeza kuwakandia waziwazi.

Tumeona namna gani Edward Ngoyai Lowassa alivyotukanwa kila tusi na viongozi wa CHADEMA. Ameitwa mwizi, fisadi, , mnyang'anyi na majina mengine mengi. Na hata wafuasi wake 4u movement tuliona walivyopewa maneno mabaya humu.

Tumeona viongozi wa CHADEMA wakiponda tabia ya kupokea wanachama waliokimbia vyama kwa sababu ya migogoro ya kimaslahi mara kwa mara.

Kwa hayo machache najiuliza hivi yale maneno ya kuponda watu yalijitokeza sababu walihama CHADEMA? Kumbe kuhama ni kosa lakini kuhamia ni sahihi? Kumbe hawa wafuasi wa Lowassa walikuwa wachafu walipokuwa CCM lakini wakiwa CHADEMA ni wasafi? Hivi mtu akija CHADEMA anasamehewa dhambi??

Tabia ya kuyarudi maneno yenu imekuwa ya kawaida sana lakini kwa hili sasa mmejifedhehesha sana. Miaka michache iliyopita mliwaita CUF kila jina baya mara CCM B, mara vibaraka, mara mas**ga nk lakini baada ya muda mkaungana nao na kuunda UKAWA. Mlimfukuza Kafulila kwa mbwembwe lakini leo mpo nae UKAWA huku mkimsifu.
Sitashangaa kesho mkiungana na ACT ili tu mtimize malengo yenu.

CHADEMA tambueni mlichokifanya ni kitendo cha hovyo mno, mmewaonesha watanzania mlivyo walaghai na opportunist wakubwa. Mmeonesha kila tabia za kinafiki na kizandiki na msivyo na msimamo.

Tabia kama hizi zitawafanya ikulu muisikie redioni tu na kuishia kulalamika kwamba mnaibiwa kura kumbe mnajihujumu wenyewe.

Watu wanajifanya wanasiasa wakati siasa hawaijui. Leo hii Chadema wanaonekana wanafiki kwa kuwapokea wanachama wa CCM, lakini pale Senzo alipohama Chadema na kujiunga na CCM hakuna aliyesema kuna unafiki. Tushasikia hapa baadhi ya viongozi wa Chadema Mbeya warudisha kadi za Chadema na kujiunga na CCM, hakuna aliyesema kuna unafiki, tushasikia Machali amehama NCCR na kujiunga na ACT, wala hakukuwa na unafiki, leo viongozi wa CCM wilaya ya Monduli wamejuinga na Chadema tena wenyewe wana sababu maalumu, tayari kuna unafiki. Mnasahau kitu kimoja muhimu kwamba mtaji wa chama cha siasa ni watu (wapiga kura) serikali imeshindwa kuwaondoa wakazi wa Jangwani pamoja na hatari zote zilizopo kwa sababu wakazi wa Jangwani ni mtaji wa baadhi ya wanasiasa, hivi ni chama gani kinaweza kumkataa mwanasiasa maarufu asijiunge nacho halafu kikategemee ushindi, hakuna kitu kama hicho.

Lowassa ana wafuasi zaidi ya milioni mbili ni chama gani cha siasa kinaweza kikamkataa asijiunge nacho ilihali kinajua kwa mtaji wake kinaweza kikavuna zaidi ya wabunge 50 na madiwani kibao, wabunge 50 utakisaidia chama kujipatia zaidi ya sh 500,000,000/- kila mwezi kama ruzuku, ni chama gani hakitaki heshima na fedha, na unafiki hapo unakujaje. Kwenye siasa ndivyo kilivyo hakuna rafiki wala adui wa kudumu.
 
Wajinga wachache bado awa amini yanayo tendeka. wamelala waache wakija kubumburuka au jogoo kuwika tutakuwa mjengoni.lala kiongozi
 
wewe! mnaanza na mungu au Mungu? Mna uadilifu gani wa kuwafundisha mafisadi waliokatwa kwa demokrasia huru. Nyie muwasombe tu pamoja ila mda si mrefu mtarudi hapa kusema 'Nyoka ni nyoka tu hawezi badilika' hata hivyo wapo watakaorudi na potential information za kuwavuruga kisiasa.
Demokrasia huru!!??..loool give me a break!...unavomuweka Magufuli,Migiro na mama mzenji unategemea nani atashinda?...kulikuwa na haja ya kura hapo?....wangemuweka Lowassa Membe Magufuli na labda Makamba ndo wapigiwe kura na wale watu elfu mbili na kitu hapo ndo ningekubaliana na wewe....but this trush can never be called democracy....Wazee wa chama ndo waliomchagua Magufuli kukiokoa chama chao na kujilinda wao......so pliz spare that word democracy from that nomination process....bye
 
Usijipe umungu usiokuwa nao eti kamwe CHADEMA haiwezi kuingia Ikulu. Chadema haina uongozi madhubuti wamejaa ukanda na bado CHADEMA inatikisa nchi nzima na kila siku mnaomba CHADEMA ife lakini haifi ng'o na ndiyo inazidi kupata umaarufu mkubwa kila kona nchini na kuvutia Watanzania wa kila rika, dini na rangi. Wewe na elimu yako ya shule mulugo endelea kutokwa na povu zito kuonyesha chuki zako za kutisha dhidi ya CHADEMA.

Kamwe ni ndoto cdm kuingia ikulu. Kwa wabunge watapata. Bado hawana uongozi mathubuti. Mwenyekiti wao amejaa ukanda mno, pia wapo kimaslahi sana na waongo kweli kweli.
 
Usijipe umungu usiokuwa nao eti kamwe CHADEMA haiwezi kuingia Ikulu. Chadema haina uongozi madhubuti wamejaa ukanda na bado CHADEMA inatikisa nchi nzima na kila siku mnaomba CHADEMA ife lakini haifi ng'o na ndiyo inazidi kupata umaarufu mkubwa kila kona nchini na kuvutia Watanzania wa kila rika, dini na rangi. Wewe na elimu yako ya shule mulugo endelea kutokwa na povu zito kuonyesha chuki zako za kutisha dhidi ya CHADEMA.

Mimi siyo msomi. Naukosoa uongozi wa chadema kwani unaelekea kuua chama. Wajirekebishe. Kwani hata sisi CCM si nyie mlikuwa mnasubiri tumpendekeze Lowasa kugombea ili mtucheke!!
 
Chadema dhambi ya ukanda itawamaliza. Badilikeni ohooo alafu muache unafiki.
Leo mbwa amegeuka halal sio nyie mlimuita najisi??
 
Sasa hivi Watanzania tunataka mtu atakayeondoa mfumo mbovu wa ccm, awe fisadi au asiwe fisadi maana mfumo huu hata mtu awe na rekodi nzuri akishaingia kwenye ccm si mzuri tena.

Ndiyo maana unaona mtu akiwa ccm ni fisadi tu. Hata Lowasa kama anauwezo wa kuiangusha ccm tunamkaribisha upinzani ilimradi tu huu mfumo utoke kwanza tuanze upya.

Tumechoshwa na utawala wa kinafiki na kizandiki wa ccm na ndiyo maana mtu yeyote anayeweza kuitoa ccm hata kama ni Boko haram au al shababu tutamuunga mkono ilimradi tu huu utawala uende kuzimu.

Duh! Nimekuelewa
 
Chilli;

Kwanza mimi napenda niongeze neno Sauce mbele ya jina lako ili lisomeke Chilli-sauce ile tunayotumia tunapokula chips mayai. Ulichoongea hapa hakina mashiko asilan. Usifikiri kuwa kuanza na gea ya habari za Mtume Mohamed(SAW) basi watu watakubaliana na wewe. Huo ni upuuzi.

CHADEMA hawajafanya kosa lolote katika kuwapokea wimbi la wana-CCM wanaohamia CHADEMA kwa sasa siyo Monduli tu baali nchi nzima baada ya kuona kuwa CCM imeshindwa kufuata misingi na haki kulingana na kanuni za chama katika kuteua mgombea wa Urais. Hakuna dhambi wala kuvunja taratibu na sheria kulingana na Katiba unapompokea mwanachama toka chama kingine au anapohama. Baba wa Taifa aliwahi kusema CCM SI BABA YAKE kwa hiyo swala la kuhama chama liko wazi na huru kwa yeyote na wakti wowote.

Swali dogo kwako Bwana Chillisauce. Je, umewahi kuwauliza hao Vigogo na Wazee wako wa CCM waliokata jina la Lowassa walikuwa na maana gani walipowatangazia Wana-CCM kwamba watachagua jina la mgombea ANAYEKUBALIKA NDANI NA NJE YA CCM? Walikuwa wanamdanganya nani? Yaelekea bado kuna wapuuzi ndani ya chama chenu wanaofikiri Watanzania wa sasa ni sawa na wale wa miaka ya 19 kweusi! Sahau hilo.

Lowasa ana haki ya kutafuta chama kingine chochote anachoona kina sera nzuri kama CHADEMA ili aendeleze mapambano yake akiwa nje ya CCM. Ukweli utabaki kwenye historia kuwa Edward Ngoyayi Lowasa amenyang'anywa haki yake ya kuwa mgombe ndani ya CCM kwa sababu ya mizengwe ya kijinga ya watu kutaka kuweka mtu wao asiyekubali ndani wala nje ya chama. Nani hajui kuwa Lowasa alikuwa anakubalika ndani na nje ya chama? Je, unataka kutuambia Mapombe na Mende walikuwa wanakubalika ndani na nje ya CCM kama siyo uhuni???

Naomba unisikilize kwa makini bwana Chilisauce, kwamba kuhama chama au kurudi kwenye chama siyo kosa wala dhambi.Tofautisha mtu anayefanya UHAINI au USALITI ndani ya chama kama alivofanya rafiki yako Zito Kabwe wa kutaka kupindua uongozi uliopo na kuchukua madaraka pasi kufuata taratibu za chama. Huyu havumiliki lazima atimuliwe. Hapa hakuna cha unafiki. Labda nikukumbushe kuwa haya yanafanyika hata ndani ya chama Twawala CCM.Mifano hai ni kama ya kina Mzee Nassoro Moyo sliyefukuzwa juzi pale Unguja na Mahafidhina wa CCM kwa vile tu alikuwa akitetea maslahi ya Wazanzibar. Wakamtimua.

Lakini pia kuna Vigogo wa CCM ambao wamewahi kuhamia vyama vya upinzani na bado wakarudi CCM na kupokelewa kama mashujaa na hivi juzi walikuwa ni moja ya wanaotangaza nia ya kuingia Ikulu. Kwa uchache ni Steven Masato Wassira na Makongoro Nyerere waliowahi kutimkia NCCR wakapewa Ubunge na baadaye kurudi CCM walipopewa Ubunge na Uwaziri na juzi wakaruhusiwa kuchukua fomu za kuwania kuingia Ikulu. Je, hapa nani mnafiki zaidi ya CCM?

Kwenye siasa hakuna adui wa kudumu. Bado kuna msemo unaosema ALIYE UPANDE wetu ni mwenzetu. Ssa kama Lowasa na Kingunge pamoja na wafuasi wao wameamua kuahmia CHADEMA ili waendeleze mapambano nje ya CCM ni ruksa. Tatizo lako ni kwamba kufikiri kwako na uwezo wa kuchanganua mambo ni mdogo sana na shida ni kwamba nyie watu mnaoegemea sana mafundisho ya SAW kwa elimu ya Madras huwapotosha sana na kuwafanya mzidi kuwa watu wa kupiga hadithi maana mafundisho kwenye vitabu vyenu kumejaa hadithi tupu na hakuna ukweli wowote.

Pole sana.

Me nimekuelewa sana na nimeupenda uchambuzi wako mahili ila jinsi ulivyomalizia umeharibu lakn nje ya hapo safi
 
Sijasoma mada yote naona umelalamika tu. Inavoonekana wewe ni wale wa kupigwa tu. Jiongeze akili kwenye siasa hakuna rafiki wa kudumu au adui. Kwani MTU aki slim huwa unamuuliza tena na kumhukumu maisha yake ya awali? Acha uchochezi aliyekutuma mwambie akale malimao.

Kwa hali hii CHADEMA ni chama hatari sana.
Kwa hiyo nyie hata chenge akija kwenu ni poa tu, alimradi ame'silimu' hakuna haja ya kujua maisha yake ya nyuma.
 
Watu wanajifanya wanasiasa wakati siasa hawaijui. Leo hii Chadema wanaonekana wanafiki kwa kuwapokea wanachama wa CCM, lakini pale Senzo alipohama Chadema na kujiunga na CCM hakuna aliyesema kuna unafiki. Tushasikia hapa baadhi ya viongozi wa Chadema Mbeya warudisha kadi za Chadema na kujiunga na CCM, hakuna aliyesema kuna unafiki, tushasikia Machali amehama NCCR na kujiunga na ACT, wala hakukuwa na unafiki, leo viongozi wa CCM wilaya ya Monduli wamejuinga na Chadema tena wenyewe wana sababu maalumu, tayari kuna unafiki. Mnasahau kitu kimoja muhimu kwamba mtaji wa chama cha siasa ni watu (wapiga kura) serikali imeshindwa kuwaondoa wakazi wa Jangwani pamoja na hatari zote zilizopo kwa sababu wakazi wa Jangwani ni mtaji wa baadhi ya wanasiasa, hivi ni chama gani kinaweza kumkataa mwanasiasa maarufu asijiunge nacho halafu kikategemee ushindi, hakuna kitu kama hicho.

Lowassa ana wafuasi zaidi ya milioni mbili ni chama gani cha siasa kinaweza kikamkataa asijiunge nacho ilihali kinajua kwa mtaji wake kinaweza kikavuna zaidi ya wabunge 50 na madiwani kibao, wabunge 50 utakisaidia chama kujipatia zaidi ya sh 500,000,000/- kila mwezi kama ruzuku, ni chama gani hakitaki heshima na fedha, na unafiki hapo unakujaje. Kwenye siasa ndivyo kilivyo hakuna rafiki wala adui wa kudumu.

Mnahubiri nini na huu ni utumbo gani umeandika?
Usiniletee mboyoyo za CCM na ACT, jiangalie kama chama, kama CHADEMA.
Yaani leo umtaje mtu fisadi kesho umuingize chamani kwa sababu ana mtaji wa wafuasi? Chama cha siasa kisichoweza kusimamia kinachokihubiri ni hatari kuliko ukoma.
 
pokeeni makapi
kazi yetu ya ccm sasa ni kuchuja pumba na mchele
kwa hili michele inajulikana na pumba zinajulikana
hayatusumbui hayo
 
Back
Top Bottom