Chilli
JF-Expert Member
- Jul 17, 2011
- 1,655
- 743
- Thread starter
- #241
Mkuu Kwanza nikupongeze kwa kuwasilisha na kuchanganua mawazo uliyonayo. Binafsi baada ya kuyasoma nami naomba pia niwasilishe mawazo yangu. Siku zote nguo inapochafuka inahitaji maji safi na sabuni ili iweze kufuliwa na kutakata. Nije sasa kwenye mada, kuhusu kilichotokea Monduli ambapo madiwani wa ccm wamerudisha kadi zao. Tukio hili lilitokea pale chadema walipokuwa kwenye harakati za kutokomeza ccm kaskazini. Hivyo basi, baada ya kusikiliza sera za Chadema na kujiona wao ni wachafu kama nguo zinazohitaji maji Safi na sabuni ndio maana walichukua hatua ya kufanya hivyo. Kuhusu unafiki sijaona kama Kuna unafikiri wowote maana kila mtanzania ana haki ya kuhamia chama chochote akipendacho ili mradi tu atimize haja yake ya kisiasa. Nawasilisha.
Kwanza hongera kwa kutoa hoja yako kistaarabu, hila shaka hapo BAVICHA utakuwa unategemewa sana.
Back to the topic, hawa jamaa ni jana tu walikuwa wanaitwa wezi, nyang'anyi, jambazi. Leo wanaitwa makamanda kisa tu taratibu zilizotumika kumtoa mtu wao hawajakubaliana nazo, huoni huu kama ni unafiki mkubwa. Halafu tusidanganyane, hawa jamaa hawajakubaliana na sera zozote za CHADEMA, hawa ni majeruhi wa kisiasa hawahitaji sera wanafhoangalia ni maslahi.
CHADEMA mmekuwa mstari wa mbele kupinga "umalaya" wa kisiasa, nikikumbuka kipindi cha Zitto, Kafulila na hata juzi juzi kwa Mzee Arfi, huoni kwamba kuwakupokea hawa jamaa kwa mbwembwe hivi ni kula matapishi yenu??
Edward Lowassa, mmekuwa mkimwita mwizi na fisadi, je hawa jamaa wameshawaeleza kama Bwana wao alishaacha huo wizi na ufisadi?
Unajua kinachotuchosha wengi sio nyinyinkuongeza wanachama bali ni aina ya wachama mnaowaongeza, kumbe hata "shetani" akiwa na uwezo wa kuwapeleka ikulu nyinyi mko tayari kuungana nae??