CHADEMA ina wasaliti wengi

CHADEMA ina wasaliti wengi

Wasema wewe, siyo lazima kuwapigia makofi Slaa na Mbowe ili nionekane kuwa ni mwanachadema. Wapo maaskari, viongozi wa serikali wanaunga mkono harakati za chadema bila kujionyesha. Kuna kuwa shabiki ili uonekane kwa watu kuwa wewe ni mwanachadema, wengine chadema iko kwenye damu

Mkuu husiangaike kubishana na mtu hasietaka kuelewa maana mwishowe wote mtaonekana mko sawa, kuna watu kwa akili zao wamaamini kuwa kama ni mwanachama mwaminifu wa CDM hutakiwi kuhoji chochote, ukioji unaitwa msaliti na matusi kibao
 
Nyie chadema hebu jiulizeni kama CCM wangekamata waraka wa kumtoa kiongozi unadhani wangefuata hatua kama mlizochukua nyie za kuuanika mitandaoni? Lengo ilikuwa nini hasa kama sio kuwadhalilisha baadhi ya viongozi wenu wenyewe?
 
Lema mmoja ni bora kuliko wana-CHADEMA wa kawaida 10,000!

mkuu, haya ni matusi makubwa kwa wanachama wa 'kawaida' CDM....I wonder kama umetafakari au umelipuka tu kama huyo lema mwenyewe!? by the way yeye ni bora kwa vigezo vp?? mie ni mwanaCDM wa kawaida tu kama ulivyotulebo lakini nakuhakikishia lema ni moja kati ya viongozi wetu wa hovyo kabisa kupata kutokea na kuingia mjengoni - actually ni kielelezo kimojawapo kati ya mapungufu makubwa ya neno 'demokrasia'!!!!!!! 2015 ningependa CDM ishinde kiti cha ar mjini, ila maombi yangu ya dhati isiwe lema awe mwengine mwenye kujitambua, kujenga hoja na kuzitetea kwa manufaa ya wana ar na tz kwa ujumla. Ni dokeze hoja moja tu aliyoisimamia bungeni hadi sasa, na nna uhakika hadi kipindi chake kiishe hawezi kufanya hivyo zaidi ya kuvizia maandamano tu ili asikike!!!
 
Nyie chadema hebu jiulizeni kama CCM wangekamata waraka wa kumtoa kiongozi unadhani wangefuata hatua kama mlizochukua nyie za kuuanika mitandaoni? Lengo ilikuwa nini hasa kama sio kuwadhalilisha baadhi ya viongozi wenu wenyewe?

mkuu hongera umeona mbali sana - inaonekana kuna wajumbe walikuwa na mihemko ya kufa mtu ndani ya ukumbi bila tafakuri ya kina - ndo maana wengine tunataka kujua wajumbe ya cc wanapatikanaje?! imani yetu baadhi ni kwamba moja kati ya sifa kuu za mjumbe wa cc ni kuwa na hekima na busara, sasa mdau tafakari mwenyewe mjumbe kama lema anayerushie wenzie vitofali kwenye mkutano wa mkoa tu nn ilikuwa reaction yake cku hiyo??!! kwa watu wenye akili timamu waraka ule umeanika mambo mazito sana na kuna uwezekano mkubwa ni ya kweli haswa ikizingatiwa wahusika walikuwa ni viongozi waandamizi ndani ya chama - sasa chama 'kisimezee' kitoe majawabu ya kina na vielelezo vya kutosha kuna wanachama tusiokuwa mashabiki tunataka kujua ukweli.
 
Vi thread vingine bwana...Haya tumeshakiona ulichoandika nenda kakojoe ukalale...!!
 
lukosi una alegena CHADEMA kama CCM amkiogopi chadema mbona kila kukicha mko mitandaoni amuzungumzii ahadi za JK
kumaliza mgao wa umeme
kutengeneza reli mpya ya kisasa
kuboresha elimu(ufaulu usio ridhisha)
kupunguza foleni dar esalaam
kuboresha haki mahakamani
maisha bora kwa kila MTANZANIA

KUBWA ZAIDI KUNGOA WATU KUCHA NA NCHEMBA NA NCHIMBI KUSHILIKI KATIKA MAUAJI YA DR MVUNGI
 
Kwa hili la CDM Vs ZZK, nmeamini siasa ni mchezo mchafu sana! hakuna mtetezi wa wanyonge wa kweli bali woote wanaangalia maslahi yao tu!
 
mkuu, haya ni matusi makubwa kwa wanachama wa 'kawaida' CDM....I wonder kama umetafakari au umelipuka tu kama huyo lema mwenyewe!? by the way yeye ni bora kwa vigezo vp?? mie ni mwanaCDM wa kawaida tu kama ulivyotulebo lakini nakuhakikishia lema ni moja kati ya viongozi wetu wa hovyo kabisa kupata kutokea na kuingia mjengoni - actually ni kielelezo kimojawapo kati ya mapungufu makubwa ya neno 'demokrasia'!!!!!!! 2015 ningependa CDM ishinde kiti cha ar mjini, ila maombi yangu ya dhati isiwe lema awe mwengine mwenye kujitambua, kujenga hoja na kuzitetea kwa manufaa ya wana ar na tz kwa ujumla. Ni dokeze hoja moja tu aliyoisimamia bungeni hadi sasa, na nna uhakika hadi kipindi chake kiishe hawezi kufanya hivyo zaidi ya kuvizia maandamano tu ili asikike!!!

Msamehe bure kulinganisha Lema na watu 10,000 nahisi akili ni punguwani
 
Kwa mtu yeyote ambae ni mwanaCHADEMA wa dhati hawezi kuandika hiki ulichokiandika na hiki hakina tofauti na maandiko ya matamko tunayoyasoma kila siku kutoka maeneo mbalimbali ambayo yanatolewa na MASALIA, WASALITI, WAHAINI na WACHUMIA TUMBO ni vema na wewe ukajiweka wazi na kuonyesha unajivua uanachama au ushabiki ili tukuelewe.

kwahiyo alitakiwa aseme fukuza ZITTO ndo anakuwa wa ukweli ? kazi kweli kweli -sikuwa najua kumbe hutakiwi kuwa na mawzo mbadala_aisee ndo maana vijana wanawaiteni MISUKULE
 
Melody ya zitto makapi imechuja kiasi cha kwamba mtu anaanzisha thread anajijibu mwenyewe poleni kwa maumivu jamaa kwisheny nguvu anayotumia lazima awe mwehu mpaka sasa
 
Mtaweweseka sana CDM ni kiboko ya wasaliti,mamluki na wachumia tumbo wengine.eti kila mtu anajifanya mwanacdm na matamko kedekede,upuuzi mtupu! Hakuna mwanacdm mwenye akili za kuku anayeweza kushabikia wasaliti,wahaini na mamluki.
 
Yote yatajidhihirisha kwenye chaguz mbalimbali zijazo, chadema tulikipenda sana lakini ukabira, ukanda, uroho wa madaraka na kung'ang'ania uongozi unakisambaratisha ndo maana magamba wanakata mbuga kuongea na wananchi wakati chadema wako busy kuchakachuwa waraka feki ili kushawishi wananchi kuwa kamati kuu ya CDM ilifanya uamzi sahihi kuwafukuza ZITTO. Naumia sana maana ndoto za kuondoa mafisadi naona zinayeyuka, niliamini 2015 magamba watakiona cha mtemakuni sasa ndoto zinayeyuka taratibu, uamzi huu utakipasua chadema vipande vipande na tunaanza kuona matokeo yake kwa baadhi ya viongozi kujiuzuru na wengine kuhama chama.

Mawe yote yatapinduliwa.shetani hawezi kukaa na Mungu.wasaliti lazima wafukuzwe kama mbwa wakapigie kelele zao kuzimu.
 
kwahiyo alitakiwa aseme fukuza ZITTO ndo anakuwa wa ukweli ? kazi kweli kweli -sikuwa najua kumbe hutakiwi kuwa na mawzo mbadala_aisee ndo maana vijana wanawaiteni MISUKULE

Ahsante kwa majibu matamu mkuu. Ni aibu kwa vijana ambao wanafuata mkumbo na kusema NDIYO MZEE ya dr Slaa na Mbowe
 
Hivi ni kambi îpi inawafurahisha na kuwanufaisha CCM zaidi?
Lema na kamati ya CC wanaona bora waikose Ikulu kuliko kumwachia nafasi Zitto anayetuhumiwa kukihujum chama.

Na kwa upande wa Zitto na tuhuma zake zote zinazoelekezwa kwake, tuchukulie kuwa ni za kweli 100 percent.

Je nani anainufaisha CCM?
 
Acha haki itendeke, mbivu na mbichi zitajulikana baada ya siku 14. Kama tunarudi Mwandiga au tunabaki Dar itajulikana baada ya siku 14
 
Back
Top Bottom