CHADEMA ina wasaliti wengi

CHADEMA ina wasaliti wengi

Mboko

JF-Expert Member
Joined
Oct 8, 2010
Posts
1,095
Reaction score
293
Leo njama za kuwagawa watu kwa misingi ya ukabila, zimeshindikana baada ya propaganda za CCM kudai CHADEMA ni chama cha Wachaga. Udini umeshindikana baada ya tuhuma za kuihusisha CHADEMA na Ukatoliki kufeli. Mbinu iliyobaki ni kuwanunua viongozi.
Mkakati huu umeanza siku nyingi, sasa ndipo mambo yameanza kujifunua baada ya waraka wa kina Zitto, Dk. Kitila na Samson Mwigamba kubainika.

Hawa ni sehemu tu, wako wengi walishakamata mshiko na kufanya mazungumzo ya kupewa ubunge wa kuteuliwa, ukuu wa wilaya na nafasi nyinginezo serikalini baada ya kukamilisha mkakati wa kuivuruga CHADEMA.

Kama nilivyotangulia kusema kuwa Watanzania wapenda mageuzi na nchi yao hawawezi kukubali CHADEMA ikafa kibudu kwa sababu tu ya kuwalea wasaliti wanaochuma rushwa kwa ajili ya matumbo yao, ukweli sasa umedhihiri, wasaliti wasakwe popote na kutoswa.
Watu wamekufa, wamemwaga damu, wamebaki vilema kwa kipigo cha mitutu ya dola wakati wakiimarisha CHADEMA, nani anaweza leo kuendelea kuwaonea haya wala rushwa na walevi wa madaraka eti wakisambaratishe chama CCM ipumue?

Ni kweli Mbowe na Katibu wake Mkuu, Dk. Willibrod Slaa, hawaiongozi CHADEMA milele, lazima wakati utafika wataondoka, lakini kwa mtu makini na mwana mageuzi asingeweza kutunga waraka wa kifisadi kuwachafua wakati wamekiletea chama mafanikio makubwa.
Kwa wasaliti wote na wapenda rushwa na vyeo vya kununuliwa na watawala ebu soma hapa kisha linganisha historia ya watu hawa.
Dk. Kitila anatoka mkoani Singida katika Jimbo la Iramba Magharibi linaloongozwa na Mwigulu Nchemba.

Katika Uchaguzi Mkuu uliopita, sijui alikisaidiaje chama chake kupata ushindi mkoani kwake, lakini CHADEMA iliambulia jimbo moja la Singida Mashariki la Tundu Lissu na madiwani wachache sana. Zitto alikuwa Naibu Katibu Mkuu, kati ya majimbo manane ya Mkoa wa Kigoma kwenye Uchaguzi Mkuu uliopita, alikiwezesha chama chake kushinda jimbo moja la kwake la Kigoma Kaskazini, lakini halmashauri yake inaongozwa na CCM.

NCCR-Mageuzi mkoani humo iliipokonya CCM majimbo manne ya Kigoma Kusini, Kasulu Mjini na Vijijini na Muhambwe, halafu CCM akaambulia Buyungu, Kigoma Mjini na Kibondo. Mbowe ambaye anatengenezewa zengwe la kuondolewa madarakani na vibaraka wa CCM, amekisaidia chama chake kupata majimbo matatu ya Hai, Rombo na Moshi Mjini pamoja na kuzoa madiwani wengi.

Hivi sasa Halmashauri yake ya Hai inaongozwa na mwenyekiti kutoka CHADEMA, Moshi Mjini inaongozwa na Meya wa CHADEMA, wakati Moshi Vijijini, CHADEMA na TLP zimegawana madaraka kwa vile zina madiwani wengi. Dk. Slaa anatoka Arusha, pamoja na kwamba aligombea urais lakini Jimbo lake la Karatu aliloliongoza kwa vipindi vitatu alifanikisha kulitetea chini ya Mchungaji Israel Natse, Jimbo la Arusha Mjini ni la CHADEMA na Arumeru Mashariki pia.

Karatu kwa Dk. Slaa halmashauri hiyo tangu mfumo wa vyama vingi kurejeshwa inaongozwa na CHADEMA, Arusha Mjini ilipaswa kuwa ya CHADEMA japokuwa CCM ilichakachua uchaguzi na hata majimbo ya mkoani Arusha mengine wana madiwani wengi. Kwa mfano huo mdogo unaweza ukatafakari mwenyewe kuwa hawa wanaotaka kuchoma nyumba yao wenyewe ndani ya CHADEMA lengo lao ni kuleta mabadiliko gani?

Wanataka kujenga misingi ya udini, ukabila, ulevi wa madaraka au rushwa ya kuhodhi mali nyingi zisizo na maelezo? CHADEMA bado ina wasaliti, iwaondoe mapema. Tafakari! ''MAKALA HII FROM EDSON KAMUKARA''Niliipenda sana ndio maana nikachukua kipande hiki.
 
Kuna watu mbalimbali wamenitumia PM kuhusu ni akina nani hasa ambao ni wajumbe wa kamati kuu ya CCM Taifa , na kwa kuwa jukwaa kwa siku kadhaa limekuwa na mjadala mzito kuhusu CHADEMA na maamuzi yake , naona ni vyema nikawaweka hapa kwa ajili ya kujulishana na kuelimishana.


1. Mhe. Jakaya Kikwete
2. Mhe.Dr. Ali Mohhamed Shein
3. Philip Mangula
4. Abrahaman Kinana
5. Ali Vuai
6. Mwigulu Nchemba
7 .Dr.Asha RoseMigiro
8. Zakhia Meghji
9. Nnape Nnauye
10. Seif Khatib
11.Pandu Kificho
12. Anne Makinda
13.Dr.Gharib Bilal
14. Seif Idd
15.Mizengo Pinda
16.sophia Simba
17. Sadiffa JUMA
18. Abdalah Bulembo
19. Dr.Salim A.Salim
20. Prof. Makame Mbarawa
21. Dr. Hussein Mwinyi
22.Maua Daftari
23. Khadijah Aboud
24. Samia S.Hassan
25. Shamsi Vuai
26. Prof.Anna Tibaijuka
27. Emmanuel Nchimbi
28.Stephen Wassira
29. Willium Lukuvi
30. Pindi Chana
31. Alhamisi Adam Kimbisa
32.Jerry Silaa
 
Kwa kifupi nasikia hata Dr Slaa ni msaliti kwani bado ana kadi ya CCM chama dume
 
CDM itakuwa inatoa mfano!! ya uthabiti wa washika dola wa kesho!! CCM walishindwa kuwatambua wasaliti tangu zamani ndiyo maana hadi sasa ina kizazi cha FISIWATU wanaitafuna nchi bila huruma!!
 
Tukishakamilisha mchakato wa kumshughulikia Zitto tutakuwa tumedhoofisha mtandao wa wasaliti woote chadema
 
Last edited by a moderator:
hongera kwa kuonesha acknowledgement ya makala haya. kuhusu ujumbe huo wahusika wanajua cha kufanya
 
dr slaa anapenda kubaki na kadi ya ccm kama souvenir. tafuta majibu ya maswali haya tusaidiane
  1. je bado anaendelea kulipia hiyo kadi?
  2. je bado anaendelea kuhudhuria vikao vya chama kwa ngazi walau ya tawi lake?
 
Hakuna mtu alie CHADEMA ambae ajapitia CCM kama ni usaliti ni kwa CHADEMA mzima tusijidanganye eti hata wakina Slaa ni wasaliti tu.
 
Hakuna mtu alie CHADEMA ambae ajapitia CCM kama ni usaliti ni kwa CHADEMA mzima tusijidanganye eti hata wakina Slaa ni wasaliti tu.

Nakumbuka huyu jamaa anamiliki kadi ya CCM. Nakumbuka pia kuna wakati kulikuwa na vuguvugu la kutaka kumshinikiza aache kadi ya CCM lakini aligoma. Kwangu mie huyu ni Msaliti nambari moja. Ni sawa sawa na Mke ambaye amevalishwa pete ya ndoa na mume. Baada ya kuachana na kuolewa na mume mwingine, anang'ang'ania kuivaa hiyo pete ya ndoa kwenye kidole kimoja na ile aliyovalishwa na mume huyu wa pili. Ni umalaya, usaliti na ulaghai ulioje hapo
 
nakumbuka mwalimu wangu wa uchumi galitushawishi sana tujiunge na ccm, alitupa kadi na tulipiga kampeini na kumuaingiza mukulu kwa asilimia 80! kumbe mwalimu alikuwa deal ya kugombea ubunge anakotoka, aliambulia kura 2 tu! hapa naona nikweli watu wapo kwenye chama fulani si kwa kupenda mageuzi ni uroho tu!
 
Ritz na chama wanasema Chadema ni Chama cha Ukoo, wanasahau au wanatumika bila kujijua.

Jakaya Kikwete
Salma Kikwete
Ridhiwani Kikwete
Halfani Kikwete

Wote hawa ni wajumbe wa NEC, Chombo cha juu kabisa cha maamuzi cha CCM

Waligombea au waliteuliwa?
 
Yote yatajidhihirisha kwenye chaguz mbalimbali zijazo, chadema tulikipenda sana lakini ukabira, ukanda, uroho wa madaraka na kung'ang'ania uongozi unakisambaratisha ndo maana magamba wanakata mbuga kuongea na wananchi wakati chadema wako busy kuchakachuwa waraka feki ili kushawishi wananchi kuwa kamati kuu ya CDM ilifanya uamzi sahihi kuwafukuza ZITTO. Naumia sana maana ndoto za kuondoa mafisadi naona zinayeyuka, niliamini 2015 magamba watakiona cha mtemakuni sasa ndoto zinayeyuka taratibu, uamzi huu utakipasua chadema vipande vipande na tunaanza kuona matokeo yake kwa baadhi ya viongozi kujiuzuru na wengine kuhama chama.
 
Yote yatajidhihirisha kwenye chaguz mbalimbali zijazo, chadema tulikipenda sana lakini ukabira, ukanda, uroho wa madaraka na kung'ang'ania uongozi unakisambaratisha ndo maana magamba wanakata mbuga kuongea na wananchi wakati chadema wako busy kuchakachuwa wara feki ili kushawishi wananchi kuwa kamati kuu ya CDM ilifanya uamzi sahihi kuwafukuza ZITTO. Naumia sana maa ndoto za kuondoa mafisadi naona zinayeyuka, niliamini 2015 magamba watakiona cha mtemakuni sasa ndoto zinayeyuka taratibu, uamzi huu utakipasua chadema vipande vipande na tunaanza kuona matokeo yake kwa baadhi ya viongozi kujiuzuru na wengine kuhama chama.

pole sana mkuu kwa maumivu hiki chama kilianzishwa kilaghai kwahiyo kisingeweza kudumu kwa mda mrefu kwenye siasa ni chama cha kundi fulani la watu.
 
Maccm bwana! Yaani yanahaha kuijenga chadema simuhamie hata Tlp? Kha! Et chama changu sasa simumchukue kwani lazima akae chama Makini cha CHADEMA? Hatakiii.nukta
 
Yote yatajidhihirisha kwenye chaguz mbalimbali zijazo, chadema tulikipenda sana lakini ukabira, ukanda, uroho wa madaraka na kung'ang'ania uongozi unakisambaratisha ndo maana magamba wanakata mbuga kuongea na wananchi wakati chadema wako busy kuchakachuwa wara feki ili kushawishi wananchi kuwa kamati kuu ya CDM ilifanya uamzi sahihi kuwafukuza ZITTO. Naumia sana maa ndoto za kuondoa mafisadi naona zinayeyuka, niliamini 2015 magamba watakiona cha mtemakuni sasa ndoto zinayeyuka taratibu, uamzi huu utakipasua chadema vipande vipande na tunaanza kuona matokeo yake kwa baadhi ya viongozi kujiuzuru na wengine kuhama chama.

Kwa mtu yeyote ambae ni mwanaCHADEMA wa dhati hawezi kuandika hiki ulichokiandika na hiki hakina tofauti na maandiko ya matamko tunayoyasoma kila siku kutoka maeneo mbalimbali ambayo yanatolewa na MASALIA, WASALITI, WAHAINI na WACHUMIA TUMBO ni vema na wewe ukajiweka wazi na kuonyesha unajivua uanachama au ushabiki ili tukuelewe.
 
Back
Top Bottom