CHADEMA ina wasaliti wengi

CHADEMA ina wasaliti wengi

Hivi ni kambi îpi inawafurahisha na kuwanufaisha CCM zaidi?
Lema na kamati ya CC wanaona bora waikose Ikulu kuliko kumwachia nafasi Zitto anayetuhumiwa kukihujum chama.

Na kwa upande wa Zitto na tuhuma zake zote zinazoelekezwa kwake, tuchukulie kuwa ni za kweli 100 percent.

Je nani anainufaisha CCM?
Jiungeni na CHAMA CHA KIGOMA CHAUMMA mnalia lia nini? ZITTO na Kafulila walishaanzisha CHAMA na kumpa Mkigoma Mwenzao si mjiunge?!! Ili muone kuwa kwa unafiki wenu kinaishia KIGOMA?
 
Ndugu wana JF, siamani kabisa kama inawezekana kuwa hivi:

  • Viongozi hawakutaki unasema mimi sielewi
  • wanachama hawakutaki unasema mimi sisikii
  • umefukuzwa kwa utaratibu wa sheria bado unasema hiyo siitambui na wala sitaitambua
  • ukiwa nje ya chama bado unaendelea kujishughlisha kama wewe mwanachama hai

Jamain CDM kweli unapendwa!!! Na si siri ni kwa sababu ya kuwa na viongozi wasionunulika!!!

Tusonge mbele!

 
Chadema inatangazwa kwa mema au mabaya... Iko kinywani mwa kila mwana CCM... Kila mbaguzi wa kanda anaisema, kila mbaguzi wa kabila anaisema, kila mbaguzi wa dini anaisema, kila fisadi anaisema, viongozi na wafuasi wa masalia wanaisema.
 
Najaribu kufikiria huu mnyukano hatima yake ni nini kwa chadema tusaidiane ndugu zangu. Watu wengine wamesimama na kutoa malalamiko na vitisho kwa viongozi wa juu wa chadema ya kwamba wasifike baadhi ya mikoa na kadhalika. Je, huu ndo mwisho wa chama hiki. Ni kweli hakuna/kuna kosa kwa walioadhibiwa?
 
MaCCM Bwana utayajua tu......

Anyway ndio imeshatokea......amevuliwa uongozi na baada ya siku si nyingi yeye pamoja na mpuuzi mwenzake Kitila watapigwa chini moja kwa moja....


Mkuu time will tell lakini tunatakiwa kuzuia mabaya yasitokee CHADEMA wengi mnapuuzia kila anaetofautiana mawazo na Mbowe, Slaa na wengine imekuwa wimbo kuitwa mhaini, traitor, masalia, msaliti... Tutumie akili zetu dont let your mind to be under their control, tumia utashi wako na uwe huru wa mawazo... As i said time will tell kwa sasa porojo nyingi lakini athari itaonekana next year unless the differences btn ZITTO and the top leaders are settled
 
Yote yatajidhihirisha kwenye chaguz mbalimbali zijazo, chadema tulikipenda sana lakini ukabira, ukanda, uroho wa madaraka na kung'ang'ania uongozi unakisambaratisha ndo maana magamba wanakata mbuga kuongea na wananchi wakati chadema wako busy kuchakachuwa waraka feki ili kushawishi wananchi kuwa kamati kuu ya CDM ilifanya uamzi sahihi kuwafukuza ZITTO. Naumia sana maana ndoto za kuondoa mafisadi naona zinayeyuka, niliamini 2015 magamba watakiona cha mtemakuni sasa ndoto zinayeyuka taratibu, uamzi huu utakipasua chadema vipande vipande na tunaanza kuona matokeo yake kwa baadhi ya viongozi kujiuzuru na wengine kuhama chama.

Wewe mwanachadema gani usiejua utaratibu wa chama chetu?
Ni marufuku kukosoa chama hata kama kuna ukweli,tukijua kadi yako lazima tukufukuze wewe utakuwa gamba tu,
 
Mleta Uzi utakuwa gamba.ungekuwa cdm ungekuwa proud na maamuzi yaliyofikiwa na chama, maamuzi yanayo onyesha tofauti ya cdm na ccm.ccm walishindwa kufanya maamuzi makubwa kama haya,wakaishia kulamba viatu vya mafisadi.salsa we we badala ya kuipongeza cdm kwa kusimamia misingi yakatiba,ndiyo uhuzunike?
 
Wewe mwanachadema gani usiejua utaratibu wa chama chetu?
Ni marufuku kukosoa chama hata kama kuna ukweli,tukijua kadi yako lazima tukufukuze wewe utakuwa gamba tu,

Hahahaa ndicho kinachoendelea ndugu yangu
 
Back
Top Bottom