SIJASHANGAZWA na kinachoendelea mitandaoni na kusambazwa na Maria Sarungi na chombo chake cha habari kilichopo huko Kenya juu ya wanasiasa wa Kenya hasa wabunge kuongelea na kukosoa uchaguzi wa Tanzania.
Hawajaanza leo! Walianza wakati ule wa kesi ya Lissu, pale Kisutu wakakodisha wanaharakati kuja Tanzania kufanya uchochezi lakini kwa umakini wa hali ya juu sana wa vyombo vya usalama wa Tanzania walizuiliwa kuingia nchini na kurudishwa kwao na wale walioingia wanajua nini kiliwapata na walikoma kurudia tena upuuzi ule.
Hawakuishiwa hapo,walikwenda mbali zaidi ambapo sasa Maria Sarungi na kundi lake wakakodisha na kulipa watu mitandaoni na kuanza kutukana viongozi na hasa Rais Samia.