CHADEMA imelinda heshima ya Sosopi

Nchi nzima ni zaidi ya majimbo 235 ambayo Sosopi anatakiwa kuyasimamia.

Msigwa kanda ya Nyasa ana simamia majimbo 33
kwa msingi huu Sosopi kwa cheo chake cha makamu mwenyekiti BAVICHA Taifa.

Ni mkubwa zaidi kiutendaji na kimamlaka kiliko msigwa. Msigwa ambae ni Mwenyekiti mpya kanda ya Nyasa ana simamia majimbo 33 katika eneo lake la kimamlaka.

Hivyo Msigwa ni mdogo sana kimamlaka.
Sosopi akiwa na ziara kanda ya Nyasa, Msigwa lazima awepo na kuandaa ziara ya makamu Mwenyekiti BAVICHA taifa.

Sosopi ni kiongozi wa kitaifa na Msigwa ni kiongozi wa kanda. Sasa kuenguliwa kwa Sosopi katika kugombea nafasi ya kanda ni katika kumpa heshma kubwa sana.

Pia chama kimetambua majukumu makubwa na heshma aliyo nayo Sosopi. Sosopi kimajukumu anatakiwa aishi DSM kuwa karibu na ofisi kuu za chama je kanda itakuwa ofisi yaendeshwaje?

Msigwa yuko Iringa na anaishi Iringa hivyo atakuwa mtu sahihi kuwa Mwenyekiti wa kanda kwakua anaishi kanda ya Nyasa muda wake mwingi.

Chama kimefanya busara za kiutendaji kumuengua Sosopi abakie na majukumu yake ya sasa ya BAVICHA.
Ahahahaha! Hii kali!
 
Ilipaswa UKUTA nao uhusike ndani ya CDM, maana kwa mtindo huu ni wazi katiba imesiginwa kwa kisingizio cha 'maamuzi ya busara'.

Ila haya yote Mbowe anayafanya kutokana na aina ya wanachama alionao. Ukiwa na wanachama makini basi maamuzi yote yatafanywa kiumakini, ila mburula/maamuma wakiwa ni wengi basi matokeo yake ndio kama hayo unawaburuza unavyotaka na bado watashangilia maamuzi yako.
 
..Ole Sosopi angechaguliwa mashambulizi kwamba cdm inapendelea watu wa "kaskazini" yangepamba moto.

..sikubaliani na siasa za kikabila , lakini ni ukweli usiopingika kwa siasa hizo zipo hapa Tz, na ni mtaji mkubwa kwa CCM.

Cc Gamba la Nyoka

Mkuu hayo ndo Matakwa ya Democracy.
Na kumbe kelele za Ccm ndo zinakua msingi wa Maamuzi ya Cdm?
Kumbe ni sahihi Mh. Alipozuia mikutano maana ana nia njema ya kuinyoosha nchi na hata kelele za kumyumbisha.
 
Hivi waliotangaza kuwa maisha ni magumu sana mabasi yamepaki hamna abiria wa kusafiri, wanajisikiaje kuona watu wamekosa mabasi ,na wengine wakidandia coaster kwa nauli mara mbili.

Aibu ya kufungia mwaka hii.
 
mbona tulisha jua, ajenda ya mbowe ni kukwepa makada ya lowasa kuwa wajumbe wa baraza kuu, kwa kuwa sasa mbowe haliziki na uwepo wa lowasa
 
Hivi siyo nyie kila siku humu na kwenye vyombo vya habari mlikuwa mnapiga kelele kuwa Rais anakanyaga katiba ya nchi?!! Inakuwaje Mbowe anakanyaga katiba ya chama mnachekelea? Hivi mna akili timamu kweli?!
Muwe mnajichunguza kwanza kabla ya kulalama!? Charity begins at home... Mheshimu katiba na demokrasia kuanzia chamani ili muwe na legitimacy ya kusema hata nje!
Hayo mkazungumzie huko kwenu maamuzi yaliyofanywa yamezingatia mambo Mengi sana kwa akili yako ndogo huwezi kujua
 
Acha uongo na unafiki, tupo naye kila siku Iringa, labda kama kuna dar ya Iringa.
Na si muongo tu bali ni juha kabisa wabunge wa Ccm ndiyo wanoishi dar hiyo ni toka zamani mpaka sasa ndiyo maana hata nyumba tu hawana hapa Iringa tofauti na Msigwa hajawahi ishi dar kama ambavyo wamekudanganya waliokwambia
 
Sasa kwanini mnampinga Rais akifanya ivo kwa maendeleo ya taifa.

..kwangu mimi katiba za vyama hazina uzito kama Katiba ya NCHI.

..hata ccm wakifanya mambo yao ya ndani kwa maslahi ya chama chao siwezi kuwapinga.
 
Du! Nyie wazee mna mahaba na unafiki sana...
Mbowe akikacha katiba ni sawa na unaipamba kabisa kuwa ni kutumia busara ikitokea pande ya pili ni udikteta, kweli wa Tz ni wa Tz tu.

..hapana.

..Magufuli akifanya maamuzi kinyume na katiba ya ccm hutanisikia nikimpinga.

..kwangu mimi katiba ya NCHI ina uzito kuliko katiba za vyama vya siasa.

..lakini hata katiba za vyama zinapokiukwa ni lazima nijiridhishe na sababu za kufanya hivyo.

..kwa suala la Ole Sosopi naamini angepitishwa tuhuma za cdm kupendelea wenyeji wa kaskazini zingepamba moto. Kazi ya kukijenga chama kanda ya ziwa Nyasa ingekuwa ngumu zaidi.



Cc runyaga
 
..YES.

..kama hali halisi inalazimisha hivyo ili kukiwezesha chama kuongeza ushawishi ktk kanda ya Nyasa.
Basi namna tena moral authority ya kuikosoa ccm au Magufuli kwamba wanasigina demokrasia...unafiki siyo mzuri kabisa
 
..hapana.

..Magufuli akifanya maamuzi kinyume na katiba ya ccm hutanisikia nikimpinga.

..kwangu mimi katiba ya NCHI ina uzito kuliko katiba za vyama vya siasa.

..lakini hata katiba za vyama zinapokiukwa ni lazima nijiridhishe na sababu za kufanya hivyo.

..kwa suala la Ole Sosopi naamini angepitishwa tuhuma za cdm kupendelea wenyeji wa kaskazini zingepamba moto. Kazi ya kukijenga chama kanda ya ziwa Nyasa ingekuwa ngumu zaidi.



Cc runyaga

Ukianza kusigina katiba ya chama chako kwa maslahi binafsi kitu gani kitakuzuia kusigina katiba ya nchi kwa maslahi binafsi? Acheni unafiki nyie wazee
 
sosopi na mwenyekiti wako wa BAVICHA mmepoa sana tofauti na kipnd cha ndg HECHE,vjana hamzunguki kuwaelimisha vjana kwa kuwapa elimu ya uraia sijui kwa nn? na niny mmesha anza kuiga matamko ya wazee wa chadema na kuwa kimya kama mhako vile'
 
Basi namna tena moral authority ya kuikosoa ccm au Magufuli kwamba wanasigina demokrasia...unafiki siyo mzuri kabisa

..na kwanini cdm wahangaike kuikosoa ccm ktk masuala yao ya ndani ya chama chao?

..Katiba ya NCHI ina uzito kuliko katiba za vyama.

..tusijaribu hata kidogo kuziweka katiba hizo ktk mizani moja.
 
..Ole Sosopi angechaguliwa mashambulizi kwamba cdm inapendelea watu wa "kaskazini" yangepamba moto.

..sikubaliani na siasa za kikabila , lakini ni ukweli usiopingika kwa siasa hizo zipo hapa Tz, na ni mtaji mkubwa kwa CCM.

Cc Gamba la Nyoka
Kwani Sosopi anatoka Kanda ya kaskazini? Ninyi ndo walewale
 
..na kwanini cdm wahangaike kuikosoa ccm ktk masuala yao ya ndani ya chama chao?

..Katiba ya NCHI ina uzito kuliko katiba za vyama.

..tusijaribu hata kidogo kuziweka katiba hizo ktk mizani moja.
Kama MTU hawezi kuheshimu cha kwake ataheshimu vipi cha wrote/wengine?
 
Nchi nzima ni zaidi ya majimbo 235 ambayo Sosopi anatakiwa kuyasimamia.

Msigwa kanda ya Nyasa ana simamia majimbo 33
kwa msingi huu Sosopi kwa cheo chake cha makamu mwenyekiti BAVICHA Taifa.

Ni mkubwa zaidi kiutendaji na kimamlaka kiliko msigwa. Msigwa ambae ni Mwenyekiti mpya kanda ya Nyasa ana simamia majimbo 33 katika eneo lake la kimamlaka.

Hivyo Msigwa ni mdogo sana kimamlaka.
Sosopi akiwa na ziara kanda ya Nyasa, Msigwa lazima awepo na kuandaa ziara ya makamu Mwenyekiti BAVICHA taifa.

Sosopi ni kiongozi wa kitaifa na Msigwa ni kiongozi wa kanda. Sasa kuenguliwa kwa Sosopi katika kugombea nafasi ya kanda ni katika kumpa heshma kubwa sana.

Pia chama kimetambua majukumu makubwa na heshma aliyo nayo Sosopi. Sosopi kimajukumu anatakiwa aishi DSM kuwa karibu na ofisi kuu za chama je kanda itakuwa ofisi yaendeshwaje?

Msigwa yuko Iringa na anaishi Iringa hivyo atakuwa mtu sahihi kuwa Mwenyekiti wa kanda kwakua anaishi kanda ya Nyasa muda wake mwingi.

Chama kimefanya busara za kiutendaji kumuengua Sosopi abakie na majukumu yake ya sasa ya BAVICHA.
Wabakaji wa demokrasia ninyi.

Tuna kila sababu ya kumuunga mkono JPM awashikie chini maana chama kinaendeshwa kufamilia, kienyeji na hovyo hovyo tu.

Sisi ni wanachama tena viongozi wa CDM lkn haturidhishwi na mwenendo wa Mwenyekiti Mbowe anavyokiendesha chama hiki atakavyo.

Unanyonga demokrasia ndani ya chama chako alafu Unataka demokrasia hiyohiyo nje ya chama,,,,,nani atakusikikiza? Mkuki kwa nguruwe mtamu kwa binadamu mchungu....

Hii haikubaliki hata kidogo na ni Bora tuache kuhubiri demokrasia maana ni unafki mtupu.
 
Back
Top Bottom