KalamuTena
JF-Expert Member
- Jul 7, 2018
- 13,189
- 17,157
Hakuna shaka yeyote, na sidhani kwamba kuna mtu anayeweza kuhoji uwepo wa CHADEMA kama chama cha kisiasa kilicho na ushindani mkubwa hapa nchini licha ya misukosuko mingi iliyoelekezwa kwao ili kuwamaliza kabisa katika miaka mitano na zaidi sasa iliyopita.
Ni sawa kabisa kusema kwamba CHADEMA wamepitia kwenye tanuru la moto mkali, na wamepikika sawasawa kuweza kuendelea na pilkapilka zao za kisiasa na kutafuta njia ya kuliongoza taifa hili.
Sioni mbele yao, kupata hujuma tena, kama walizozipata miaka hii ya karibuni chini ya utawala wa Marehemu Magufuli. Tanzania itakuwa na bahati mbaya sana, kama patatokea hivi karibuni misukosuko iliyolitingisha taifa kama ilivyotokea wakati wa serikali ya Magufuli.
Watu wanaweza kuhoji kwamba kuendelea kuwepo kwa CCM madarakani hiyo ndiyo hatari kubwa kwa CHADEMA na vyama vingine vya upinzani.
Mimi hilo silioni hivyo kwa sasa, na hata katika CCM ya enzi za Kikwete. Hatari iliongezeka zaidi alipoingia madarakani Magufuli na kutangaza waziwazi kutopenda uwepo wa vyama vya upinzani.
CCM wenyewe kama chama, hila zao zilikuwa ni za kawaida, mradi tu wanapata ushindi, hawakuwa na lengo maalum la kuua upinzani.
CHADEMA wafanye nini (samahani kwa kuwasema CHADEMA, badala ya vyama vya upinzani, kwa sababu vingine ndio hivyo tena vimetekwa).
Huu ni wakati wa CHADEMA kuwa wazi kabisa na sera zao. Wananchi waelewe chama kinasimamia nini.
Kati ya sifa chache, lakini muhimu alizojijengea Magufuli (sio CCM) ni kuonekana kuwa mtetezi wa mali na utajiri wa nchi hii na maendeleo ya wananchi wake.
Amejitambulisha bila shaka yoyote, kwamba yeye alikuwa ni mtetezi mkubwa wa maslahi ya Tanzania na wananchi wake. Amejenga hata ukuta, kulinda Tanzanite yetu iliyokuwa inatoroshwa kwenda nchi za nje na kuwanufaisha hao zaidi ya sisi tulivyokuwa tunanufaika kwayo.
Swala la madini aliliwekea mkazo sana; hata kama ilionekana kama kulikuwa na makosa katika juhudi hizo, lakini wananchi walielewa madhumuni yake. Kuna mifano mingi kuhusu msimamo wake juu ya mali za Tanzania.
Hatujui kuhusu mikataba mbalimbali nchi yetu iliyoiingia na nchi na mashirika mbalimbali ya kimataifa, lakini bado inaelekea wananchi waliamini kwamba mikataba hiyo ilikuwa ni kwa maslahi yao.
Jambo ambalo inawezekana hakulifanya vizuri ni kuhusu mashirikiano yetu na nchi mbalimbali duniani kwa vile alikazia zaidi "ubeberu" na mambo mengine kama masimango yao.
Nimeyaandika haya, ili CHADEMA watambue kwamba kama sera zao hazieleweki kwa wananchi, kazi yao itaendelea kuwa ngumu zaidi kuwashawishi wananchi hao kuwapa madaraka. Ni lazima wajieleze waziwazi kwa wananchi, wao ni nini hasa wanakisimamia kama chama cha siasa, na nchi yetu itafaidika vipi na misimamo yao hiyo kama watapewa ridhaa ya kuongoza serikali.
Kwa hiyo, nadhani ni halali sasa kusema kwamba adui mkubwa aliye mbele ya CHADEMA ni CHADEMA yenyewe. CCM wataendelea na hadaa zao kwa wananchi, hadaa za "Hawa ni Wenzetu" kama ilivyowahi kuwa huko nyuma, na wananchi kama hawaoni mbadala wa kuwapa madaraka, watarudi huko huko kwenye chama kilichooza ndani kwa ndani.
Niseme hapa, sijui kama Samia atakuwa na nguvu za kukibadilisha hiki chama kiwe chama cha wananchi wenyewe kwelikweli. Sijui.
Hatujui
Ni sawa kabisa kusema kwamba CHADEMA wamepitia kwenye tanuru la moto mkali, na wamepikika sawasawa kuweza kuendelea na pilkapilka zao za kisiasa na kutafuta njia ya kuliongoza taifa hili.
Sioni mbele yao, kupata hujuma tena, kama walizozipata miaka hii ya karibuni chini ya utawala wa Marehemu Magufuli. Tanzania itakuwa na bahati mbaya sana, kama patatokea hivi karibuni misukosuko iliyolitingisha taifa kama ilivyotokea wakati wa serikali ya Magufuli.
Watu wanaweza kuhoji kwamba kuendelea kuwepo kwa CCM madarakani hiyo ndiyo hatari kubwa kwa CHADEMA na vyama vingine vya upinzani.
Mimi hilo silioni hivyo kwa sasa, na hata katika CCM ya enzi za Kikwete. Hatari iliongezeka zaidi alipoingia madarakani Magufuli na kutangaza waziwazi kutopenda uwepo wa vyama vya upinzani.
CCM wenyewe kama chama, hila zao zilikuwa ni za kawaida, mradi tu wanapata ushindi, hawakuwa na lengo maalum la kuua upinzani.
CHADEMA wafanye nini (samahani kwa kuwasema CHADEMA, badala ya vyama vya upinzani, kwa sababu vingine ndio hivyo tena vimetekwa).
Huu ni wakati wa CHADEMA kuwa wazi kabisa na sera zao. Wananchi waelewe chama kinasimamia nini.
Kati ya sifa chache, lakini muhimu alizojijengea Magufuli (sio CCM) ni kuonekana kuwa mtetezi wa mali na utajiri wa nchi hii na maendeleo ya wananchi wake.
Amejitambulisha bila shaka yoyote, kwamba yeye alikuwa ni mtetezi mkubwa wa maslahi ya Tanzania na wananchi wake. Amejenga hata ukuta, kulinda Tanzanite yetu iliyokuwa inatoroshwa kwenda nchi za nje na kuwanufaisha hao zaidi ya sisi tulivyokuwa tunanufaika kwayo.
Swala la madini aliliwekea mkazo sana; hata kama ilionekana kama kulikuwa na makosa katika juhudi hizo, lakini wananchi walielewa madhumuni yake. Kuna mifano mingi kuhusu msimamo wake juu ya mali za Tanzania.
Hatujui kuhusu mikataba mbalimbali nchi yetu iliyoiingia na nchi na mashirika mbalimbali ya kimataifa, lakini bado inaelekea wananchi waliamini kwamba mikataba hiyo ilikuwa ni kwa maslahi yao.
Jambo ambalo inawezekana hakulifanya vizuri ni kuhusu mashirikiano yetu na nchi mbalimbali duniani kwa vile alikazia zaidi "ubeberu" na mambo mengine kama masimango yao.
Nimeyaandika haya, ili CHADEMA watambue kwamba kama sera zao hazieleweki kwa wananchi, kazi yao itaendelea kuwa ngumu zaidi kuwashawishi wananchi hao kuwapa madaraka. Ni lazima wajieleze waziwazi kwa wananchi, wao ni nini hasa wanakisimamia kama chama cha siasa, na nchi yetu itafaidika vipi na misimamo yao hiyo kama watapewa ridhaa ya kuongoza serikali.
Kwa hiyo, nadhani ni halali sasa kusema kwamba adui mkubwa aliye mbele ya CHADEMA ni CHADEMA yenyewe. CCM wataendelea na hadaa zao kwa wananchi, hadaa za "Hawa ni Wenzetu" kama ilivyowahi kuwa huko nyuma, na wananchi kama hawaoni mbadala wa kuwapa madaraka, watarudi huko huko kwenye chama kilichooza ndani kwa ndani.
Niseme hapa, sijui kama Samia atakuwa na nguvu za kukibadilisha hiki chama kiwe chama cha wananchi wenyewe kwelikweli. Sijui.
Hatujui