CHADEMA ime-savaivu, sasa nini?

CHADEMA ime-savaivu, sasa nini?

wakina Mbowe kinawauma zile mali na miradi yao ambayo ilibanwa kwelikweli na nyingine mpaka kupigwa mnada hii iliwauma kwelii hapo wakaona wamefanyiwa udikteta wa hali ya juu wakasahau kuna wafuasi wao walikua wanashinda bila hata kula hukoo mikoani kwa ajili wa matumbo yao rukuku ya kila mwezi lakini walirudi kwa wafuasi wao na kupitisha tena bakuri kwa ajili ya chama kifupi walikua wanajari maslahi yao hawakujua kula na vipofu kabisaa ila kwa fimbo hii imewapiga kweli kweli sijui watakuja na sera gani tena sidhani kama wanaweza muhubiria mwananchi kuhusu demokrasia wakati tayari wameshaonja utamu wa kasi ya hayati JPM uongozi uliokua na msingi wa kazi mbele kwa Maslahi mapana ya Taifa
ajira ngapi zimeletwa ?
 
Mbona Chadema wanakuwaga na sera nzuri kuliko vyama vingine vyote, Mfano ilani ya Uchaguzi mkuu mwaka 2015 ya CHADEMA ilikua moja ya sera zilizokua zinakitisha chama cha kijani kuondoka madarakani, hata hivyo kura hazikutosha ila uchaguzi uliofanyika hivi 2020 ulikua uchafuzi.Bi samia atuletee katiba mpya ikiwa na tume huru ya uchaguzi
Bi Samia hawezi kukubali chama kifie mikononi mwake kwa hiyo suala la katiba mpya na tume huru hawezi hata kuvigusia. Sahau mkuu
 
Huko unakotaka twende tulishafika na kumaliza kazi , hii ndio sababu ya Mahera kupokea maagizo ya ccm ( Bashiru , Polepole na Magufuli ) ya kuondoa wagombea wa Chadema nchi nzima na kwingine kupeleka kura za mabegi , labda nikutoe shaka , Chadema imo mpaka ndani ya ccm na atakayejaribu kuihujumu atakiona cha mtemakuni , nimemaliza
Chadema inaongea Ccm inatenda, hapo ndipo tofauti inapokuja.
Chadema walileta habari za elimu bure ccm ikazifanyia kazi, hapo ndipo wanapowawini raia
 
wakina Mbowe kinawauma zile mali na miradi yao ambayo ilibanwa kwelikweli na nyingine mpaka kupigwa mnada hii iliwauma kwelii hapo wakaona wamefanyiwa udikteta wa hali ya juu wakasahau kuna wafuasi wao walikua wanashinda bila hata kula hukoo mikoani kwa ajili wa matumbo yao rukuku ya kila mwezi lakini walirudi kwa wafuasi wao na kupitisha tena bakuri kwa ajili ya chama kifupi walikua wanajari maslahi yao hawakujua kula na vipofu kabisaa ila kwa fimbo hii imewapiga kweli kweli sijui watakuja na sera gani tena sidhani kama wanaweza muhubiria mwananchi kuhusu demokrasia wakati tayari wameshaonja utamu wa kasi ya hayati JPM uongozi uliokua na msingi wa kazi mbele kwa Maslahi mapana ya Taifa
Nyoko wenu hayupo kapewa kibano na Mungu kupitia korona anafukiwa futi 6 chini ya ardhi. Sasa uwanja wa mapambano umebadilika. Uaminifu kwenu umebakia kwa wadhaifu wachache ambao nao muda wao unayoyoma. TUTAELEWANA TU NA KUONGEA LUGHA MOJA. Sisi wenye chama cha CHADEMA hatutachoka kuwasitiri viongozi wetu kwa hali na mali na kuwakabidhi kwa Mungu.
 
Chadema inaongea Ccm inatenda, hapo ndipo tofauti inapokuja.
Chadema walileta habari za elimu bure ccm ikazifanyia kazi, hapo ndipo wanapowawini raia
Kama una watoto wanaosoma ungejua kama kuna elimu bure au kuna utopolo
 
Mama Samia akifungulia tu ajira na kupandisha mishahara Chadema mjue hamna chenu na hakuna atakae wasikiliza tena.
 
Kwa kutumia mtutu wa bunduki labda si kupitia uchaguzi huru na wa haki.
Uzuri wataalamu wa kuiba kura Mungu kawapangia majukumu mengine, ikiwemo kuongoza malaika.Ccm hawana jipya
 
  • Nzuri
Reactions: BAK
Hakuna shaka yeyote, na sidhani kwamba kuna mtu anayeweza kuhoji uwepo wa CHADEMA kama chama cha kisiasa kilicho na ushindani mkubwa hapa nchini licha ya misukosuko mingi iliyoelekezwa kwao ili kuwamaliza kabisa katika miaka mitano na zaidi sasa iliyopita.

Ni sawa kabisa kusema kwamba CHADEMA wamepitia kwenye tanuru la moto mkali, na wamepikika sawasawa kuweza kuendelea na pilkapilka zao za kisiasa na kutafuta njia ya kuliongoza taifa hili.

Sioni mbele yao, kupata hujuma tena, kama walizozipata miaka hii ya karibuni chini ya utawala wa Marehemu Magufuli. Tanzania itakuwa na bahati mbaya sana, kama patatokea hivi karibuni misukosuko iliyolitingisha taifa kama ilivyotokea wakati wa serikali ya Magufuli.

Watu wanaweza kuhoji kwamba kuendelea kuwepo kwa CCM madarakani hiyo ndiyo hatari kubwa kwa CHADEMA na vyama vingine vya upinzani.

Mimi hilo silioni hivyo kwa sasa, na hata katika CCM ya enzi za Kikwete. Hatari iliongezeka zaidi alipoingia madarakani Magufuli na kutangaza waziwazi kutopenda uwepo wa vyama vya upinzani.

CCM wenyewe kama chama, hila zao zilikuwa ni za kawaida, mradi tu wanapata ushindi, hawakuwa na lengo maalum la kuua upinzani.

CHADEMA wafanye nini (samahani kwa kuwasema CHADEMA, badala ya vyama vya upinzani, kwa sababu vingine ndio hivyo tena vimetekwa).

Huu ni wakati wa CHADEMA kuwa wazi kabisa na sera zao. Wananchi waelewe chama kinasimamia nini.

Kati ya sifa chache, lakini muhimu alizojijengea Magufuli (sio CCM) ni kuonekana kuwa mtetezi wa mali na utajiri wa nchi hii na maendeleo ya wananchi wake.

Amejitambulisha bila shaka yoyote, kwamba yeye alikuwa ni mtetezi mkubwa wa maslahi ya Tanzania na wananchi wake. Amejenga hata ukuta, kulinda Tanzanite yetu iliyokuwa inatoroshwa kwenda nchi za nje na kuwanufaisha hao zaidi ya sisi tulivyokuwa tunanufaika kwayo.

Swala la madini aliliwekea mkazo sana; hata kama ilionekana kama kulikuwa na makosa katika juhudi hizo, lakini wananchi walielewa madhumuni yake. Kuna mifano mingi kuhusu msimamo wake juu ya mali za Tanzania.

Hatujui kuhusu mikataba mbalimbali nchi yetu iliyoiingia na nchi na mashirika mbalimbali ya kimataifa, lakini bado inaelekea wananchi waliamini kwamba mikataba hiyo ilikuwa ni kwa maslahi yao.

Jambo ambalo inawezekana hakulifanya vizuri ni kuhusu mashirikiano yetu na nchi mbalimbali duniani kwa vile alikazia zaidi "ubeberu" na mambo mengine kama masimango yao.

Nimeyaandika haya, ili CHADEMA watambue kwamba kama sera zao hazieleweki kwa wananchi, kazi yao itaendelea kuwa ngumu zaidi kuwashawishi wananchi hao kuwapa madaraka. Ni lazima wajieleze waziwazi kwa wananchi, wao ni nini hasa wanakisimamia kama chama cha siasa, na nchi yetu itafaidika vipi na misimamo yao hiyo kama watapewa ridhaa ya kuongoza serikali.

Kwa hiyo, nadhani ni halali sasa kusema kwamba adui mkubwa aliye mbele ya CHADEMA ni CHADEMA yenyewe. CCM wataendelea na hadaa zao kwa wananchi, hadaa za "Hawa ni Wenzetu" kama ilivyowahi kuwa huko nyuma, na wananchi kama hawaoni mbadala wa kuwapa madaraka, watarudi huko huko kwenye chama kilichooza ndani kwa ndani.

Niseme hapa, sijui kama Samia atakuwa na nguvu za kukibadilisha hiki chama kiwe chama cha wananchi wenyewe kwelikweli. Sijui.
Hatujui
Sawa
 
Hakuna ccm imara bila upinzani imara,ccm ni tindo bila nyundo haiendi.Upinzani ndio chuo pekee cha Siasa kilichobakia.
 
Umesema sawa kabisa. Tatizo, inaelekea CHADEMA wenyewe wanachoamini ni kwamba wanafeli kwa sababu tu ya kuibiwa kura na hujuma zingine zinazofanywa na CCM. Sidhani kama wanaweka mkazo kwenye kuhakikisha wana sera mbadala zinazoeleweka kwa wananchi.

Sidhani ni swala la sera ndio linakiangusha CCM. Upinzani una maono sawasawa na CCM tofauti iliyopo ni kuwa siasa chafu ni sehemu kubwa sana ya siasa za nchi!! Upinzani hauna namna ya kuendesha siasa kwa maono yao. Hivi ni kweli umeshindwa kukumbuka misemo ya “Sera zinazotekelezwa ni za CCM?” - kwenye halmashauri upinzani ulishinda?? Ni halmashauri gani zilizokuwa zikiendeshwa na CCM madiwani walijiuzulu - utapata jibu kwanini mkazo wa kujiuzulu ulikuwa kwa halmashauri za upinzani!! Siaza zetu ni za kuzuiana, hata kama maana yake ni kuzuia jambo zuri kufanyika!! Chama kushika hatamu!!

Tunasahau mapema sana!!
 
Kazi kubwa iliyo mbele yao (CHADEMA), ni kuwaendea wananchi walipo,huko mitaani. Wasitegemee sana hizi siasa za majukwaani.
CCM imetumia udhaifu wao huo kwa vile wao CCM wako kila sehemu mitaani.

CHADEMA inabidi warekebishe muundo wao wa chama ili ngazi za mashina ziwe na sehemu muhimu zaidi ndani ya chama hicho.
Mkuu nimependa hoja yako lakini hili suala lilifanyiwa kazi tokea 2012 ilipoanzishwa CHADEMA ni msingi na ndio iliopelekea hata kuimarishwa kwa kanda ili chama kishuke kwenye grassroots.

Kwahyo utekelezaji ulianza changamoto iwe ni ufuatiliaji tu lakini tukiwa wakweli CHADEMA imefanikiwa sana kushuka chini tofauti na miaka 10 iliyopita. Leo hii kanda zina ofisi zao na zinaendesha oparesheni bila kusubiri makao makuu so kuna hatua zimechukuliwa ila changamoto ni pesa tu maana wengi hapo wanajitolea tu zao mfukoni.
 
Kazi kubwa iliyo mbele yao (CHADEMA), ni kuwaendea wananchi walipo,huko mitaani. Wasitegemee sana hizi siasa za majukwaani.
CCM imetumia udhaifu wao huo kwa vile wao CCM wako kila sehemu mitaani.

CHADEMA inabidi warekebishe muundo wao wa chama ili ngazi za mashina ziwe na sehemu muhimu zaidi ndani ya chama hicho.

Umesahau!! Nia halisi ya CCM ilikuwa ni kuzuia siasa na kuzifanya ni za uchaguzi tu! Kuwa “uchaguzi umekwisha sasa tujenge nchi”!! Kuwa anayeruhusiwa kufanya siasa ni mshindi wa eneo husika tu! Hii ikawafanya viongozi wa kitaifa wa Chadema kushindwa hata kufanya siasa za ndani. Ni mikutano mingapi ya ndani ilizuiwa kwa kuwa ilikuwa ikihusisha viongozi wa kitaifa?? Na wakati huo huo Polepole, Bashiru na marehemu wakizunguka nchi nzima wakifanya mikutano na kupokea wanachama na viongozi walioasi upinzani??!!

CCM imetumia dola kufanya siasa! Madhaifu ya Chadema yameletwa kimkakati, unachoona kama ni kushindwa kwa Chadema ni matokeo ya mikakati ya CCM na serikali. Kama vile unacheza mechi dhidi ya mpinzani wako ambaye ana refa, VAR na FA upande wake!!!
 
Hilo linawezekana kama vyama vingine vya siasa vitaruhusu iwe hivyo.

Kuruhusu kunatokana na sababu mbalimbali, kama vyama hivyo kutoweka bidii kuwaondoa CCM.

Wananchi hawawezi kukabidhi nchi kwa chama chochote kisichokuwa tayari kulinda maslahi mapana ya nchi yao.

Kumbuka, ni wananchi wenyewe ndio wenye mamlaka ya mwisho, sio mtu mmoja tena au kikundi cha watu wachache walio na mabunduki na mabomu ya kutoa machozi.

Tanzania hatutegemei kurudi tena kiongozi wa aina hiyo hivi karibuni.
Mkuu CHADEMA ilijijenga kupitia Agenda ya kupigania haki za wananchi hasa kiuchumi pale walipopambana na ufisadi, pingana na mikataba ya kinyonyaji na sheria kandamizi bungeni na majukwaani.

However toka awamu ya 5 inaingia utoaji taarifa umebanwa sana na uhuru wa kufanya siasa bungeni na majukwaani ulipokwa hata vikao vya ndani tu ikawa shida. Hii ilipelekea panic hasa upinzani hadi ikabidi wengine wahamie CCM ili kunusuru political career zao.

Maadam ameingia kiongozi mpya ambaye naamini ni lenient kidogo kuliko aliyetoka. Hivyo naona upinzani ukipata motisha mpya na kurudi kwa nguvu zaidi kusimamia agenda zao ambazo wengi waliziacha kwa hofu ya kumiminiwa risasi au kuswekwa ndani kwa makosa ya Uchochezi!!

But all in all CHADEMA haikuwahi acha kusimamia agenda zake hii ni kma ulikua unafuatilia michango yao bungeni na vitabu vya sera toleo la 2018. Otherwise waliendeleza struggle kupitia CHADEMA ni msingi na ofisi za kanda na kma uchaguzi ungekua huru trust me wange retain majimbo mengi tu na kata mpya nyingi na hapo tungefanya evaluation nzuri zaidi.
 
Kimeozaje mkuu. Kujidanganya kwako ndo kosa kubwa sana. Unaongea as if CHadema imejaaa kila kitu safi na haki. Hapo ndo unaonekana mjinga. Kuwa mkweli hata kama inauma ndo dawa ya kweli. Kosa kubwa sana. MlifanyA kwa Dr slaa. Kama mbunge alifanya kazi kubwa jimboni kwake. Hivyo watu walimwamini. Sio maneno maneno ambayo ukiuliza kafanya Nini ohhhh anajua kutukana.
Dr slaa? Mbona jimboni kwake waliipa CHADEMA kuanzia ubunge hadi halmashauri? Sidhani kma hyo ni sababu....... Otherwise Lissu asingepata mapokezi ya kishujaa vile Karatu.

Nachofahamu upinzani ni ideology sio mtu.... Ndio maana kina Slaa Zitto Mashinji wameondoka ila bado ni chama kikuu cha upinzani
 
Back
Top Bottom