CHADEMA ime-savaivu, sasa nini?

CHADEMA ime-savaivu, sasa nini?

... Huu ni wakati wa CHADEMA kuwa wazi kabisa na sera zao. Wananchi waelewe chama kinasimamia nini.
... Sidhani kama wanaweka mkazo kwenye kuhakikisha wana sera mbadala zinazoeleweka kwa wananchi.

Kwa uzoefu wangu mdogo nilioupata kuhusu siasa za Bongo, sehemu kubwa ya wananchi hawana muda hata wa kupima kitu kinachoitwa sera. Ni mihemko tu, ukiwaudhi wanakutosa kwa mihemko, ukiwateka kwa hoja nyepesi nyepesi tu, wanakupigia makofi na kukuchagua kwa mihemko pia. Sera zipo kwenye documents za vyama, ila wananchi wengi wala huwa hawana muda wa kuzitathmini. Pengine hata wewe ukiulizwa sera gani kumi zilikuvutia ukakichagua chama ulichokipigia kura, huenda ukajitahidi kukumbuka tatu tu, tena si kwa sababu umezitathmini, ila kwa sababu zimeimbwaimbwa ukazikariri
 
Kimeozaje mkuu. Kujidanganya kwako ndo kosa kubwa sana. Unaongea as if CHadema imejaaa kila kitu safi na haki. Hapo ndo unaonekana mjinga. Kuwa mkweli hata kama inauma ndo dawa ya kweli. Kosa kubwa sana. MlifanyA kwa Dr slaa. Kama mbunge alifanya kazi kubwa jimboni kwake. Hivyo watu walimwamini. Sio maneno maneno ambayo ukiuliza kafanya Nini ohhhh anajua kutukana.
Tatizo lako nalijua kutokana na maandiko yako humu.

Unajibu nilichoandika kwa pupa bila kuelewa kimeelezwa kitu gani.

Ni sehemu gani ya anadiko hilo nililoweka hapo inaeleza kwamba niko CHADEMA, au kwa vile tu ninaisuta CCM?

Ndiyo, CCM tokea enzi za Mwinyi hakijawa tena chama cha kutetea maslahi ya wananchi. Kimekuwa chama cha 'opportunists' tu wanaojitafutia maslahi.
Sasa kama unadhani kwa kusema hivyo ndio kwamba nasema CHADEMA ni malaika, huo utakuwa ni upotofu wako.

CCM hadi mwisho wa Magufuli ilikuwa imekufa, lilibaki kopo tu alilotumia Magufuli kufanya yake atakayo.

Sasa sijui kama huyu mama atakuwa na lolote la kuiimarisha tena CCM kiwe chama cha kuiletea Tanzania manufaa.

Akifanya hivyo, sina tatizo kumsifu na kukisifu chama.
 
Kalamu1
nimeshiliki kwa ukamilifu uchaguzi wa 2021

Nimeshiriki vyema mchakato mzima wa kampeni mwanzo mwisho itoshe kusema, wanachokosa CHADEMA ni jeshi la kulinda kura zao na vyombo vya kutangaza huo ushindi wao!

hiki chama kipo zaidi ya 80% maeneo ya nchi hii!

Sera zao mbona zinaeleweka vizuri tu!

elimu bure(jpm) akaikwapua 2015, serikali za majimbo ili kupunguza centralization ya uchumi na upendeleo katika maendeleo ya nchi, katiba mpya na ushirikishwaji wa wananchi katika maamuzi ya nchi kidemokrasia!

Cha kuwashauri CHADEMA ni kupunguza tu zile siasa za kihanarakati zisizo na tija yoyote.

Ule uporaji wa kura wa mwaka jana ndyo taswira ya uimara wa CHADEMA!

JPM hajakwapua wewe. Soma historia yake. Ndo mana ukitaka kujua CHadema waliandika taarabu ya kutafuta Kura. Ukiwa mpinzani sera yako haiwezi kuwa mbaya mana unajua hutaweza kuitekeleza mpaka Uwe madarakani. Ndo mana unaona JPM aliwachanganya sana mkawa watu wa matukio. Yeye Ni Mtendaji. Nyie kazi yenu ohh. Demokrasia. Sijui hata kama mnaelewa maana yake. Kwenu mmeshindwa. Ila kuongea mnaweza.

Hivi umefanya tathmini ya utendaji wa CHadema wakati wa Kikwete. Ile ndo Demokrasia. Kutukana na kufanya nchi isitawalike. JPM aliwasoma so alichokuja nacho Ni dawa yenu. Siasa Siasa haziwezi ijenga Tz ambayo kila mtu Ni mjuaji. Kila kijana anataka utajiri kabla hata ya jacho halali. Kila mtu anataka kuiba nk.

Acheni kuanza hoja kwa prejudices. Zinawaangusha sana. Embu jiangalieni wenyewe. Mgombea wa uraisi Yuko anaongea na Kenya kuhusu mambo ya Tz. Hivi odinga aliwahi kuja Tz kutukana wakenya. Mlipoangukia hamuoni. Ila badilikeni Ila Lissu hatawapeleka popote. Huku mnadanganyA sana. Nenda kakiwashe huko Insta na FB. Utajua
 
Mwaka jana hapakuwepo na uchaguzi mkuu 'guwe_la_manga', huo ulikuwa ni uchafuzi.

Lakini swali ambalo bado ninajiuliza ni hili, labda nawe utasaidia kulijibu:
Hivi kweli CHADEMA waliingia kwenye uchaguzi huo wakitegemea kwamba utakuwa huru na wa haki? Zingatia hapa kilichofanyika na ule uchaguzi wa serikali za mitaa uliokuwa umetangulia!

Ni nini hasa kilichowaaminisha CHADEMA kwamba wangeweza kushiriki na kupata ushindi katika hali iliyokuwa bayana kabla ya kupiga kura!

Siwezi kamwe kukubishia juu ya utayari wa ushindi walioutegemea kutoka kwa wananchi kama ulivyoeleza kuwa hali uliyoishuhudia wewe mwenyewe. Sasa jiulize, wananchi wakawapigia kura CHADEMA, CCM wakazipora, na kukwa kimya kana kwamba hakuna kilichotokea! Huoni hitilafu katika hali hiyo?

Maoni yangu ni kwamba, hata kama CHADEMA walipewa kura nyingi na wananchi, wananchi hao hawakuwa na msisimuko wa kuiunga mkono CHADEMA. Hata kama waliwapa kura zao, hiyo ilikuwa ni kwa sababu hapakuwa na mwingine wa kumpa; zilipoporwa, wananchi hawakuwa na mori wa kukataa uharamia huo.

Kazi waliyokuwa waifanye CHADEMA kabla ya kura kupigwa, ni kuwaandaa wananchi wasikubali kunyang'anywa haki yao ya msingi, haki ya kuwachagua viongozi wanaowataka.

Mwisho, kutokana na niliyoandika hapo juu, sina hakika sana kwamba wananchi hata kama waliwapa kura zao nyingi CHADEMA, sababu ya kufanya hivyo ilikuwa ni kwa sababu walielewa na kuzikubali sera, kama zile ulizozitaja wewe.

Kunawezekana sana kama waliwapigia CHADEMA kura, sababu inaweza kuwa ni kwa sababu ya kuwakataa CCM, na hasa kutokana na aliyokuwa ameyafanya mwenyekiti wa chama hicho kama rais.

Sitapenda unielewe kwamba wananchi hawazipendi sera za CHADEMA, lakini ningependa kupata ushahidi unaojitegemea zaidi.
Mosi, naamini kwamba CHADEMA waliingia uchaguzi wa 2020 sababu hawakuamini kwamba CCM wangeendesha uporaji wa kiwango hicho katika uchaguzi mkuu. Walitarajia uwepo wa waangalizi wengi wa kimataifa. Magufuli alikwepa hili la waangalizi kwa kukataa fedha za UN, ambazo ndio huambatana na waangalizi hao. Kwa hiyo akadai kwa wananchi kwamba uchaguzi huu haitumiki fedha ya nje bali ya ndani tuuu!!! Kumbe kazima taa ili akwibe kwa amani na utulivu.
Pili CHADEMA wali-underestimate kiwango cha kukosa aibu cha Magufuli, hawakuamini angeweza kuendesha kiwango hicho cha ujambazi.

Kuhusu wananchi kulinda kura zao, ni vile tu kwamba hawajafikia kiwango hicho, ipo siku watafikia. Lakini pengine matokeo ya wizi huo ni kutengwa kimataifa kiasi kwamba kuendesha nchi sasa ni ngumu zaidi. Serikali inazidi kuwapora wananchi wake. Angalia package za bima ya afya za Magufuli. Ni wizi mtupu. Ni mradi wa kukusanya fedha ya miradi yake na siyo huduma ya Afya kwa wote.

Sidhani, kama ulivyosema pia, kwamba serikali itathubutu kuiba kura tena kwa viwango vya serikali za mitaa 2019 na uchaguzi mkuu 2020. Inahitaji 'kichaa' na sidhani kama hao waliopo CCM sasa ivi kuna mwenye kiwango hicho cha ukichaa.

Ni kweli CHADEMA wanaendelea kuenjoy kura za chuki na pia sympathy. Wanateseka mno na pia maisha kwa wote ni magumu sana. Wakiboresha meseji yao itakuwa vema zaidi
 
Mbona Chadema wanakuwaga na sera nzuri kuliko vyama vingine vyote, Mfano ilani ya Uchaguzi mkuu mwaka 2015 ya CHADEMA ilikua moja ya sera zilizokua zinakitisha chama cha kijani kuondoka madarakani, hata hivyo kura hazikutosha ila uchaguzi uliofanyika hivi 2020 ulikua uchafuzi.Bi samia atuletee katiba mpya ikiwa na tume huru ya uchaguzi
 
Kwa uzoefu wangu mdogo nilioupata kuhusu siasa za Bongo, sehemu kubwa ya wananchi hawana muda hata wa kupima kitu kinachoitwa sera. Ni mihemko tu, ukiwaudhi wanakutosa kwa mihemko, ukiwateka kwa hoja nyepesi nyepesi tu, wanakupigia makofi na kukuchagua kwa mihemko pia. Sera zipo kwenye documents za vyama, ila wananchi wengi wala huwa hawana muda wa kuzitathmini. Pengine hata wewe ukiulizwa sera gani kumi zilikuvutia ukakichagua chama ulichokipigia kura, huenda ukajitahidi kukumbuka tatu tu, tena si kwa sababu umezitathmini, ila kwa sababu zimeimbwaimbwa ukazikariri
Nimekusoma vyema.

Wananchi kutowachagua viongozi kufuatana na sera za vyama vyao, sio kosa la wananchi, ni kosa la viongozi wa vyama hivyo na vyama vyao kiujumla.
Kazi ya kuwaelimisha wananchi kuacha kuchagua viongozi kwa mihemuko, ni ya vyama vyenyewe na viongozi wao. Wananchi hawajakataa kujifunza na kuelewa hizo sera.
Kwa hiyo, tukubali tu kwamba kwa kuwa vyama vinashindwa kutimiza wajibu wao, basi tuliache tu mradi linakwenda?

Umedadisi kama hata mimi nikiulizwa sera gani kumi - huhitaji kuniuliza sera kumi. nieleze mbili tu zitakazonipa uwezo wa kujua unasimamia wapi, na ziwe za msingi kabisa, nitakuunga mkono. Huhitaji kunipa rundo la sera zote hizo kupata ufahamu wa kipi unakisimamia kwa maslahi ya taifa letu.
 
Kazi kubwa iliyo mbele yao (CHADEMA), ni kuwaendea wananchi walipo,huko mitaani. Wasitegemee sana hizi siasa za majukwaani.
CCM imetumia udhaifu wao huo kwa vile wao CCM wako kila sehemu mitaani.

CHADEMA inabidi warekebishe muundo wao wa chama ili ngazi za mashina ziwe na sehemu muhimu zaidi ndani ya chama hicho.
Chadema imewekeza sana kwenye mitaa na vijiji,ushahidi kamili ni uchaguzi wa uliopita. Bila figisu CCM ingeng'oka
 
Mosi, naamini kwamba CHADEMA waliingia uchaguzi wa 2020 sababu hawakuamini kwamba CCM wangeendesha uporaji wa kiwango hicho katika uchaguzi mkuu. Walitarajia uwepo wa waangalizi wengi wa kimataifa. Magufuli alikwepa hili la waangalizi kwa kukataa fedha za UN, ambazo ndio huambatana na waangalizi hao. Kwa hiyo akadai kwa wananchi kwamba uchaguzi huu haitumiki fedha ya nje bali ya ndani tuuu!!! Kumbe kazima taa ili akwibe kwa amani na utulivu.
Pili CHADEMA wali-underestimate kiwango cha kukosa aibu cha Magufuli, hawakuamini angeweza kuendesha kiwango hicho cha ujambazi.

Kuhusu wananchi kulinda kura zao, ni vile tu kwamba hawajafikia kiwango hicho, ipo siku watafikia. Lakini pengine matokeo ya wizi huo ni kutengwa kimataifa kiasi kwamba kuendesha nchi sasa ni ngumu zaidi. Serikali inazidi kuwapora wananchi wake. Angalia package za bima ya afya za Magufuli. Ni wizi mtupu. Ni mradi wa kukusanya fedha ya miradi yake na siyo huduma ya Afya kwa wote.

Sidhani, kama ulivyosema pia, kwamba serikali itathubutu kuiba kura tena kwa viwango vya serikali za mitaa 2019 na uchaguzi mkuu 2020. Inahitaji 'kichaa' na sidhani kama hao waliopo CCM sasa ivi kuna mwenye kiwango hicho cha ukichaa.

Ni kweli CHADEMA wanaendelea kuenjoy kura za chuki na pia sympathy. Wanateseka mno na pia maisha kwa wote ni magumu sana. Wakiboresha meseji yao itakuwa vema zaidi
Niseme tu mkuu wangu 'Mindi'; mada hii ni kuwahimiza CHADEMA "Wagange yajayo", yaliyopita liwe fundisho.

Wizi wa kura hautakoma, utaendelea kuwepo, hata kama utakuwa ni wizi wa kistaarabu chini ya utawala mpya.

CHADEMA walijue hili, na wawe tayari kufanya kazi nzito zaidi kuwavuta wananchi upande wao ili kufidia kura zinazoingia upande mwingine kwa wizi.

Ni kazi ngumu sana, lakini ni kazi inayowezekana kwa viongozi waliojizatiti kuifanya kwa ufanisi.

Hakuna mbadala wa kuwaendea wananchi kila kona ya nchi walipo na kuwaelimisha chama chao kinasimamia nini. Wananchi wakielimika, sina shaka watachagua kwa utashi wao wanachokitaka.
 
Hakuna shaka yeyote, na sidhani kwamba kuna mtu anayeweza kuhoji uwepo wa CHADEMA kama chama cha kisiasa kilicho na ushindani mkubwa hapa nchini licha ya misukosuko mingi iliyoelekezwa kwao ili kuwamaliza kabisa katika miaka mitano na zaidi sasa iliyopita.

Ni sawa kabisa kusema kwamba CHADEMA wamepitia kwenye tanuru la moto mkali, na wamepikika sawasawa kuweza kuendelea na pilkapilka zao za kisiasa na kutafuta njia ya kuliongoza taifa hili.

Sioni mbele yao, kupata hujuma tena, kama walizozipata miaka hii ya karibuni chini ya utawala wa Marehemu Magufuli. Tanzania itakuwa na bahati mbaya sana, kama patatokea hivi karibuni misukosuko iliyolitingisha taifa kama ilivyotokea wakati wa serikali ya Magufuli.

Watu wanaweza kuhoji kwamba kuendelea kuwepo kwa CCM madarakani hiyo ndiyo hatari kubwa kwa CHADEMA na vyama vingine vya upinzani.

Mimi hilo silioni hivyo kwa sasa, na hata katika CCM ya enzi za Kikwete. Hatari iliongezeka zaidi alipoingia madarakani Magufuli na kutangaza waziwazi kutopenda uwepo wa vyama vya upinzani.

CCM wenyewe kama chama, hila zao zilikuwa ni za kawaida, mradi tu wanapata ushindi, hawakuwa na lengo maalum la kuua upinzani.

CHADEMA wafanye nini (samahani kwa kuwasema CHADEMA, badala ya vyama vya upinzani, kwa sababu vingine ndio hivyo tena vimetekwa).

Huu ni wakati wa CHADEMA kuwa wazi kabisa na sera zao. Wananchi waelewe chama kinasimamia nini.

Kati ya sifa chache, lakini muhimu alizojijengea Magufuli (sio CCM) ni kuonekana kuwa mtetezi wa mali na utajiri wa nchi hii na maendeleo ya wananchi wake.

Amejitambulisha bila shaka yoyote, kwamba yeye alikuwa ni mtetezi mkubwa wa maslahi ya Tanzania na wananchi wake. Amejenga hata ukuta, kulinda Tanzanite yetu iliyokuwa inatoroshwa kwenda nchi za nje na kuwanufaisha hao zaidi ya sisi tulivyokuwa tunanufaika kwayo.

Swala la madini aliliwekea mkazo sana; hata kama ilionekana kama kulikuwa na makosa katika juhudi hizo, lakini wananchi walielewa madhumuni yake. Kuna mifano mingi kuhusu msimamo wake juu ya mali za Tanzania.

Hatujui kuhusu mikataba mbalimbali nchi yetu iliyoiingia na nchi na mashirika mbalimbali ya kimataifa, lakini bado inaelekea wananchi waliamini kwamba mikataba hiyo ilikuwa ni kwa maslahi yao.

Jambo ambalo inawezekana hakulifanya vizuri ni kuhusu mashirikiano yetu na nchi mbalimbali duniani kwa vile alikazia zaidi "ubeberu" na mambo mengine kama masimango yao.

Nimeyaandika haya, ili CHADEMA watambue kwamba kama sera zao hazieleweki kwa wananchi, kazi yao itaendelea kuwa ngumu zaidi kuwashawishi wananchi hao kuwapa madaraka. Ni lazima wajieleze waziwazi kwa wananchi, wao ni nini hasa wanakisimamia kama chama cha siasa, na nchi yetu itafaidika vipi na misimamo yao hiyo kama watapewa ridhaa ya kuongoza serikali.

Kwa hiyo, nadhani ni halali sasa kusema kwamba adui mkubwa aliye mbele ya CHADEMA ni CHADEMA yenyewe. CCM wataendelea na hadaa zao kwa wananchi, hadaa za "Hawa ni Wenzetu" kama ilivyowahi kuwa huko nyuma, na wananchi kama hawaoni mbadala wa kuwapa madaraka, watarudi huko huko kwenye chama kilichooza ndani kwa ndani.

Niseme hapa, sijui kama Samia atakuwa na nguvu za kukibadilisha hiki chama kiwe chama cha wananchi wenyewe kwelikweli. Sijui.
Hatujui
Umeandika mengi mkuu why unazungukazunguka?waambie chama dola wa LEVEL playing field na itisha mechi even today uone makali ya CDM,inasikitisha mno middle class wetu kuingiza vichwa vyao mchangani,walete tume huru ya uchaguzi ,kampeni huru(cdm wanahitaji mikutano 10 tu nchi nzima.
 
Kazi kubwa iliyo mbele yao (CHADEMA), ni kuwaendea wananchi walipo,huko mitaani. Wasitegemee sana hizi siasa za majukwaani.
CCM imetumia udhaifu wao huo kwa vile wao CCM wako kila sehemu mitaani.

CHADEMA inabidi warekebishe muundo wao wa chama ili ngazi za mashina ziwe na sehemu muhimu zaidi ndani ya chama hicho.
Huko unakotaka twende tulishafika na kumaliza kazi , hii ndio sababu ya Mahera kupokea maagizo ya ccm ( Bashiru , Polepole na Magufuli ) ya kuondoa wagombea wa Chadema nchi nzima na kwingine kupeleka kura za mabegi , labda nikutoe shaka , Chadema imo mpaka ndani ya ccm na atakayejaribu kuihujumu atakiona cha mtemakuni , nimemaliza
 
Niseme tu mkuu wangu 'Mindi'; mada hii ni kuwahimiza CHADEMA "Wagange yajayo", yaliyopita liwe fundisho.

Wizi wa kura hautakoma, utaendelea kuwepo, hata kama utakuwa ni wizi wa kistaarabu chini ya utawala mpya.

CHADEMA walijue hili, na wawe tayari kufanya kazi nzito zaidi kuwavuta wananchi upande wao ili kufidia kura zinazoingia upande mwingine kwa wizi.

Ni kazi ngumu sana, lakini ni kazi inayowezekana kwa viongozi waliojizatiti kuifanya kwa ufanisi.

Hakuna mbadala wa kuwaendea wananchi kila kona ya nchi walipo na kuwaelimisha chama chao kinasimamia nini. Wananchi wakielimika, sina shaka watachagua kwa utashi wao wanachokitaka.
Wizi kistaarabu ndio nini? Hivi huwa una akili timamu?
 
Hakuna shaka yeyote, na sidhani kwamba kuna mtu anayeweza kuhoji uwepo wa CHADEMA kama chama cha kisiasa kilicho na ushindani mkubwa hapa nchini licha ya misukosuko mingi iliyoelekezwa kwao ili kuwamaliza kabisa katika miaka mitano na zaidi sasa iliyopita.

Ni sawa kabisa kusema kwamba CHADEMA wamepitia kwenye tanuru la moto mkali, na wamepikika sawasawa kuweza kuendelea na pilkapilka zao za kisiasa na kutafuta njia ya kuliongoza taifa hili.

Sioni mbele yao, kupata hujuma tena, kama walizozipata miaka hii ya karibuni chini ya utawala wa Marehemu Magufuli. Tanzania itakuwa na bahati mbaya sana, kama patatokea hivi karibuni misukosuko iliyolitingisha taifa kama ilivyotokea wakati wa serikali ya Magufuli.

Watu wanaweza kuhoji kwamba kuendelea kuwepo kwa CCM madarakani hiyo ndiyo hatari kubwa kwa CHADEMA na vyama vingine vya upinzani.

Mimi hilo silioni hivyo kwa sasa, na hata katika CCM ya enzi za Kikwete. Hatari iliongezeka zaidi alipoingia madarakani Magufuli na kutangaza waziwazi kutopenda uwepo wa vyama vya upinzani.

CCM wenyewe kama chama, hila zao zilikuwa ni za kawaida, mradi tu wanapata ushindi, hawakuwa na lengo maalum la kuua upinzani.

CHADEMA wafanye nini (samahani kwa kuwasema CHADEMA, badala ya vyama vya upinzani, kwa sababu vingine ndio hivyo tena vimetekwa).

Huu ni wakati wa CHADEMA kuwa wazi kabisa na sera zao. Wananchi waelewe chama kinasimamia nini.

Kati ya sifa chache, lakini muhimu alizojijengea Magufuli (sio CCM) ni kuonekana kuwa mtetezi wa mali na utajiri wa nchi hii na maendeleo ya wananchi wake.

Amejitambulisha bila shaka yoyote, kwamba yeye alikuwa ni mtetezi mkubwa wa maslahi ya Tanzania na wananchi wake. Amejenga hata ukuta, kulinda Tanzanite yetu iliyokuwa inatoroshwa kwenda nchi za nje na kuwanufaisha hao zaidi ya sisi tulivyokuwa tunanufaika kwayo.

Swala la madini aliliwekea mkazo sana; hata kama ilionekana kama kulikuwa na makosa katika juhudi hizo, lakini wananchi walielewa madhumuni yake. Kuna mifano mingi kuhusu msimamo wake juu ya mali za Tanzania.

Hatujui kuhusu mikataba mbalimbali nchi yetu iliyoiingia na nchi na mashirika mbalimbali ya kimataifa, lakini bado inaelekea wananchi waliamini kwamba mikataba hiyo ilikuwa ni kwa maslahi yao.

Jambo ambalo inawezekana hakulifanya vizuri ni kuhusu mashirikiano yetu na nchi mbalimbali duniani kwa vile alikazia zaidi "ubeberu" na mambo mengine kama masimango yao.

Nimeyaandika haya, ili CHADEMA watambue kwamba kama sera zao hazieleweki kwa wananchi, kazi yao itaendelea kuwa ngumu zaidi kuwashawishi wananchi hao kuwapa madaraka. Ni lazima wajieleze waziwazi kwa wananchi, wao ni nini hasa wanakisimamia kama chama cha siasa, na nchi yetu itafaidika vipi na misimamo yao hiyo kama watapewa ridhaa ya kuongoza serikali.

Kwa hiyo, nadhani ni halali sasa kusema kwamba adui mkubwa aliye mbele ya CHADEMA ni CHADEMA yenyewe. CCM wataendelea na hadaa zao kwa wananchi, hadaa za "Hawa ni Wenzetu" kama ilivyowahi kuwa huko nyuma, na wananchi kama hawaoni mbadala wa kuwapa madaraka, watarudi huko huko kwenye chama kilichooza ndani kwa ndani.

Niseme hapa, sijui kama Samia atakuwa na nguvu za kukibadilisha hiki chama kiwe chama cha wananchi wenyewe kwelikweli. Sijui.
Hatujui
Mimi siamini kama wapiga kura wa nchi hii wanachagua viongozi baada ya kusoma,kuchambua na kuelewa Sera za vyama vyao.Sidhani kama tumefikia umakini wa kiwango hicho kama taifa.
 
Huko unakotaka twende tulishafika na kumaliza kazi , hii ndio sababu ya Mahera kupokea maagizo ya ccm ( Bashiru , Polepole na Magufuli ) ya kuondoa wagombea wa Chadema nchi nzima na kwingine kupeleka kura za mabegi , labda nikutoe shaka , Chadema imo mpaka ndani ya ccm na atakayejaribu kuihujumu atakiona cha mtemakuni , nimemaliza
Sidhani, na wala sitegemei kuona uhujumu kiasi ya tuliouona chini ya Magufuli, sidhani.

Ndiyo maana sasa CHADEMA wajizatiti zaidi kuvuna walichopanda, kama kweli mbegu ilishapandwa kama unavyoeleza.

Wakati huo huo, usisahau kwamba CCM ni chama kikongwe sana na wana miundo mbinu kila mahala.

Wao pia wanayo nafasi ya kuji-'re-invent'; kama kuvua gamba hivi kwa kutumia miundo mbinu nyingi walizonazo kujisafisha kwa wananchi.

Hizi ndizo tahadhari tunazowaeleza mzijue
 
Mimi siamini kama wapiga kura wa nchi hii wanachagua viongozi baada ya kusoma,kuchambua na kuelewa Sera za vyama vyao.Sidhani kama tumefikia umakini wa kiwango hicho kama taifa.
Ninakubaliana na wewe kwa kiasi; lakini haitakuwa hivyo milele.

Wakati ndio huu.

Lakini pengine tunaweza kudadavua maana ya sera hasa ni nini. Wananchi hawana shida ya kudadavua kiundani maana ya sera hizo ndipo waelewe chama kinasimamia nini.

Hata tokea enzi zile za akina Mtemvu na Mwalimu Nyerere, bila shaka wananchi waliweza kujua TANU na Chama cha Mtemvu walisimamia nini, hata kama haikuwa kwa undani zaidi.
 
kuna vyama kazi yao ni kupima upepo ataenata na biti ndo uyouyo 2010 2015 2020 hata na 2025
kuna vyama haviaminiki wanachama wake hawana msimamo yani muda wowote wanasaliti,wengine ofisi haifanani na jina lao, haijulikani wanapigania nini mara watutishie mabeberu mara watutishie kenya mara waseme barabara,umeme sio maendeleo

uzalendo wa wapinzani unatiashaka
kwenye mambo makubwa ya kuisaidia nchi wanajitenga na kuicheka inchi inapokosea na kuiombea nchi mabàya

sera ya majimbo hii kitu badilisheni asee wabongo hawaipendi na wanaambukizana kuichukia sera iyo

always upinzani ni malalamiko tuu na kueneza chuki zenu binafsi dhidi ya viongozi wa nchi kuongea point ni kwa bahatimbaya

wananchi wanaona hayohapo juu na ndo maana wanawatosaga na nyie mkitoswa mnaanza kuwatukana tena wapigakura😁😁😁😁😁
hamuwezi kuibua agenda yenu always mnadandiaga matukio mnasubiriaga myb DC achape watu ndo muibuke asipochapa mtu hamuonekani 😂😂😂😂
uhuni panyaroad wote wapo upinzani muangalie hata mayor Jacob alivokua 😂😂 mara mbowe kamkula sjui nani mara lipumba karuka ukuta kajifungia ofisini mara rungwe anasema ubwabwa buree 😂😂😂😂😂 mara zito kamtongoza diva


asee upinzani kwa kifupi jipangeni sana
 
wakina Mbowe kinawauma zile mali na miradi yao ambayo ilibanwa kwelikweli na nyingine mpaka kupigwa mnada hii iliwauma kwelii hapo wakaona wamefanyiwa udikteta wa hali ya juu wakasahau kuwa kuna wafuasi wao walikua wanashinda bila hata kula hukoo mikoani kwa ajili wa matumbo yao Ruzuku ya kila mwezi lakini walirudi kwa wafuasi wao na kupitisha tena bakuri kwa ajili ya chama kifupi walikua wanajali maslahi yao hawakujua kula na vipofu kabisaa ila kwa fimbo hii imewapiga kweli kweli sijui watakuja na sera gani tena sidhani kama wanaweza muhubiria mwananchi kuhusu demokrasia wakati tayari wameshaonja utamu wa kasi ya hayati JPM uongozi uliokua na msingi wa kazi mbele kwa Maslahi mapana ya Taifa
 
Sidhani, na wala sitegemei kuona uhujumu kiasi ya tuliouona chini ya Magufuli, sidhani.

Ndiyo maana sasa CHADEMA wajizatiti zaidi kuvuna walichopanda, kama kweli mbegu ilishapandwa kama unavyoeleza.

Wakati huo huo, usisahau kwamba CCM ni chama kikongwe sana na wana miundo mbinu kila mahala.

Wao pia wanayo nafasi ya kuji-'re-invent'; kama kuvua gamba hivi kwa kutumia miundo mbinu nyingi walizonazo kujisafisha kwa wananchi.

Hizi ndizo tahadhari tunazowaeleza mzijue
Tulionya mapema sana kwamba shetani hajawahi kumshinda Mungu , nadhani sasa somo linaanza kueleweka
 
Back
Top Bottom