CHADEMA ime-savaivu, sasa nini?

CHADEMA ime-savaivu, sasa nini?

CCM wakitaka watawale kwa raha,wasitulaze njaa tu kwa miradi yao aliyoiacha JPM,maana mh,tumepigika😂😂😂jamaa ametunyoosha

Wanawake,wanaume wote tunanyoa vipala kwa kwenda mbele🤓🤓
 
Ila Chadema ni chuma cha pua.Jiwe pamoja na figisu zote ameshindwa kuifuta chadema.Ameondoka ameiacha chadema!
 
Mkuu nimependa hoja yako lakini hili suala lilifanyiwa kazi tokea 2012 ilipoanzishwa CHADEMA ni msingi na ndio iliopelekea hata kuimarishwa kwa kanda ili chama kishuke kwenye grassroots.

Kwahyo utekelezaji ulianza changamoto iwe ni ufuatiliaji tu lakini tukiwa wakweli CHADEMA imefanikiwa sana kushuka chini tofauti na miaka 10 iliyopita. Leo hii kanda zina ofisi zao na zinaendesha oparesheni bila kusubiri makao makuu so kuna hatua zimechukuliwa ila changamoto ni pesa tu maana wengi hapo wanajitolea tu zao mfukoni.
Inasemwa, mara kwa mara; kwamba wanaofanikisha mipango mingi ya uchafuzi wa chaguzi, hasa huko mitaani ni hawa watu wa CCM walioko huko, kila sehemu.

Kuwepo kwa CHADEMA kwenye maeneo hayo, na wakawa tayari kabisa kuwakabili wenzao hao huko huko mitaani, nadhani hii itakuwa ni sehemu muhimu sana kwa CHADEMA kulinda haki yao.

Kumbuka, hawa wenye mabunduki wanaotumiwa na CCM, hawana mabunduki na mabomu ya machozi kila mtaa na kila kitongoji.
Wananchi watapata ujasiri sana wa kusimamia kura zao wakiona kwamba kuna uongozi mbele zao. Hawatakaa kimya kuona kura zao zikiharibiwa.

Kwa hiyo, kuwepo kwa CHADEMA hadi huko chini, sio faida ya kueneza sera zao pekee, bali pia wanawapa wananchi ujasiri wa kukataa uhujumu wa kura zao.

Ninakubaliana nawe juu ya hatua wanazo/walizochukua CHADEMA kwenda huko mitaani; nimeisikia sana habari hiyo. Nisichojua ni kiasi gani wamefanikiwa kuleta matokeo chanya kwa chama chao.
Lakini najua msemo wa wahenga kuhusu mji wa Roma.

Kama wamefika huko mitaani, basi kazi sasa ni kukaza kamba zaidi, pamoja na kuwa na hali ngumu ya ukata. Hao wanaojitolea kwa ajili ya chama wakati hali ikiwa ngumu, huenda ndio viongozi imara wa chama.
 
Umesahau!! Nia halisi ya CCM ilikuwa ni kuzuia siasa na kuzifanya ni za uchaguzi tu! Kuwa “uchaguzi umekwisha sasa tujenge nchi”!! Kuwa anayeruhusiwa kufanya siasa ni mshindi wa eneo husika tu! Hii ikawafanya viongozi wa kitaifa wa Chadema kushindwa hata kufanya siasa za ndani. Ni mikutano mingapi ya ndani ilizuiwa kwa kuwa ilikuwa ikihusisha viongozi wa kitaifa?? Na wakati huo huo Polepole, Bashiru na marehemu wakizunguka nchi nzima wakifanya mikutano na kupokea wanachama na viongozi walioasi upinzani??!!

CCM imetumia dola kufanya siasa! Madhaifu ya Chadema yameletwa kimkakati, unachoona kama ni kushindwa kwa Chadema ni matokeo ya mikakati ya CCM na serikali. Kama vile unacheza mechi dhidi ya mpinzani wako ambaye ana refa, VAR na FA upande wake!!!
Ndiyo maana haya tunayaandika sasa mkuu NewOrder, kuwakumbusha/kuwahimiza CHADEMA. Zama zile zimepita, wasiendelee kubweteka.
Tunawapongeza kwa "ku'savaivu' hayo yote, wakabaki wamesimama; sasa ni mwendo wa kwenda mbele.

Tunayasema yote haya sasa kwa kuamini kwamba utawala wa kikatili kama aliouonyesha hayati Magufuli umeondoka naye.
Itakuwa ni bahati mbaya sana kwa taifa letu hili, aibuke mara moja hii wa kumfikia Magufuli katika eneo hili.

Kwa hiyo ni wakati mzuri kwa CHADEMA kufanya "SIASA za chama KOMAVU," wasije wakajisahau na kuendeleza siasa za kukandamizwa.
 
Inasemwa, mara kwa mara; kwamba wanaofanikisha mipango mingi ya uchafuzi wa chaguzi, hasa huko mitaani ni hawa watu wa CCM walioko huko, kila sehemu.

Kuwepo kwa CHADEMA kwenye maeneo hayo, na wakawa tayari kabisa kuwakabili wenzao hao huko huko mitaani, nadhani hii itakuwa ni sehemu muhimu sana kwa CHADEMA kulinda haki yao.

Kumbuka, hawa wenye mabunduki wanaotumiwa na CCM, hawana mabunduki na mabomu ya machozi kila mtaa na kila kitongoji.
Wananchi watapata ujasiri sana wa kusimamia kura zao wakiona kwamba kuna uongozi mbele zao. Hawatakaa kimya kuona kura zao zikiharibiwa.

Kwa hiyo, kuwepo kwa CHADEMA hadi huko chini, sio faida ya kueneza sera zao pekee, bali pia wanawapa wananchi ujasiri wa kukataa uhujumu wa kura zao.

Ninakubaliana nawe juu ya hatua wanazo/walizochukua CHADEMA kwenda huko mitaani; nimeisikia sana habari hiyo. Nisichojua ni kiasi gani wamefanikiwa kuleta matokeo chanya kwa chama chao.
Lakini najua msemo wa wahenga kuhusu mji wa Roma.

Kama wamefika huko mitaani, basi kazi sasa ni kukaza kamba zaidi, pamoja na kuwa na hali ngumu ya ukata. Hao wanaojitolea kwa ajili ya chama wakati hali ikiwa ngumu, huenda ndio viongozi imara wa chama.
Mungu amejibu maombi ya wana Chadema na watanzania kwa ujumla.Dhulumaji Namba Wahedi wa kura,Kaelekea Jongomeo!
 
Kalamu1
miaka mitano ya Magufuli ilififisha confidence ya watu ya Nguvu ya Umma!
Zile kashkash za jpm ziliwatisha wengi!
Kumbuka mwamuko wa watu katika chaguzi za 2010 kwenda juu na ule wa 2015!

Wananchi kabla ya jpm waliandamana na kulinda kura zao,we pia ni shahidi wa hili!

Ila siyo muumini wa siasa za kashkash na maandamano!

Cha msingi Serikali iweke usawa katika siasa,ipeleke mswada bungeni wa mabadiliko ya katiba,ili jasho linalomwagika katika operesheni za kuiba kura lielekezwe pengine kwenye tija!
Ngoja nikwambie jambo mkuu wangu 'guwe_la_manga', CHADEMA wanastahiri kupewa pongezi sanaaana kwa waliyoyafanya katika miaka mitano ya hayati Magufuli.

Kazi hiyo kubwa waliyofanya ni kuepusha uhai wa waTanzania usipotee. Dalili zilikuwa wazi sana, kuwa jamaa alikuwa tayari sana kuiona damu ya waTanzania ikimwagika; na kwa ufundi mkubwa sana CHADEMA wakaiepusha.

Nikupe mfano mmoja uliotokea mapema kabisa - 'UKUTA' wa CHADEMA. Lile tukio lingekuwa ndio mwanzo wa damu kutiririka Tanzania.

Wapo waliosema CHADEMA wameogopa; sawa, na kama ni woga ndio uliosababisha UKUTA kutomwaga damu za waTanzania, woga ule ulikuwa ni woga mzuri. Hakuna kubwa sana walilopoteza CHADEMA kwa kutofanya maandamano yale; na kama yangefanyika wengi wao wangepoteza maisha na pengine wakati huu tusingekuwa tunaandika haya juu ya CHADEMA Ku'savaivu.

Kwa hiyo, CHADEMA walifanya vizuri kuwa wastahimilivu wa misukosuko mingi waliyopelekewa. Bila shaka wamejifunza mengi pia kutokana na uzoefu wa hiyo mikikimikiki iliyowapata.

Mwishoni tulianza kuona hisia za wananchi juu yao. Walipoitisha michango, wananchi waliitikia, kwa vile hapakuwepo na mabunduki ya kuwazuia wasiwachangie.
 
CCM WAJIFUNZE KUISHI NA CHADEMA AMA WAHAME NCHI VINGINEVYO CHADEMA WAPO MIAKA 1000
 
Hakuna shaka yeyote, na sidhani kwamba kuna mtu anayeweza kuhoji uwepo wa CHADEMA kama chama cha kisiasa kilicho na ushindani mkubwa hapa nchini licha ya misukosuko mingi iliyoelekezwa kwao ili kuwamaliza kabisa katika miaka mitano na zaidi sasa iliyopita.

Ni sawa kabisa kusema kwamba CHADEMA wamepitia kwenye tanuru la moto mkali, na wamepikika sawasawa kuweza kuendelea na pilkapilka zao za kisiasa na kutafuta njia ya kuliongoza taifa hili.

Sioni mbele yao, kupata hujuma tena, kama walizozipata miaka hii ya karibuni chini ya utawala wa Marehemu Magufuli. Tanzania itakuwa na bahati mbaya sana, kama patatokea hivi karibuni misukosuko iliyolitingisha taifa kama ilivyotokea wakati wa serikali ya Magufuli.

Watu wanaweza kuhoji kwamba kuendelea kuwepo kwa CCM madarakani hiyo ndiyo hatari kubwa kwa CHADEMA na vyama vingine vya upinzani.

Mimi hilo silioni hivyo kwa sasa, na hata katika CCM ya enzi za Kikwete. Hatari iliongezeka zaidi alipoingia madarakani Magufuli na kutangaza waziwazi kutopenda uwepo wa vyama vya upinzani.

CCM wenyewe kama chama, hila zao zilikuwa ni za kawaida, mradi tu wanapata ushindi, hawakuwa na lengo maalum la kuua upinzani.

CHADEMA wafanye nini (samahani kwa kuwasema CHADEMA, badala ya vyama vya upinzani, kwa sababu vingine ndio hivyo tena vimetekwa).

Huu ni wakati wa CHADEMA kuwa wazi kabisa na sera zao. Wananchi waelewe chama kinasimamia nini.

Kati ya sifa chache, lakini muhimu alizojijengea Magufuli (sio CCM) ni kuonekana kuwa mtetezi wa mali na utajiri wa nchi hii na maendeleo ya wananchi wake.

Amejitambulisha bila shaka yoyote, kwamba yeye alikuwa ni mtetezi mkubwa wa maslahi ya Tanzania na wananchi wake. Amejenga hata ukuta, kulinda Tanzanite yetu iliyokuwa inatoroshwa kwenda nchi za nje na kuwanufaisha hao zaidi ya sisi tulivyokuwa tunanufaika kwayo.

Swala la madini aliliwekea mkazo sana; hata kama ilionekana kama kulikuwa na makosa katika juhudi hizo, lakini wananchi walielewa madhumuni yake. Kuna mifano mingi kuhusu msimamo wake juu ya mali za Tanzania.

Hatujui kuhusu mikataba mbalimbali nchi yetu iliyoiingia na nchi na mashirika mbalimbali ya kimataifa, lakini bado inaelekea wananchi waliamini kwamba mikataba hiyo ilikuwa ni kwa maslahi yao.

Jambo ambalo inawezekana hakulifanya vizuri ni kuhusu mashirikiano yetu na nchi mbalimbali duniani kwa vile alikazia zaidi "ubeberu" na mambo mengine kama masimango yao.

Nimeyaandika haya, ili CHADEMA watambue kwamba kama sera zao hazieleweki kwa wananchi, kazi yao itaendelea kuwa ngumu zaidi kuwashawishi wananchi hao kuwapa madaraka. Ni lazima wajieleze waziwazi kwa wananchi, wao ni nini hasa wanakisimamia kama chama cha siasa, na nchi yetu itafaidika vipi na misimamo yao hiyo kama watapewa ridhaa ya kuongoza serikali.

Kwa hiyo, nadhani ni halali sasa kusema kwamba adui mkubwa aliye mbele ya CHADEMA ni CHADEMA yenyewe. CCM wataendelea na hadaa zao kwa wananchi, hadaa za "Hawa ni Wenzetu" kama ilivyowahi kuwa huko nyuma, na wananchi kama hawaoni mbadala wa kuwapa madaraka, watarudi huko huko kwenye chama kilichooza ndani kwa ndani.

Niseme hapa, sijui kama Samia atakuwa na nguvu za kukibadilisha hiki chama kiwe chama cha wananchi wenyewe kwelikweli. Sijui.
Hatujui
Well said.. Ngoja tuone
 
Nyoko wenu hayupo kapewa kibano na Mungu kupitia korona anafukiwa futi 6 chini ya ardhi. Sasa uwanja wa mapambano umebadilika. Uaminifu kwenu umebakia kwa wadhaifu wachache ambao nao muda wao unayoyoma. TUTAELEWANA TU NA KUONGEA LUGHA MOJA. Sisi wenye chama cha CHADEMA hatutachoka kuwasitiri viongozi wetu kwa hali na mali na kuwakabidhi kwa Mungu.
Kumbuka huyu unaemwita Nyoko ndio huyo aliye kufanya ukatambua nn maana ya uongozi wa umma kwa maslahi mapana ya Taifa
 
Mkuu nimependa hoja yako lakini hili suala lilifanyiwa kazi tokea 2012 ilipoanzishwa CHADEMA ni msingi na ndio iliopelekea hata kuimarishwa kwa kanda ili chama kishuke kwenye grassroots.

Kwahyo utekelezaji ulianza changamoto iwe ni ufuatiliaji tu lakini tukiwa wakweli CHADEMA imefanikiwa sana kushuka chini tofauti na miaka 10 iliyopita. Leo hii kanda zina ofisi zao na zinaendesha oparesheni bila kusubiri makao makuu so kuna hatua zimechukuliwa ila changamoto ni pesa tu maana wengi hapo wanajitolea tu zao mfukoni.
Mungu akulinde sana
 
Mungu akulinde sana
Mkuu 'Erythro', huyo jamaa kajibu kwa kujiamini sana, bila shaka ni mmoja kati ya viongozi wenu waandamizi.

Pamoja na hayo, tunaelewa sasa kwamba mmekwisha jpanga, lakini kazi inasubiri kufanywa.

Huo alioleza hapa ni muundo tu, mlioueneza hadi huko chini. Sasa fanyeni kazi huko huko mitaani.

Msisubiri wakati wa uchaguzi ndipo kazi ifanyike. Uhai wa chama chenu huko unategemea ufanisi wa kazi itakayofanyika huko, sio kuwepo kwenu huko.

Sasa huenda ukashindwa kuelewa ninachowahimiza hapa.

Wakati huu wa kimya kingi kisiasa nchini, ndiyo nafasi yenu ya kujijenga barabara nyumba kwa nyumba, kimya kimya huko huko vijijini/mitaani.

Hakuna sababu ya kupiga makelele mengi na kuwastua wabaya wenu.

Mkuu 'Zitto junior' kaeleza matatizo yenu ya kupungukiwa nyenzo za kufanyia kazi, lakini hilo pia linaweza kuwa ni motisha nzuri ya kujenga viongozi imara zaidi wasiotegemea kujazwa matumbo yao na kumbe vichwa vyao vikiwa kwingine. Kazi yenu kubwa hapa ni kuwatia mori hawa viongozi wenu huko matawina na wao kujua kwamba kazi zao zinatambulika kwenye chama.

Mwisho, kama kawaida yangu ya siku zote katika kuwashauri nyinyi- sera zenu ndiyo kila kitu katika kuwavuta waTanzania upande wenu.
Kubali au ukatae, hapa ndipo penye shida kubwa sana kwenu. Baadhi ya sera zenu ni ngumu sana kuziuza kwa Tanzania ya leo.

Kuzing'ang'ania hivyo hivyo, mradi mjionyeshe kuwa mpo tofauti sana na maisha wanayoyaishi waTanzania wa kawaida itaendelea kuwapa shida kubwa sana kuwashawishi waTanzania wawakubali, hata kama CCM wenyewe wameoza 'beyond recognition'.

Ninakuacha na haya machache.
 
Kumbuka huyu unaemwita Nyoko ndio huyo aliye kufanya ukatambua nn maana ya uongozi wa umma kwa maslahi mapana ya Taifa
Hamna kitu, linganisha na kiwango cha uharibifu alioufanya, halafu tafakari aina na namna ya kifo chake.
 
Back
Top Bottom