Ulifikiri lakini kumbe hujui, lengo na madhumuni ya vyama vya kisiasa duniani kote ni kutawala dola na si zaidi ya hapo, na inapotokea dola inatawaliwa na chama ambacho si chako kazi yako inakuwa kuangalia ni wapi wamekosea, ili uwatumikie wananchi inakupasa kukusanya kodi na kuzitumia kuwaletea maendeleo na wakusanya kodi hao ni chama tawala, upinzani unawatumikia kwa kukosoa chama tawala, chama cha siasa sio charitable organization kinakosoa chama tawala na kuhakikisha chama tawala kinapeleka huduma muhimu, utawala wa haki na sheria na matumizi bora ya rasilimali, kwa kuzingatia hayo chadema kimekuwa chama pekee kinachowatumikia wananchi kwa kuikosoa ccm na serikali yake kwa kila kona na hapo ndipo mnapoumia, vumilieni kwakuwa nyie ni chama tawala na mmeshindwa kutimiza malengo ya watanzania.