CHADEMA hawajakaguliwa! #FACT

CHADEMA hawajakaguliwa! #FACT

...Umeangalia taarifa ya habari ya ITV jana usiku? CHADEMA wamesema CAG asiishie kwenye hela za ruzuku akague pesa zote! I hope UMEELEWA SASA msimamo wa CHADEMA.

Sio msimamo wa chadema. Ndio sheria inasema hivo na Mwanaukweli amesha tufafanulia. Sema chadema wameamua kuunga mkono sheria. Bahati mbaya sikuona hiyo taarifa huku hakuna umeme. Kama walisema hivo basi my assumption kua hawajui sheria is correct maana hawawezi kupendekeza kitu ambacho tayari ni sheria na kusema eti ndio mapendekezo ya chama. Si waseme tu kua chama kinapendekeza sheria iwe applied. Nani alisema hapo itv? Soma sheria kwanza:

18A. Notwithstanding the provisions of sections 14 and 18, every political party receiving subvention in accordance with this Act shall, not later than 3151 October every year, submit to the Registrar financial statements and audited accounts reflecting any other source of funds and details regarding the manner in which such funds were used.” (became law in 2009)
 
Last edited by a moderator:
Hesabu za mwaka wa fedha zilizokaguliwa za miaka yote ya nyuma na 2009/2010, 2010/2011 na 2011/2012 zilishawasilishwa kwa msajili wa vyama vya siasa.
The topic under discussion sio kukaguliwa bali kukaguliwa na kuwa endorsed na CAG; PEERIOD! Je, vyama vilivyotajwa vimekukaguliwa na kuwa approved na CAG? Tuanzie hapo kwanza.
 
Uzuri ni kwamba hata wakague vp..hizo ela za umma zitaliwa tu...si unakumbuka bil 250(kama sijakosea) za wizara ya ujenzi na magufuli....zitto alipigia kelele weeee yameishia wapi? ni siasa tu!! Tena ni upepo utapita!! Sana sana watatoa matamko basi maisha yanazidi kuwa magumu kwa upande wetu!

"Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) Bw. Ludovick S.L. Utouh amekutana na Waandishi wa Habari katika Ukumbi wa Ubungo Plaza jijini Dar es Salaam ambapo ametoa ufafanuzi kukanusha tuhuma zilizotolewa kupitia baadhi ya vyombo vya habari vikimnukuu Mbunge wa Kigoma Kaskazini Mhe. Zitto Zuberi Kabwe ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya PAC kwamba, kuna ufisadi katika matumizi ya fedha zilizotolewa katika bajeti ya 2011/2012 kwa ajili ya mradi maalum wa barabara unaosimamiwa na Wizara ya Ujenzi.Bw. Utouh amebainisha kwamba kiasi cha Shs. 252,975,000,000.00 kilichohojiwa katika ukaguzi, ni fedha ambazo zimeonyeshwa kwenye taarifa za hesabu za Wizara kama ni miradi mipya ya mwaka 2011/2012 tofauti na uhalisia wenyewe ulivyo.
Serikali katika dhamira ya kuimarisha mtandao wa barabara nchini, iliweka kwenye bajeti yake ya mwaka wa fedha 2011/12 Kasma maalum ya ujenzi wa miradi ya barabara na kuitengea jumla ya shilingi 252,975,000,000.00 kwa ajili ya kulipia kazi za barabara zinazoendelea.
Fedha zote zilitolewa na HAZINA kwa madhumuni hayo na kwa kufuata taratibu za Serikali. Wizara ya Ujenzi kupitia TANROADS ililipia kazi hizo za barabara kwa maana ya madai ya Wakandarasi na Wahandisi Washauri wa miradi mbalimbali inayoendelea.
 
...Umeangalia taarifa ya habari ya ITV jana usiku? CHADEMA wamesema CAG asiishie kwenye hela za ruzuku akague pesa zote! I hope UMEELEWA SASA msimamo wa CHADEMA.
Hapo kwenye RED ni porojo za kisiasa...danganyaneni wenyewe kwa wenyewe. Na pesa zote zipi? Including ile michango ya papo kwa papo kama ile through M4C? Wewe binafsi unafahamu huwa zinakusanywa kiasi gani? Utafahamu vipi matumizi kabla hujafahamu mapato?
 
Kinachonikera ni wale wanaojifanya siku zote wana uchungu na nchi na huchukia UFISADI wa fedha za UMMA wako mstari wa mbele kuhalalisha uharamia huu wa vyama vya siasa! Huu ni unafiki, undumilakuwili na upuuzi first class!
Khaa, wewe!! Ulikuwa hujashituka tu?
 
Kwa maana nyingine hawa ndugu wanamaanisha kuwa ufisadi ukifanywa na CHADEMA ni sawa!

Kwenye thread nyingine kuna mtu (jina kapuni) alisema kua Zitto kakosea maana ikiwa Chadema watakutwa na makosa basi na yeye ataumia maana hakuna Zitto bila chadema. This thinking shows how people are selective in the way integrity should apply. Kwa mujibu ya kauli hii Zitto anatakiwa kwanza ku-assess impact ya integrity kwa chama chake before he requires all parties to be accountable. Ikiwa kuna uchafu chini ya zulia lao basi aufyete kama alivo ufyeta mwenyekiti alie mtangulia.
 
Si nimeanza kwa kuwapongeza kwa kua tayari? Ila lazima tuseme tu ukweli, kukaguliwa hawajakaguliwa. CAG Hajafanya kazi yake, sio kosa la vyama. But isiwe sababu ya byama kupiga kifua na kusema "sisi tumekaguliwa" wakati bado hawajakaguliwa.
Sasa waunge mkono harakati ya vyama kukaguliwa ili tujue 64bln zi.eenda wapi na kwanini
Ningependa utudadavulie kukaguliwa maana yake nini kwa mapana sharia za matumizi ya fedha kwa taasisi au kampuni vikiwemo vyama ni kuwa na mahesabu yaliyokaguliwa , na Kama kuna vyama ambavyo vilitafuta maoditor walioaudit kazi mahesabu yao, hawa nao tunawatuhumu kwa lipi labda tunaweza kusema kwa nini CAG hakuweka muhuli kwenye mahesabu yao, lakini CAG hakuwa na nyenzo za kufanyia kazi, hapo wa kulaumiwa itakuwa chama husika au wote CAG,Msajili na Vyama
Kwa jinsi ulivyoweka posti unataka kuudhihirishia umma kwamba kwako wewe ni chama kimoja tu kinachotakiwa kuthubitisha hizo bilioni 97 na ushehe ulizozitaja nadhani kama kuna nia njema ya Kamati wenyewe wanapaswa kujiwajibisha kwa sababu hawawezi kutuambia tangu 2009 walikuwa hawajaitisha makatibu wakuu mbele ya kamati kuwajibika kuhusu ukiukwaji wa sharia ya ukaguzi wa mahesabu ya serikali Japo nia ni njema, ya kuhakikisha kila chama lazima kifuate misingi ya sharia sasa hivi zoezi limeshageuka kwa sababu ya kuanza kunyoshea kidole chama kimoja badala ya vyama vitano, siasa imeengia kati na zoezi Zima limevurugika kwa sababu ya mwenyekiti wa kamati kulistage swala Zima kisiasa nchi yetu ni ya watu wenye maneno maneno tu hakuna mwenyekiti wa kamati ya mahesabu ya umma wala makatibu wakuu wa vyama wala msajili wala CAG.
 
Kwenye thread nyingine kuna mtu (jina kapuni) alisema kua Zitto kakosea maana ikiwa Chadema watakutwa na makosa basi na yeye ataumia maana hakuna Zitto bila chadema. This thinking shows how people are selective in the way integrity should apply. Kwa mujibu ya kauli hii Zitto anatakiwa kwanza ku-assess impact ya integrity kwa chama chake before he requires all parties to be accountable. Ikiwa kuna uchafu chini ya zulia lao basi aufyete kama alivo ufyeta mwenyekiti alie mtangulia.
Kama ulikuwepo vile kuna madundu mengi ndani ya chadema kuhusu pesa lakini wenye chama ndiyo wanacheza hizo mishe zito kawekwa kando kwa hiyo kaamua liwalo na liwe kamwaga mboga ngoja tusubiri nani atamwaga ugari.
 
Ni kweli chadema hawajakaguliwa lazima watueleze wanavyotumia hizo pesa za ruzuku.

Mwali anasema CCM hawana hata hesabu ya ukurasa mmoja uliokaguliwa na kuonyeshwa popote, Chadema wamepeleka mahesabu kwa msajili wa vyama swali ni kwa nini msajili hakupeleka kwa CAG au CAG kwa nini hakuenda kukagua vyama na kwa nini chadema hawakupeleka kwa CAG, CCM ndio walanguzi wa njia zote manake wana serikali na hazina haijatenga fedha kwa ajili ya CAG
 
Sio msimamo wa chadema. Ndio sheria inasema hivo na Mwanaukweli amesha tufafanulia. Sema chadema wameamua kuunga mkono sheria. Bahati mbaya sikuona hiyo taarifa huku hakuna umeme. Kama walisema hivo basi my assumption kua hawajui sheria is correct maana hawawezi kupendekeza kitu ambacho tayari ni sheria na kusema eti ndio mapendekezo ya chama. Si waseme tu kua chama kinapendekeza sheria iwe applied. Nani alisema hapo itv? Soma sheria kwanza:

18A. Notwithstanding the provisions of sections 14 and 18, every political party receiving subvention in accordance with this Act shall, not later than 3151 October every year, submit to the Registrar financial statements and audited accounts reflecting any other source of funds and details regarding the manner in which such funds were used.” (became law in 2009)

So ulitaka CDM wawe na msimamo siofuata sheria kama guadline?
 
Last edited by a moderator:
Kwenye thread nyingine kuna mtu (jina kapuni) alisema kua Zitto kakosea maana ikiwa Chadema watakutwa na makosa basi na yeye ataumia maana hakuna Zitto bila chadema. This thinking shows how people are selective in the way integrity should apply. Kwa mujibu ya kauli hii Zitto anatakiwa kwanza ku-assess impact ya integrity kwa chama chake before he requires all parties to be accountable. Ikiwa kuna uchafu chini ya zulia lao basi aufyete kama alivo ufyeta mwenyekiti alie mtangulia.

Kila mtu anajua Zitto ni show off anapenda kushow face kwenye mambo ambayo wakati mwingine yamemgeuka na kumdharilisha rejea mifuko ya hifadhi kawa kimya kama nzi sasa , fedha za uswisi kimya, je kwamba linaweza, Kumpa credit yeyote ya kisiasa probably, Lakini kwa sababu yumo kwenye hiyo kamati kwa kipindi kirefu japo hakuwa mwenyekiti lakini haku influence Kamati ya POAC basi na yeye analolakujibu sasa sijui yeye ataitwa na chombo gani achunguzwe: kamati yake haijitengi na ukweli kwamba waliufyata, na wataufyata , chezea CCM wewe: Kwa hili la mahesabu anaonekana kujichanganya kwa sababu ameonekana yuko biased na ametarget chama chake kwa kusema kuwa yeye hayupi kutetea chama chake bali nchi yana toka wapi hayo angekuwa kwa nchi asingethubutu kutaja chama chake popote angetaja vyama vyote kama vinavyopokea ruzuku lakini hili la kujionyesha kwamba anakifix chama chake kwanza kwa ghiriba ya kutumwa halitamsaidia, Nia ya kulazimisha ukakuguzi kwa vyama vyote ni la muhimu lakini maudhui ya ujumbe anavyoutoa mwenyekiti unaonyesha anajenga mazingira ya kuonyesha chama chake hakifuati taratibu, sasa hivi kuna kauli mbili tayari chama chake wanaonyesha na nyaraka kwamba tulipeleka kwa msajili yeye anasema hawakupeleka na barua wamejiandikia sasa huoni yupo pale kushusha hadhi ya chama chake kwa sababu anathibitishia umma kwamba anachoongea mkurugenzi wa fedha wa chadema ni mwongo
 
Kama ulikuwepo vile kuna madundu mengi ndani ya chadema kuhusu pesa lakini wenye chama ndiyo wanacheza hizo mishe zito kawekwa kando kwa hiyo kaamua liwalo na liwe kamwaga mboga ngoja tusubiri nani atamwaga ugari.

Huwezi kupata political gain kutaka kumchonganisha Zitto na chama chake hata kama namna anavyoongea anaweza kudamage image ya chama chake, chama cha Zitto wanalifahamu hilo muda mrefu wameshafanya mahesabu yao na wamepeleka kwa msajili, sasa kama leo unataka kukwepesha habari za ripoti ya Nape yakuwa na mkaguzi wa mahesabu wa aina moja mmoja tangu mwaka 1977 hapo utueleze tukusikie,kwamba CCM mahesabu yao hajapelekw apopote ,na kwamba mkaguzi wao anatoka china nadhani manake wamesema anatoka nje ya nchi pia utuambie na kama huyo mkaguzi anayetoka nje ya nchi amekuwa accredit na board ya wahasibu nchini pia utueleza
 
Kila mtu anajua Zitto ni show off anapenda kushow face kwenye mambo ambayo wakati mwingine yamemgeuka na kumdharilisha rejea mifuko ya hifadhi kawa kimya kama nzi sasa , fedha za uswisi kimya, je kwamba linaweza, Kumpa credit yeyote ya kisiasa probably, Lakini kwa sababu yumo kwenye hiyo kamati kwa kipindi kirefu japo hakuwa mwenyekiti lakini haku influence Kamati ya POAC basi na yeye analolakujibu sasa sijui yeye ataitwa na chombo gani achunguzwe: kamati yake haijitengi na ukweli kwamba waliufyata, na wataufyata , chezea CCM wewe: Kwa hili la mahesabu anaonekana kujichanganya kwa sababu ameonekana yuko biased na ametarget chama chake kwa kusema kuwa yeye hayupi kutetea chama chake bali nchi yana toka wapi hayo angekuwa kwa nchi asingethubutu kutaja chama chake popote angetaja vyama vyote kama vinavyopokea ruzuku lakini hili la kujionyesha kwamba anakifix chama chake kwanza kwa ghiriba ya kutumwa halitamsaidia, Nia ya kulazimisha ukakuguzi kwa vyama vyote ni la muhimu lakini maudhui ya ujumbe anavyoutoa mwenyekiti unaonyesha anajenga mazingira ya kuonyesha chama chake hakifuati taratibu, sasa hivi kuna kauli mbili tayari chama chake wanaonyesha na nyaraka kwamba tulipeleka kwa msajili yeye anasema hawakupeleka na barua wamejiandikia sasa huoni yupo pale kushusha hadhi ya chama chake kwa sababu anathibitishia umma kwamba anachoongea mkurugenzi wa fedha wa chadema ni mwongo

yule kijana.
 
muhusika mkuu yupo hapa, ila hathubutu kutia neno kwa sababu anajua makosa yake.

Slaa ni mwanasiasa mlaghai...

ni heri dr. Slaa amejitanabaisha hapa kwa uwazi akifuatilia hoja hii, naaamini rika yako haifai kuficha jina lako halisi kama kweli umedhamiria kuifia nchi hii.

Sisi ni vijana ambao tumeamua kujivika majina hewa na kwa heshima hiyo hatujishughulishi na majina ya watu, why wewe unayetuhumiwa kuwa daktari tena wa wanadamu unaficha jina lako halisi ilihali uko imara kuwasakama wenzako kwa uhalisia wa majina yao?!!! Napata shida kukuelewa. Come out clean and truly utuonyeshe mfano wa ufia nchi tutafuata nyayo mkuu daktari...
 
Interesting naona unajitahidi kuonesha ur true colours. Why Chadema na siyo vyama vyote vinavyopewa ruzuku? Hypocrisy.
 
Kama inaelekeza kisheria kuwa CAG ndiye mwenye mamlaka ya kufanya ukaguzi kwanini hakufanya hivyo? je, CHADEMA walikataa wasikaguliwe na CAG?

Mimi nadhani kuna upotoshaji, na kuna mpango wa kuhamisha mawazo ya watu makusudi kutoka kwenye kujadili Mswada wa Katiba mpya, badala yake tunajadili jambo ambalo kama sheria iko wazi linaweza kufanyika.
Kimsingi hakuna chama ambacho kimekataa kukaguliwa, vyama vyote wanahoji inakuwaje vyama vijikague vyenyewe? Kama utaratibu utawekwa wazi siyo ccm wala chadema, vyote vitakaguliwa kwa mujibu wa sheria za ukaguzi.

Mkuu upo sahaihi hapo kwenye RED, Sijui kwa nini hili swala lije muda huu wakati utaratibu upo wazi. Kushindwa kwa CAG kufanya kazi zake isiwe adhabu kwa vyama vya siasa.

 
Kama inaelekeza kisheria kuwa CAG ndiye mwenye mamlaka ya kufanya ukaguzi kwanini hakufanya hivyo? je, CHADEMA walikataa wasikaguliwe na CAG?

Mimi nadhani kuna upotoshaji, na kuna mpango wa kuhamisha mawazo ya watu makusudi kutoka kwenye kujadili Mswada wa Katiba mpya, badala yake tunajadili jambo ambalo kama sheria iko wazi linaweza kufanyika.
Kimsingi hakuna chama ambacho kimekataa kukaguliwa, vyama vyote wanahoji inakuwaje vyama vijikague vyenyewe? Kama utaratibu utawekwa wazi siyo ccm wala chadema, vyote vitakaguliwa kwa mujibu wa sheria za ukaguzi.


Mungi mkuu hebu tunza heshima yako bana!!!!!

Hivi hawa watu wako busy na kufungua matawi nje kumbe hawajakaguliwa halafu the excuse ni kuwa mkaguzi hajawafikia??????!!!!!!!

Mbona ruzuku zikichelewa hawakai kusubiri ila huwa vibrant kuhakikisha wanapata?????


Please let them succumb
 
Interesting naona unajitahidi kuonesha ur true colours. Why Chadema na siyo vyama vyote vinavyopewa ruzuku? Hypocrisy.

Because it is the next on the move and we dont need excuses for the second time!!!!!!!
 
Back
Top Bottom