CHADEMA Hawa waondolewe kabla ya 2014

CHADEMA Hawa waondolewe kabla ya 2014

Mleta mada anatafuta mume! , taarifa , dr. Slaa , mbowe, lissu, na tare wote wana wake zao,!
 
Mleta mada ni mzalendo wa nchi yake nakubaliana naye.

Angekuwa mzalendo wa kweli angeanzia kwanza kule kwa majangili waua tembo wetu, wanaouza ardhi ya Loliondo kwa mwarabu, waliotusababishia deni la USD 100,000,000/= la DOWANS, n.k, n.k., angeanzia huko ningemuona ni mzalendo wa kweli.lakini kwa huu ushauri wake mi namwita MCHUMIA TUMBO, MGANGA NJAA, MFUASI JANGILI, MWIZI WA RASILIMALI ZETU, NA majina mengine yanayofanana na hayo
 
Nilipoanza kusoma mwanzoni, nilishawishika na mawazo yako, lakini nilipofikia kwenye sababu za kwanini waondolewe, nikapoteza imani kama wewe ni mpenda mabadiliko au ni mmoja wa wale wanaomtumikia khafir ili kufanikisha malengo yao.

Katika sababu zote ulizotaja hakuna yoyote ya msingi na yenye ukweli. Kwa kuwa umezitaja kutokana na hisia.
katika pendekezo lako la kwamba watolewe hujaweza kupambanua ni akina nani wanafaa na kwanini? Inawezekana hapa kuna watu mnachezo beats za mtu fulani ambaye anatafuta kwa hali na mali kushika madaraka ya juu ya chama au mnamhofia mtu fulani ndani ya CHADEMA na hivyo mnatafuta kila sababu ya kumtoa ili mpate kukimaliza chama.

CHADEMA imepita katika misukosuko mikubwa na migumu tangu ya wakati wa Wangwe, lakini ni timu hii hii unayosema leo haifai ndiyo iliyoivusha CHADEMA katika mazingira magumu na ya shida hata kukiwezesha CHADEMA kuwa chama kikuu cha upinzani. Leo inakuwaje tuseme hawa ndiyo wanakiua chama? Tunataka kusema wamesahau machungu na magumu waliyoyapitia katika kukikuuza chama kwa pesa zao za mfukoni, wakati huo kikiwa hakina hata ruzuku?

Hivi kuna yeyote anayefahamu taabu adha na shida walizokutana nazo akina Zitto, mbowe, Bob Makani (RIP) slaa na wengineo wengi katika harakati ya kukijenga chadema? Mimi nasema hawa wachache ndiyo wanaojua uchungu wa chadema, na wanajua wamepitia mangapi magumu. Demokrasia ya ndani ya chama ndiyo iamue kwamba waendelee au hapana na si hisia za mtu mmoja tu anayekuja na sababu zisizo na msingi na kusema hawa watoswe. Hatutakuwa wepesi kudanganyika kirahisi kiasi hicho.

kaka umejaribu sana kuwatetea lakini bado unaungana n hoja yangu waondolewe kwasababu hawa sasa hivi wanajilipa pesa zao walizotumia kukikuza chama badala ya kutuongoza kwenye mabadiliko ya kweli, na kwa maneno yako unataka niamini kweli chadema ni chama cha watu binafsi kwasababu wana hisa na chama.
watanzania tuamke sasa tutafute mabadiliko ya kweli na si mapenzi binafsi kwa hawa wanaojiita watetezi wetu tusimamie haki.
 
Last edited by a moderator:
Mleta mada ni mzalendo wa nchi yake nakubaliana naye.

Lazima ukubaliane nae, wote mnamtumikia mtu mmoja, vipi leo hutakikwenda kunywa mataputapu majata? Hata Kikwete pia anatakiwa aachi madaraka nchi imemshinda, anachofanya ni kueneza udini na kuiba rasilimali za watanzania
 
mmeshikwa pa baya kumbe ndo wanaowaumiza vichwa na bado Dr. Slaa, Mboye na Tudnu kaza buti hadi kieleweke 2015 hakuna kulala tumechoka na chama cha mafisadi hata leo jpili chakula cha kupika tabu maisha yamekuwa magumu hadi

mapenzi binafsi kwa hawa haya saidii cha muhimu ni maendeleo ya watanzania. ingekua marekani wanamsimamo kama wako obama asingekuwa rais, watu tunataka maendeleo na si mapenzi binafsi ya mtu, hawa lazima watuachie chama utake usitake.

Wewe (MAJATA) tayari umeshajipambanua kuwa ni GAMBA, MCHUMIA TUMBO, MTETEA MAJANGILI, UPO TAYARI KUONA WATANZANIA WENZAKO WANAENDELEA KUNYANYASWA NA UTAWALA MBOVU ULIOPO SASA HIVI (Mfano wale wananchi wa LOLIONDO), wew upo tayari hata kumuuza BABA yako mzazi ili tu Mkono uende Kinywani. Mnajitafutia LAANA bure tu kwa kutetea MAJANGILI na WAUZA NCHI.
 
hivi wewe unaumwa kifafa? Una ugonjwa gani,hujajifahamu kuwa wewe ni mgonjwa? Umelogwa na nani? Ugonjwa wako waganga wa kienyeji hawauwezi, hata mhimbiri hawataweza....nenda wanakoponea wenzako India. Wewe umetumwa nya..mbafu
 
kaka umejaribu sana kuwatetea lakini bado unaungana n hoja yangu waondolewe kwasababu hawa sasa hivi wanajilipa pesa zao walizotumia kukikuza chama badala ya kutuongoza kwenye mabadiliko ya kweli, na kwa maneno yako unataka niamini kweli chadema ni chama cha watu binafsi kwasababu wana hisa na chama.
watanzania tuamke sasa tutafute mabadiliko ya kweli na si mapenzi binafsi kwa hawa wanaojiita watetezi wetu tusimamie haki.
Hakuna popote niliposema CHADEMA Ni chama cha watu binafsi. Soma mstari wangu wa mwisho, ninasema demokrasia ndiyo aimua na si mtizamo wa mtu binafsi kama wewe. Waache wanachama waamue kama bado wanawaamini hao uliowataja, kuendelea kuwa viongozi wao au hawana mpango nao tena. Si kazi yangu mimi na wewe kupiga baragumu kutaka hawa waondolewe.
 
Mleta mada ni mzalendo wa nchi yake nakubaliana naye.

huna hoja, una kelele...wewe ni moja wa watesi wa wtanzania,siku mkihamia iliko KANU ndio utamjua mjusi kwa lugha ya kichina
 
Back
Top Bottom