CHADEMA: Hatima ya Shibuda leo..

Ben hapa kweli nakuunga mkono kupata maoni ya wengi kuwa wanamtaka au hawamtaki lakini unaona wewe mwenyewe mfano hapa JF wengi tunataka Shibuda aondoke kabisa ili iwe fundisho kwa wale wote wanaoenda kinyume na msimamo wa chama, any way najua CDM viongozi wetu ni watu makini sana tunaamini watafanya maamuzi sahihi..
 

Ni kweli mkuu,hata ile position alyochukua against South Africa's position on Libya at UN security council ilikuwa even worse.Sipati Picha kama angekuwa mwenyekiti wa vijana wa chama cha siasa Tanzania.

Nilikuwa nae Nairobi last month aliniambia jinsi ilivyokuwa burning issue kwenye mkutanao wao wa party caucas uliofanyika Port Elizabeth mwezi April.It was a fire lakini walikuja na healing therapy na kumlea kisiasa ili awe consistent na party lines.He's a rare young Revolutionary comrade tulio nao Africa. Anyways,tutafika tu hata kwa Gharama ya Damu ili waafrika wapate ukweli na wafurahie kinyume na kile wanachodanganywa
 
Tatizo sio kumfukuza,tujiulize je anachokitetea Kinamaslai kwetu.Mimi nafikili kwanza tuanzie Hapo.
Mfinyanzi karibu Jf..achokitetea Shibuda hakina maslahi kwa Taifa au wewe unaona ongezeko la posho ktk vikao mbalimbali hasa vya wabuunge lina maslahi kwako?
 

Kwa kweli kumfananisha Shibuda na Malema ni kumpaisha Shibuda. Pamoja na ujeuri wa Malema, mara zote anatetea wazawa au chama chake cha ANC. Malema hashabikii vyama vya upinzani. Sidhani kama Shibuda alikuwa anatetea wananchi au chama chake cha CDM. Kwa nini Colin Powell (rep) alimuunga mkono Obama(demo)? One can say, because they are both African-American. Naamini, muktadha wa haya mawili ni tofauti kabisa.

Mim sitashangaa kama watu wanaopenda chadema ianguke watataka kumtetea Shibuda. Kwanini Shibuda anashangiliwa sana na wabunge wa magamba anapoongea? Mwenendo wa Shibuda utakatisha tamaa wengi ambao wako 50-50, yaani watu ambao wako vuguvugu kiushabiki wa siasa . Mtu atajiuliza kwanini niwape kura hawa kama na wao hawawezi kuwajibishana?

Wakati mwingine, hata mm naombea hivi vyama uchwara vya upinzani vife ili tuweze kufikiria plan B, maana kila unapoanza kufikira kwamba upinzani unakua, ghafla chama kinaporomoka. Jamani kulikuwa na NCCR na CUF, viko wapi hivi vyama siku hizi? Chadema kimekuwa haraka haraka sana kuanzia 2005 mpaka leo, kiasi kwamba ukuaji wake unatishia uhai wake maana kinakua kwa idadi ya wanachama na wafuasi bila kukua mifumo ya kukiendesha chama. Chadema wasipokuwa makini, they are going the way of the Dodo!
 
shibuda lazima yafanyike maamuzi magumu ya kuumundoa kwani kwani anabomoa chama badala ya kujenga wananich tunamwona ,tunamsikia avyofanya hakuna wakati wa kupoteza mda bora jimbo liende kwa CCM kuliko kuwa na mbunge anayejifanya ni CHADEMA kumbe ni CCM
 

..not so fast, we ar talking about a young man who is alleged to have unexplained wealth.
 
Hivi bado hajafukuzwa tu???

CHADEMA just be serious, mbona mnakua kama magamba?

Hawa watu itabidi wani-convince sana kuwaamini tena wasipo mfukuza
shumbuda,watakua wanalea tabia mbofu mbofu katika chama,...

ni chama kukosa mbunge kabisa,kuliko kuwa na mbunge kama shumbuda
 

You said it boss,no wonder kuna mtu anatoa "likes" sana humu hajakupa maana umemgusa!
 
Fikra zilizokufa always huwafaa wafu mana dunia yao ni nyingine kabisa,Fikra hai always ni kwa walio hai so tuache mfu arudishwe kwenye wafu wenziwe na kutacha sisi tulio hai na huai wetu.Aipingae kweli ni shabiki wa uongo
 
Shibuda mtu wa shoka sana! CDM ebu achane kumnyanya Shibuda au kwa sababu msukuma, mbona kina Selasini wamesifia shule za kata kamsifia JK, mbona mlikuwa mmekaa kimya au kwa sababu ni Mchagga mwenzenu? Wasukuma zindukeni hamtakiwi CDM
 
Amin nawaambia,mtu kama shibuda ingempasa jiwe la kusagia lifungwe shingoni mwake akatupwe kwenye vilindi vya bahari.
 
jamani CHADEMA hili gamba lililopo ndani halijabanduliwa tu? libandueni likagande kwenye magamba menzake
 
Shibuda mtu wa shoka sana! CDM ebu achane kumnyanya Shibuda au kwa sababu msukuma, mbona kina Selasini wamesifia shule za kata kamsifia JK, mbona mlikuwa mmekaa kimya au kwa sababu ni Mchagga mwenzenu? Wasukuma zindukeni hamtakiwi CDM
Hawa jamaa wanaonewa sana,wabunge wao waliokuwepo mtandaoni tuliwauliza kuhusu posho(haswa mkopo wa magari)...walikuwa wanajing'atang'ata tu!!,mnyika alisema atakuja march nane...mpaka leo.Regia akasema nimeambiwa mshahara wetu ni siri kubwa...but people found out anywayz.
Ukijaribu kuchunguza,hawa wabunge kweli ni wanafiki tu,wote wanataka posho kubwa na Zitto kuongelea sitting allowances was a bit of suprise to them.Ndio maana utaona wanavyomchukia humu ndani.

Shibuda ni mchumia tumbo kama wabunge wengi tu mjengoni....acheni unafiki,hamna cha falsafa wala nini.Mlijua kabla,mkataka ruzuku iongezeke,sasa inawatokea puani.
 

kaka pleas stop,

haya maneno yako yanataka kuturudisha kule tulikovuka tayari, kule kwenye dhana ya cdm ni ya ukabila na ukanda.
so unapoaanza kuwataja watu wa eneo fulani kuwa hawaaminiki ni dalili ya wewe kutaka kutuchonganisha wanachadema.
Hili lako la kutoa takwimu za watu na liwe lako tu, na hutafanikiwa kuwahadaa wana chadema kwa mlengumo wako wa ulimi mnyoofu wa mipambino na pamabaja za ulimi.
ukabila na ukanda unaotaka kuupanda upya tulishauzika na hauoti kamwe.
 
Wanachama wa magamba mliochangia mada hii kwanza mna kilio kwenye chama chenu kauguzeni madonda yenu msilete za kuleta hapa,shibuda ni nani ndani ya chadema,kama alitumwa na magamba party eti kuisambaratisha chadema kama alivyofanya mrema amenoa atafukuzwa tu.analeta kiswahili cha kizanzibari tuone kama kitamsaidia maamuzi ya chama yatachukua mkondo wake.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…