Wont be the same
JF-Expert Member
- Aug 15, 2024
- 1,564
- 2,483
Mkurugenzi wa mawasiliano CHADEMA Brenda Rupia ameandika kupitia ukurasa wake wa X kuwa hadi sasa hawafahamu ni wapo alipo John Mnyika na John Heche. Ameandika;
"Mpaka sasa, hatujui aliko Katibu Mkuu wetu John Mnyika na John Heche Makamu Mwenyekiti ! Walitekwa waziwazi na maofisa wa maeneo ya Fire na Salenda walipokuwa wakielekea mahakamani—na tangu hapo wamepotea bila maelezo yoyote.
Soma Pia: Baada ya Heche, Katibu Mkuu CHADEMA John Mnyika amekamatwa na Polisi
Tunataka majibu sasa hivi: YUKO WAPI KATIBU MKUU,YUKO WAPI MAKAMU MWENYEKITI? Acheni kugeuza Jeshi la Polisi kuwa chombo cha utekaji, mateso na uonevu wa kisiasa.
Huu ni mchepuko hatari kuelekea utawala wa kiimla!Wanaotumia nguvu dhidi ya haki leo, wasahau amani kesho—nguvu ya wananchi huwa haijawahi kushindwa.MWISHO WA YOTE, TUTASHINDA."
"Mpaka sasa, hatujui aliko Katibu Mkuu wetu John Mnyika na John Heche Makamu Mwenyekiti ! Walitekwa waziwazi na maofisa wa maeneo ya Fire na Salenda walipokuwa wakielekea mahakamani—na tangu hapo wamepotea bila maelezo yoyote.
Soma Pia: Baada ya Heche, Katibu Mkuu CHADEMA John Mnyika amekamatwa na Polisi
Tunataka majibu sasa hivi: YUKO WAPI KATIBU MKUU,YUKO WAPI MAKAMU MWENYEKITI? Acheni kugeuza Jeshi la Polisi kuwa chombo cha utekaji, mateso na uonevu wa kisiasa.
Huu ni mchepuko hatari kuelekea utawala wa kiimla!Wanaotumia nguvu dhidi ya haki leo, wasahau amani kesho—nguvu ya wananchi huwa haijawahi kushindwa.MWISHO WA YOTE, TUTASHINDA."