CDF Mabeyo: Natamani Jeshi letu liwe la kisasa, tutengeneze zana zetu

CDF Mabeyo: Natamani Jeshi letu liwe la kisasa, tutengeneze zana zetu

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
3,177
Reaction score
7,472

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania, Jenerali Venance Mabeyo amesema anatamani Jeshi letu liwe la kisasa zaidi na liweze kuchangia uchumi wa nchi na liwe la kujitegemea ‘sustainable military’.

“Kwa nini wenzetu wanatengeneza zana kutuuzia sisi, na kwa nini na sisi tusitengeneze zana za kututosheleza sisi wenyewe, wenzetu wana nyumba nzuri, hoteli, wanachangia uchumi wa nchi.

“Napenda Wanajeshi wote wawe na afya ya akili na wawe wanafikiria maendeleo muda wote,” anasema Mabeyo alipokuwa akihojiwa na ITV.

Kuhusu Jeshi kuaminiwa
"Wosia wangu kwa Watanzania ni kulisaidia Jeshi...tukifanya mambo mazuri wananchi wanatusifia, tukifanya mambo mabaya kwa bahati mbaya hata kama ni mtu mmoja kafanya...tunajumuishwa Wanajeshi wote, tunashutumiwa vibaya sana, nawaomba msiwashutumu," - Jenerali Mabeyo.

Kuhusu ugaidi Tanzania
"Baada ya kutoka Kibiti waliteremka Kusini mikoa ya Mtwara, Ruvuma...kuna wananchi wetu waliathirika...kuna baadhi ya vijiji ukienda kule Tandahimba...Nanyamba...Mtwara Vijini wameathirika... mpaka Newala baadhi ya maeneo...

"Wengine wamevamiwa, wamechomewa nyumba zao, wameharibiwa mali zao, baadhi ya Watanzania wametekwa na vile vikundi na kulazimishwa kuvuka upande wa pili," Jenerali Mabeyo.

Chanzo: ITV
 
Waachane na vitu, waangalie Ukraine inavyojitetea
Waangalie Urusi inavyoshambulia
 

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania, Jenerali Venance Mabeyo amesema anatamani Jeshi letu liwe la kisasa zaidi na liweze kuchangia uchumi wa nchi na liwe la kujitegemea ‘sustainable military’.

“Kwa nini wenzetu wanatengeneza zana kutuuzia sisi, na kwa nini na sisi tusitengeneze zana za kututosheleza sisi wenyewe, wenzetu wana nyumba nzuri, hoteli, wanachangia uchumi wa nchi.

“Napenda Wanajeshi wote wawe na afya ya akili na wawe wanafikiria maendeleo muda wote,” anasema Mabeyo alipokuwa akihojiwa na ITV.

Kuhusu Jeshi kuaminiwa
"Wosia wangu kwa Watanzania ni kulisaidia Jeshi...tukifanya mambo mazuri wananchi wanatusifia, tukifanya mambo mabaya kwa bahati mbaya hata kama ni mtu mmoja kafanya...tunajumuishwa Wanajeshi wote, tunashutumiwa vibaya sana, nawaomba msiwashutumu," - Jenerali Mabeyo.

Kuhusu ugaidi Tanzania
"Baada ya kutoka Kibiti waliteremka Kusini mikoa ya Mtwara, Ruvuma...kuna wananchi wetu waliathirika...kuna baadhi ya vijiji ukienda kule Tandahimba...Nanyamba...Mtwara Vijini wameathirika... mpaka Newala baadhi ya maeneo...

"Wengine wamevamiwa, wamechomewa nyumba zao, wameharibiwa mali zao, baadhi ya Watanzania wametekwa na vile vikundi na kulazimishwa kuvuka upande wa pili," Jenerali Mabeyo.

Chanzo: ITV
Nakuunga mkono kubwa la maadui, tatizo ni hao jamaa zetu wa kijani awataki kabisa kusikia m Tanzania ana akili za ziada ni hayo tu salute kwako.

Sent from my SM-A037G using JamiiForums mobile app
 
Kuhusu ugaidi Tanzania
"Baada ya kutoka Kibiti waliteremka Kusini mikoa ya Mtwara, Ruvuma...kuna wananchi wetu waliathirika...kuna baadhi ya vijiji ukienda kule Tandahimba...Nanyamba...Mtwara Vijini wameathirika... mpaka Newala baadhi ya maeneo...

"Wengine wamevamiwa, wamechomewa nyumba zao, wameharibiwa mali zao, baadhi ya Watanzania wametekwa na vile vikundi na kulazimishwa kuvuka upande wa pili," Jenerali Mabeyo.
haukuwa ugaidi, ilikuwa ni visasi vya mambo ya kisiasa. toka 2015 hadi 2021 tuliharibu sana sana kwenye hii sekta muhimu wa maendeleo ya nchi.
 
Jeshi linalo ajiri darasa la saba na kidato cha nne walio feri haliwezi kuwa la kisasa hata siku moja.

Jeshi linalo ajiri askari mpaka wajenge majengo (anifiti) mzee haliwezi kuwa la kisasa.

Jeshi linalo ajiri askari kisa kujuana haliwezi kuwa la kisasa. Siku ikitokea vita hawa watu hawataenda kwa sababu waliajiriwa jeshini kwa maelekezo.

Mabeyo unaondoka kwenye uongozi ila tambua askari wako wote ulio waajiri katika kipindi chako asilimia 99% wote wameajiriwa kwa maelekezo hii ni hasara.

Urusi inapata tabu Ukraine kwa sababu iliajiri wanajeshi wake kwa style aliyo itumia Mabeyo.
 
Jeshi linalo ajiri darasa la saba na kidato cha nne walio feri haliwezi kuwa la kisasa hata siku moja.

Jeshi linalo ajiri askari mpaka wajenge majengo (anifiti) mzee haliwezi kuwa la kisasa.

Jeshi linalo ajiri askari kisa kujuana haliwezi kuwa la kisasa. Siku ikitokea vita hawa watu hawataenda kwa sababu waliajiriwa jeshini kwa maelekezo.

Mabeyo unaondoka kwenye uongozi ila tambua askari wako wote ulio waajiri katika kipindi chako asilimia 99% wote wameajiriwa kwa maelekezo hii ni hasara.

Urusi inapata tabu Ukraine kwa sababu iliajiri wanajeshi wake kwa style aliyo itumia Mabeyo.

Hio Aya mwisho umeandika ujinga kabisa.
 
Back
Top Bottom