Mbowe kafungwa wakati Magufuli keshakufa na kuoza [kwa maneno yao].
Magufuli hahusiki na chochote kuhusu Mbowe kufungwa!
Namsikitikia Tundu Lissu maana alipo anaumia
Nani anmsifu Hangaya, please Kama hujui kitu uliza. Hii kesi mwanzo wake ulikuwa kipindi cha Magufuri, kamsikilize Hangaya vizuri. Alisema wenzake na Mbowe walikamatwa lakini Mbowe akakimbia nje ya nchi. Sasa fuatilia wale makomandoo walikamatwa kipindi Cha Nani akiwa Rais.
Wahenga wa Kati (si zamani sana) walinena "Siasa ni mchezo mchafu"
Yaani wanakutengenezea kosa harafu wanakusamehe na wewe unawasifia harafu wanakutumia
Hashtag Mbowe siyo Gaidi
Na wewe ni miongoni mwa mliochukizwa na mbowe kwenda ikulu jana? Poleni sanaAnakukamata anakusweka ndani baada ya kulalamikiwa na watu wengi anakutoa mwenyewe afu watu wajinga wajinga wanaanza kuimba, Tanzania imepata chifu msikivu mwenye huruma, na upendo, asingekuwa chifu angeozea ndani nyooolooo!!![emoji57][emoji57][emoji57][emoji57][emoji57][emoji57][emoji57]
[emoji15][emoji15][emoji15] nawewe umechukia Mbowe kuitwa ikulu ?Mkuu umenena vema,naomba huu uzi ubaki.Mods wanapambana kuondoa threads kama hizi...
Jiwe alishakufa!Mbowe na makomandoo watatu wanaonekena kuwa wahanga wa utawala na siasa za jiwe zaidi kuliko mrithi wake na CCM kwa ujumla. Wanaoonekana kukerwa na kuteseka zaidi Mbowe kuachiwa ni mataga na hardliners kwenye system waliorithiwa kutoka enzi za jiwe na hao ndio watatupiwa lawama yote katika sakata la Mbowe. Hili ni jambo zuri kwa afya ya taifa letu na demokrasia yetu.
Ni fursa nzuri kwa upinzani nchini.
Kweli Mbowe alikimbia nje ya nchi? Unatetea nini? Hii case ni ya Hangaya na shida ni katiba na kama ingelikuwa ni kuhusu siasa za Magufuli angeifuta toka mwanzo maana kipindi chake ndio ilipamba moto na kupelekwa kwa kasi....
Shida ilikuwa kudai katiba! Kwanini unafikiri case haijafutwa bali imesitishwa?
Mbowe amefanikiwaje kwenye hii kesi?Post yako imeongozwa na chuki kwa Mbowe na Chadema. Wewe ni mmoja ya watu walioumia sana kuona Mbowe na Chadema wamefanikiwa kwenye hii kesi. Na bado.... kuna mengi yanakuja. Mwaka huu mtakufa kwa kihoro.
Mbowe ni mwamba wa siasa nchini... just wait and see. Hujui waliongea nini. We unadhani Mbowe ni mjinga ameenda kupiga picha ikulu? Na jiulize kwanini kila mmoja alisisitiza kuaminiana? Wanaaminiana juu ya nini? Kuna makubaliano yalifikiwaIt’s now not even debatable that CCM know how to play the game of politics better than anybody.
They have an indescribable svengali type of hold on the rest of the opposition parties that renders them [the opposition] functionally ineffective.
For the life of me, somebody explain it to me. Make it make sense;
1. Unakamatwa na kufungwa bila kosa/ makosa.
2. Unafunguliwa mashitaka ya uongo/ kizushi ambayo hayana dhamana [ili usote mahabusu].
3. Tunaambiwa eti wewe ni gaidi na ushahidi upo unaothibitisha hilo [licha ya kwamba mtu yeyote mwenye akili anajua wewe siyo gaidi].
4. Kesi inaendeshwa kwa mwendo wa konokono kwa makusudi tu ili uendelee kutaabika jela.
5. Kwa vile mashitaka ni ya uongo/ kizushi, kesi inadhihirika kuwa kituko baada ya mashahidi kuanza kutoa ushuhuda wao.
6. Baada ya miezi takriban minane [8], mwendesha mashitaka ananena kuwa hana nia ya kuendelea na kesi.
7. Sijui hiyo nia ya kutotaka kuendelea na kesi imemjia lini? Labda alioteshwa usiku 🤣.
8. Mashitaka yanatupiliwa mbali. Unaachiwa huru baada ya kusota lupango kwa muda wote huo.
9. Wamekupotezea muda kwa mambo ya kizushi. Wamekutesa. Wamekunyanyasa. Wamekuvunjia heshima. Wamekuzushia mambo ya ajabu.
10. Licha ya yote hayo ambayo ni dhahiri shahiri waliyafanya kwa makusudi tu ili unyanyasike, hutopewa fidia yoyote ile.
11. Ulichoambulia ni kualikwa ikulu kwenda kukutana na mtu aliyesababisha madhila yote hayo dhidi yako. Kwenye picha nilizoziona, sikuona bilauri za juisi kama tulivyowahi kuziona hapo zamani mlipoitwa ikulu baada ya kupigwa virungu na kumwagiwa maji ya upupu. Safari hata juisi ya Sayona hukupewa! Au ulikunywa?
12. Unatoka jela, badala ya kukutana na kuongea na watu waliosimama na wewe muda wote huo ambao uliporwa uhuru wako, wewe unaenda moja kwa moja kuonana na kucheka cheka na mtu aliyekusababishia madhila yote hayo uliyoyapitia katika hizo siku 200 na kitu.
13. Umekosea sana aisee. Yeye ndo alipaswa aje kwako kukuona. Yeye na serikali yake ndo wanapaswa kukuomba radhi kwa usumbufu waliokuletea wewe pamoja na familia yako. Wao ndo wanapaswa kukufidia vyote ulivyopoteza pindi walipokuwa wamekufunga.
14. Umeonyesha udhaifu mkubwa sana ambao CCM wataendelea kuutumia kuwapumbaza na kuwahadaa kwa siku, miaka, na miongo ijayo.
15. CCM wataendelea kuwapiga, kuwanyanyasa, kuwatendea vibaya, na mwisho wa siku watawaalikeni ikulu muende kupiga picha, kunywa juisi, na kula biskuti halafu mnasahau kabisa mabaya yote mliyotendewa. Mko wepesi mno wa kusamehe na kusahau.
Sioni kabisa CCM ikitoka madarakani kwa upinzani huu tulionao. Hata kwenye katiba mpya, kama ikija kupatikana, mtahadaiwa na kurubuniwa tu. Na mtalia weee hadi mtachoka na kunyamaza.
16. Wapinzani wa Tanzania wakiongozwa na CHADEMA, hamna kabisa uti wa mgongo.
Just a bunch of weak weasels.
Nyie ndio wapumbavu mnaosababisha hata Mbowe kwenda kusujudu kwa Hangaya pamoja na kujifanya nunda!Wasukuma bana mlichelewa wapi? Sasa Raisi akikuomba ukitoka gerezani pita ikulu nikukombe msamaha uende zako kuna shida gani?
Juzi mlimlaumu lisu kwa kutoitikia wito wa kuongea na Raisi, mkasema ana kiburi, na anapoteza fursa,
Leo Raisi kajishusha kamwita wakutane kwenye ofisi za umma Ili kumwomba mbowe msamaha mnambagaza mbowe kweli?
We ulitaka Raisi amfuate mbowe mikocheni? Hata kama logistic haziruhusu
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]Chadema wakuhurumiwa mkuuKwamba Madam President Samia kamuomba Chairman Mbowe msamaha?
Wewe!!
Talk sense to a fool and he will call you foolish. You have nailed it.
Sana sana watakutukana na kuku ignore lakini umesema ukweli.
Hakuna credible upinzani Tanzania. Kuna part time politicians wenye kusimamia maslahi yao kwanza.
Hahahha... Yani bado tu hamtaki kuamini kama Samia kawazidi akili na mnataka hata hili kumdondoshea zigo Magu?Hii kesi ilifunguliwa tangu July, 2020! Je, kipindi hicho Hangaya alikuwa Rais? Je, Hangaya ndiye aliye watuma akina Kingai, Sabaya, J4, Goodluck, na Swilla kuendesha kikundi cha watu wasio julikana?
Usihamishe magoli mheshimiwa. Hii kesi ilifunguliwa wakati wa yule kipenzi wako magufuli. Na ndiyo muasisi wa huu utaratibu wa kutengeneza matukio, na mwisho anakuja kuyatatua ili kujiongezea ujiko.
Tuliona wakati wa kikotoo kwa wafanyakazi, wakati alipo watumbua kwa fedheha wateule wake yeye mwenyewe, nk. Lakini pia ni magufuli huyo huyo ndiye muasisi wa huu mgawanyiko mkubwa kwa watanzania, baada ya kuendekeza ubaguzi, ukatili, uonevu, dhuluma, kuwakumbatia matapeli kama akina Sabaya, nk.
Sasa anapotokea Mtawala mwingine, akachagua njia tofauti na mtangulizi wake, nadhani ni wakati wetu wapenda maridhiano kumtia moyo.
Nyie ndio wapumbavu mnaosababisha hata Mbowe kwenda kusujudu kwa Hangaya pamoja na kujifanya nunda!
Sasa Zitto alipomwambia Samia amsamehe Mbowe mkaanza kumtukana eti amsamehe kwa kosa gani!
Unaona sasa Mbowe kakaza weee mwishowe kaona wafuasi wake hawamjali akaona aende kusujudu.
Sent from my SM-T295 using JamiiForums mobile app
Mataga ndio wanasema hivyo![emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]Chadema wakuhurumiwa mkuu
Sent from my SM-T295 using JamiiForums mobile app
Hwataki kuamini kama Samia keshawazidi kete! Ila wanajaribu kujifariji kwamba Magufuli ndio alimkamata Mbowe!Kesi ilifunguliwa July 2020 na Mbowe akakamatwa July 2021???
Only in Tanzania where you’ll find this kind of fuckery [emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
Sukuma gang naona unataka kulia Mbowe ametoka. Mlikuwa mnajitekenya kuwa atafungwa.🚮🚮🚮Mbowe amefanikiwaje kwenye hii kesi?
Kusujudu? Ndio kufanikiwa huko?
Sasa si bora angesujudu tu toka day 1 kuliko kukaa rumande miezi yote 8?
Sent from my SM-T295 using JamiiForums mobile app