econonist
JF-Expert Member
- Jul 11, 2015
- 23,336
- 35,229
It’s now not even debatable that CCM know how to play the game of politics better than anybody.
They have an indescribable svengali type of hold on the rest of the opposition parties that renders them [the opposition] functionally ineffective.
For the life of me, somebody explain this to me. Make it make sense;
1. Unakamatwa na kufungwa bila kosa/ makosa.
2. Unafunguliwa mashitaka ya uongo/ kizushi ambayo hayana dhamana [ili usote mahabusu].
3. Tunaambiwa eti wewe ni gaidi na ushahidi upo unaothibitisha hilo [licha ya kwamba mtu yeyote mwenye akili anajua wewe siyo gaidi].
4. Kesi inaendeshwa kwa mwendo wa konokono kwa makusudi tu ili uendelee kutaabika jela.
5. Kwa vile mashitaka ni ya uongo/ kizushi, kesi inadhihirika kuwa kituko baada ya mashahidi kuanza kutoa ushuhuda wao.
6. Baada ya miezi takriban minane [8], mwendesha mashitaka ananena kuwa hana nia ya kuendelea na kesi.
7. Sijui hiyo nia ya kutotaka kuendelea na kesi imemjia lini? Labda alioteshwa usiku 🤣.
8. Mashitaka yanatupiliwa mbali. Unaachiwa huru baada ya kusota lupango kwa muda wote huo.
9. Wamekupotezea muda kwa mambo ya kizushi. Wamekutesa. Wamekunyanyasa. Wamekuvunjia heshima. Wamekuzushia mambo ya ajabu.
10. Licha ya yote hayo ambayo ni dhahiri shahiri waliyafanya kwa makusudi tu ili unyanyasike, hutopewa fidia yoyote ile.
11. Ulichoambulia ni kualikwa ikulu kwenda kukutana na mtu aliyesababisha madhila yote hayo dhidi yako. Kwenye picha nilizoziona, sikuona bilauri za juisi kama tulivyowahi kuziona hapo zamani mlipoitwa ikulu baada ya kupigwa virungu na kumwagiwa maji ya upupu. Safari hata juisi ya Sayona hukupewa! Au ulikunywa?
12. Unatoka jela, badala ya kukutana na kuongea na watu waliosimama na wewe muda wote huo ambao uliporwa uhuru wako, wewe unaenda moja kwa moja kuonana na kucheka cheka na mtu aliyekusababishia madhila yote hayo uliyoyapitia katika hizo siku 200 na kitu.
13. Umekosea sana aisee. Yeye ndo alipaswa aje kwako kukuona. Yeye na serikali yake ndo wanapaswa kukuomba radhi kwa usumbufu waliokuletea wewe pamoja na familia yako. Wao ndo wanapaswa kukufidia vyote ulivyopoteza pindi walipokuwa wamekufunga.
14. Umeonyesha udhaifu mkubwa sana ambao CCM wataendelea kuutumia kuwapumbaza na kuwahadaa kwa siku, miaka, na miongo ijayo.
15. CCM wataendelea kuwapiga, kuwanyanyasa, kuwatendea vibaya, na mwisho wa siku watawaalikeni ikulu muende kupiga picha, kunywa juisi, na kula biskuti halafu mnasahau kabisa mabaya yote mliyotendewa. Mko wepesi mno wa kusamehe na kusahau.
Sioni kabisa CCM ikitoka madarakani kwa upinzani huu tulionao. Hata kwenye katiba mpya, kama ikija kupatikana, mtahadaiwa na kurubuniwa tu. Na mtalia weee hadi mtachoka na kunyamaza.
16. Wapinzani wa Tanzania wakiongozwa na CHADEMA, hamna kabisa uti wa mgongo.
Just a bunch of weak weasels.
Please, no research no right to speak. Wewe unaongea bila utafiti.
1. Kwanza, Mh Mbowe alipotoka gerezani jana alielekea nyumbani kwake, na kusema kwamba Jana asingeweza kuongea na waandishi wa habari bali anapanga kuonana na Viongozi wake wa CHADEMA Kwanza halafu baadae ndio ataongea na wananchi. Kuna kosa gani Hapo?. Mbowe ana leadership qualities. Amejipa muda kwanza kabla ya kuongea na umma, maana angeweza kutamka neno kwa hisia likaleta chuki na tafakuri.
2. Pili, Rais Samiah baada ya kikao Cha Jana na Mh Mbowe, alisema kwa kauli yake , kuwa yeye binafsi ndio alimuomba Mh Mbowe waonane Jana hiyo hiyo. Unadhani Ni kwanini aliamua iwe Jana na sio siku nyingine?. Rais Samiah ndio alikuwa wa kwanzan kuiambia dunia kuwa Mbowe ni Gaidi ilibidi achukue initiative kuonana naye kiutu uzima na kufanya mapatano ingali mapema.
3. Tatu, Fahamu ya kwamba Mh Mbowe kapoteza vingi Sana. Kabomolewa bilcanas, kuharibiwa shamba lake, kufungiwa gazeti lake la Tanzania daima, kufukuzwa kwenye Jengo la NHC ambalo kiasili ni Mali yao, kutajwa kwenye madawa ya kulevya na makonda, kuvamia na wasiojulikana na kusingiziwa alikuwa amelewa , kufungiwa akaunti yake na pesa zake kuchukuliwa na mwisho kuibiwa ubunge wake ambao hata museveni alithibitisha siku ya kuapishwa Magufuri.
Hivyo, wakati wengine wakikimbia Mbowe alisimama imara na Leo watesi wake wanashangaa, tumefanyia ubaya wote lakini hajalipa kisasi wala kuonesha chuki.
4. Nne Fahamu ya kwamba sio kila mtu ana roho ya kulipiza kisasi na kutaka kuonekana shujaa. Kuna watu siku wakiondoka duniani ndio watu wataujua unuhimu wao. Mmoja wapo Ni Mbowe kwamba yote aliyofanyiwa lakini hajalipiza kisasi maana hiyo siyo hulka yake.
5. Tano, hivi nikuulize Kati ya muoneaji na muonewa nani mbaya?. Yani mtu anayeonea wenzake na yule anayeonewa tunamlaumu nani?. Yani wewe unamlaumu Mbowe kwa kuonewa baadala umlaumu aliyemuonea kwa nini anaonea roho isiyo na hatia.
6. Sita, CHADEMA na Mh Mbowe hawaitaji kupambana na waoneaji au kulipiza kisasi maana Karma inafanya kazi yake. karma imelipia karibia wote waliomuonea Mbowe, kuanzia mwendazake, makonda, Sabaya, Byakanwa na Spika Ndugai. Ndio maana mama kwa kulijua Hilo akaona akutane na Mh Mbowe wayamalize.
Mwisho, hii dunia tunapita tuishi kwa upendo maana kila mtu ataiacha dunia na huko anapokwenda atawajibika kwa maonevu aliyewatendea wanadamu wenzake walioumbwa na Mungu. Tuache chuki za kisiasa hazitatufikisha popote tutambuane kama watanzania na sio kwa vyama vyetu.