CCM’s svengali hold

CCM’s svengali hold

Umeanalyse too brief but very brilliant arguments bro [emoji41] you never let me down as always and usual. Hakuna nyumbu alie too critical atakae eza kustand against those points narrated above, period.
Mara ya Kwanza nilipousikia wimbo wa 2pac WA 'how long will they mourn me' nikasema kwangu Mimi sijui km utatokea wimbo mwingine nitakaoupenda zaidi ya huo. Kabla sijakaa vizuri, dmx (r.i.p) akaachia Ile kitu 'who we be'. Nikajikuta najishangaa Kwa maneno yangu.

Ni vigumu kupangua hoja za nyani ngabu, lkn tusihitimishe hivyo haraka haraka tu......
 
Yaliyoongelewa kabla ya kutoka ,hakuna anayejua na kwa akili yangu ya Kinyakyusa najua hakwenda mwenyewe, bali alipelekwa ili yule mkuu aliyetoa shutuma BBC ajisafishe kwenye uso wa mabeberu
 
Kwa kuwa wewe si mwanasiasa unapaswa kusamehewa kwa ulichokiandika. Tuna references nyingi sana za matukio kama hayo duniani, lakini hazikuwamaliza watu kisiasa bali ziliwapaisha
  1. NELSON MANDELA: Hakuna binadamu aliekaa jela kwa wakati mrefu kwa kesi ya mchongo ya uhaini kama yeye lakini hakuomba msamaha kwa watesi wake ili wamwachie ingawa walitamani sana afanye hivyo, alipotoka Gerezani hakuwasusa maadui zake kisiasa waliomfunga na kumtesa kwa miaka 27 alikaa nao wakazungumuza kichozaliwa ndio hiyo afrika kusini ya sasa.
  2. JOMO KENYATTA: Alifungwa kwa kesi ya uhaini ya kuchonga na kukaa gerezani kapengurya,alipotoka alikaa chini na watawala wakajadiriana ndio hiyo kenya unayoiona leo.
Hiyo ni mifano miwili iliyotokea hapa jirani kwetu, mazungumuzo,majadiriano,na watawala ndio njia pekee inayoweza kumfikisha mbowe na CHADEMA kwenye malengo yao.

Njia anayopaswa kuipita mbowe ni ile waliyopita kina Nelson Mandela mashujaa wa afrika,Kwa hiyo akisusa atakuwa anamkomoa nani?

Kamwe Mbowe hataingia kwenye njia za kihaini na kigaidi ili kupigania haki za watanzania, na njia halali ndio hiyo ya kuzungumuza.
Lakini kwenu vijana poleni sana maana ujana ni maji ya moto.
Hawa vijana wa shule za kata hawajui nguvu ya mazungumzo/kukaa meza moja.
Kwa mifano hiyo hapo juu uliyowatolea kwa ufupi,naamini hawataelewa chochote.
Kongole.
 
Ujinga imewajaa sana, ulitegemea Mbowe akae ndani miaka yote? Unajuaje Kama Mbowe ndo aliomba kuonana na Mh Rais? Je yale unayoyasema kuridhiana huo ni maridhiano yapi?

Suala la mtu kumtesa mtu kwa kesi ya uongo siyo upande wa Upinzani tu...rejea matajiri waliokamatwa na kuswekwa ndani kipindi Cha Marehemu kisa na mkasa wamekataa pesa zao zisiguswe na Serikali.

Mtu yeyote anaweza kuguswa na Serikali chini ya katiba na Sheria zetu hizi awe Rais au kapuku Kama wewe na Mimi..
Punguzeni ujinga na piganieni Sheria na katiba ibadilishwe tofauti na hapo mtawasingizia sana CCM...au hujui kua Ndugai ameguswa kuliko ata huyo Mbowe?
Kuna watu wanaandika upumbavu mpaka basi.
Mimi ni mhanga wa "umafia wa kidola" wa kuvamiwa kwa duka la kubadilisha fedha za kigeni.
Kuna wafanyabiashara wengi ambao tumekuwa wahanga wa uovu wa kidola wa mwendazake.
Watu wanaandika tu kwa kuwa hawajakumbwa na hayo mambo.
Katiba mpya ni suluhisho.
 
Sema unautetea Uislamu tu, hayo mengine yoote mbwembwe tu!
Argumentum ad hominem?!!!

😳😳Dini ya mtu inaingiaje katika maslahi kuntu ya nchi ?!!!

Taifa kwanza kabla ya hizo imani zilizoletwa....

Wewe unaitetea dini gani na kuliweka taifa nyuma?!!!
 
Kwa saa 24 nilitafakari nikidhani kuna kitu sielewi, baada ya kuliona bandiko wasi wasi umenitoka.

1. Wanopinga hoja za Nyani Ngabu sizioni hoja zao.
Kusema ana chuki tu bila kujibu hoja ni kukosa hoja.

2. Mbowe (FAM) hakupaswa kwenda Ikulu jana.
Sababu alizotoa NN ni za kweli na naongezea, kwamba, Mbowe aliomba kuonana na Rais SSH kabla ya kukamatwa ,barua haikuwahi kujibiwa.

Ni kwa mantiki gani anakwenda Ikulu kabla ya kuonana na waliompigania akiwa gerezani!

3. Kuna hoja kwamba '' watu walitaka FAM afanye nini''. Well, hakutakiwa kwenda Ikulu katika muda mfupi bila kujua mazingira ya nchi. Sijui kama alikutana na kamati kuu ya CDM.

4. ''Kwamba Mbowe hataki kulipa kisasi'' hakuna anayemtaka alipe kisasi, kujipa muda wa kutathmini si kulipa kisasi ni kujijenga kifikra baada ya mateso ya miezi 8.

5. Kwamba ''alijipa muda na kwenda nyumbani'', si kweli , aliwaambia watu hataongea hadi muda utakapofika, ilikuwaje muda wa kuonana na Rais SSH ulipatikana?

Kwa waliofuatilia kesi, kulikuwa na 'presha' kutoka ndani na nje ya nchi.
Mahakama ilikuwa ma wakati mgumu achilia mbali ilivyovurunda mwenendo wa kesi.

Rais SSH kukutana na viongozi wa dini ilikuwa njia tu ya 'kutokea''

Kwa hali yoyote CDM na Mbowe walikuwa na 'upper hand''. CCM, wakati mgumu.

Mbinu iliyotumiwa na CCM inamwacha FAM na swali '' kwanini alikwenda''

Rais SSH alijua Mbowe naungwa mkono, kitendo cha kutoka tu kinatosha kuongeza ari ya Chadema na Wananchi kudai haki ikiwemo katiba. FAM alikuwa na ''leverage' na ni wazi ame squander

Mbinu iliyotumiwa kwa Masheikh wakitoka wakae kimya haikufanya kazi kwa Mbowe.

Mbinu mpya ni kumwita 'kumtia adabu'' tunaweza kukuweka ndani na kukutoa!
Je hilo mnaliona sawa?

Mbinu ya kupiga picha na kutoa hotuba za maridhiano ni ''kumfunga Mbowe mdomo'' .

Mbinu ya kumwita ni kumlazimisha 'akiri kwamba amesamehewa''

Ukitaka kujua mbinu ya 'kusamehewa' imetumikaje, siku Mbowe anakwenda Ikulu ni siku hiyo hiyo vijana wa JKT wanasamehewa. Kwa maana kwamba Rais SSH ni mtu wa kusamehe.

Je, Mbowe alihitaji kusamehewa? Kwa kosa gani? Lilithibitishwa wapi? Je alipewa kujitetea?

CCM wanasema hizo ndizo siasa safi! kwamba wanamwambia Mbowe atulie , siasa chafu zitamrudisha kule, si ugaidi ni siasa ! hilo ndilo Mbowe alitesekea?

Kwa namna yoyote ile Chadema na uongozi chini ya Tundu Lissu wana la kueleza Wanachama wao likuwaje wakamwacha ''mfungwa'' akakimbilia Ikulu bila kumpa taarifa za chama na bila kumpa muda wa kutafakari!!!

''Mashtaka ya NN'' yana mashiko! kuna ''hoja za kujibu''

JokaKuu Pascal Mayalla
 
It’s now not even debatable that CCM know how to play the game of politics better than anybody.

They have an indescribable svengali type of hold on the rest of the opposition parties that renders them [the opposition] functionally ineffective.

For the life of me, somebody explain it to me. Make it make sense;

1. Unakamatwa na kufungwa bila kosa/ makosa.

2. Unafunguliwa mashitaka ya uongo/ kizushi ambayo hayana dhamana [ili usote mahabusu].

3. Tunaambiwa eti wewe ni gaidi na ushahidi upo unaothibitisha hilo [licha ya kwamba mtu yeyote mwenye akili anajua wewe siyo gaidi].

4. Kesi inaendeshwa kwa mwendo wa konokono kwa makusudi tu ili uendelee kutaabika jela.

5. Kwa vile mashitaka ni ya uongo/ kizushi, kesi inadhihirika kuwa kituko baada ya mashahidi kuanza kutoa ushuhuda wao.

6. Baada ya miezi takriban minane [8], mwendesha mashitaka ananena kuwa hana nia ya kuendelea na kesi.

7. Sijui hiyo nia ya kutotaka kuendelea na kesi imemjia lini? Labda alioteshwa usiku 🤣.

8. Mashitaka yanatupiliwa mbali. Unaachiwa huru baada ya kusota lupango kwa muda wote huo.

9. Wamekupotezea muda kwa mambo ya kizushi. Wamekutesa. Wamekunyanyasa. Wamekuvunjia heshima. Wamekuzushia mambo ya ajabu.

10. Licha ya yote hayo ambayo ni dhahiri shahiri waliyafanya kwa makusudi tu ili unyanyasike, hutopewa fidia yoyote ile.

11. Ulichoambulia ni kualikwa ikulu kwenda kukutana na mtu aliyesababisha madhila yote hayo dhidi yako. Kwenye picha nilizoziona, sikuona bilauri za juisi kama tulivyowahi kuziona hapo zamani mlipoitwa ikulu baada ya kupigwa virungu na kumwagiwa maji ya upupu. Safari hata juisi ya Sayona hukupewa! Au ulikunywa?

12. Unatoka jela, badala ya kukutana na kuongea na watu waliosimama na wewe muda wote huo ambao uliporwa uhuru wako, wewe unaenda moja kwa moja kuonana na kucheka cheka na mtu aliyekusababishia madhila yote hayo uliyoyapitia katika hizo siku 200 na kitu.

13. Umekosea sana aisee. Yeye ndo alipaswa aje kwako kukuona. Yeye na serikali yake ndo wanapaswa kukuomba radhi kwa usumbufu waliokuletea wewe pamoja na familia yako. Wao ndo wanapaswa kukufidia vyote ulivyopoteza pindi walipokuwa wamekufunga.

14. Umeonyesha udhaifu mkubwa sana ambao CCM wataendelea kuutumia kuwapumbaza na kuwahadaa kwa siku, miaka, na miongo ijayo.

15. CCM wataendelea kuwapiga, kuwanyanyasa, kuwatendea vibaya, na mwisho wa siku watawaalikeni ikulu muende kupiga picha, kunywa juisi, na kula biskuti halafu mnasahau kabisa mabaya yote mliyotendewa. Mko wepesi mno wa kusamehe na kusahau.

Sioni kabisa CCM ikitoka madarakani kwa upinzani huu tulionao. Hata kwenye katiba mpya, kama ikija kupatikana, mtahadaiwa na kurubuniwa tu. Na mtalia weee hadi mtachoka na kunyamaza.

16. Wapinzani wa Tanzania wakiongozwa na CHADEMA, hamna kabisa uti wa mgongo.

Just a bunch of weak weasels.
Hakuna adhabu kubwa kwa mkosaji kama msamaha.
 
Mkosaji ni nani hapa?
Nafsi ya hatia haiwezi kutulia mpaka angalau isikie NENO toka kwa aliyekosewa. Mwanamke akifumaniwa na mumewe na mume asichukue hatua yoyote, yaani ajifanye kama hakuna kilichotokea, hutamani hata apigwe au afokewe kwa kosa lingine. Mbowe kauweza sana huu mchezo, natoka gerezani na wewe ndo uliyenipeleka gerezani lakini nakusalimia tu katika jina la Yesu!! Mtu katoka Dodoma kwenda Dar kupata angalau NENO tu la mfungwa wa michongo mnaona ni jambo dogo hilo?
 
It’s now not even debatable that CCM know how to play the game of politics better than anybody.

They have an indescribable svengali type of hold on the rest of the opposition parties that renders them [the opposition] functionally ineffective.

For the life of me, somebody explain it to me. Make it make sense;

1. Unakamatwa na kufungwa bila kosa/ makosa.

2. Unafunguliwa mashitaka ya uongo/ kizushi ambayo hayana dhamana [ili usote mahabusu].

3. Tunaambiwa eti wewe ni gaidi na ushahidi upo unaothibitisha hilo [licha ya kwamba mtu yeyote mwenye akili anajua wewe siyo gaidi].

4. Kesi inaendeshwa kwa mwendo wa konokono kwa makusudi tu ili uendelee kutaabika jela.

5. Kwa vile mashitaka ni ya uongo/ kizushi, kesi inadhihirika kuwa kituko baada ya mashahidi kuanza kutoa ushuhuda wao.

6. Baada ya miezi takriban minane [8], mwendesha mashitaka ananena kuwa hana nia ya kuendelea na kesi.

7. Sijui hiyo nia ya kutotaka kuendelea na kesi imemjia lini? Labda alioteshwa usiku 🤣.

8. Mashitaka yanatupiliwa mbali. Unaachiwa huru baada ya kusota lupango kwa muda wote huo.

9. Wamekupotezea muda kwa mambo ya kizushi. Wamekutesa. Wamekunyanyasa. Wamekuvunjia heshima. Wamekuzushia mambo ya ajabu.

10. Licha ya yote hayo ambayo ni dhahiri shahiri waliyafanya kwa makusudi tu ili unyanyasike, hutopewa fidia yoyote ile.

11. Ulichoambulia ni kualikwa ikulu kwenda kukutana na mtu aliyesababisha madhila yote hayo dhidi yako. Kwenye picha nilizoziona, sikuona bilauri za juisi kama tulivyowahi kuziona hapo zamani mlipoitwa ikulu baada ya kupigwa virungu na kumwagiwa maji ya upupu. Safari hata juisi ya Sayona hukupewa! Au ulikunywa?

12. Unatoka jela, badala ya kukutana na kuongea na watu waliosimama na wewe muda wote huo ambao uliporwa uhuru wako, wewe unaenda moja kwa moja kuonana na kucheka cheka na mtu aliyekusababishia madhila yote hayo uliyoyapitia katika hizo siku 200 na kitu.

13. Umekosea sana aisee. Yeye ndo alipaswa aje kwako kukuona. Yeye na serikali yake ndo wanapaswa kukuomba radhi kwa usumbufu waliokuletea wewe pamoja na familia yako. Wao ndo wanapaswa kukufidia vyote ulivyopoteza pindi walipokuwa wamekufunga.

14. Umeonyesha udhaifu mkubwa sana ambao CCM wataendelea kuutumia kuwapumbaza na kuwahadaa kwa siku, miaka, na miongo ijayo.

15. CCM wataendelea kuwapiga, kuwanyanyasa, kuwatendea vibaya, na mwisho wa siku watawaalikeni ikulu muende kupiga picha, kunywa juisi, na kula biskuti halafu mnasahau kabisa mabaya yote mliyotendewa. Mko wepesi mno wa kusamehe na kusahau.

Sioni kabisa CCM ikitoka madarakani kwa upinzani huu tulionao. Hata kwenye katiba mpya, kama ikija kupatikana, mtahadaiwa na kurubuniwa tu. Na mtalia weee hadi mtachoka na kunyamaza.

16. Wapinzani wa Tanzania wakiongozwa na CHADEMA, hamna kabisa uti wa mgongo.

Just a bunch of weak weasels.
Hivi ulitaka Mbowe aanzishe maandamano baada ya kuachiwa?
Are you serious?
 
Umeanalyse too brief but very brilliant arguments bro [emoji41] you never let me down as always and usual. Hakuna nyumbu alie too critical atakae eza kustand against those points narrated above, period.
Analysis is parochial and addresses the simpletons way of thinking.
 
Anakukamata anakusweka ndani baada ya kulalamikiwa na watu wengi anakutoa mwenyewe afu watu wajinga wajinga wanaanza kuimba, Tanzania imepata chifu msikivu mwenye huruma, na upendo, asingekuwa chifu angeozea ndani nyooolooo!!![emoji57][emoji57][emoji57][emoji57][emoji57][emoji57][emoji57]
Teh teh haya maajabu yako Tanzania pekee yake tu.
 
Kwa namna yoyote ile Chadema na uongozi chini ya Tundu Lissu wana la kueleza Wanachama wao likuwaje wakamwacha ''mfungwa'' akakimbilia Ikulu bila kumpa taarifa za chama na bila kumpa muda wa kutafakari!!!
Inasemekana alialikwa kwenda huko na mweny nchi ?
 
Hata kama inaenda mrama, wapinzani are not capitalizing on it!

Very disappointing.
Watu wamechoshwa na hizi komedi za siasa!

Wapinzani hakuna bongo! Ni matawi madogo ya CCM, binafsi naamini hivyo!
Wote wachumia tumbo! Hakuna mwenye kuwaza masuala taifa!
 
Back
Top Bottom