CCM Zanzibar wajipanga kukwamisha Serikali tatu

nngu007

JF-Expert Member
Aug 2, 2010
15,862
5,797


KITAIFA
[h=1][/h]




CCM+clip.jpg

Bendera ya Chama Cha Mapinduzi(CCM) Picha na Maktaba

Na Mwinyi Sadallah, Mwananchi

Posted Januari18 2014 saa 10:17 AM

KWA UFUPI

  • Ni katika mkakati wa pamoja katika kikao cha pamoja kilichofanyika mapema wiki hii.



Zanzibar.
Wabunge na Wawakilishi wa CCM Zanzibar tayari wamekutana na kupanga mkakati wa pamoja kwa nia ya kupinga Mfumo wa Muungano wa Serikali tatu uliopendekezwa katika Rasimu ya Tume ya Mabadiliko ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, imefahamika juzi visiwani Zanzibar.


Uchunguzi wa Mwananchi umebaini kuwa kikao hicho kilifanyika Ofisi Kuu ya CCM Kisiwanduwi kuanzia saa 9.00 Alasiri hadi saa 1:00 ya usiku chini ya Uenyekiti wa Makamo wa Pili wa Rais, Balozi Seif Ali Iddi na Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho Zanzibar, Vuai Ali Vua.

Vyanzo mbalimbali vya habari kutoka ndani ya kikao hicho vinaeleza kwamba, wabunge hao wa Bunge la Katiba walipokea msimamo wa chama chao na kutakiwa kuutetea kwa umoja wao watakapojadili rasimu hiyo.

Baada ya kuwasilishwa ajenda hiyo kikaoni, wajumbe mmoja baada ya mwingine walitoa maoni yatakayofanikisha kufuzu kwa mkakati huo huku wengine wakishauri wajumbe wapewe nafasi ya kuijadili rasimu kupitia semina ili kujua ni maeneo gani yana manufaa na hasara.

Imeelezwa Mwakilishi Hamza alisema kutokana na umuhimu wa rasimu hiyo,waandaliwe semina maalumu ili kukijadili kwa kina kifungu baada ya kifungu kabla ya kufikia uamuzi wa kupitisha na kutopitisha mambo yasiyokuwa na manufaa kwa Zanzibar na Usalama wa Muungano wenyewe.

Alisema suala la Katiba halipaswi kujadiliwa haraka,linahitajika umakini kwa manufaa ya Zanzibar na wananchi wake na kukiomba chama hicho kitayarishe semina hiyo ya uchambuzi, kujenga uwezo na ufahamu kabla ya Bunge la Katiba halijakutana na kujadili rasimu hiyo.

Hata hivyo kwa upande wake, Asha Bakari aliweka wasiwasi wake kwa wajumbe kuhusu kukosa msimamo wa pamoja na kutaka kila mjumbe aulizwe kama anataka Serikali tatu au mbili badala ya kuja kupanga na baadaye kusalitiana mbele ya safari na kuhatarisha misingi ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.

Hata hivyo, mfanyabiashara maarufu na Mbunge wa Mpendae ,Salum Turkey alisema kutokana na uzito wa suala la mfumo wa Muungano ni vizuri kukafanyika kisomo maalumu (halbadiri) na mjumbe yoyote atakayekwenda kinyume na msimamo wa chama apate laana duniani na akhera.

Wazo hilo licha ya kuwashtuwa baadhi ya wajumbe, wengi walionekana kukubaliana naye ili mkakati wa chama hicho uweze kufikiwa huku Waziri wa zamani,Hamza Hassan akisisitiza rasimu yote ya katiba ichambuliwe yanayokubalika na yasiyokubalika kabla ya Bunge la Katiba kukutana mwaka huu.

Hata hivyo Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar, Vuai Ali Vuai hakuweza kupatikana kuelezea kikao hicho na maazimio yaliyofikiwa baada ya kuulizwa kwa njia ya simu na kueleza yupo katika kikao na atafutwe muda mwengine mara baada ya kikao hicho.

Vuia aliwahi kutoa msimamo wake wakati akifungua mkutano wiki mbili zilizopita akisema atakuwa wa mwisho kuafiki.

 
Kwani hii KATIBA ikimalizika WANANCHI hatutakuwa na UHURU wa kuipigia KURA kama tunaipenda au hatuipendi?

KENYA waliweza kupigia kura KATIBA yao Sisi ni kwasababu ya kutukuza MATAKWA ya CCM sisi Wananchi hatutapiga KURA?

Kweli huo sio UDIKTETA?
 
Gharama za kuendesha serikali yao na Muungano!!waliambiwa wakawa wabishi!sasa wamepewa serikali yao kamili wanaanza albadiri!upuuzi!
 
SISIEM wanajaribu kuzuia kimbunga kwa kuweka kuta za mifuko ya mchanga, Kenya mwaka 2005 waliikataa katiba iliyopendekezwa na Rais Kibaki, mwaka 2007 wakaingia kwenye machafuko baada ya uchaguzi kuchakachuliwa, mwaka 2010 wakapata katiba nzuri na iliyomridhisha kila raia. Naamini Tanzania tutaipata tu katiba tunaiyoitaka tena ndani ya miaka 10 ijayo na hapo CCM hatakuwa wameshasahalika kama KANU.

Kwani hii KATIBA ikimalizika WANANCHI hatutakuwa na UHURU wa kuipigia KURA kama tunaipenda au hatuipendi?

KENYA waliweza kupigia kura KATIBA yao Sisi ni kwasababu ya kutukuza MATAKWA ya CCM sisi Wananchi hatutapiga KURA?

Kweli huo sio UDIKTETA?
 
Jamani, Zanzibar wanataka nini?!
Niliwahi kusema kuwa hawajui wanataka nini nikaambiwa nawatukana. Sijui hili tutasemaje.

Wazushi wanasema asilimia 60 hawataki muungano, asilimia 90 wanatapika wakisikia neno muungano.
Wanasema Tanganyika imewashikilia, inawazuia. Wamefunguliwa mikono ndiyo haya tunayoyaona.

Adui yao mkubwa ni Tanganyika, akiondoka sijui nani atachukua nafasi yake.
Miaka nenda rudi wamepiga kelele Tanganyika irudi, Tanganyika inarudi wanasema hapana isirudi!
FJM wamelalamika mambo ya muungano yalikuwa 11 yakaongezwa hadi 22.
Warioba kaja kupunguza hadi 7 in fact 5 ukiyaangalia kwa akili timamu. Leo hawataki tena.
22-17= 5. Tulitegemea washangilie sana hakuna shamra shamra. Mtanganyika hakuguswa na lolote katika hayo 17

Hawajui wanataka nini, na ninarudia tatizo si muungano tatizo ni zaidi ya hapo...........
 
Last edited by a moderator:
Watuwache watanganyika tupumuwe na serikali yetu. Hiyo ya muungano hata ikifa sawa tu.
 
Hawa watu ni wa ajabu sana kwa muda mrefu walikuwa wanaomba serikali ya Tanganyika ambayo ni mshirika wa muungano irudi ili waweze kujadiliana nayo kuhusu muundo bora wa muungano, jambo ambalo ni sahihi. Jambo la kushangaza ni kuona kuwa baada ya kilio chao kusikilizwa wanakuwa mstari wa mbele kuhakikisha kuwa serikali ya Tanganyika haipatikani. Wajuzi wa mambo ya Zanzibar naomba mnifahamishe; hivi hawa ndugu zetu wanahitaji nini hasa? maana wanakuwa kama mgonjwa anaekaribia kufa, kila kitu huwa kwake ni kibaya.
 

Kuna kuchagua moja kati ya mawili. Kama wanahitaji kuwa katika Muungano, wachague Serikali mbili ndio zitakazowasaidia wao ila wapiganie mambo ya Fedha na Ushuru isiwe ya Muungano, mengine yote hayana tatizo. Wakiweza hivyo, maana yake ni kwamba iwe na power ya kujitungia sera zake za Biashara, Fedha na Ushuru.

Namna ya pili ni kuukataa Mungano kabisa, absolutely (sitaki kujadili madhara yake hapa bali wenyewe wanajua). Lakini kama wangali wanataka Muungano, basi Serikali tatu si muafaka kwao, hivyo naunga mkono hoja kama wanataka kupitisha azimio la kuipinga.
 
Kuna kuchagua moja kati ya mawili. Kama wanahitaji kuwa katika Muungano, wachague Serikali mbili ndio zitakazowasaidia wao ila wapiganie mambo ya Fedha na Ushuru isiwe ya Muungano, mengine yote hayana tatizo. Wakiweza hivyo, maana yake ni kwamba iwe na power ya kujitungia sera zake za Biashara, Fedha na Ushuru.

Namna ya pili ni kuukataa Mungano kabisa, absolutely (sitaki kujadili madhara yake hapa bali wenyewe wanajua). Lakini kama wangali wanataka Muungano, basi Serikali tatu si muafaka kwao, hivyo naunga mkono hoja kama wanataka kupitisha azimio la kuipinga.
Zinedine kwanini unadhani serikali 3 ni matatizo kwao?

Nadhani walitaka serikali ya Tanganyika ili kusiwepo na kujificha katika muungano.
Kile walichokitaka cha mbia mwenza si ndio serikali 3.

Mambo waliyotaka yaondolewe imefanyika kwa kuondoa 17 na kubaki na 7.
Kati hayo katiba ni nyaraka hivyo yanabaki 6.
Ukiondoa la vyama vya siasa yanabaki 5.
Sasa hapo wanalalamika nini tena? Hiyo si nzuri kwao na kwamba wamepata walichokitaka?

Swali la pili, unadhani serikali 2 zitawezekana? Kuna malalamiko kutoka bara ambayo ni mazito tu, nani atawashawishi Watanganyika kufuata kila wznz wanachotaka?
Je si kuwa wznz wameamsha simba aliyekuwa amelala na kumkaribisha tembo sebuleni?

Swali la tatu, kwa kuondoa ushuru na na fedha kunasababu gani za kuendelea na muungano?
Nani atalipia huo muungano wa serikali 2 na kwa kiasi gani?

Nne, kwanini unadhani kuvunja muungano ni disaster wakati hilo litatoa mamlaka kamili kwa znz


Hebu tusaidiane kidogo
 
Kwa taarifa hizi, watajua wanataka nini baada ya kupewa semina elekezi.
Mkuu semina elekezi itashirikisha kundi gani?
Kuna znz kwanza na mamlaka kamili
Kuna muungano wa mkataba
Kuna serikali 2
Kuna serikali 3
 
Zinedine kwanini unadhani serikali 3 ni matatizo kwao?



Swali la pili, unadhani serikali 2 zitawezekana? Kuna malalamiko kutoka bara ambayo ni mazito tu, nani atawashawishi Watanganyika kufuata kila wznz wanachotaka?


Swali la tatu, kwa kuondoa ushuru na na fedha kunasababu gani za kuendelea na muungano?
Nani atalipia huo muungano wa serikali 2 na kwa kiasi gani?

Nne, kwanini unadhani kuvunja muungano ni disaster wakati hilo litatoa mamlaka kamili kwa znz


Hebu tusaidiane kidogo

Swali la Kwanza, Serikali tatu zitatoa usawa wa kuchangia muungano lakini itaondoa fursa za kufaidika na Muungano, hope umenielewa!

Swali la Pili: Kwa Bara hakuna tatizo, wenyewe hawanaga msimamo linapokuja suala la Zanzibar; na pia kwa kuwa kiwango cha uelewa wa muungano ni mdogo kwa Bara (not interested at al) kwa jamii ya watu wengi, hivyo ushawishi wowote wa viongozi wao watafuata. Kwamba naamini mpaka sasa hawajaamua na hata hawajui impact ni nini maana wapo wanaoamini hizi nchi ni mbili kinadharia lkn practically ni kama nchi moja toka enzi na enzi hivyo hawajui wapige kura ya vipi? 2/3/1 hata 4 naamini wako tayari. Issue ni kule kwa upande wa Zanzibar ambapo watu wako interested ingawa hali ni kama ulivyomjibu Mchambuzi

Swali la tatu: Itabidi nipitie mfumo wa utawala wa China na Taiwan then nitakuwa na fact za kujibu, lakini idea hapa ni kwamba Sera za Uchumi za Zanzibar ni viwanda vidogo, na utalii wakati Tanganyika ni pamoja na Kilimo, Rasilimali na Viwanda vikubwa hivyo ni ngumu kuwa na Sera ya pamoja ya Biashara vinginevyo itabidi Katiba iweke kifungu kiitwacho "Special and Differential Treatment (SDT)" kama ilivyo WTO na nchi maskini. Hii ingehusisha na "relaxation" za kutekeleza baadhi ya mambo ya Muungano na rationale ziko za kutosha za kutetea hili. Aidha, kwa kuwa na Sera yake ya Biashara (inaweza kuachia ya Fedha), ingeweza kujiunga na mashirika kama WTO na mengineyo na hivyo kuwa na uwezo wa moja kwa moja wa ku-affects economic policies zake kama nilivyozigusia hapo juu.

Tena nashangaa sana Wazanzibari hawakupendekeza suala hili la SDT kwenye Katiba-Nadhani nimekujibu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom