CCM yawaruka Mussa Mkangaa na wenzake

CCM yawaruka Mussa Mkangaa na wenzake

Mii naona hapa Chadema ndo wamechemsha, sasa akishindwa kulipa watamfanyaje? hata akifungwa watakuwa wamefaidika vipi?

Waliochemsha ni wao waliofungua kesi isiyo wahusu, kamahawawezi kulipa jela ipo na watafanywa kama Lusinde alivyosisitiza kwenye uchaguzi wa Arumeru.
 
Mbona alipovuliwa ubunge Lema CCM walishangilia na kuwapongeza waliofungua kesi, leo tena wamewageuka...duuuh
 
Mii naona hapa Chadema ndo wamechemsha, sasa akishindwa kulipa watamfanyaje? hata akifungwa watakuwa wamefaidika vipi?

kama ambavyo mahakama imetenda haki kurejesha ubunge wa lema ndivyo hivyo hivyo mahakama itatoa suluhisho la haki kama wakishindwa kulipa, itakachoamua mahakama ndio haki yenyewe!
 
Hahahahahaha! Hao wamasai akina mollel na kivuyo wana ngombe bana watawauza watalipa gharama hizo! Chezea chama cha mafisadi ww? Wangeshinda wangewapongeza sana....thats a lesson kwa wengine kufungua kesi za kijinga jinga like that
 
TL: "wakishindwa kulipa gharama ya kesi tangu mwanzo tatawafunga"
 
Hivi wanasheria wote waliojazana huko CCM na maprofesa kibao hawakung'amua hii kitu inaitwa "locus standi" ingewatoa knockout? The ruling was so simple: wale waliofungua kesi (wanajiita wapiga kura) hawakuwa na haki ya kufanya hivyo kwani shauri lililoletwa mahakamani halikuathiri haki zao kama wapiga kura!

Eti Batilda alitukanwa; rubbish! So what? Alipaswa alalamike Batilda mwenyewe na sio hao vitimbakwira. Na iwe mwisho kwa CCM kutumia "mawakala" kufungua kesi za uchaguzi.
 
Yess. Wakome kuchumia matumbo nyambafu

Na Tundulisu akiongea na Hotmix ya EATV leo alisema yafuatayo na ninanukuu,"Najua hawana uwezo wa kulipa hizi garama ila tutaziandika na kuzipeleka mahakamani na wasisipolipa tutawafunga ili iwe fundisho kwa wengine."
 
Chama cha mapinduzi CCM kimesema kama chama wao hawawezi kulipa gharama ya kupinga kesi ya ubunge wa Lema kwa kuwa wao hawakuwa na mashaka na ubunge wa Lema. Kwa hiyo gharama hizo zilipwe na waliokuwa na mashaka na ubunge wa Lema.

Duh hawa jamaa sahaulifu sana... Si nakumbuka hata yule katibu mkuu wao wa zamani (Marope) aliwaambia wakafungue kesi wote walioshindwa!!!!!! Kaazi kweli kweli...
 
Leo mwanasheria wa CHAMA CHA DEMOCRASIA NA MAENDELEO MH. tundu lisu wakati akiongea Kuhusu hukumu ya Lema kwenye kituo cha EATV amesema kuwa Viongozi wa CCM wamekuwa wakiwatuma wanaowaita wapiga kura kufungua kesi dhidi ya wabunge wa CHADEMA, Hivyo basi wanatakiwa kulipa gharama zote walizotumia kwenye kesi, Vinginevyo watafungwa
 
kesi hii imeleta madhara ya kiuchumi,kiafya,kielimu n.k wanapaswa kuwajibishwa ili iwe fundisho.
 
hapo patamu sana na nilishato angalizo humu ndani ,nikauiza CCm watakuwa tayari wafaa hawa rafiki wako wasio wa kweli katika dhiki?
 
Safi, ni stahiki a malipo ya watu wasio na akili wanatumwa na kutekeleza kwa kufuata bendera ya mafisadi.

Ni funzo kwa wengine wote bendera hufuata upepo
 
He is absolute right!

WASHTAKI WOTE HAWA 3 hawana nguvu za kiuchumi kupata ada ya zaidi ya tsh MILLION 15 ZINAZOTAKIWA KULIPWA MAHAKAMA KUU kwenye kesi za uchaguzi!Ni dhahiri hela hizo za kufungulia kesi walipewa na CCM!

Hawa walitumwa tu na inavyoijua CCM watawaruka kuwa HAWAKUWATUMA!CHADEMA mdai hela zenu zote na wakishindwa wafungeni jela ili liwe fundisho kwa mtu kuingilia kesi zisizomhusu!

Haki yako ya kupiga na kupigiwa kura HAZIKUVUNJWA unaenda kufungua kesi ya nini?Jina lako lilikuwepo kwenye ballot?Ulitukanwa na Lema directly kwenye mikutano yake?CHADEMA funga hawa jamaa!
 
Chama cha mapinduzi CCM kimesema kama chama wao hawawezi kulipa gharama ya kupinga kesi ya ubunge wa Lema kwa kuwa wao hawakuwa na mashaka na ubunge wa Lema. Kwa hiyo gharama hizo zilipwe na waliokuwa na mashaka na ubunge wa Lema.

nani ametoa kauli hiyo?
 
Back
Top Bottom