CCM yapata aibu kubwa huko Temeke

CCM yapata aibu kubwa huko Temeke

Mtemvu ndiye mbunge pekee wa Dsm atakayerudi mjengoni mwaka 2015


Sina uhakika sana na hili. Sasa kwa nini watu waligomea mkutano wake? I am just being curious?

Tiba
 
Mkuu weka kumbukumbu sawa sema Mtemvu anawasaidia vijana kwenda "utumwani" huko Uarabuni.

Tiba
YUVA HERI MIMI SIJASEMA! Tiba !shauri yako ngoja watoke nanii utajuta kuwachokoza!
 
Mzungu ndiye aliyeleta utumwa angalia mabaki ya watu weusi yako wapi katika mabara ya dunia ?
Du mmeanza!
Hata kama ndivyo lakini angalau waliacha waliktubu na hadi leo wanatubu,kwahiyo unachotaka kusema kwa kuwa wazungu walileta basi Waarbu wanaendeleza!
 
Asilimia kubwa ya wakazi maskini jijini Dsm wanaishi Temeke. Umaskini unaweza kutafsiriwa kulingana na mazingira au utamaduni wa wahusika. Hata hivyo, kwa ujumla wake makazi duni, miundo mbinu duni na vipato vidogo vinaiweka Temeke kuwa maskini zaidi.
Kuondoa umaskini Temeke ni muhimu kubadilisha fikra za wakazi kwanza na siyo kutegemea mbunge binafsi kuendeleza eneo hilo.
 
Na bado hadi mshuke daraja
mwaka huu.Mbinu zimewaishia.

 
Kwa hali hii mtu utaacha kuumia moyoni na kumalizia hasira zako kwa chadema?
 
Tuwekeeni na ile Picha ya Kamanda Msigwa akifungua Kampeni za Udiwani kata ya Nduli.
 
Asilimia kubwa ya wakazi maskini jijini Dsm wanaishi Temeke. Umaskini unaweza kutafsiriwa kulingana na mazingira au utamaduni wa wahusika. Hata hivyo, kwa ujumla wake makazi duni, miundo mbinu duni na vipato vidogo vinaiweka Temeke kuwa maskini zaidi.
Kuondoa umaskini Temeke ni muhimu kubadilisha fikra za wakazi kwanza na siyo kutegemea mbunge binafsi kuendeleza eneo hilo.
Ila ndo ndo pato kubwa la nchi linapotokea......nadhani hilo ulisahau kuandika
 
Huku kunduchi jana zilikuja daladala 3 zimeleta wafuasi wa ccm kutoka tabata,gongolamboto na ukonga!!Yaani aibu tupu.na kila aliyeletwa alipewa sh5000.CCM inapata tabu sana kukusanya watu kwa ajili ya mikutano yake
 
Mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni. Kusema kweli mimi binafsi nina m-admire mbunge wa temeke kwa kazi nzuri ya kuhakikisha barabara zinakuwa za lami kwenye vichochoro vyote. Kwa hili nampongeza huyu mbunge. Hakuna wilaya ambayo barabara zake nyingi ni lami kama temeke.

Tiba

Mkuu Tiba Temeke ni makazi yangu, huyu mbunge hajafanya lolote, kumbuka kuwa 2010 aliponea chupu chupu na kama si chakachua asingekuwepo. Miradi ya barabara chache kwa siku hizi imefanikishwa sana na manispaa yenyewe hata kama Mtemvu asipokuwepo zingejengwa tu. Na zilizojengwa si nyingi kiasi kile. Temeke ni chafu sana, hakuna maendeleo, wachina wamekimbilia kupanga huko hasa maeneo ya Chang'ombe kwa sababu ni maeneo ambayo ni sawa kama vile hakuna uongozi. Kazi kubwa ya madiwani na mbunge wao ni kukusanya mafao kupitia magodauni na biashara haramu kwa wachina. Wakazi wana matatizo sana, mathalan kiwanda cha bia cha seerengeti kinachafua sana makazi kwa waste na mbunge alifika pale akawapa wananchi namba fake ya simu hadi leo huwa haipatikani, diwani wake aitwaye Noel mwenye bar maeneo ya chang'ombe jirani na kota za serikali ndiyo hatari kabisa hana mpango na wananchi. Kuna kampuni ya taka ya MP environment imagine imeweka sehemu ya parking ya gari za taka ndani ya makazi na wakati mwingine huwa wanamwaga taka kwenye mtaa kama dampo dogo wakisubiri kupakia magari makubwa. Imekuwa ni kero na taka nyingine ni sumu kabisa. Diwani yuko jirani kiasi na sehemu wanapomwaga taka hizo lakini hasemi chochote kwa kuwa mwenye MP Environment ni yule mzee wa CCM ambaye walikuwa na tender ya kukusanya ushuru stendi ya mabasi ubungo na ambaye mwanaye amekuwa kinara wa ile kitu mbaya. Mtemvu hafai, na 2015 atadondoka.
 
Mbunge wa Temeke mh, Abasi Mtemvu na diwani mh. Zena Mgaya jana walipata aibu kubwa katika kata ya Tandika baada ya kuhutubia watu kumi katika viwanja vya Mbonde yangu macho.



Mtevu amewadanganya wananchi wa Temeke kwamba Temeke kuna barabara nzuri kuliko Masaki na mwisho kaishia kuwatuhumu
CHADEMA kwamba wanawadanganya watu wa Temeke kwamba CCM aifai.
.
View attachment 134996

Hahahahaaa! CCM imekufa!
 
Mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni. Kusema kweli mimi binafsi nina m-admire mbunge wa temeke kwa kazi nzuri ya kuhakikisha barabara zinakuwa za lami kwenye vichochoro vyote. Kwa hili nampongeza huyu mbunge. Hakuna wilaya ambayo barabara zake nyingi ni lami kama temeke.

Tiba

Njoo Moshi uone lami vichochoroni
 
Mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni. Kusema kweli mimi binafsi nina m-admire mbunge wa temeke kwa kazi nzuri ya kuhakikisha barabara zinakuwa za lami kwenye vichochoro vyote. Kwa hili nampongeza huyu mbunge. Hakuna wilaya ambayo barabara zake nyingi ni lami kama temeke.

Tiba
Kamani kweli basi ahame kwa maCCM.
 
Sina uhakika sana na hili. Sasa kwa nini watu waligomea mkutano wake? I am just being curious?

Tiba

Wamepata ajira viwandani. Wakiwa na kazi siyo rahisi kuacha pesa na kuhudhuria mikutano
 
Back
Top Bottom