Elections 2010 CCM yapangua hoja za Chadema

Wa Ndima

JF-Expert Member
Aug 13, 2010
1,526
323
CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kimemuomba Msajili wa Vyama vya Siasa kuiagiza Chadema kuisoma na kuielewa vizuri Sheria ya Gharama za Uchaguzi na sheria nyingine za uchaguzi ili kuepuka usumbufu.

Ombi hilo ni miongoni mwa maombi matatu yaliyotolewa na CCM wakati wa kujibu malalamiko yaliyotolewa na Chadema, dhidi ya Mgombea wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia CCM,
Jakaya Kikwete.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa jana na Katibu Mkuu wa CCM, Yusuf Makamba kwa vyombo vya habari, Chadema haijaelewa Sheria ya Gharama za Uchaguzi na kama
inaelewa, imeamua kufanya usumbufu usiokuwa wa lazima kumwekea pingamizi Kikwete.

Taarifa hiyo imenukuu kifungu 21 (1), “wakati wa uteuzi, kampeni
za uchaguzi au uchaguzi, kitendo kinachokatazwa ni…” Kwa tafsiri ya asili kwa mujibu
wa taarifa hiyo, maneno ya kifungu hicho hayahusu ahadi zitakazotekelezwa
baada ya uchaguzi kwa kutumia fedha za Serikali, bali kinahusu ahadi zinazotekelezwa wakati wa mchakato wa uteuzi wa wagombea, kampeni au wakati wa uchaguzi.

Pia kinakataza wagombea kutumia fedha binafsi kutekeleza ahadi zake. “Kama sheria hiyo ingekataza kutoa ahadi zitakazotekelezwa baada ya uchaguzi, ingeua dhana nzima
ya kampeni inayovitaka vyama vya siasa na wagombea kuelezea mambo gani wanayoahidi iwapo watachaguliwa,” alisema Makamba.

Makamba amesisitiza kuwa malalamiko ya Chadema hayahusu sheria hiyo kwa sababu haipingani na dhana nzima ya kampeni kama ilivyoainishwa ndani ya Sheria ya
Uchaguzi, pamoja na maadili ya uchaguzi kwa ajili ya uchaguzi wa rais, wabunge na madiwani.

CCM inasema inashangazwa na hatua iliyochukuliwa na Chadema kwa kuwa jambo lililofanywa na mgombea wa CCM, linafanywa pia na wagombea wa vyama vingine
akiwamo Dk. Willibrod Slaa. CCM inamshangaa Kaimu Katibu Mkuu wa Chadema, John Mnyika anayejiita raia mwema kwa kutomuwekea Dk. Slaa pingamizi kwa kutoa ahadi kemkem katika kampeni zake kama kweli anaamini kuwa kutoa ni ukiukwaji wa sheria.
 
swala si liko kwa Tendwa .
MAKAMBA HAKUNA ANACHOJUA KWA KWELI Aibu,hawana waongeaji wengine huyu kichwa maji anaboa
 
Na ndo maana Tendwa aliomba aende ITV ili atoe huo "ufafanuzi" wake wa sheria hiyo katika kipindi cha Kipima Joto leo saa 3 usiku. Hii nadhani Tendwa anafanya kinyume cha utaratibu katika azma yake ya kuizima pingamizi la Chadema. Inakuwa kama vile kabla ya hakimu kutoa hukumu yake katika kesi anayoisikiliza, kwanza anakwenda kwenye TV kufanya mjadala na watu wengine kuhusu sheria ambayo chini yake ndiyo mshtakiwa anashitakiwa. Is this right? Nadhani hii ichukuliwe kama hoja moja ya kukata rufaa huko mbele iwapo pingamizi la Chadema litatupwa.
 
Wa Ndima
Member

Join Date
Fri Aug 2010
Posts
44
Thanks : 0
Thanked 10 Times in 5 Posts
 
Wa Ndima
Member

Join Date
Fri Aug 2010
Posts
44
Thanks : 0
Thanked 10 Times in 5 Posts


Una maana gani kuNOTE kujiunga kwangu. Sio wote unaowaona wamejiunga hapa ni wapya!!! Wengine tumefungua ID mpya. Soma hoja sio unaorodheka nimejiunga lini, unataka kumaanisha nini? Kwamba sijui kitu au? Acha hizo
 
Na ndo maana Tendwa aliomba aende ITV ili atoe huo "ufafanuzi" wake wa sheria hiyo katika kipindi cha Kipima Joto leo saa 3 usiku. Hii nadhani Tendwa anafanya kinyume cha utaratibu katika azma yake ya kuizima pingamizi la Chadema. Inakuwa kama vile kabla ya hakimu kutoa hukumu yake katika kesi anayoisikiliza, kwanza anakwenda kwenye TV kufanya mjadala na watu wengine kuhusu sheria ambayo chini yake ndiyo mshtakiwa anashitakiwa. Is this right? Nadhani hii ichukuliwe kama hoja moja ya kukata rufaa huko mbele iwapo pingamizi la Chadema litatupwa.


Umeona enh??
 
makamba simuamini allisema bashe si raia mara akasema raisi kikwete alidanganywa, anasema mtu akimtukana baba yako inabidi usinyamaze wakati kikwete alimtukana baba yangu mfanyakazi kuwa ni mzandiki,mfitini,muongo na mnafiki.nitampinga kikwete kurejesha thamani ya mzazi wangu so makambba usijichanganye
 

Attachments

  • je akifikisha miaka 25 itakuwaje.jpg
    je akifikisha miaka 25 itakuwaje.jpg
    16.4 KB · Views: 42
Huyu Mkuu ndo maana Alibaka akafukuzwa Kazi ya Ualimu Hana analojua kwani ukiangalia kwa Nyekundu utaona tu kwani Rais Kikwete anatumia madaraka yake vibaya sasa hawezi akampandisha waziri kuahidi kitu hii ni kutumia madaraka yake KIBABE, Sasa huyu Mzee kweli amezeeka maana anajibu vingine. Angalizo Tendwa Ofisi imekushinda au wewe si msomi au umechanguliwa tuu Fuatasheria usifuate watu wansema nini? Utajiaibisha sana wakienda mahakamani.:mad2:


CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kimemuomba Msajili wa Vyama vya Siasa kuiagiza Chadema kuisoma na kuielewa vizuri Sheria ya Gharama za Uchaguzi na sheria nyingine za uchaguzi ili kuepuka usumbufu.

Ombi hilo ni miongoni mwa maombi matatu yaliyotolewa na CCM wakati wa kujibu malalamiko yaliyotolewa na Chadema, dhidi ya Mgombea wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia CCM,
Jakaya Kikwete.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa jana na Katibu Mkuu wa CCM, Yusuf Makamba kwa vyombo vya habari, Chadema haijaelewa Sheria ya Gharama za Uchaguzi na kama
inaelewa, imeamua kufanya usumbufu usiokuwa wa lazima kumwekea pingamizi Kikwete.

Taarifa hiyo imenukuu kifungu 21 (1), "wakati wa uteuzi, kampeni
za uchaguzi au uchaguzi, kitendo kinachokatazwa ni…" Kwa tafsiri ya asili kwa mujibu
wa taarifa hiyo, maneno ya kifungu hicho hayahusu ahadi zitakazotekelezwa
baada ya uchaguzi kwa kutumia fedha za Serikali, bali kinahusu ahadi zinazotekelezwa wakati wa mchakato wa uteuzi wa wagombea, kampeni au wakati wa uchaguzi.

Pia kinakataza wagombea kutumia fedha binafsi kutekeleza ahadi zake. "Kama sheria hiyo ingekataza kutoa ahadi zitakazotekelezwa baada ya uchaguzi, ingeua dhana nzima
ya kampeni inayovitaka vyama vya siasa na wagombea kuelezea mambo gani wanayoahidi iwapo watachaguliwa
," alisema Makamba.

Makamba amesisitiza kuwa malalamiko ya Chadema hayahusu sheria hiyo kwa sababu haipingani na dhana nzima ya kampeni kama ilivyoainishwa ndani ya Sheria ya
Uchaguzi, pamoja na maadili ya uchaguzi kwa ajili ya uchaguzi wa rais, wabunge na madiwani.

CCM inasema inashangazwa na hatua iliyochukuliwa na Chadema kwa kuwa jambo lililofanywa na mgombea wa CCM, linafanywa pia na wagombea wa vyama vingine
akiwamo Dk. Willibrod Slaa. CCM inamshangaa Kaimu Katibu Mkuu wa Chadema, John Mnyika anayejiita raia mwema kwa kutomuwekea Dk. Slaa pingamizi kwa kutoa ahadi kemkem katika kampeni zake kama kweli anaamini kuwa kutoa ni ukiukwaji wa sheria.
 
Yap!! Hii Sheria lazima itawakamata tu wana CCM, Wakuu tunawaomba mkaze buti kwani ukibadili kitu mfano Rangi kwa nyumba itakubidi utumie gharama muda mwingi ili ubadilishe sasa CHADEMA mtaweza tu
 
Mshahara Jk anaowaahidi wafanyakazi utalipwa na serikali yake ikiwa watamrudisha madarakani au unaanza kulipwa katika miezi ya kipindi cha campaign? Na kama ni katika kipindi hicho ni kwa nini isiwe rushwa? Maana mwenye dhamana ya kutangaza mishahara mipya ni waziri baada ya pesa hizo kuidhinishwa na bunge. Tumuulize makamba mpayukaji, ni wapi na lini mshahara mpya ulitangazwa kwa mujibu wa sheria na kanuni za nchi? Kuahidi ni jambo moja na utekelezaji wa ahadi ni jambo jingine linalopaswa kutumia taratibu na sheria za nchi. Kweli chama tawala kimekosa umakini na kupoteza mwelekeo. Hapa Chadema wanachotakiwa ni kujiandaa kukiburuza ccm mahakamani ikiwa Tendwa hatatenda haki, ili wakamuumbue makamba kule kama ilivyotokea kwa kihiyo wa Temeke.
 
Una maana gani kuNOTE kujiunga kwangu. Sio wote unaowaona wamejiunga hapa ni wapya!!! Wengine tumefungua ID mpya. Soma hoja sio unaorodheka nimejiunga lini, unataka kumaanisha nini? Kwamba sijui kitu au? Acha hizo
=====

Mbona unaripuka kana kwamba hujui kitu kabisa!?
 
Una maana gani kuNOTE kujiunga kwangu. Sio wote unaowaona wamejiunga hapa ni wapya!!! Wengine tumefungua ID mpya. Soma hoja sio unaorodheka nimejiunga lini, unataka kumaanisha nini? Kwamba sijui kitu au? Acha hizo


Unataka tuchangie nini? Makamba ni kichefu chefu kama amekutuma, hatuna matarajio ya jema toka kwake ni mpinzani wa haki za wengine isipokuwa zenu
 
Una maana gani kuNOTE kujiunga kwangu. Sio wote unaowaona wamejiunga hapa ni wapya!!! Wengine tumefungua ID mpya. Soma hoja sio unaorodheka nimejiunga lini, unataka kumaanisha nini? Kwamba sijui kitu au? Acha hizo
ID mpya august?
wewe ni Augusteez kwishney.
Kwani ukileta hoja yako kwa id yako ya awali itakosa mashiko?

uzuri ni kwamba huwezi kushindana na saikolojia yako mwenyewe.
mtajiumbua sana hapa kipindi hiki
 
Back
Top Bottom