benzemah
JF-Expert Member
- Nov 19, 2014
- 1,504
- 3,034
Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa, ikiongozwa na Mwenyekiti wa CCM a Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Ndugu Dkt. Samia Suluhu Hassan, imekutana katika kikao chake maalum, kilichofanyika Ikulu ya Chamwino, jijini Dodoma, leo Alhamis, Agosti 17, 2023.
Pamoja na mambo mengine, Kamati Kuu imefanya uteuzi wa Ndugu Bahati Keneth Ndingo kuwa mgombea wa ubunge kwa tiketi ya CM katika Jimbo la Mbarali, mkoani Mbeya, kwenye uchaguzi mdogo wa ubunge uliopangwa kufanyika tarehe 19 Septemba 2023, kufuatia kifo cha aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo, Ndugu Francis Leonard Mega, aliyefariki dunia tarehe 1 Julai, 2023.
Aidha, Kamati Kuu ya CCM, imezipongeza Serikali zake zote mbili, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, inayoongozwa na Dkt.Samia Suluhu Hassan na Seriali ya Mapinduzi ya Zanzibar, chini ya Dkt. Hussen Ali Mwinyi, kwa namna zinavyoendelea kuwatumikia wananchi kwa vitendo kupitia utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya Mwaka 2020 - 2025.
Pamoja na mambo mengine, Kamati Kuu imefanya uteuzi wa Ndugu Bahati Keneth Ndingo kuwa mgombea wa ubunge kwa tiketi ya CM katika Jimbo la Mbarali, mkoani Mbeya, kwenye uchaguzi mdogo wa ubunge uliopangwa kufanyika tarehe 19 Septemba 2023, kufuatia kifo cha aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo, Ndugu Francis Leonard Mega, aliyefariki dunia tarehe 1 Julai, 2023.
Aidha, Kamati Kuu ya CCM, imezipongeza Serikali zake zote mbili, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, inayoongozwa na Dkt.Samia Suluhu Hassan na Seriali ya Mapinduzi ya Zanzibar, chini ya Dkt. Hussen Ali Mwinyi, kwa namna zinavyoendelea kuwatumikia wananchi kwa vitendo kupitia utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya Mwaka 2020 - 2025.