1.Hoja ya Uislamu na ukristo ilishajibiwa mara nyingi hapa jamvini. Hata hivyo kama wananchi wamempigia kura mbunge wa CDM sio kwa sababu ya ukristo au uislamu wake ni kwa sababu ya kukubalika kwake. Labda tuzungumzie viti maalum.Wapendwa wana JF, nimesikia mara nyinyi CHADEMA wakihusishwa na Udini, Ukanda, Dhuluma na sasa Ufisadi. Inaniumiza sana, maana nina imani sana na CDM, lakini kama hizo hoja ni za kweli……....mmmmm.
Jana nilikuwa na mkongwe wa siasa na mwanazuoni maarufu sana hapa Tanzania, katika zungumza yake alisema na ninamnukuu "CHADEMA is a gang of criminals, am just deeply sorry for Dr. Slaa, Zitto Kabwe and my great comrade Prof. Baregu……You know, CDM is not a political party rather…..a group of frustrated and disparate individuals under the umbrella of politics….". Ukweli niliumia sana kimoyomoyo na nikaamua kutoka mahala pale. Kwa hiyo nimeona ni vema nijaribu kujua zaidi juu ya CDM.
Kwa yeyote mwenye takwimu au ufahamu naomba anisaidie kujua yafuatayo:
1. Uwiano wa waislamu kwa wakristo miongoni mwa wabunge wa CDM
2. Uwiano wa waislamu kwa wakristo miongoni mwa wajumbe wa Halmashauri Kuu na Sekretariat ya CDM
3. Kati ya wabunge wote wa CDM ni wabunge wangapi wa CDM wanatoka Kanda ya Kaskazini hususani mikoa ya Arusha, Kilimanjaro, Manyara+ na Singida?
4. Je ni kweli Mh. Mbowe kawauzia CDM magari 3 yaliyotumika kwa TSh 480,000,000?
5. Kama ni kweli, ni magari mangapi, aina gani (kama ni Fuso truck, je ni 4ton au 10ton) na ya mwaka gani?
6. CHADEMA ati wamewadhulumu watu wengi waliojitoa kupiga kampeni kwa matarajiyo ya kurudishiwa japo kidogo walichotumia, hii ni kweli? Mfano ni yule M/kiti wa CDM aliyekimbilia CCM majuzi...na wengine wengi wanalalamika....
Hata hivyo wabunge wa Majimboni baadhi yao ni kama wafuatao
Mnyika (Ubungo-Mkristo), Zitto (Kigoma-Muislamu), Ndesamburo (Moshi-Mkristo), Selasini (Rombo-Mkristo), Lema (Arusha-Mkristo), Said Arfi (Mpanda- Muislamu), Mustaafa Akunaay (Mbulu-Muislamu) n.k.
Upande wa viti maalum ambako ndiko kunakoweza kuzua maswali angalia hapa: Mhonga said (Kigoma-Muislamu), Paulina Gekul (Manyara- Mkristo), Chiku Abwao (Iringa-Muislam), Sabrina Sungura (Kigoma-Muislamu),Raya Ibrahimu Khamis (Pemba- Muislamu), Mariam Salum Msabaha (Unguja-Muislam), Rose Kamili -Manyara (Muislamu), Leticia Nyerere -Mwanza (Mkristo), Lucy Owenya, Grace Kiwelu Kilimanjaro (Mkristo), Conjesta Rwamlaza -Kagera (Mkristo). Christowaja Mtinda- Singida (Mkristo) na Esther Matiko Mara ( Mkristo) kwa kuwa taja wachahce tu kati ya wabunge 23 wa Majimbo na 25 wa viti Maalum. Sijui tatizo hapa liko wapi?
2. Hivi Singida nayo ipo kaskazini? Huu ugonjwa kuwachukia kaskazini tuwaachie CCM waliosema Lowassa na Sumaye hawatakuwa Maraisi wa Tanzania kwa kuwa ni zamu ya watu wa Pwani
3. Kwenye Katiba hakuna Halmashauri Kuu kama CCM ila kuna Kamati Kuu, Baraza Kuu na Mkutano Mkuu. Wajumbe wengi katika vyombo hivyo huingia kwa nafasi zao au kwa kuchaguliwa. Mfano Wenyeviti wote wa wilaya wa CDM ni wajumbe wa Baraza Kuu. Wenyeviti na makatibu wa Majimbo ni wajumbe wa Mkutano Mkuu akiwemo huyu anayeandika hapa. Mwenyekiti, Katibu mkuu, Makamu wenyeviti na Manaibu Katibu (Bara Na visiwani), Wenyeviti wa Mabazara na Wajumbe wa kuchaguliwa pamoja na wachache wa kuteuliwa huunda Kamati Kuu. Sijui huyo Mwanazuoni wako anaijua katiba ya CDM au ndio Dr Bana?
4. Hoja ya magari fuatilia tamko la la Kamati Kuu na Baraza Kuu na majibu ya marando na Komu kwa Nape Nnauye. Si busara kurudia rudia kitu hichohicho.
5.CDM sio CCM kwamba wakati wa uchaguzi ndio wa kunnemeka na kukwapua. Kama kuna mtu alipoteza mali zake kwa ajili ya CDM (mimi nikiwemo) hakuna sababu ya kulaumu CDM bali mfumo uliopo unaotulazimisha tupiganie nchi mara ya pili. Sisi wengine huwa inafika muda familia zetu zinakosa hata chai lakini hatuwezi kulalamika.
6. Sekretariet nenda kwenye website ya CDM utaona kila kitu. Mwmabie na huyo mwanazuoni asiwe mvivu wa kusoma awe mdadisi sio kuleta uzushi mitaani huku akijua kuwa kuna watu kama wewe wanaohitaji kupewa facts na sio jungu.
7. Mwisho lakni kwa Uzito Mpe ujumbe huyo Mwanazuoni kama ni Dokta au profesa, ni afadhali asingesoma kuliko kusoma na kuwa na fikra mgando kama hizo. Akuambie nini maana ya Politicala party kama CDM sio kimojawapo. Amshauri na JK kuwa hicho kikundi cha msimu kitamng'oa sipokuwa makini.
Ujumbe : AKILI ZA KUAMBIWA CHANGANYA NA ZA KWAKO (JK)