CCM Wameishika CHADEMA PABAYA...

Kaka umenena, ukitaka kutunga uwongo jitahidi ufanane na ukweli japo kwa mbali!!
 
Nimekuwa nifukifuatuatilia hoja zinazotolewa na wapenzi wa Chama cha Magamba juu ya ufisadi wa Dr Slaa,Mbowe na Ndesa pesa nikagundua kuwa kweli mtu anapoishiwa hoja ni sawa na gari bovu linapokosa break linakwenda popote. Kwani hata kutunga uwongo unaofanana na ukweli ni tatizo kwa sababu breki hamna. Fikiria Ndesamburo jinsi anavyojitoa kuwasaidia watu wa jimbo lake na jinsi alivyosaidia CHADEMA kwa hali na mali tena kwa uwazi na biashara zake ni za uwazi, Angalia Mbowe jinsi anavyojitoa kwa hali na mali kukisaidia chama chake na wananchi kwa ujumla na biashara zake zote ni za uwazi tofauti na wafanyabiashara wa chama cha magamba wanaotoa michango kwa kificho na hata hiyo wanayosema ameuzia chama magari yaliotumika ni kitu kimejadiliwa kwenye vikao na kuwekwa wazi. Tazama mtu kama Dr Slaa alivyojitoa kwa hali na mali kuwapa watanzania elimu ya uraiya na hata kuahatarisha maisha yake, mtazame Zitto kazi aliyoifanya juzi juzi hapa eti hawa ni mafisadi kama ndiyo hivyo basi mimi natangaza ufisadi wa CHADEMA tunauhitaji kabisa na waendelee kuwa na ufisadi huo.

Watanzania sii wapumbavu kiasi hicho cha watu kufikiri kuwa uanaweza kuwadanganya kama kuwa hawaoni wala hawatambui kinachofanyika. Ni dhambi kubwa chama CCM kinafanya kuwaona wa TZ hawawezi kutambua ni nani fisadi na nani mzalendo. Hivi ninyi ndugu zangu hamumuogopi hata Mungu kwa uovu mnaowafanyia wa TZ waliopewa nchi yenye utajiri mkubwa kiasi hicho mkawafanya masikini kiasi hicho. Jamani maisha yetu ya kuishi hapa Dunia ni mafupi ni miaka sabini ukiwa na nguvu miaka 80 sasa yanini kuhangaikia mambo ya rushwa, wizi na kupenda madaraka nasema malipo ya mwovu huanzia hapa hapa Duniani na wengine wenu mmeshaanza kulipwa. Hivi kunaraha gani ya wewe kusomesha nje mtoto wako kwa fedha za rushwa ili hali kuna mtoto wa masikini licha ya kwenda shule hana uhakiaka wa kula.Mshahara wa Dhambi ni mauti wanyonge wanalia na Kitabu cha Mungu kinasema kilio cha mnyonge kinamfikia Mungu moja kwa moja na washauri mbadilike na kuacha uongozi wa nchi hii kwa wengine bila hivyo huko tuendako mtakuja ona hasira ya Mungu.

Mkuu nakugongea SENKS kubwa.
Tungekuwa na watu wa aina yako 100 tuu ambao kwa tarakimu zangu nafikiri mpaka January 2012,tutakuwa tumeshawapa,mapambano yatakuwa yameiva na hakuna kurudi nyuma.
Tutatoa majina ya watu walioandika analysis za kuitoa hii nchi kwenye mikono ya mafisadi na kuirudisha kwenye mikono salama ya wananchi wazalendo wa Tanzania.Tutawatunuku kwa heshima kulingana na juhudi zao za kupambana na ufisadi wa hii nchi.wanajulikana na tunapendekeza watokeze wengi zaidi ili idadi iwe kubwa.
 
Mimi title tu, presha ilipanda.

lakini hoja yako ni kali sana. waambie hao Chama Cha Magamba ambao walijivua MAKAMBA wakabaki na MAGAMBA wajifunze uongo endelevu.
 
Watanganyika,japo ni wakimya sana,..wanajua ukweli ni upi na
propaganda ni zipi!
Hivi chama cha magamba,kinapo jivua magamba kinabaki kuwa chama cha nini?
CCM-M=CC?

CCM is dead
 
Sasa mnashtuka nn?cku mkickia uchafu wao mtafanya nn!tusiwaamin sana wanadamu,wao ni watu tu..they will surprise u..no one is clean.
 
Wapendwa wana JF, nimesikia mara nyinyi CHADEMA wakihusishwa na Udini, Ukanda, Dhuluma na sasa Ufisadi. Inaniumiza sana, maana nina imani sana na CDM, lakini kama hizo hoja ni za kweli……....mmmmm.
Jana nilikuwa na mkongwe wa siasa na mwanazuoni maarufu sana hapa Tanzania, katika zungumza yake alisema na ninamnukuu “CHADEMA is a gang of criminals, am just deeply sorry for Dr. Slaa, Zitto Kabwe and my great comrade Prof. Baregu……You know, CDM is not a political party rather…..a group of frustrated and disparate individuals under the umbrella of politics….”. Ukweli niliumia sana kimoyomoyo na nikaamua kutoka mahala pale. Kwa hiyo nimeona ni vema nijaribu kujua zaidi juu ya CDM.
Kwa yeyote mwenye takwimu au ufahamu naomba anisaidie kujua yafuatayo:
1. Uwiano wa waislamu kwa wakristo miongoni mwa wabunge wa CDM
2. Uwiano wa waislamu kwa wakristo miongoni mwa wajumbe wa Halmashauri Kuu na Sekretariat ya CDM
3. Kati ya wabunge wote wa CDM ni wabunge wangapi wa CDM wanatoka Kanda ya Kaskazini hususani mikoa ya Arusha, Kilimanjaro, Manyara+ na Singida?
4. Je ni kweli Mh. Mbowe kawauzia CDM magari 3 yaliyotumika kwa TSh 480,000,000?
5. Kama ni kweli, ni magari mangapi, aina gani (kama ni Fuso truck, je ni 4ton au 10ton) na ya mwaka gani?
6. CHADEMA ati wamewadhulumu watu wengi waliojitoa kupiga kampeni kwa matarajiyo ya kurudishiwa japo kidogo walichotumia, hii ni kweli? Mfano ni yule M/kiti wa CDM aliyekimbilia CCM majuzi...na wengine wengi wanalalamika....
 
Wapendwa wana JF, nimesikia mara nyinyi CHADEMA wakihusishwa na Udini, Ukanda, Dhuluma na sasa Ufisadi. Inaniumiza sana, maana nina imani sana na CDM, lakini kama hizo hoja ni za kweli……....mmmmm.
Jana nilikuwa na mkongwe wa siasa na mwanazuoni maarufu sana hapa Tanzania, katika zungumza yake alisema na ninamnukuu “CHADEMA is a gang of criminals, am just deeply sorry for Dr. Slaa, Zitto Kabwe and my great comrade Prof. Baregu……You know, CDM is not a political party rather…..a group of frustrated and desparate individuals under the umbrella of politics….”. Ukweli niliumia sana kimoyomoyo na nikaamua kutoka mahala pale. Kwa hiyo nimeona ni vema nijaribu kujua zaidi juu ya CDM.
Kwa yeyote mwenye takwimu au ufahamu naomba anisaidie kujua yafuatayo:
1. Uwiano wa waislamu kwa wakristo miongoni mwa wabunge wa CDM
2. Uwiano wa waislamu kwa wakristo miongoni mwa wajumbe wa Halmashauri Kuu na Sekretariat ya CDM
3. Kati ya wabunge wote wa CDM ni wabunge wangapi wa CDM wanatoka Kanda ya Kaskazini hususani mikoa ya Arusha, Kilimanjaro, Manyara+ na Singida?
4. Je ni kweli Mh. Mbowe kawauzia CDM magari 3 yaliyotumika kwa TSh 480,000,000?
5. Kama ni kweli, ni magari mangapi, aina gani (kama ni Fuso truck, je ni 4ton au 10ton) na ya mwaka gani?
6. CHADEMA ati wamewadhulumu watu wengi waliojitoa kupiga kampeni kwa matarajiyo ya kurudishiwa japo kidogo walichotumia, hii ni kweli? Mfano ni yule M/kiti wa CDM - Mbeya Mjini aliyekimbilia CCM majuzi...na wengine wengi wanalalamika....
 
Nadhani tukiamua kufanya na CCM pia itakuwa safi saana... Ili tujue kuwa CCM na CHADEMA vinachagua watu kwa udini au kwa kuwa wana sifa?? Pia tuangalie na wabunge wa kuchaguliwa na raisi ni wa dini gani pia... Ili tujue CCM na chadema wapi ni wapi
 
Wewe Ulimwamini Huyo jamaa!? na je ni nini lengo lako katika hayo maswali!, kwani hulizii CUF,CCM?.

Nakushauri usipende sana kusikia, fanya uchunguzi, fikiri na gundua ukweli na Jambo zuri kwako acha umbea na uchochezi.
 
Joblube,

Umenena. Tatizo liko kwenye title ya thread hii. Nashauri ubadilishe na isomeke:Uongo/Propaganda za CCM kuhusu ufisadi wa Mbowe,Ndesamburo na Dr.Slaa. Maana kwa sasa unavosomeka ni kuwa Mbowe,Ndesamburo na Dr. Slaa ni kama wanahusika na ufisadi wa kutisha ilhali si kweli.

Ni kweli CCM wanawafanya wa-TZ kuwa ni mbumbumbu wasioweza kutofautisha kati ya MAFISADI wa CCM na watu au viongozi wa kawaida kama kina Mbowe,Ndesamburo na Dr. Slaa.

Ukweli unabaki kuwa CCM wanatapatapa maana swala la UFISADI ni kama ugonjwa wa CANCER au UKIMWI unaokitafuna chama cha Magamba-CCM.

Na huyu Nnauye wao a.k.a. vuvuzela ndiyo anaonekana kurikoroga kabisa. Maana badala ya kujivua magamba kama alivokubaliana kwenye kikao chao fake ameanzisha KUVAA MAGAMBA MENGINE na kwa hiyo hali ndiyo inazidi kuwa worse!

Mimi nashauri CCM wamtimue Nnauye atoke CCM maana tayari alishaamua kuondoka kwenda kuanzisha CCJ baada ya Mpendazoe kumwanika hadharani kuwa yeye(Nnauye)alikuwa ni mojawapo ya waasisis wa CCJ. Hivo basi Nnauye si mwaminifu hata kidogo yawezekana bado anajipanga kukimaliza CCM kabla ya Uchaguzi wa 2015!
 
Duh!!hiyo title hapo juu ilinistua nikajua viwavi wa magamba,kumbe tupo pamoja kaka.Mungu ibariki Tanzania wabariki na watu wake.Tunawataka watu kama nyie
 
Sasa mnashtuka nn?cku mkickia uchafu wao mtafanya nn!tusiwaamin sana wanadamu,wao ni watu tu..they will surprise u..no one is clean.

ZIMWI LIKUJUALO HALIKULI LIKAKUMALIZA, ila chama cha magamba wametumaliza yani HAWATUJUIIIIII!
 
Mkuu umeeleza vzr sana japo na mimi mara ya kwanza nilianza kuogopa tittle ya thread yako, nakupa tano! bravo CHADEMA!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom