sulphadoxine
JF-Expert Member
- Nov 1, 2010
- 2,257
- 645
Nape = nepi
Nimekuwa nifukifuatuatilia hoja zinazotolewa na wapenzi wa Chama cha Magamba juu ya ufisadi wa Dr Slaa,Mbowe na Ndesa pesa nikagundua kuwa kweli mtu anapoishiwa hoja ni sawa na gari bovu linapokosa break linakwenda popote. Kwani hata kutunga uwongo unaofanana na ukweli ni tatizo kwa sababu breki hamna. Fikiria Ndesamburo jinsi anavyojitoa kuwasaidia watu wa jimbo lake na jinsi alivyosaidia CHADEMA kwa hali na mali tena kwa uwazi na biashara zake ni za uwazi, Angalia Mbowe jinsi anavyojitoa kwa hali na mali kukisaidia chama chake na wananchi kwa ujumla na biashara zake zote ni za uwazi tofauti na wafanyabiashara wa chama cha magamba wanaotoa michango kwa kificho na hata hiyo wanayosema ameuzia chama magari yaliotumika ni kitu kimejadiliwa kwenye vikao na kuwekwa wazi. Tazama mtu kama Dr Slaa alivyojitoa kwa hali na mali kuwapa watanzania elimu ya uraiya na hata kuahatarisha maisha yake, mtazame Zitto kazi aliyoifanya juzi juzi hapa eti hawa ni mafisadi kama ndiyo hivyo basi mimi natangaza ufisadi wa CHADEMA tunauhitaji kabisa na waendelee kuwa na ufisadi huo.
Watanzania sii wapumbavu kiasi hicho cha watu kufikiri kuwa uanaweza kuwadanganya kama kuwa hawaoni wala hawatambui kinachofanyika. Ni dhambi kubwa chama CCM kinafanya kuwaona wa TZ hawawezi kutambua ni nani fisadi na nani mzalendo. Hivi ninyi ndugu zangu hamumuogopi hata Mungu kwa uovu mnaowafanyia wa TZ waliopewa nchi yenye utajiri mkubwa kiasi hicho mkawafanya masikini kiasi hicho. Jamani maisha yetu ya kuishi hapa Dunia ni mafupi ni miaka sabini ukiwa na nguvu miaka 80 sasa yanini kuhangaikia mambo ya rushwa, wizi na kupenda madaraka nasema malipo ya mwovu huanzia hapa hapa Duniani na wengine wenu mmeshaanza kulipwa. Hivi kunaraha gani ya wewe kusomesha nje mtoto wako kwa fedha za rushwa ili hali kuna mtoto wa masikini licha ya kwenda shule hana uhakiaka wa kula.Mshahara wa Dhambi ni mauti wanyonge wanalia na Kitabu cha Mungu kinasema kilio cha mnyonge kinamfikia Mungu moja kwa moja na washauri mbadilike na kuacha uongozi wa nchi hii kwa wengine bila hivyo huko tuendako mtakuja ona hasira ya Mungu.
Sasa mnashtuka nn?cku mkickia uchafu wao mtafanya nn!tusiwaamin sana wanadamu,wao ni watu tu..they will surprise u..no one is clean.