Uchaguzi 2020 "CCM tumeanza vizuri, tumalize vizuri pia"

Zanzibar-ASP

JF-Expert Member
Nov 28, 2013
10,115
35,124
Kwakuwa tumeanza kujibu hoja za Chadema basi tujibu zote ili tutoke kwenye wakati mgumu huu, maana wananchi kipindi hiki wanasikiliza wagombea wote na kupima hoja zao.

MOSI. Chadema kwa kupitia mgombea wao amekuja na hoja ya kutaka kufifisha kazi nzuri na kubwa iliyofanywa na serikali ya ccm katika miradi yote mikubwa ya kununua Ndege, Bwawa la Umeme na Treni ya SGR. Miradi hii yote ya maendeleo kwa kuwa haihakisi maendeleo ya watu ni bure tu. Kwani hata Wakoloni na Makaburu Africa Kusini wamefanya zaidi ya hayo yote, lakini kwa kushindwa kuwapa maendeleo watu wao walikataliwa na kupingwa. Chadema wakazungumzia mfano wa nchi ya Ethiopia wanayo yote hayo lakini wananchi wake wako tayari kufia kwenye Makontena au kwenye mitumbwi kwenda nchi nyingine kwa kuzamia kutafuta maendele. CCM tunatoa majibu mepesi tu. Hii hoja ijibiwe tusiahibike.

PILI. Chadema wamekuja na hoja ya kuwa na Majimbo kwa maana kuwa, kila sehemu (kwa maana ya mkoa na wilaya) waongozwe na viongozi waliochaguliwa na wananchi ili waweze kuwawajibisha. CCM tunajibu kwa hoja nyepesi kwamba wanataka kutugawa kwa kuwa tumechanganyika Makabila italeta ukabila. Tunasahau kwamba ua tunachagua Wabunge bila kujali hilo. Inahitajika hoja nzito kujibu hili sio jepesi kama hivyo.

TATU. Chadema wamezungumzia kuhusu wafanyakazi kutoongezwa kwa mishahara kwa kipindi chote cha miaka mitano na wanaahidi kuwalipa walicho kosa tena na riba. Sisi tunakuja na majibu mepesi kwamba tutaongeza, hii ni kama kumwambia mtoto usilie nitakununulia Pipi. Tutoe suluhisho la hili na jinsi tutakavyoaminika mbele ya wafanyakazi, la sivyo kura zao na wategemezi wao tutazikosa.

NNE . Chadema wametoa shutuma nzito kabisa kwamba Serikali ya ccm, imeua watu Kibiti, watu wameokotwa kwenye viroba baharini, watu wametekwa, watu wanafunguliwa Kesi kubwa kubwa bila hata hizo kesi kuendeshwa wanaozea magerezani mpaka ulipe Pesa ndiyo uachiwe na ufilisiwe. Pia mgombea wao Tundu Lissu anashutumu serikali kwamba ndiyo ilimpiga risasi na hamna hata mtu mmoja aliwahi kukamatwa, kunyimwa matibabu, kuvuliwa Ubunge na hila kama hizo. Haya yote hata hayajajibiwa au kukanushwa kabisa ina maana ni kweli serikali imeyafanya?. Kama tumeamua kujibu kila hoja hizi zisikae kimya bila kujibiwa.

TANO . Chadema wameelezea kwamba wafanya biashara wanafilisiwa na TRA kwa kukwapua pesa zao kwa njia ya Agency Notice kwenye Mabenki, na Biashara nyingi zimeumia na hiki tumekaa kimya. Je ukimya wetu ndiyo kukubali kwamba haya yanatendeka? Mimi ni kada tu sio mfanyabiashara je, kweli Wafanyabiashara wanafanyiwa hivyo? Au propaganda za Chadema? Tukikaa kimya tunawapa point bure kwa kuwa tunajibu hoja na hizi tuzijibu.

SITA. Chadema wanakuja na hoja ya kwamba NEC inawahujumu kwa mambo ya kishenzi hili tuliangalie maana kuna mambo mgombea wetu anavunja kabisa taratibu na NEC haisemi kitu lakini ikitokea kidogo Chadema wanajitokeza kujifanya wanafuatilia. Kwa hili niseme wazi NEC inaihujumu CCM kiaina. Ukimya wetu juu ya vitendo vya NEC unatugharimu mbele ya wananchi.

SABA . Chadema imekuja na hoja ya uwanja wa Ndege cha Chato. Kwa kweli Mgombea wetu jibu la kwamba nikifa sitazikwa nacho ni ya kuzalilisha nafasi aliyo nayo anayogombea ingawa hata Mjumbe wa nyumba kumi hasingeweza kujibu hivyo. Kweli tulishindwa hata kusema kwa ajili ya Utalii.

NANE. Chadema wamekuja na shutuma dhidi ya Rais kuwa amejimilikisha ardhi yenye ukubwa wa zaidi ya ekari 25000. Hili tukiliacha kulijibu vyema sasa litatugharimu sana, maana watu wameanza kuliamini hasa baada ya waziri wa ardhi kusema 'wakubwa' wamemilikishwa ardhi hizo kihalali.

Kabla hatuja ahidi nini tutafanya miaka mitano ijayo tuanze kwanza kuzijibu hizi hoja kwa kweli na uwazi ama sivyo tutakuwa na wakati mgumu kwa wapiga kura.

(Makala hii imeandikwa na Buzer Mpangale, mimi nimeinakili kutoka mtandao fulani na kuileta hapa JF)
 
Tuhuma hizo za uzushi zinajibiwa kwa ushahidi usio na mashaka na wagombea wa Udiwani na Ubunge. Kwenye kampeni ngazi hizo wapiga kura hupata nafasi ya kuuliza maswali na kupewa majibu papo hapo. Nina uhakika wagombea wa chama cha Lissu wanao ubavu wa kutetea tuhuma anazoibua? Anawajengea hali tete ya kujinadi. Na baadhi niliofanikiwa kuwasikia nao wanatukana, kulaumu na wakizidiwa kukosa hoja za kisera wanatoa ahadi za maendeleo ya vitu
 
Tuhuma hizo za uzushi zinajibiwa kwa ushahidi usio na mashaka na wagombea wa Udiwani na Ubunge. Kwenye kampeni ngazi hizo wapiga kura hupata nafasi ya kuuliza maswali na kupewa majibu papo hapo. Nina uhakika wagombea wa chama cha Lissu wanao ubavu wa kutetea tuhuma anazoibua? Anawajengea hali tete ya kujinadi. Na baadhi niliofanikiwa kuwasikia nao wanatukana, kulaumu na wakizidiwa kukosa hoja za kisera wanatoa ahadi za maendeleo ya vitu
Acha kuwaabisha waalimu wako kiasi hiki! Umesomea wapi ugolo huu ulioandika hapa?
 
Tuhuma hizo za uzushi zinajibiwa kwa ushahidi usio na mashaka na wagombea wa Udiwani na Ubunge. Kwenye kampeni ngazi hizo wapiga kura hupata nafasi ya kuuliza maswali na kupewa majibu papo hapo. Nina uhakika wagombea wa chama cha Lissu wanao ubavu wa kutetea tuhuma anazoibua? Anawajengea hali tete ya kujinadi. Na baadhi niliofanikiwa kuwasikia nao wanatukana, kulaumu na wakizidiwa kukosa hoja za kisera wanatoa ahadi za maendeleo ya vitu
Endelea kuota, vipi kuhusu fao la kujitoa,nyongeza ya mishahara, utekaji, ubambikaji kesi na kutunga sheria za kikandamizaji?
Ccm ni genge la wahuni na wauaji tu
 
Ni faida kwa Lisu kama CCM wanaendelea kujivuta kutoa majibu ya hoja hizi. Siku zinasonga, uchaguzi unafika mshindi anakuwa Lisu.
 
Tuhuma hizo za uzushi zinajibiwa kwa ushahidi usio na mashaka na wagombea wa Udiwani na Ubunge. Kwenye kampeni ngazi hizo wapiga kura hupata nafasi ya kuuliza maswali na kupewa majibu papo hapo. Nina uhakika wagombea wa chama cha Lissu wanao ubavu wa kutetea tuhuma anazoibua? Anawajengea hali tete ya kujinadi. Na baadhi niliofanikiwa kuwasikia nao wanatukana, kulaumu na wakizidiwa kukosa hoja za kisera wanatoa ahadi za maendeleo ya vitu
Magufuli mwizi sana ndio maana hawezi jibu kwa nini doto james kawa pay mastet
 
Hakuna mwana fisiem anayeweza kujibu hoja hizo,wote wameshakoswa uhalali wa kuongoza Taifa hili,kama siyo Lissu kuongoza nchi hii,BORA TUTAWALIWE KIJESHI
 
Endelea kuota, vipi kuhusu fao la kujitoa,nyongeza ya mishahara, utekaji, ubambikaji kesi na kutunga sheria za kikandamizaji?
Ccm ni genge la wahuni na wauaji tu
Unamwakilisha mwajiriwa au wewe mwenyewe? Kama ni wewe mwenyewe, soma kwa umakini mabadiliko ya sheria ya mafao ya pensheni.

Umebambikwa kesi au unaandika ya kusimuliwa? Kama umebambikwa kesi tafuta ushauri wa kisheria upate tafsiri sahihi ili ikuwezeshe kujua kama una kesi ya kujibu au la.

Hata huyo mgombea akifanikiwa kuingia madarakani (ambayo ni ndoto) akitawala kwa mujibu wa Katiba na sheria ataacha sheria zichukue mkondo wake. Au unasahau Wabunge waliokataa kutii amri ya M/Kiti wa chama kususia kikao cha Bunge cha bajeti kwa sababu ya korona, wakafukuzwa chama? Viongozi gani hao wa Chama wasio heshimu Katiba yao na kudai Uhuru na Haki kwa maneno?. AIBU
 
Hakuna mwana fisiem anayeweza kujibu hoja hizo,wote wameshakoswa uhalali wa kuongoza Taifa hili,kama siyo Lissu kuongoza nchi hii,BORA TUTAWALIWE KIJESHI
Hoja gani za kujibu?

Wananchi ambao ni wapiga kura watazijibu hoja hizo tarehe 28/10/2020 kwa kura nyingi za CCM. Hao ni WanaChato, Wavuvi, Wajawazito, Wafanya biashara ndogondogo (machinga + mama ntilie), wachimbaji madini wadogo wadogo, wenye viwanda, wanafunzi, na hasa asilimia 70 ya wanaoishi vijijini ambao huduma za jamii na miundo mbinu zimeboreshwa (huduma za afya, barabara, reli, meli, maji, nk).
 
CCM kosa lao ni kutegemea dola kubaki madarakani. Walifanya hivyo akina Ghaddafi, Mobutu, na wengine wengi lakini mwisho wa siku walitoka kwa maumivu makubwa.
 
Tuhuma hizo za uzushi zinajibiwa kwa ushahidi usio na mashaka na wagombea wa Udiwani na Ubunge. Kwenye kampeni ngazi hizo wapiga kura hupata nafasi ya kuuliza maswali na kupewa majibu papo hapo. Nina uhakika wagombea wa chama cha Lissu wanao ubavu wa kutetea tuhuma anazoibua? Anawajengea hali tete ya kujinadi. Na baadhi niliofanikiwa kuwasikia nao wanatukana, kulaumu na wakizidiwa kukosa hoja za kisera wanatoa ahadi za maendeleo ya vitu
Yaweke hapa hayo majibu, kwani pale Chato uwanja upo, haupo? Ni wa kazi gani? kwa nini haukujengwa makao makuu ya mkoa Geita? Vitambulisho vya wamachinga mbona wanapolita hawapewi risiti za EFD? Na mbona vimefutwa rasmi leo tena katikati ya kampeni, nini kimetokea? Uzushi uko wapi? Je waliolipa tayari watarudishiwa hela zao? Jibu kwanza hayo. Mengine yanafuata
 
Yaweke hapa hayo majibu, kwani pale Chato uwanja upo, haupo? Ni wa kazi gani? kwa nini haukujengwa makao makuu ya mkoa Geita? Vitambulisho vya wamachinga mbona wanapolita hawapewi risiti za EFD? Na mbona vimefutwa rasmi leo tena katikati ya kampeni, nini kimetokea? Uzushi uko wapi? Je waliolipa tayari watarudishiwa hela zao? Jibu kwanza hayo. Mengine yanafuata
Rudia kusoma hoja zangu kabla ya kukurupuka na jibu.

Uliowataja wao ndio wenye majibu sahihi kinachoendelea. Ni majibu hayo ndiyo yatawapa uamuzi wa nani wampigie kura. Au unaamini wapiga kura wote ni watoto wa chekechea?

Nikuulize swali na ulijibu kwa nia ya dhati. Kwa kuwa sijui maisha yako unayaendesha kwa shuguli gani, je, utawala wa Serikali inayomaliza muda wake, imakuathiri kwa kiasi gani? Jibu/majibu yake yawe na mifano. Ukifanya hivyo utakujiweka kwenye hali ya huru, kimawazo, daima badala ya kutegemea mawazo ya mtu mwingine.

KUMBUKA NI WEWE MWENYEWE UTAPEWA KARATASI YA KURA, UKAINGIA KWENYE KISANDUKU NA KUPIGA KURA.
 
Tuhuma hizo za uzushi zinajibiwa kwa ushahidi usio na mashaka na wagombea wa Udiwani na Ubunge. Kwenye kampeni ngazi hizo wapiga kura hupata nafasi ya kuuliza maswali na kupewa majibu papo hapo. Nina uhakika wagombea wa chama cha Lissu wanao ubavu wa kutetea tuhuma anazoibua? Anawajengea hali tete ya kujinadi. Na baadhi niliofanikiwa kuwasikia nao wanatukana, kulaumu na wakizidiwa kukosa hoja za kisera wanatoa ahadi za maendeleo ya vitu
Kama ni za uzushi ukweli ni upi??
 
Back
Top Bottom