CCM/TANESCO wizi huu utaisha lini?

CCM/TANESCO wizi huu utaisha lini?

afsa

JF-Expert Member
Joined
Dec 6, 2012
Posts
1,986
Reaction score
1,592
Nilinunua umeme ambao umeisha baada ya miezi sita leo naambiwa nilipie service charge ya miezi sita? service ipi kwa muda wote huo hakuna fundi aliyewahi kuja kuigusa hata mita? Wanakata VAT, EWURA na pesa za UNIT hizi haziwatoshi kuedesha shughuli zao hadi tuibiwe kivingine? NMB,NBC,CRDB etc nao wanatuibia kwa staili hiyo wakati kila muamala wanachukua chao, monthly service ya nini? Tunaibiwa kupitia monthly service TANESCO, NMB, NBC, CRDB(bank) hakuna anayejali. Tanzania tunawanasheria makanjanja(wapiga pesa). Tunaibiwa hakuna mwanasheria anayetetea si Tundu Lisu wala Pro. Safari wanaoliona hili. Wanasheria mpaka sehemu ya kupiga pesa ndo mnashughulisha ubongo? Hili hamulioni? SERVICE CHARGE INABOA NI WIZI, MIRIJA YA KUPIGA PESA.
 
ccm na serikali yake imejaa dhuluma hawana nia ya kuleta maendeleo ili watu wawe na maisha bora...hata watawale miaka 1000 hakuna mabadiliko
 
Mkuu service charge sio lazima waje nyumbani kwako, hata service ya transformer inayosambaza umeme mtaani kwako nayo inahusika, kurekebisha hitilafu katika service line yenu pia inahusika.
 
Mkuu service charge sio lazima waje nyumbani kwako, hata service ya transformer inayosambaza umeme mtaani kwako nayo inahusika, kurekebisha hitilafu katika service line yenu pia inahusika.
Ni kweli lakini kama kuna shida nyumbani kwako lazima ulipe hao mafundi vinginevyo waweza kuishi bila umeme kwa hadi wiki huku wakitoa visingizio mbali mbali lakini ukitoa kitu kidogo tatizo lako linashughulikiwa hapo hapo
 
Mkuu service charge sio lazima waje nyumbani kwako, hata service ya transformer inayosambaza umeme mtaani kwako nayo inahusika, kurekebisha hitilafu katika service line yenu pia inahusika.

Kama wanauza umeme wanakata kodi zote wanazojua wao, service chaji ya nn tena kila mwezi hata kama kuna mwezi haukununua umeme unalimbikiziwa?
 
Ni kweli lakini kama kuna shida nyumbani kwako lazima ulipe hao mafundi vinginevyo waweza kuishi bila umeme kwa hadi wiki huku wakitoa visingizio mbali mbali lakini ukitoa kitu kidogo tatizo lako linashughulikiwa hapo hapo

Kitu kidogo!!
 
Hiyo ni tabia ya mtu binafsi sio ya shirika.
Shirika halijatoa mwongozo dhabiti na pia kuusimamia ili kuondoa hii kitu jambo linalopelekea wananchi kuamua kuchukua uamuzi mbadala. mfano wakisema kuwa tatizo lishughulikiwe ndani ya muda fulani say masaa ishirini na nne na wakasimamia hilo basi tabia itakufa lakini kama wanaacha hivi hivi nafikiri mtu hatakubali vitu vioze kwenye fridge wakati huyu mfanyakazi wa Tanesco anataka 10,000/=.
Mfano nilienda sehemu fulani Kimara kilungule kuna nguzo imeoza kabisa watu wamepiga ripoti zaidi ya mara 20 lakini wapi nao wameeacha ingawa ni hatari kwa maisha ya watoto wa mitaa hiyo
 
Ulinunua umeme wa tshs ngapi ?

Angalia kama unatumia Units chini ya 75 kwa mwezi nenda Tanesco wakubadilishie Tariff, utakuwa haulipi service charge na bei ya unit itakuwa ni tshs 100 tu
 
Back
Top Bottom