CCM, siasa za visasi hazifai kamwe

CCM, siasa za visasi hazifai kamwe

Hahaha kiongozi wao mtu wa visas, inategemea wanachama waweje?!
 
Wajumbe wa ngazi za chini licha ya kufanya yao na kuwapiga chini wahamiaji kutoka upinzani, kumbe waligeuzwa kuwa mabwege kwa kuwa viongozi wao walikuwa na yao mioyoni kwao. Wajumbe hawakujua kuwa biashara ilikwisha kufanyika na dau kupangwa.

CCM ya sasa si mali tena ya wanachama, bali ni mali ya Mwenyekiti Taifa. Kipaumbele kwa nafasi za uungozi na hata sifa za uwakilishi ni wahamiaji walionunuliwa kutoka upinzani, kujitenga kwa namna yoyote ile na timu Membe ama kufanya jitihada zenye kudhihirika za kutaka kuua upinzani, kutoa matusi kwa viongozi wa upinzani na juhudi za wazi ktk kudhoofisha upinzani hasa CDM.
 
Yaani watanzania hivi sasa tumekubali kuishi na shetani na tumekuwa mashetani!
 
Kwa mfano: Alichofanyiwa Stephen Masele, hakika Mimi sijaelewa!

Kura 152 dhidi ya 12!!! Sielewi bado!
Ccm taasisi kubwa kujuana na wajumbe haimanishi kwamba wewe unafaa kuongoza jimbo !mwenendo wa masele jimboni ulikuwa mbaya sana hasa utatuzi wa kero za wananchi kwa awamu zote aliona jimbo lipo mfukoni ! Intelijensia ya magufuli imemlarua vipandevipande na alimfanyia figisu kubwa mgombea mwenzie patrobas katambi! Malipo ni hapahapa
 
Asante ndugu kwa hoja yako. Agenda yetu Watanzania sasa iwe ni utawala bora. Miundo mbinu tumepata, n.k. lakini kilichikosekana ni utawala wa sheria na kwa sababu tumempata mgombea mwanasheria wacha tumtwishe zigo ya kutengeneza katiba bora isiyochezewa chezewa.
Na hii ndo nafasi adhimu tuliyopata watanzania mwaka huu ambapo hatupaswi kuichezea.

Hii nchi kwa maendeleo ya kweli ya watu na vitu na kwa mustakabali wa afya njema ya nchi hii NI MUHIMU SANA MWAKA HUU TUNDU LISSU AKAWA RAISI 2020 - 2025 ILI ATUPATIE KATIBA MPYA YA WANANCHI ITAKAYOWEKA VYOMBO HURU NA IMARA KUISIMAMIA HII NCHI NA KUPUNGUZA MAMLAKA YA RAISI. Hili ni muhimu sana!
 
Ccm taasisi kubwa kujuana na wajumbe haimanishi kwamba wewe unafaa kuongoza jimbo !mwenendo wa masele jimboni ulikuwa mbaya sana hasa utatuzi wa kero za wananchi kwa awamu zote aliona jimbo lipo mfukoni ! Intelijensia ya magufuli imemlarua vipandevipande na alimfanyia figisu kubwa mgombea mwenzie patrobas katambi! Malipo ni hapahapa
Mwambie mwenyekiti wenu , kwa udhalimu aliouonesha wazi yafuatayo yanaenda kutokea

1. Watu wake wote aliowapitisha kwa nguvu wanaenda kupigwa chini! Na ole wake atumie polisi au NEC kuwapitisha maana hakutatosha. Ndo ataona hiyo nguvu ya umma tena ya wanachama wote wa CCM na Chadema/ upinzani. Na yoyote yakitokea mwambieni atawajibika yeye kama yeye. Na Kuna watu wanakusanya ushahidi tu kwa yaliyotokea na yanayoenda kutokea kwa ajili ya hatua kali za kisheria kimataifa huko! So mfikishieni taarifa kuwa ajiandae!

2. Yeye mwenyewe ajiandae kumkabidhi nchi Tundu Antipas Lissu baada ya uchaguzi huu wa 2020. Hakuna vyovyote vile atamshinda Lissu na lolote atakalojaribu kulifanya, arejee niliyosema kwenye hoja no 1 hapo juu!
 
Kwa mfano: Alichofanyiwa Stephen Masele, hakika Mimi sijaelewa!

Kura 152 dhidi ya 12!!! Sielewi bado!
Masele alitunishiana msuli na supika, naona Ndugai alisema ni bora akatwe yeye kuliko Masele arudi mjengoni.. Basi, akashikishwa adabu!
 
Dah! mtu yoyote mwenye akili timamu hawezi kukubali huu ujinga. Magufuli ameleta madhara makubwa sana kwenye uhuru wa watu hapa nchini. CCM wanaugumia/wanaugulia maumivu kuliko hata wapinzani.
Mkuu, tulikuwa wagombea elfu kumi kwa viti mia mbili na ushee! Hata Malaika wangefanya kazi ya uteuzi, kwanza mimi nisingetoswa, pili malalamiko lazima yangekuwepo tu kwa kuwa kulingana na katiba, kila mgombea alistahili kuteuliwa.
All in all, tuwaache walioteuliwa wawatumikie wananchi... Wengine tusubiri awamu ya sita Mungu akituweka hai.
 
Kupitishwa jina wanaangalia mchango wako kwenye chama unakuta mbunge hawezi hata kutetea chama kinaposhambuliwa na wapinzani yupo tu hakuna aliyeonewa hapo.
 
Kupitishwa jina wanaangalia mchango wako kwenye chama unakuta mbunge hawezi hata kutetea chama kinaposhambuliwa na wapinzani yupo tu hakuna aliyeonewa hapo.
Akili za uvccm bana yaan badala ya kutetea wananchi unatetea chama Basi bunge lijalo litakua la ovyo Sana tutegemee wa kina kibajaji,msukuma ,kessy kuwa wehu zaidi
 
Masele alitunishiana msuli na supika, naona Ndugai alisema ni bora akatwe yeye kuliko Masele arudi mjengoni.. Basi, akashikishwa adabu!
Huu ndio ukweli.kumbuka spike ni mjumbe wa kamati kuu.
Lazima Alitaka Masele akatwe
 
Back
Top Bottom