Candid Scope
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 11,883
- 6,884
Vyombo vya dola, serikali na CCM walifanya jitihada za ziada kuzima kashfa ya Rage kupanda na silaha kali hadharani wakati wa kampeni huko Igunga. Kwa bahati wanaotegemea nguvu ya Mungu hulindwa pale bila Rage kujua shati lake limefunuliwaje hadi wenye uchu wa kutopitwa na taswiras za matukio kunasa picha kwa nafasi nzuri isiyo na utata.
Polisi, Maofisa wasimamizi wa kampeni na uchaguzi, serikali na CCM yenyewe kufanya jitihada zisizo za kawaida kufifisha jambo hilo kwa kuudanganya umma kwamba amepata adhabu ya kulipa faini ya Tsh 100, 000. Faini hiyo ilikuwa ni kinyume cha sheria za uchaguzi kwani jambo hilo lingefanyika na chama cha upinzani mambo yangekuwa makubwa.
Hatimaye pamoja na hoja nyingine kadhaa kati ya saba, moja ya hoja nzito ambazo Mahakama Kuu kanda ya Tabora imeegemea kumvua ubunge Dr. Kafumu ni hili la Aden Rage kupanda jukwaani na silaha kali kutishia wapiga kura.
Binafsi napongeza makama za Tanzania kuanza kufunguka na kulinda haki kwa misingi ya kufuata sheria bila kujali sura ya mtu ikoje. Kama mahakama zitazidi kufunguka hivyo itasaidia kujenga utawala wa kisheria ambao kwa sasa unapindishwa kila kukicha na wenye malengo binafsi ya kuhodhi nchi hii kama yao.