Tanzania sio Marekani, Marekani ni Marekani na Tanzania ni Tanzania!. Huwezi kulinganisha mbungu na nchi!.
Kule uongozi na siasa ni utumishi wa wananchi, watu wanashughuli zao za kuwapatia kipato cha kuendesha maisha yao, tena wamejitosheleza, ndipo wanaingia kwenye siasa kwa wito wa kuwatumikia watu, huku kwetu siasa ni full time job, mtu anaingia kwenye siasa kwa njaa zao, sio ili kuwatumikia watu, bali kama full time job ya kuyatumikia matumbo yao!.
Anachofanya Magufuli ni kutoa soma kwa Watanzania, tusikalie siasa, tufanye kazi uchaguzi mwingine ni 2020, hii inamaanisha kazi ya siasa ni wakati wa uchaguzi tuu pekee, baada ya uchaguzi ni kufanya kaziya kujenga nchi na sio kukalia siasa tuu!.
NB, sisi tusio na kazi ndio huwa tunakalia siasa kutwa kucha, mfano mimi, niliyangoja kwa hamu sana yale maandamano ya UKUTA na nikaahidi kushiriki, lakini bahati mbaya yaliahirishwa!.
Kufuatia Umuhimu wa Maandamano ya UKUTA: Nimehamasika, Nitashiriki ...
Japo Ruti ya Maandamano ya UKUTA Sio Kuelekea Direction ya Ikulu ...
Ombi Muhimu Kwa Jeshi Letu La Polisi."Nyinyi ni Wenzetu, September ...
Paskali
Paskali