CCM na Magufuli mmejifunza nini?

CCM na Magufuli mmejifunza nini?

Kiongozi ni yule anayeishi ndani ya mioyo ya watu, sio yule anayetegemea nguvu za dola kukaa madarakani, sio yule anayetegemea dola kutisha na kuumiza, kudhuru watu na kuwafunga midomo kwa nguvu za dola.


Uchaguzi uliopita ni uchaguzi mbaya zaidi kuwahi kutokea katika Tanganyika hadi Tanzania huru historia itaandika.
Upo sahihi ndg, kama kuna mtanzania anaonakilichofanyika ktk uchaguzi huu ni sahihi, sawa ila akiri za watu wenye akiri wanaona kilichofanyika ni aibu tupu.
 
Naomba kuuliza maswali matatu na kutoa maoni kwa Rais JPM
1. Hivi kuna tatizo gani linamzuia rais kuunda tume huru?
2. Jee tume huru huwa ni mhimili unaojitegemea kama Bunge?
3. Jee kuunda tume huru lazima pia kuwe na katiba mpya?
Maoni.
Rais wangu JPM utakumbukwa na vizazi vya nchi yetu kama utaunda tume huru ya uchaguzi haraka iwezekanavyo na ikiwezekana tume hiyo ipe mamlaka yake pekee ambayo haiingiliwi na chombo chochote cha dola. Namuomba Mungu akupe ujasiri huo na nchi yetu itaendelea kuwa salama na ya mfano duniani.
 
Rais wangu JPM utakumbukwa na vizazi vya nchi yetu kama utaunda tume huru ya uchaguzi haraka iwezekanavyo na ikiwezekana tume hiyo ipe mamlaka yake pekee ambayo haiingiliwi na chombo chochote cha dola. Namuomba Mungu akupe ujasiri huo na nchi yetu itaendelea kuwa salama na ya mfano duniani.
Yaaji akifanya hilo atakuwa amemaliza wala sitanung'unika tena! Upande wa CHADEMA nawapendekeza John Heche na Ali Bananga wawe kwenye hiyo Tume!
 
Kaja kushituka asubuhi kumeshakucha kwamba kumbe Watz hawamtaki, ikabidi atumie nguvu za dola kufunga bao la mkono wa kushoto mchana kweupe .

He has forcebly clinched the 5yrs term, now it is a ripe time for him to make appropriate reforms and adjustments in his governance.
Huu ndio ukweli ,yale yaliyotokea kule kwa Trump ndio yalikuwa yanaenda kutokea Tanzania.
 
Sijui wanatoa wapi huu upuuzi? Yanaanzisha nyuzi za ajabu ajabu tu daily! Yaani ni kero humu. Yanajifanya yako theoretical and proffesorial lakini ni idiots tu.
Wanakera sana hawa watu kila mmoja anakuja na kitheory chake cha hovyo hovyo
 
Tulichojifunza ni kwamba CCM 'inapendwa' na Watanzania hadi na Mola / Maulana na kwamba 'Watanzania' wanataka Rais Magufuli atawale Milele.


Baadhi ya Watz wanaonufaika katika mfumo wa utawala wa Magufuli wangependa atawale milele.

Lakini Watz wengi (majority) waliopigika katika hii miaka 5 iliyopita hawataki kusikia "utawala wa milele".

Juu ya yote Magufuli anayo nafasi katika hii miaka 5, kufanya marekebisho ya mfumo wa utawala/uongozi wake na uwe ni Kazi na bata na sio hapa kazi tuuuu bila kuangalia welfare za watu kwanza, akifanya hivyo, hata akistaafu au atake kuendelea kutawala/ kuongoza milele hakutakuwa na kikwazo kwani atakuwa yumo mioyoni mwa watu wengi. Kumbuka Magu kavuruga uchumi wa nchi na hivyo uchumi wa jamii vibaya sana.
 
Usiwasemee watu wewe ! Hauko mioyoni mwa watu! Hivi mikutano ya JPM ulikua huioni ? Kila kona alikokua anapita watu walijaa barabarani na kwenye mikutano kumsikiliza alafu! Unasema sehemu kubwa walikua wanamkubali TL kwa Vigezo vipi? Au humu Jf? Mjifunze kuficha aibu basi! Tatizo lenu mnadhani kura zinapigwa humu jf ! Tanzania bado hakuna Upinzani imara uliojijenga kitaasisi wa kuitoa CCM ,hakuna!
Watu walienda kumtazama Alikiba , Simba (mondi) na Kondeboy.
Chukua nyomi ya fiesta itoe waliobaki ndio walioenda kumsikiliza.
 
Magufuli alikua na wasiwasi wa kuwa rais wa kwanza wa mhula mmoja Tanzania. Amefanya aliyoyafanya sasa ameshaapishwa. Lakini ni kheri angekua rais wa mhula mmoja mwenye amani kuliko hali aliyonayo sasa hivi.
Vipi Lissu sialisema sasa basi tutaingia barabarani ?
 
Tunachopinga na ambacho ni ukweli nikuwa uchaguzi uligubikwa na udanganyifu na wizi mkubwa sana!
Tunaamini kuwa ccm haikufanikiwa hata asilimia 60 ( na wao ccm wanalijua hili vizuri)
 
Back
Top Bottom