CCM mpya imetugawa sana Watanzania

CCM mpya imetugawa sana Watanzania

Kamba ukata jiwe..!
Unaweza kusema hivyo ila kiuhalisia kila mwanaccm anajua na kufahamu fika kuwa chama kimepata mtu hasa!

Ni nani wa kumfunga paka kengere HAKUNA.

Mwamba hakujua nguvu aliyo nayo kutokana na nafasi aliyokalia na hii imeonekana ndani ya miaka mitatu iliyopita baada ya hapo ndipo kiburi, umwamba na kuanza kunyoosha makucha, baadaye anasema "mimi ndiye rais wa nchi hii, nikisema nimesema"

Hapo ndipo unaweza kupata picha kwa nini mzee Kinana aliamua kusema wazi kuwa "NAOMBA MSAMAHA" hapo ndipo kika mtu ajue chama 'kimepata mtu hasa' na mwaka huu wengi hawasemi, wapo kimya (wanaccm) ila wanalazimishwa wapande jukwaani wapige kampeni na ole wako ukatae au kutoa sababu.
 
Ninapozungumzia CCM mpya ninamaanisha hii CCM iliyoibuka kuanzia 2015, kuna wanaoiita CCM ya Magufuli. Matatizo yalianzia kwenye kusimamisha shughuli za ziasa kwa vyama vya upinzani baada ya uchaguzi.

Kazi ya vyama vya upinzani zaidi ya kuikosoa serikali ni kutoa elimu ya uraia kwa wananchi na wanachama wao. Faida ya elimu ya uraia ni kumuwezesha mtu kufanya maamuzi katika maisha yake akiwa na upeo na uelewa.

Nunua nunua ya wabunge na madiwani ilivunja morali wa siasa kwa wengi. Hata wale wagombea wasio na ushawishi katika jamii, wengi walipata kura kwakua tu walikuwa wagombea wa upinzani. Wananchi waliunganisha nguvu wakitegema wanaing’oa CCM na watu hawa walipata kura zlizolindwa na wananchi usiku kucha mpaka walitangazwa washindi. Baada ya uchaguzi Polepole anapopita kufanya ziara za kukiimarisha chama, kesho yake madiwani na wabunge wanaunga mkono juhudi.

Ninawapongeza wabunge wa upinzani waliokataa kupitisha miswaada kwa kushinikizwa na Spika Pamoja na wabunge walio wengi wa CCM. CCM inaposema wabunge wa upinzani huwa wanasusia vikao na kutoka nje, wawe wanaeleza pia sababu za wabunge hao kutoka nje.

Hili la kupita bila kupingwa limeitia CCM doa kubwa. Mama Samia akiwa anafanya kampeni Ludewa, mbunge na madiwani karibu wote wamepita bila kupingwa. Katika ushindani mpinzani wako akikuzidi kwa asilimia 90, kuna dalili kuwa ulie shindana nae ana matatizo au ulimminya kwa mbinu zote asipate ushindi. Cha ajabu huko CCM hata viongozi wakubwa katika serikali wamepita bila kupingwa kwenye majimbo yao.
Bwabwaja upuuzi wako,zimebaki siku 30. Utapotea humu jukwaani.
 
Back
Top Bottom