Acha kuwa na akili za kushikiliwa CCM ndiye nani hapa???JK+Pinda au huyo mpayukaji NapeBila shaka ni habari njema,kwamba CCM nao watatusupport kwenye hayo maandamano yanayokuja kuipinga kwa nguvu zote DOWANS.Lakini bado najiuliza JK bado hajamjua mmiliki?
Wamesubiri kuangalia upepo unaelekea kipande ipi katika hii issue ili na wao wafuate upepo. Tunasubiri kusikia kauli ya Mwenyekiti na Makamu wa Mwenyekiti wa CCM na yule Katibu Mkuu wao kama nao wanapinga malipo fisadi kwa Dowans.
Yeah, CCM watakuwa kwenye maandamano kuishinikiza serikali isiilipe Dowans, kiongozi wa maandamano ni m/kiti CCM taifa Jk! Umesasau wakati wa kikao cha NEC CCM iliilalamikia serikali kwa kupandisha bei ya mafuta?Kwa hiyo wana ipinga serikali ya ya CCM, kwahiyo tutakuwa wote kwenye maandamano, kumshinikiza Kikwete asijilipe mabilion ya walala njaa wa tanzania na pengine kumtaka angoke yeye pamoja na vibara wake............!?
Yeah, CCM watakuwa kwenye maandamano kuishinikiza serikali isiilipe Dowans, kiongozi wa maandamano ni m/kiti CCM taifa Jk! Umesasau wakati wa kikao cha NEC CCM iliilalamikia serikali kwa kupandisha bei ya mafuta?
Wanazunguka mbuyu hao, haiwezekani mazuri yawe associated na CCM halafu mabaya ya serikali yasiusianishwe na CCM. Nao saizi wanaipinga mahakama!CCM kupitia msemaji wake ambaye anakaribia kupoteza umaarufu wa jina la baba yake Nape Nauye akiongea na TBC1 amesema CCM hawatambui uamuzi wa mahakama kuu kwa kubariki na kuridhia Tanesco kuilipa DOWANS.
source: habari kwa ufupi TBC1 saa 10
Ukitaka kuwawin watz 2015 ni kuwa na ela lukuki za kununua fulana na tshirt bila kusahau khanga
Na ela za Dowans ndo starting capital kwa ajili ya izo kazi
tunataka kauli ya mwenyekiti sio ya mwenezi kwa sababu hana nguvu hata igunga kapigwa marufuku.
Filamu ndiyo Part II imeshaanza, kama hujui hilo ni changa la macho TANESCO itashindwa makamani kila kona itabanwa halafu CCM nao watakuwa kama kenge kwenye msafara wa mamba yaani kama walivyoaanza watajitia wanapinga lakini itafika hatu watasema WANAHESHIMU MAAMUZO YA MAHAKAMA KAMA MHIMILI UNAJITEGEMEA NA DOLA hivyo wasingependa kupinga maamuzi hayo japokuwa wanajua inawaauma wananchi. Huo ndiyo mwisho wa movie kisha hazina itavunjwa kwa 111bill kulipwa kwa Dowans kiiiiiiiiii.Si unamjua Mwenyekiti wa Magamba alivyo msanii wa hali ya juu? Sidhani kama atatoa kauli ya kupinga haya malipo kwa Rostam hasa ukitilia maanani kwamba fisadi Rostam na mafisadi wenzie ndio waliombeba kuhakikisha anaingia Ikulu 2005.